NHC YAWATANGAZIA KIAMA WANAOGUSHI FOMU ZA UPANGISHAJI

June 01, 2017

 Meneja wa Shirika la Taifa la Nyumba(NHC) mkoani Tanga Mussa Kamendu katikati akionyesha moja kati ya chemba ambazo zinafanyiwa ukarabati eneo la mtaa wa market Jijini Tanga  na Fundi Mchundo wa Shirika hilo jana wakati alipotembelea kuona hali ya ukarabati huo unavyoendelea
 Meneja wa Shirika la Taifa la Nyumba(NHC) mkoani Tanga Mussa Kamendu katikati akionyesha waandishi wa habari maeneo mbalimbali waliokarabati
 Meneja wa Shirika la Taifa la Nyumba(NHC) mkoani Tanga Mussa Kamendu katikati akionyesha waandishi wa habari maeneo mbalimbali waliokarabati
Meneja wa Shirika la Taifa la Nyumba(NHC) mkoani
Tanga Mussa Kamendu kulia akionyeshwa moja kati ya chemba ambazo zinafanyiwa ukarabati eneo la mtaa wa market Jijini Tanga  na Fundi Mchundo wa Shirika hilo wakati alipotembelea kuona hali ya ukarabati huo unavyoendelea
 Meneja wa Shirika wa Shirika la Taifa la Nyumba Mkoani Tanga (NHC),Mussa Kamendu akikagua ukarabati wa nyumba za shirika hilo ambazo zinafanyiwa marekebisho
 Mafundi wakiendelea na kazi kama wanavyoonekana
Meneja wa Shirika wa Shirika la Taifa la Nyumba Mkoani Tanga (NHC),Mussa Kamendu akikagua mitaro iliyochimbwa kwa ajili ya kupitisha mfumo wa maji taka
SHIRIKA la Nyumba la Taifa Mkoani Tanga (NHC) limewa tahadharisha watu wanaoghushi fomu za maombi ya kupangisha katika nyumba zao na kuziuza kwa wananchi kuacha mara moja tabia hiyo kwani watakabanika watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya dola.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Meneja wa Shirika hilo,Mussa Kamendu wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mipango mbalimbali ya shirika hilo ikiwemo kuzifanyia ukarabati nyumba wanazozimiliki ili ziweze kuwa katika muonekana mzuri kwa zile ambazo zimeonekana  kuchakaa.

Alisema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wananchi kughusi fomu ambazo zinatolewa na shirika hilo kwa kuzisambaza kwa wengine na kuwauzia jambo ambalo ni kinyume na utaratibu uliopo.

“Ukiangalia sisi kama shirika tumekuwa tukitoa fomu kwa wananchi ambao wanataka kupangisha kwenye nyumba zetu lakini katika hilo kumejitokeza baadhi ya watu wanazitoa kopi na kuziuza kitendo ambacho ni uvunjifu wa taratibu tulizoziweka “Alisema.

“Jambo hili ni hatari hasa kwa ustawi wa shirika letu kwani
linachangia kukosesha mapato hivyo tutahakikisha tunawa shughulikia watakaobainika kufanya hivyo bila kuangalia nafasi yake kwa maslahi ya ustawi wa shirika letu “Alisema Meneja huyo.

Aidha alisema licha ya jitihada hizo lakini pia wameweka mpango
kabambe wa kuhakikisha wadaiwa wote wanalipa madeni yao ya pango kwa wakati ili kuweza kutoa fursa kwa shirika hilo kuweza kujiendesha na kuweza kufanikisha mipango ya maendeleo.

Kamendu aliwataka pia wapangaji wao wazingatie mikataba walioingia na shirika hilo ikiwa pamoja na utunzaji mazingira ya nyumba hizo na kulipa kodi kwa wakati kabla ya hatua za kisheria hazijachukuliwa.

Aidha pia alisema hivi sasa tayari shirika hilo limekwisha anza
kufanya ukarabati wa nyumba hizo ikiwa pamoja na kuboresha mifumo ya maji taka, kuweka bati mpya na upakaji wa rangi katika nyumba zilizopo katika maeneo mbalimbali ndani ya Jiji la Tanga.

Alisema miongoni mwa nyumba walizoanza kuzifanyia ukarabati ni pamoja na zilizopo maeneo ya Chumbageni,kwa karatunga,barabara 4,6,Bombo na Raskazoni ambapo marekebisho hayo yanafanyika kwa lengo la kurudisha ubora wa nyumba hizo.

Aliongeza kuwa marekebisho yanayofanywa na shirika hilo yana lengo la kuhakikisha nyuma zao zinakuwa katika ubora mzuri ambao utamfanya mpangaji aweze kuishi kila kukumbana na usumbufu wa aina yeyote.

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA KITUO KUTUNZA TAARIFA NA MFUMO WA KUKUSANYIA MAPATO KIELEKTRONIKI

June 01, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli akihutubia baada ya wakati wa kutembelea Kituo cha Kutunzia Taarifa (Data centre) na na  kuzindua Mfumo wa Ukusanyaji Mapato wa Serikali kwa Njia ya kielektronini  kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein akihutubia katika Kituo cha Kutunzia Taarifa (Data centre) wakati wa kuzindua Mfumo wa Ukusanyaji Mapato wa Serikali kwa Njia ya kielektronini  kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine akitoka kutembelea kituo cha kutunzia taarifa (Data Centre) kabla ya kuzindua  Mfumo wa Serikali wa Ukusanyaji Mapato kwa Njia ya kielektroniki   kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli akisalimiana na Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirika la simu Tanzania TTCL Bw. Waziri Kindamba wakati wa kutembelea Kituo cha Kutunzia Taarifa (Data centre)  na  kuzindua Mfumo wa Ukusanyaji Mapato wa Serikali kwa Njia ya kielektronini  kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli akisalimiana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Bw. Joseph Kichere wakati wa kutembelea Kituo cha Kutunzia Taarifa (Data centre)  na  kuzindua Mfumo wa Ukusanyaji Mapato wa Serikali kwa Njia ya kielektronini  kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli akionesha Ipad maalumu aliyopewa ili kumuwezesha  kufuatilia ukusanyaji wa mapato ya kila siku. Kulia kwake ni  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein na kushoto kwake ni  Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wakati wa  kutembelea kituo cha kutunzia taarifa (Data Centre) kabla ya kuzindua  Mfumo wa Serikali wa Ukusanyaji Mapato kwa Njia ya kielektroniki   kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein  akionesha Ipad maalumu aliyopewa kumuwezesha  kufuatilia ukusanyaji wa mapato ya kila siku. kushoto kwake ni  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli na Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wakati wa  kutembelea kituo cha kutunzia taarifa (Data Centre) kabla ya kuzindua  Mfumo wa Serikali wa Ukusanyaji Mapato kwa Njia ya kielektroniki   kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu
 Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akionesha Ipad maalumu itayomuwezesha kufuatilia ukusanyaji wa mapato ya kila siku. Kulia kwake ni  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John pombe Magufuli na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein na viongozi wengine wakati wa  kutembelea kituo cha kutunzia taarifa (Data Centre) kabla ya kuzindua  Mfumo wa Serikali wa Ukusanyaji Mapato kwa Njia ya kielektroniki   kwenye sherehe zilizofanyika Kijitonyama jijini Dar es salaam leo June 1, 2017. Picha na Ikulu

TAIFA STARS YAANZA KUJIFUA NCHINI MISRI KUIKABILI LESOTHO JUNI 10 UWANJA WA TAIFA

June 01, 2017

Wachezaji wa Taifa Stars wakipasha joto miili yao kabla ya kuanza mazoezi ya nguvu kwenye Uwanja wa Tolip Sports City jijini Alexandria leo asubuhi Juni 01, 2017. Taifa Stars  inajiandaa kushindana na Lesotho Juni 10, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika Cameroon.
 Makipa wa Taifa Stars kutoka kushoto, Said Mohammed, Aishi Manula na Benno Kakolanya wakivuta pumzi baada ya mazoezi ya timu ya Tanzania ya Mpira wa Miguu ‘Taifa Stars’ yaliyofanyika jana usiku kwenye Uwanja wa Tolip Sports City jijini Alexandria jana usiku Mei 31, 2017. Taifa Stars  inajiandaa kushindana na Lesotho Juni 10, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataiafa ya Afrika (AFCON) za mwaka 2019 zitakazofanyika Cameroon.

YALIOJIRI KATIKA KIKAO CHA 39,MKUTANO WA SABA WA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO

June 01, 2017
  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk. Tulia Ackson akijibu miongozo mbalimbali ya wabunge mara baada ya kumaliza kipindi cha Maswali ya Kawaida katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 01, 2017.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akijibu maswali ya papo kwa papo mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe.George Simbachawene katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Naibu Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Edwin Ngonyani  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Mhe.Anastazia Wambura  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 aziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akisoma Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe.Hussein Mwinyi akizungumza jambo na Mbunge wa Viti Maalum(CHADEMA) Mhe.Catherine Ruge katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma June 1, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe.Anna Mollel akiuliza swali katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kantui kutoka Kilosa wakiwa Bungeni kujifunza Shughuli mbalimbali katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.
 Wabunge wakifuatilia hoja mbalimbali katika kikao cha 39 cha Mkutano wa Saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Juni 1, 2017.

Picha zote na Daudi Manongi,MAELEZO, DODOMA.
OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YAWAPIGA MSASA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO SERIKALINI KUHUSU SHERIA YA TAKWIMU YA MWAKA 2015

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YAWAPIGA MSASA MAAFISA HABARI NA MAWASILIANO SERIKALINI KUHUSU SHERIA YA TAKWIMU YA MWAKA 2015

June 01, 2017
unnamed
 Mwanasheria wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Oscar Mangula akiwasilisha mada inayohusu Sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015 wakati wa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini yaliyofanyika leo mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuifahamu Sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015.
 1
Meneja wa Idara ya Mbinu za kitakwimu, Viwango na Uratibu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Emilian Karugendo akitoa ufafanuzi wa namna Ofisi ya Taifa ya Takwimu inavyokusanya takwimu rasmi nchini kwa kuzingatia kanuni za kitaifa na kimataifa wakati wa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini yaliyofanyika leo mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuifahamu Sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015.
 2
Baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati wa mafunzo kwa Maafisa hao yaliyofanyika leo mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuifahamu Sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015.
 3
 Baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati wa mafunzo kwa Maafisa hao yaliyofanyika leo mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuifahamu Sheria mpya ya Takwimu ya mwaka 2015.
………………………………
Na: Emmanuel Ghula
Morogoro
1 Juni, 2017.

OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imetoa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini leo mkoani Morogoro kuhusu Sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 ili kuwajengea uwezo wa kufahamu namna sheria hiyo inavyofanya kazi.
Akifafanua sheria hiyo, Mwanasheria wa NBS, Oscar Mangula amesema sheria ya Takwimu No. 9 ya mwaka 2015 imeipa Ofisi ya Taifa ya Takwimu jukumu la kuratibu na kusimamia ukusanyaji wa takwimu rasmi nchini.
“Sheria ya Takwimu No. 9 ya mwaka 2015 ni sheria inayoipa NBS jukumu la kuratibu na kusimamia shughuli zote za upatikanaji wa takwimu rasmi nchini. Hivyo, kama taasisi yoyote inataka kufanya utafiti kwa minajili ya kutoa takwimu rasmi ni lazima iwasiliane na NBS ili kupata miongozo ya ukusanyaji wa takwimu rasmi,” amesema Mangula.
Mangula amesema kuwa, ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ama taasisi kuendesha utafiti na kuchapisha au kutoa takwimu rasmi bila kuwasiliana na NBS kwani inaweza kukusanya takwimu ambazo hazina ubora na zinazoweza kupotosha umma.
Aidha, Meneja wa Takwimu za Kodi kutoka NBS Fred Matola amesema NBS hutoa takwimu rasmi kwa kuzingatia miongozo ya kitaifa na kimataifa inayotolewa na Umoja wa Mataifa ili kukidhi mahitaji ya nchi pamoja na kutumika kimataifa.
“Takwimu rasmi zinakusanywa kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na umoja wa kimataifa ili kukidhi mahitaji ya nchi, hivyo NBS ina wajibu kisheria kusimamia upatikanaji wa takwimu rasmi nchini”, amesisitiza Matola.  
Ofisi ya Taifa ya Takwimu ina jukumu la kuratibu na kusimamia ukusanyaji, uchambuzi na upatikanaji wa takwimu rasmi nchini.

BUNGE LAPITISHA BAJETI YA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO SHILINGI TRILIONI 11.752

June 01, 2017
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akihitimisha mjadala wa Bajeti ya Wizara yake ambapo Bunge limepitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) na Naibu wake Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakifuatilia kwa makini hoja mbalimbali za Wabunge wakati wakijadili Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni Mjini Dodoma, ambapo Bunge hilo limepitisha Bajeti ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) ndani ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, baada ya wabunge kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, akimpongeza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.  Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ndani ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, baada ya Wabunge kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo ya jumla ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Mkurugenzi wa Idara ya Mipango-Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Richard Mkumbo (kulia), akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa, Bw. Samwel Kamanga kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya wizara hiyo.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Babati Vijijini Mhe. Jitu Soni nje ya Ukumi wa Bunge mara baada ya Wabunge kupitisha Bajeti ya Wizara hiyo ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Gavana wa Benki Kuu (BOT), Prof. Beno Ndullu (kushoto), akimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), baada ya Bunge kupitisha makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Mjini Dodoma
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akipeana mkono na Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Bw. Mohamed Mtonga, nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma baada ya Bunge kupitisha bajeti ya Wizara hiyo ya shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoro) akimshukuru na kumpongeza Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kusimamia na kuhakikisha kuwa Bajeti ya Wizara hiyo inaandaliwa kwa viwango vya juu na hatimaye kupitishwa na Bunge Mjini Dodoma ambapo Wizara hiyo imeidhinishiwa kukusanya nakutumia shilingi trilioni 11.752 kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa saba kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wakuu wa Wizara na Taasisi zilizochini ya Wizara hiyo nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma baada ya kuhitimishwa kwa mjadala wa bajeti wa Wizara hiyo.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)

UPDATES; MSIBA WA MBUNGE MSTAAFU WA JIMBO LA MOSHI MJINI PHILEMONI NDESAMBURO

June 01, 2017
Nyumbani kwa Marehemu Mzee Philemoni Ndesamburo aliyefariki dunia jana katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi.
Baadhi ya waombolezaji wakiwemo ndugu wakijiandaa kwenda kutizama mwili wa Mzee Ndesamburo katika HospItali ya Rufaa ya KCMC.
Baadhi ya Waombolezaji wakiwemo Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wakia nyumbani kwa Mzee Ndesamburo.
Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini ,Godbless Lema pamoja na mkewe Neema Lema wakiwasili nyumbani  kwa marehemu Mzee Ndesamburo.
Mbunge wa jimbo la Arusha mjini ,Godbless Lema akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Rombo ,Joseph Selasini mara baada ya kukutana nyumbani kwa marehemu Mzee Ndesamburo .
Mtoto wa Marehemu Ndesamburo ,Ndohorio Ndesamburo akiwaeleza jambo waombolezaji waliofika nyumbani kutoa pole kwa familia.
Mwenyekiti wa Chadema kanda ya Kaskazini,Aman Golugwa akitia saini katika kitabu cha waombolezaji nyumbani kwa marehemu Ndesamburo.
Baadhi ya viongozi wa Chadema wakiwa katika kikao kifupi nyumbani kwa mareheu Ndesamburo.
Familia ya marehemu Ndesamburo wakiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa ajili ya kutizama mwili wa mpendwa wao.
 
Mkurugenzi wa kampuni ya World Frontier,John Hudson akimfariji ,mtoto wa marehemu Ndesamburo,Lucy Owenya nyumbani kwao eneo la Mbokomu mjini Moshi.
Baadhi ya waombolezaji wakiwafariji wafiwa.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.