KIONGOZI WA MABOHORA DUNIANI ATUA NCHINI KUFANYA ROYAL TOUR TANZANIA

June 16, 2022

 




 
 

 Na John Mapepele,
 
Kiongozi Mkuu wa madhehebu ya Kiislamu ya Mabohora (Dawoodi Bohoras); Sheikh Syedna Mufaddal Saifuddin, ametua nchini leo Alhamisi Juni 16, 2022, tayari kufanya ziara ya kiimani na mapumziko mafupi. 

Saydna Mufaddal, atakuwa nchini kwa takribani wiki mbili ambapo pamoja na shughuli za kiimani amekuja kuunga mkono azma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuitangaza na kuifungua nchi hasa kupitia filamu ya Royal Tour.

“Akiwa nchini amekuja kuunga mkono malengo ya Royal Tour na yeye mwenyewe na wafuasi wake watakwenda mapumziko hapa nchini na msafara wake wote katika maeneo mbalimbali na pia iwapo taratibu zitakamilika na akaridhia anaweza kufanya mhadhara wake mkubwa wa kidini Julai hapa nchini ambapo wafuasi wake kati ya 30,000 hadi 40,000 kutoka sehemu mbalimbali duniani humfuata na tunajipanga ikitokea hivyo tutawaonesha watu hao na mabohora wengine duniani filamu ya Royal Tour,” alisema mmoja wa viongozi wa dhehebu hilo nchini Bw. Zainuldeen Adamjee. 

Akimpokea Kiongozi huyo, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema amewasilisha kwa kiongozi huyo salaam za Mhe Rais Samia ikiwemo utayari wa Tanzania kuwa mwenyeji wa mhadhara mkubwa wa mwaka wa kiongozi huyo utakaoleta maelfu ya watu hapa nchini.

“Hii ni sehemu ya muendelezo wa Royal Tour (post royal tour) ambapo Mhe Rais wetu amefanya kazi kubwa ya kuitangaza nchi yetu na sasa wawekezaji na watalii wakiwemo viongozi wa kimataifa wa kiimani na wa kijamii nao wanazidi kuja Tanzania. Kwa eneo letu sisi la utamaduni tumemhakikishia Sheikh kuwa Tanzania ni salama na aendelee kutuombea amani lakini pia alete wafuasi wake wengi zaidi kuja kutembelea na kuwekeza Tanzania,” alisema Waziri Mchengerwa.

Katika mapokezi hayo, Waziri Mchengerwa, aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi, ambaye pia anasimamia Kamati ya Rais iliyoratibu Royal Tour.

TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUJENGA MABWAWA 14 NA HEKTA ELFU 10 ZA UMWAGILIAJI KWAAJILI YA UZALISHAJI WA MBEGU, SHILLINGI BILIONI 420 KUTUMIKA.

June 16, 2022


Mheshimiwa Hussein Bashe Waziri waKilimo akizungumza wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro

Mheshimiwa Hussein Bashe Waziri waKilimo akizungumza wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro


Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji,Bw, Raymond Mndolwa akizungumza wakati wa semina hiyo

Picha ya Pamoja ya Wajumbe mbalimbali walioudhuria Semina hiyo Walioketi. Katikati ni Waziri waKilimo Mheshimiwa Hussein Bashe.






NA MWANDISHI WETU,MOROGORO

Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe, amesema kwa Mwaka wafedha ujao Wizara yake itatumia Shilingi Bilioni 420 katika ujenzi wa Miundo mbinu ya Skimu za umwagiliaji ikiwemo Hekta elfu kumi kwa ajili ya uzalishaji wa Mbegu ambapo wadau wa sekta binafsi watapewa kipaumbele kwa ajili ya kuzalisha Mbegu, ujenzi wa mabwawa 14 yatakayokuwa na miundombinu ya umwagiliaji kwa matumizi ya kilimo na mifugo.
 

Aliyasema hayo leo Mjini Morogoro wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro, Waziri Bashe ameendelea kusema kuwa utekelezaji wa kazi hiyo utakwenda sambamba na kuanzishwa kwa Ofisi za Umwagiliaji za Wilaya nchi nzima pamoja nakuajiri wasimamizi wa Skimu za umwagiliaji watakaohusika kusimamia zoezi la ukusanyaji wa ada na tozo za umwagiliaji kwa uhakika.

Eneo lingine la kipaumbele kwa Waziri Bashe ni pamoja na kuwasaidia Wakulima Wadogowadogo kupataTeknolojia bora za kilimo cha umwagiliaji kwa bei nafuu ili waweze kupata tija na kuchangia ongezeko la mavuno katika sekta ya umwagiliaji, zoezi hilo litawahusu pia Vijana wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw,Raymond Mndolwa amewataka watumishi wote wa tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya kazi kwa bidi na ubunifu ili kutimiza matarajio yaliyowekwa na serikali, akiamini taasisi yake inauwezo wakutekeleza majukumu yaliyopangwa na serikali kwa wakati, ufanisi na ubora unaotakiwa katika kuhudumia wananchi.

“ Nitamsapoti kila mtumishi aweze kutimi za wajibu wake, tumejipanga na lililopo mbele yetu tunaweza kulitekeleza”

Semina hiyo ya siku mbili imewashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo sekta binafsi, Wakulima wadogo, Wataalam waBenki, Vyama vya Ushirika, Wahandisi na Maafisa kilimo wa Wilaya ikiangazia namna ya kuboresha maeneo matatu muhimu katika kilimo cha umwagiliaji ,uzalishaji, huduma za u mwagiliaji na njia bora yakukusanya Ada naTozozaUmwagiliaji.

 

MTUME BONIFACE MWAMPOSA AFIKA NYUMBANI KWA MBUNGE WA KISESA, LUHAGA MPINA KUHANI MSIBA MAMA YAKE NA KUMBUKUMBU YA MZEE MPINA

June 16, 2022

 

 

Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza  akiendesha maombi maalum  kwa wazazi wa Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina, Marehemu Mpina Gabisi Samweli Luchemba na Marehemu Kephrine Kabula Masaga alipofika katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15, 2022. Marehemu Mzee Mpina alifariki Juni 14, 2021 na Mama alifariki Juni 1, 2022.
Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akiendesha maombi ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kufariki kwa Baba mzazi wa Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina, Marehemu Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama yake Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga aliyezikwa Juni 8, 2022. Hafla hii imefanyika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15, 2022.

Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akimbariki Diwani wa Kata ya Lubiga, Mhe. Juma Isack Mpina ambaye ni Kaka wa Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina wakati wa ibada maalum ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama yake Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu, Juni 15,2022
Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akiwapaka mafuta ya upako wananchi wa Jimbo la Kisesa walifika nyumbani kwa Mbunge wa Kisesa Mhe. Luhaga Joelson Mpina wakati wa ibada maalum ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama yake Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15,2022
Mtume Boniface Mwamposa akiwa katika picha ya pamoja na watoto wa Marehemu Kabula Kephrine Masaga baada ya ibada ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama mzazi wa Mpina aliyefariki  Juni 1, 2022. Hafla hii imefanyika katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15, 2022.
Mtume Boniface Mwamposa akiiombea Baraka ardhi ya nyumbani kwa Mzee Mpina baada ya ibada ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa mama yake Mzazi Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, Kephrine Kabula Masaga leo Juni 15, 2022 katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu.
Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akimpaka mafuta ya Baraka Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina wakati wa ibada maalum ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama yake Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15,2022


Mtume Boniface Mwamposa akiweka shada la maua katika Kaburi la Mama yake Mzazi, Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga aliyefariki Juni 1, 2022. Hafla hii imefanyika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu leo Juni 15, 2022.

Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akiendesha maombi kwenye Kaburi la Mama yake mzazi Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga aliyezikwa Juni 8, 2022 pamoja na kumuombea Baba Mzazi wa Mpina Marehemu Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba Hafla hii imefanyika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15, 2022.
Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza (kulia) akiendesha maombi maalum ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kufariki kwa Baba mzazi wa Mbunge wa Kisesa, Mhe. Luhaga Mpina (kushoto), Marehemu Mpina Gabisi Samweli Luchemba na kuhani msiba wa Mama yake, Marehemu Kephrine Kabula Masaga katika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu leo Juni 15, 2022