DEO NJIKU,KAMOTE KUMALIZA UBISHI LEO:

October 15, 2013
BONDIA ALLAN KAMOTE WA TANGA.

BONDIA DEO NJIKU WA MOROGORO

ALLAN KAMOTE AKIPIMA UZITO JANA.

DEO NJIKU NAE AKIPIMA UZITO.

HAPO KAMOTE NA NJIKU WAKITAMBIANA.

MRATIBU WA PAMBANO HILO,ABASI MWAZOA.
Na Oscar Assenga, Tanga.
BONDIA Allen Kamote wa Tanga ametamba kumtwanga vibaya mpinzani wake Deo Njiku wa Morogoro kwenye raundi ya pili ya pambano lao la kuwania ubingwa wa Dunia WBF litakalokuwa la raundi kumi na mbili lenye uzito wa kg 61 ambalo litafanyika katika uwanja wa Mkwakwani leo.

Pambano hilo linatarajiwa kuanza majira ya saa kumi jioni leo octoba 16 katika uwanja huo ambapo pia kutakuwa na 
mapambano nane ya utangulizi.

Kamote alitoa kauli hiyo jana mara baada ya kumaliza kupima uzito 
katika ukumbi wa CCM Hall jijini hapa na  kueleza kutokana na maandalizi ambayo ameyafanya upo uwezekano mkubwa wa kuibuka na ushindi katika pambano hilo ambalo litakuwa na upinzani.
 
"Njiku namfahamu vizuri sana niliwahi kupambana naye na kumchapa vibaya na hii itakuwa ni mara ya pili kucheza nae,natamka kumwambie nilichokifanya kwenye pambano lililopita kitakuwa zaidi yake "alisema Kamote.

Kwa upande wake,Bondia Deo Njiku alisema atamkalisha chini mpinzani 
wake huyo katika raundi ya pili katika pambano hilo kutokana na umahiri aliokuwa nao.
 
 “Ninachoweza kusema nimetoka Morogoro kwa lengo moja tu la kuhakikisha nachukua mkanda huo ili kuwapa heshima watu wa mkoa wangu “Alisema Njiku.

Mratibu wa Pambano hilo,Abasi Mwazoa alisema maandalizi yake
yanaendelea vizuri na kuyataja mapambano ya utangulzi kuwa ni bondia Rajabu Mahoja wa Tanga ambaye atapanda ulingoni kuzichapa na  J.J Ngotiko wa Tanga watakaocheza pambano la raundi kumi lenye uzito wa kg 57.

Mwazoa aliongeza kuwa bondia Khamis Mwakinyo wa Tanga atazichapa na 
Haruna Magali wa Morogoro katika pambano la raundi sita lenye uzito wa kg 64 wakati Saimon Zabron na Mohamed Kibari wote wa Tanga watachuana kwenye pambano la raundi sita lenye uzito wa kg 61.

Aliyataja mapambano mengine kuwa ni bondia Said Mundi wa Tanga 
atazichapa na David Maina wa Kenya katika pambano la raundi sita lenye uzito wa kg 61 ambalo linatarajiwa kuwa na ushindani wa hali ya juu.

Pambano mengine yatakuwa ni bondia Zuberi Kitandula wa Tanga
atazichapa na Hajji Juma wa Tanga katika mpambano utakaokuwa wa raundi nane lenye uzito wa kg 55 huku Jumanne Mohamed wa Tanga atapanda ulingoni kuzichapa na Obote Ameme wa Dsm wataocheza pambano la raundi nne lenye uzito wa kg 57.

Mratibu huyo alilitaja pambano la mwisho la utangulizi litakuwa ni
kati ya bondia Alli Boznia wa Kenya ambaye atazichapa na Jacob Maganga wa Tanzania litakalokuwa la raundi nne lenye uzito wa kg 69.

EID MUBARAK

October 15, 2013
Mmiliki wa Tanga Raha blogspot anapenda kuwatakia waislamu wote hapa nchini Eid Mubarak njema na yenye mafanikio ikiwemo kusherekea kwa amani

RC GAWALA AKABIDHI ZAWADI ZA RAIS KIKWETE KWA VITUO VIWILI TANGA.

October 15, 2013

MKUU WA MKOA WA TANGA ,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KULIA AKISALIMIANA NA AFISA MFAWIDHI WA MAHABUSU YA WATOTO JIJINI TANGA NG'WANZA MUHANGWA LEO KABLA YA KUWAKABIDHI ZAWADI KUTOKA KWA RAIS WA JAMHURI WA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE ZA SIKUKUU YA  IDD EL HAJI

KULIA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIMKABIDHI MBUZI AFISA MFAWIDHI WA MAHABUSU YA WATOTO  NGWANZA MUHANGWA WA KWANZA KUSHOTO ANAYESHUHUDIA NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO NA DIWANI WA KATA YA USAGARA CARLOS HIZZA

KULIA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIKABIDHI MBUZI KWA KITUO CHA KUTUNZA WAZEE MWANZANGE

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA ALIYESIMAMA AKIZUNGUMZA NA WAZEE WANAOISHI KATIKA KITUO CHA KUTUNZIA WAZEE MWANZANGE WA KUSHOTO KWANZA NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO NA KULIA KWAKE NI DIWANI WA KATA YA DUGA MH.KOMBO

WAZEE WAKIMSIKILIZA MKUU WA MKOA KWA UMAKINI MKUBWA LEO

MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAZEE WANAOISHI KATIKA KITUO CHA KUWATUNZA WAZEE MWANZANGE MARA BAADA YA KUWAKABIDHI ZAWADI ZA IDDI EL HAJ KUTOKA KWA MH RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE.
MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIKABIDHI ZAWADI ZA SIKUKUU YA IDDI EL HAJI ZILIZOTOLEWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,MH JAKAYA MRISHO KIKWETE WAZEE WANAOISHI KWENYE KITUO CHA KUWALEA MWANZANGE JIJINI TANGA.

PICHA ZOTE NA PASKAL MBUNGA,TANGA.
TANGA.
MKUU wa Mkoa wa Tanga ,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa leo amekabidhi zawadi zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwet kwa vituo viwili kwa ajili ya sikukuu ya Idd El Haji.

Zawadi zilizotolewa ni pamoja na mbuzi mmoja kwa kila kituo,mchele,mafuta ya kupikia,chumvi na sabuni.

Vituo hivyo ni kituo cha mahabusu nya watroto cha barabara ya 15/16 na kituo cha kutunzia wazeee cha mwanzange vyote vya jijini Tanga.

Awali akisoma kwa mkuu wa mkoa wa Tanga,Afisa Ustawi wa Jamii kwenye kituo hicho,Clara Kibanga walimshukuru Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kikwete kwa kuwapatia msaada huo na kuwakumbuka wazee.

Katika msafara huo kulikuwa na viongozi mbalimbali akiwemo mkuu wa wilaya ya Tanga, Halima Dendego,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Juliana Malange na wakuu wa idara kutoka halmashauri ya Jiji la Tanga.

RC TANGA AKERWA NA UCHAFU KATA YA USAGARA NA MZINGANI.

October 15, 2013
MKUU WA MKOA WA TANGA AKITOA MAELEKEZO KWA VIONGOZI WA KATA YA MZINGANI NA USAGARA BAADA YA KUKERWA KUTOKANA NA UCHAFUA ULIOKITHIRI MAENEO YA KATA HIZO.
Na Oscar Assenga,Tanga.
MKUU wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Jiji la Tanga Juliana Malange kuwasimamishia mshahara wa mwezi wa kumi maafisa watendaji wa kata Mzingani na Usagara kutokana na maeneo yao kukutwa yakiwa machafu.

Amesema wasimamishiwe mishahara hiyo mpaka hapo mkurugenzi atakapokwenda kuyakagua maeneo hayo na kuyakuta kwenye hali ya usafi na baadae ampelekee taarifa mkuu huyo wa mkoa ili aruhusu wapewe mishahara.

Gallawa ametoa agizo hilo wakati alipotembelea maeneo hayo kuangalia hali ya usafi ambapo alibaini baadhi ya maeneo kuwa na uchafu uliokithiri na ndipo alipotoa kauli hiyo.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kila mara anapopita katika maeneo hayo huyakuta machafu kila siku kitendo ambacho kinalifanya eneo hilo kutokuwa katika mandhara nzuri.

Maafisa watendaji hao ni Said Bendera ambaye ni mtendaji wa kata ya Mzingani na Senyenge Mbaruku wa kata ya Usagara.

Mkuu huyo wa mkoa wa Tanga asema wakati wa ziara yake ya kuzunguka maeneo mbalimbali jijini Tanga mtaa utakaokutwa na uchafu atawajibika Afisa Mtendaji.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwataka maafisa watendaji kuhakikisha wanasimamia kikamilifu suala la usafi katika maeneo yao ili kuyaweka mazingira yao katika hali ya nzuri.

Hata hivyo watendaji hao walimuhaidi mkuu wa mkoa huyo kuwa watahakikisha ndani ya wiki moja maeneo yao yatakuwa katika halai nzuri ya usafi.