HIVI NDIVYO MGAMBO SHOOTING ILIVYOCHUKUA POINTI TATU ZA MAJI MAJI KWENYE DIMBA LA MKWAKWANI

September 19, 2015






RC MPYA TANGA ATEMA CHECHE

September 19, 2015



Tangakumekuchablog

MKUU wa Mkoa wa Tanga aliehamishiwa Mkoa wa Rukwa, Said Magalula, amemtisha zigo la migogoro ya ardhi aliyodai kufanya na watendaji wa Idara ya Mipango miji  mbadala wake , Mwantumu Mahiza aliehamia Tanga.

Akimkaribisha  Leo  ukumbi wa ofisi ya mikutano jengo la Mkuu wa Mkoa, Magalula alisema migogoro ya ardhi inasababishwa na watendaji wa mipango miji na sio wananchi hivyo kumuachia zigo hilo ambalo limekuwa likiwatesa wananchi.

Alisema Idara hiyo imekuwa ikiwagombanisha wananchi wenyewe kwa wenyewe  pasina sababu na linapobumbuluka hutoa visingizio vya sheria na mwaka hivyo kumtaka kulivalia njuga ikiwa na pamoja na kulikomesha.

“Mheshimiwa dada yangu Mwantumu Mahiza karibu Tanga na niwaage watu wa Tanga kwa kusema kwaherini-----ila kuna jambo moja ambalo niseme waziwazi pasina kuoneana haya kuwa Idara ya mipango miji ni mabingwa wa kugombanisha wananchi” alisema Magalula na kuongeza

“Wao ndio wanaofanya hiyana kwa kufanya mavirigisa na ujanja ujanja halafu husikilizia----pale linapobumbuluka hukaa pembeni kisha kutoa vifungu vya sheria na mwaka baada ya watu kugombana kuhamasiana” alisema

Alimtaka Mkuu huyo mpya kulikomesha tatizo hilo ambalo kwa muda mrefu limekuwa likirudisha nyuma maendeleo ya wananchi badala ya kufanya kazi za maendeleo wamekuwa wakipanga foleni ofisi za mipango miji ambako ndiko kiini cha tatizo.

Akizungumza baada ya makabidhiano, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza, alisema hatomuonea huruma kiongozi yoyote katika kazi bila kujali cheo wala nasaba hivyo kuwataka kuwatumikia wananchi kwa haki na uwazi.

Alisema yote ambayo ameelezwa na mtangulizi wake atayafanyia kazi na yule ambaye amefanya madudu ajisafishe kabla ya operesheni katika ofisi na idara hajaianza.

“Mheshimiwa Magalula changamoto na kero zote ambazo umeniambia hapa mbele ya wakuu wa idara na watendaji ofisini nimezipokea na niko tayari kwa lolote kwani uwezo ninao” alisema Mahiza

Alisema kinachotakiwa ni kufanya kazi kwa uwazi na uwajibikaji ili kuwaletea maendeleo wananchi na kudai kuwa yeyote ambaye ataonyesha ukiukwaji wa maadili ni vyema akajiengua mapema.


Mkuu wa Mkoa mpya wa Tanga, Mwantumu Mahiza, akizungumza na wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Idara na  Taasisi mbalimbali za Serikali pamoja na viongozi wa vyama vya siasa mara baada ya makabidhiano na mtangulizi wake aliehamishiwa Mkoa wa Katavi.

BARAZA LA VYUO VIKUU AFRIKA MASHARIK(IUCEA)KUWA NA MAONESHO YA VYUO VIKUU UGANDA

September 19, 2015

Katibu Mtendaji wa Baraza la Vyuo Vikuu Afrika Mashariki(IUCEA)Profesa Mayunga Nkunya akizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha jana kuhusu hali ya wahitimu katika nchi za Afrika Mashariki na ushirikiano wa Baraza la Wafanyabiashara Afrika Mashariki(EABC) kuwajengea uwezo wahitimu ili kumudu soko la ajira .Taasisi hiyo itakuwa na maonesho ya vyuo katika nchi za EAC  Kampala ,Uganda mwezi Oktoba ,2015.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Wafanyabiashara wa Afrika Mashariki(EABC)Lilian Awinja akizungumza katika mkutano huo.

Waandishi wa habari wakifatilia kwa makini kwaajili kuuhabarisha umma.
Imeandaliwa na www.rweyemamuinfo.blogspot.com

Dk Shein Aendelea na Kampeni Zake na Kusema Ataendeleza Kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa na Kuleta Maendeleo Zaidi kwa Wazanzibar katika Wananchi Wake na Elimu Bure Zanzibar.

September 19, 2015

Mgombea Urais wa Zanzibar Kupitia Chama cha Mapinduzi pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa CCM Zanzibar alipowasili katika viwanja vya Mpira Konde Kisiwani Pemba kuendelea na Kampeni Kisiwani Pemba.
Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi waliofika katika uwanja wa kunde kuhudhuria mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein.wakati akiwasili katika viwanja hivyo vya mpira Konde Wilaya ya Micheweni Pemba.
Wanachama wa CCM Wakimshangilia Mgombea wao wa Urais Dk Shein, wakati akiwasili katika viwanja vya mpira Konde kwa ajili ya mkutano wake wa Tatu wa Kampeni zake kisiwani Pemba.
Taswira ya wakati wa mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais kupitia CCM katika viwanja vya mpira Konde Pemba kama inavyooneka Mwanachama huyu wa CCM akishangilia akiwa na picha ya Mgombea Urais wa CCM Dk Shein.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ndg Hamad Mberwa Hamad akiwahutubia na kutuoa Sere za CCM zilivotelekezwa na kuiletea Maendeleo Zanzibar katika kipindi chake Dk Shein cha miaka mitano na kuwataka kumpa kura kwa mara ya pili kuendeleza mafanikio ya Maendeleo Zanzibar katika sekta mbalimbali za Jamii

Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi Dk Shein akiwana na Viongozi wakifuatilia mkutano huo wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya mpira Konde kisiwani Pemba ikiwa ni mkutano wake wa tatu kisiwani Pemba akiwa katika kampeni zake.
Katibu wa Idara ya Uenezi Afisi Kuu Zanzibar Ndg Waride Bakari Jabu akiwahutubia Wananchi wa Konde katika mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein uliofanyika katika uwanja wa mpira Konde Kisiwani Pemba.

LOWASSA APOKELEWA KWA KISHINDO MJINI BUKOBA LEO

September 19, 2015

 Umati wa Wananchi wa Mji wa Bukoba ukiwa umefurika kwenye Uwanja wa Aghakhan kuhudhulia Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, leo Septemba 19, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akihutubia wananchi Bukoba waliofika kwenye Mkutano wa Kampeni, kusikiliza sera zake, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.

Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwanadi baadhi ya wagombea wa Udiwani wa vyama vinavyouda UKAWA, kwenye Mkutano wa Kampeni, kusikiliza sera zake, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na mmoja wa wadau wa Mabadiliko, Prof. Azaveli Rwaitama, katika Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Jijini Mwanza, Mh. Ezeckiel Wenje akihutubia wananchi kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Mke wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CHADEMA, Willfred Lwakatare, akimuombea Mumewe Kura kwa Wananchi wa Mji wa Bukoba, wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akimpongeza Mke wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CHADEMA, Willfred Lwakatare, mara baada ya kuzungumza na Wananchi wa Bukoba.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukoba Mjini kupitia CHADEMA, Willfred Lwakatare, akihutubia wananchi kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye akihutubia wananchi kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.
Aliekuwa Meya Mji wa Bukoba, Anatory Amani akizungumza kwenye Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera leo Septemba 19, 2015.

KONGAMANO LA WAJASIRIAMALI WANAWAKE NCHINI LAFANA

September 19, 2015

 Meneja wa Mpango wa  Uchangiaji wa Hiari kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bi. Mwanjaa Sembe (katikati) akimfafanulia jambo Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi katika Kongamano la Wajasiriamali Wanawake nchini kabla ya uzinduzi wa Kampuni ya Voice of Women Entrepreneures Tanzania (VoWET) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo (jana).wa kwanza kushoto ni Meneja Msaidizi wa Mfuko huo Bi Matilda Nyallu. 
 Meneja wa Mpango wa  Uchangiaji wa Hiari kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bi. Mwanjaa Sembe (katikati) akimfafanulia jambo Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi katika Kongamano la Wajasiriamali Wanawake nchini  kabla ya uzinduzi wa Kampuni ya Voice of Women Entrepreneures Tanzania (VoWET) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo (jana).
 Wafanyakazi wa Mfuko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakiwa katika Banda la Mfuko huo wakati katika Kongamano la Wajasiriamali Wanawake nchini kabla ya uzinduzi wa Kampuni ya Voice of Women Entrepreneures Tanzania (VoWET) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo (jana), wa kwanza kulia ni Meneja wa Mpango wa  Uchangiaji wa Hiari kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bi. Mwanjaa Sembe.
 Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi akizindua Kampuni ya Voice of Women Entrepreneures Tanzania (VoWET) katika Kongamano la Wanawake Wajasiriamali nchini lililofanyika jijini Dar es Salaam, kushoto ni Rais wa VoWET nchini Bi. Mahida Waziri
 Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Media, Reginald Mengi akimlisha keki Rais wa VoWET nchini Bi. Mahida Waziri katika Kongamano la Wanawake Wajasiriamali nchini mara baada ya uzinduzi wa Kampuni ya Voice of Women Entrepreneures Tanzania. (Picha na Benjamin Sawe)

MGOMBEA UDIWANI KATA YA MBAGALA KUU (CCM) YUSUF MANJI AZINDUA KAMPENI ZAKE DAR ES SALAAM LEO

September 19, 2015

 Kiongozi wa Kamati ya Ushindi kwa CCM kutoka Kigoma, Nicholaus Zacharia (kulia), akimtambulisha Yusuf Manji katika uzinduzi huo.
 Mgombea nafasi ya udiwani Kata ya Mbagala Kuu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Manji (kushoto), akihutubia wananchi na makada wa chama hicho katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika eneo la Kichemuchemu Kaskazini Dar es Salaam leo jioni.
  Kiongozi wa Kamati ya Ushindi kwa CCM kutoka Kigoma, Nicholaus Zacharia, akihutubia katika uzinduzi huo.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Temeke, Sophia Kinega akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Mchumi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Neema Urio akihutubia kwenye uzinduzi huo.
 Kada wa CCM, Godbertha Kinyondo akisalimia wananchi kwenye uzinduzi huo.
 Makada wa CCM wakiserebuka
 Vijana wa hamasa wa CCM wakiwa kazini.
 Wananchi wakiwa kwenye mkutano huo.
 Michango mbalimbali ikitolewa.
 Umati ukimsikiliza Yusuf Manji.
 Mkazi wa eneo hilo, Sharifa Ali akimueleza Manji kuhusu kero ya kutokuwa na soko.
 Dogo akihubia kwenye uzinduzi huo. Dogo huyo alisema wana CCM wanapaswa kumchagua Magufuli kuwa Rais, Mbunge Mangungu na Diwani Manji.
 Chipukizi wakifanya vitu vyao.
 Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
Yusuf Manji (kulia) akifuatilia matukio mbalimbali kwenye uzinduzi huo.