Naibu
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba (MB)
akizungumza kwenye uzinduzi wa Azam TV uliofanyika Hyatt Regency The
Kilimanjaro Hotel mwishoni mwa Juma ambapo amesema Azam TV imekujali
kuleta mapinduzi katika ulimwengu wa Digitali na kutoa fursa ya ajira
kwa Vijana wa Tanzania wenye vipaji sanjari na kuitangaza nchi yetu
katika bara la Afrika hasa kwenye upande wa Soka na Filamu.
Azam
TV itaanza kurusha matangazo yake Desemba 6 mwaka huu, Watanzania kaeni
mkao wa kula kupata King’amuzi kwa bei rahisi ambacho kitakuwa na
chaneli zisizopungua 50.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Azam Tv, Rhys Torrington akizungumza na wageni
waalikwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Azam Television jijini Dar es
Salaam mwishoni mwa Juma.
Naibu waziri Januari Makamba akifuatilia maelezo ya awali ya Azam TV