NEWS ALERTL IGP MWEMA AFANYA MABADILIKO KADHAA KATIKA JESHI LA POLISI

November 30, 2013

 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema   amefanya mabadiliko ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera pamoja na baadhi ya Wakuu wa Upelelezi wa mikoa na  wakuu wa Polisi wa Wilaya katika baadhi ya mikoa hapa Nchini. 

 Katika mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kagera, Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Philipo Kalangi  amehamishiwa Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam, kuwa Mkuu  wa kikosi cha kusimamia usalama wa Mazingira na nafasi yake  inachukuliwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi  (SACP) George Mayunga ambaye alikuwa Mkuu wa kikosi cha  kusimamia mazingira Makao Makuu ya Polisi Dar es Salaam.

KOCHA WA CAMEROON ASAINI MIAKA MWILI AZAM

November 30, 2013

Kocha mpya wa Azam FC. Joseph Marius Omog (katikati) akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kusaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo.


KLABU ya Azam inapenda kuufahamisha umma hususan wapenzi wa mpira wa miguu kuwa imeingia mkataba na kocha Joseph Marius Omog raia wa Cameroon kwa kipindi cha miaka miwili (2) kuanzia leo.

Kocha Omog ni bingwa kwani anakuja kuifundisha Azam akiwa ametoka kuiongoza klabu ya A.C Leopards ya Jamhuri ya Kongo (Brazaville) kutwaa ubingwa wa ligi ya nchi hiyo kwa misimu miwili mfululizo (2012 na 2013).

Timu hii ilikuwa haijatwaa ubingwa wa ligi kwa zaidi ya miaka 30. Kwa mwaka huu wametwaa ubingwa wakiwaacha wapinzani wao, Diables Noirs kwa pengo la pointi kumi (10) wakikusanya pointi 87 katika ligi yenye timu 18.

Pia ni mwaka jana tu (2012) aliiwezesha A.C Leopards kunyakua ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Afrika kwa kuzipiga kumbo timu ngumu na zenye uzoefu mkubwa kama vile Mas de Fes ya Morocco, Heartlands ya Nigeria na Sfaxien ya Tunisia.

Mafanikio hayo ya kutwaa ubingwa wa Afrika yalifikiwa baada ya miaka 38 tangu klabu ya Jamhuri yas Kongo ifanye hivyo, na kumfanya kocha Omog kuwa moja ya makocha wa kupigiwa mfano barani Afrika.

Kigoda: Kamanda wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM)

November 30, 2013


WAZIRI wa Biashara na Viwanda nchini, Dr.Abdalla Kigoda ameteuliwa kuwa kamanda wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Tanga (UVCCM) katika uteuzi ambao ulifanywa na kamati ya utekelezaji Taifa chini ya Mwenyekiti wao Sadifa Juma.

Akizungumza na Tanga Raha, katika ofisi za Umoja huo mkoani hapa, Mwenyekiti wa Umoja huo, Abdi Makange alisema mchakato huo ulianzia ngazi ya mkoa ambapo wao waliamua kumpendekeza Kigoda na hatimaye kupata baraka kutoka kamati ya utekelezaji na kumuidhinisha kwa kumpitisha.

LAAC WAIAGIZA HALMASHAURI HANDENI KUPELEKA ZAIDI YA MILI 105 KWA VIJIJI RUZUKU YA SERIKALI.

November 30, 2013
MWENYEKITI wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajabu Mbaruku imeiagiza Halmashauri ya wilaya ya Handeni kuhakikisha kwamba inapeleka kiasi cha sh.milioni 105,779,260 kwa vijiji vilivyostahili kuzipata ikiwa ni michango ya lazima ya asilimia 20 ya ruzuku ya serikakali kuu kwa ajili ya maendelo vijijini,

Kauli ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo ilitokana na halmashauri hiyo kushindwa kuzipeleka vijijini fedha za ruzuku ya serikali kuu kwa ajili ya miradi ya maendeleo hali ambayo inapelekea kuchangia kudhorotesha kasi yao katika shughuli mbalimbali.
Licha ya kutoa agizo hilo pia aliiagiza halmashauri hiyo kuandaa mchanganuo wa madeni inayodai na kudaiwa kwa kuonyesha majina ya wadai na wadaiwa ikiwemo kuchukua hatua za makusudi za kupatikana kwa fedha zinazodaiwa.

Rais Kikwete atimiza ahadi yake ya kujenga daraja la Mwanhuzi wilayani Meatu

November 30, 2013



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongozwa na Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kukagua daraja la Mwanhuzi lililoko Meatu Mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongozwa na Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kukagua daraja la Mwanhuzi lililoko Meatu Mkoani Simiyu.

MAKAMU WA RAIS DKT.BILAL AENDESHA ZOEZI LA HARAMBEE YA KUCHANGIA MADAWATI MFUKO WA MAENDELEO YA ELIMU JIMBO LA KENGE

November 30, 2013

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi chaeti, Mkurugeniz wa Kagera Sugar, Hamadi Yahaya, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wake wa kuchangia maendeleo ya Elimu ya Jimbo la Nkenge mkoa wa Kagera,wakati wa hafla ya harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Elimu Jimbo la Nkenge kununua madawati ili kusadia shule za msingi za Jimbo hilo. Harambee hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam, jana usiku. Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumta Mshana na (kushoto kwa Makamu) ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanal Fabian Masawe.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza wakati wa hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Elimu Jimbo la Nkenge kununua madawati ili kusadia shule za msingi za Jimbo hilo. Harambee hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam, jana usiku. Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Asumta Mshana na (kushoto kwa Makamu) ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanal Fabian Masawe.

WAZEE WA NGWASUMA KUWAPAGAWISHA WAKAZI WA MOROGORO.

November 30, 2013

BENDI ya Mziki wa Dansi ya nchini FM Academia “Wazee wa Ngwasuma”inatarajiwa kufanya onyesho kali la Mlipuko wa Burudani mkoani Morogoro  Desemba 6 mwaka huu katika ukumbi wa Kingstone Night Club.

Onyesho hilo linatarajiwa kuanza majira ya saa tatu usiku ambalo litakuwa la aina yake kutokana na aina ya wanamuziki wa bendi hiyo iliyojizolewa umaarufu mkubwa hapa nchini.


FAINALI YA KOMBE LA UHAI CHAMAZI

November 30, 2013
Mechi ya Fainali ya michuano ya Kombe la Uhai inayoshirikisha timu za umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu itachezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.