WAZAZI WATAKAOWAOZESHA WATOTO WAO BADALA YA KUWAPELEKA SHULE WILAYANI NZEGA KUKIONA CHA MTEMAKUNDE

October 04, 2016
 Mkuu wa Wilaya ya Nzega Mhe Gedfrey Ngupula

Na Mathias Canal, Tabora

Tatizo la Mimba za utotoni na kuozesha wanafunzi katika umri mdogo limetajwa kuwa ni kikwazo kikubwa katika jamii kwani watoto wa kike wananyimwa haki ya kupata elimu ili kujikwamua na fikra mpya katika uchumi na namna ya kuwa na familia bora na endelevu katika kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Mkuu wa Wilaya ya Nzega Mhe Gedfrey Ngupula Ameyabainisha hayo katika mahojiano maalumu na Mwandishi wa Mtandao wa www.wazo-huru.blogspot.com kuhusu mikakati ya kukabiliana na mimba za utotoni pamoja na wazazi kuwaachisha masomo watoto wao wa kike ili kuwaozesha kwa fikra potofu za kupata mali zikiwemo Ng'ombe na fedha.

DC MTATURU AWAONYA WANASIASA WANAOWAZUIA WANANCHI KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

October 04, 2016
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mkunguakihendo wakati wa ziara ya kikazi
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Rustika Turuka akisisitiza jambo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Kuzungumza na baadhi ya viongozi wa Vitongoji, Kata na Vijiji katika ukumbi wa shule ya sekondari Mkunguakihendo wakati wa ziara ya kikazi
 Wananchi wakisikiliza kwa makini maagizo ya serikali kupitia  kwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi

Tigo yadhamini mbio za Tigo Igombe Charity Marathon

October 04, 2016

Mgeni rasmi, Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza na wanariadha wa Tigo Igombe Charity Marathon, kabla ya kuzindua mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni wa wiki iliyopita mjini Tabora.

Mtoa huduma Mwl Mwajuma Mwamba akiwasajili wanariadha mara baada ya kumaliza mbio za Tigo Igombe Marathon zilizofanyika mjni hapa.

Mkurugrnzi wa Tigo kanda ya Ziwa Ally Maswanya akizungumza na wanariadha wa mbio za baiskeli kabla ya kuzindua shindano hilo.

Wanaridha wakiwa tayari kusubiria kipyenga cha Tigo Igombe Charity Marathon

Vijana wa mkoa wa Tabora wakishindana kukimbia wakati wa mashindano ya Tigo Igombe Charity Marathon yaliyofanyika leo mjini hapa.

Mgeni rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akizungumza na mwakilishi wa Tanzania Breweries Ltd ambao ni wadhamini wenza wa mbio za Tigo Igombe Marathon, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa, Ally Maswanya, mbio hizo zimefanyika leo mjini hapa.

hoto Best Regards Krantz Mwantepele| Managing Director KONCEPT | Mikocheni B, House No 58. Opp Clouds Media. Dar es Salaam, Tanzania | M: + 255 624053989 / +255 658123310 E: Krantz.charles@koncept.co.tz Blog: www.mwanaharakatimzalendo.blogspot.com W: www.koncept.co.tz

RAIS DKT MAGUFULI ASHUHUDIA RAIS KABILA WA DRC AKIWEKA JIWE LA MSINGI KWENYE JENGO LA MAMLAKA YA BANDARI (TPA) JIJINI DAR ES SALAAM LEO

October 04, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli akihutubia  katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila kuhutubia katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016

 Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila akihutubia katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila akipokea zawadi ya picha ya Bandari ya Dar es salaam kutoka kwa mwenyekiti wa Bodi ya TPA  Bw. Ignas Aloys Rubaratuka  katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la wakipata maelezo toka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkr John Pombe Magufuli akimshuhudia mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Joseph Kabila akifunua pazia kuashiria kuwekwa kwa jiwe la msingi la Jengo la ONE STOP CENTRE la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) jijini Dar es salaam leo Oktoba 4, 2016

  PICHA NA IKULU.
MALINZI: SITAWAACHA SERENGETI BOYS

MALINZI: SITAWAACHA SERENGETI BOYS

October 04, 2016
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amesema kwamba ataendelea kuwa karibu na vijana na Timu ya Tanzania ya vijana ‘Serengeti Boys’ licha ya kuondolewa na Congo kwenye harakati za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana zitakazofanyika Madagascar, hapo Aprili, mwakani.
Mipango ya TFF kwa sasa inayoongozwa na Malinzi kwa sasa ni kuiiingiza timu hiyo kwenye program ya timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 maarufu kwa jina la Ngorongoro Heroes baada ya kuguswa na kilio cha vijana hao ambao walishindwa kujizuia kumwaga machozi mbele ya Malinzi ambaye alifanya kazi kubwa kuwatuliza pamoja na viongozi wengine.

Serengeti Boys ilipoteza mchezo dhidi ya Congo Oktoba 2, 2016. Kwa kupoteza mchezo huo dakika ya pili kati ya nne ya nyongeza baada ya kumalizika kwa dakika 90, kumefanya vijana hao wa Tanzania kuenguliwa kwenye mashindano ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika – fainali zitakazofanyika Madagascar.
Dakika moja ndiyo iliyoipoteza Serengeti Boys kufuzu kwa fainali hizo kwa bao la dakika ya 92 la lililofungwa na Mountou Edoward.
“Niko nanyi, najua mna group la WhatsApp, naomba msifute namba yangu. Iwe humo na mambo yenu mengi naomba mniambie humo, na nitayashughulikia iwe binafsi au kiofisi. Nawahakikishia sitawaacha,” alisema Malinzi alipowafariji vijana hao ambao wanatarajiwa kuingia leo saa 3.00 usiku huu kwa ndege ya Shirika la Ndege ya Rwanda.
“Umri wenu bado sana wa kucheza soka. Program za TFF, CAF na FIFA ziko nyingi pia mnaweza kupata nafasi ya kucheza Olimpiki na kuna michuano mingi, sitawaacha,” alisema Malinzi na kusisitiza ana imani na timu hiyo ambayo kwa dakika 90 za mchezo dhidi ya Congo walipambana kwelikweli kutetea taifa lao pendwa Tanzania.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA KONGAMANO LA 30 LA KIMATAIFA LA WANASAYANSI LILILOANDALIWA NA TAASISI YA TAIFA YA UTAFITI WA MAGONJWA YA BINADAMU

October 04, 2016
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 30 la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR), lililoanza leo Oktoba 4 na kilelele chake kukoma Oktoba 6,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
 .....................................................
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amelalani vikali mauaji ya watafiti WAWILI wa kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Selian cha Arusha na dereva MMOJA waliokuwa kazi katika kijiji cha Mvumi Makulu wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo leo 4-Oct-2016 wakati akifungua kongamano ya 30 la Kimataifa la Wanasayansi lililoandaliwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais amesema kuwa tukio hilo ni baya na amewahakikishia watafiti wanaoshiriki kongamano hilo kuwa serikali itachukua hatua stahiki kwa watu  waliofanya kitendo hicho cha kinyama ili kukomesha tabia hiyo.
“Haiwezekani hata kidogo watu kufanya mauaji hayo ya kikatili na waachwe bila kuchukuliwa hatua kali za kisheria alisisitiza Makamu wa Rais”
Akizungumzia masuala ya utafiti, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema serikali inatambua kazi nzuri inayofanywa na watafiti hao hivyo serikali itaendelea kutoa mchango wake wa hali na mali ili kuhakikisha watafiti hao wanafanya kazi zao kwa ufanisi unaotakiwa.
Makamu wa Rais pia amewahimiza wafadhili waendelee kusaidia watafiti hasa wanaofanya tafiti za afya nchini kwa sababu tafiti hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa namna ya kukabiliana na magonjwa mbalimbali.
Amesema kuwa watafiti wanamchango mkubwa katika kuleta maendeleo kupitia matokeo ya tafiti zao nchini hivyo jitihada hizo ni muhimu zikaimarishwa ipasavyo.
 Kongamano hilo la 30 la Kimataifa la Wanasayansi lililoandaliwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu -NIMR- linajumuisha watafiti mbalimbali kutoka Ulaya,Afrika na Amerika.
Katika kongamano hilo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ameshiriki katika zoezi utoaji wa tuzo kwa wanasayansi waliofanya tafiti mbalimbali za afya nchini.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Baadhi ya Washiriki kutoka sehemu mbalimbali ndani nje ya nchi wakisikiliza hotuba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 30 la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR), lililoanza leo Oktoba 4 na kilelele chake kukoma Oktoba 6,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Dkt Mwele Malecela akizungumza mapema leo,alipokuwa akimkaribisha Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan,wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 30 lililoanza leo Oktoba 4 na kilelele chake kukoma Oktoba 6,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.Katika kongamano hilo kauli mbiu yake ni “Uwekezaji katika tafiti zenye ubunifu ili kufikia malengo endelevu ya dunia.”. 
Dkt Mwele alieleza pia Mada zitakazojadiliwa ndani ya kongamano hilo kuwa zitajikita zaid kwenye maeneo kama vile 1. Mkakati wa kuboresha afya ya uzazi, ya mama, watoto wachanga na vijana. 2. Magonjwa sugu yasiyoambukiza na changamoto zake,3. Kuendeleza mafanikio yaliyopatikana katika mapambano dhidi ya UKIMWI, kifua kikuu na malaria,4. Usalama wa Maji, Usafi wa mazingira na usafi binafsi,5. Mkakati wa afya moja katika kudhibiti magonjwa ya milipuko,pamoja na 6. Magonjwa ya kitropiki yasiyopewa kipaumbele.


Baadhi ya Washiriki wa kongamano hilo kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje ya chi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo,ambapo mada zaidi ya 200 zitawasilishwa na kujadiliwa kwa siku tatu.
Baadhi ya Washiriki wa kongamano hilo kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje ya chi wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo,ambapo mada zaidi ya 200 zitawasilishwa na kujadiliwa kwa siku tatu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya,Dkt.Hamis Kigwangala,alipokuwa akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam leo,kwa ajili ya uzinduzi wa Kongamano la 30 la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),pichani kushoto ni Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Dkt Mwele Malecela
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu,Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Dkt Mwele Malecela,alipokuwa akiwasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam leo kufungua Kongamano la 30 la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR),pichani kati ni Naibu Waziri wa Afya,Dkt.Hamis Kigwangala.
Baadhi ya Washiriki wa kongamano hilo kutoka sehemu mbali mbali ndani na nje ya chi wakiimba wimbo wa Taifa kabla ufunguzi wa Kongamano hilo,lililoanza leo jijini Dar.
BOFYA HAPA KUSOMA HOTUBA YA MAKAMU WA RAIS KUHUSU KONGOMANO HILO BOFYA HAPA KUSOMA HOTUBA YA MKURUGENZI MKUU WA NIMR DKT MWELE MALECELE BOFYA HAPA
ETHIOPIA YAFUTA MCHEZO DHIDI YA TAIFA STARS

ETHIOPIA YAFUTA MCHEZO DHIDI YA TAIFA STARS

October 04, 2016
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea barua kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Ethiopia (EFF), ikielezea juu ya kufutwa kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliokuwa ufanyike Oktoba 8, 2016.
EFF imesema kwamba imelazimika kufuta mchezo huo ulikuwa kwenye kalenda ya FIFA kwa sababu za hali ya hewa si rafiki kwa sasa nchini Ethiopia.

Kwa barua hiyo, Kocha Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Tanzania (Taifa Stars), Charles Boniface Mkwasa atalazimika kuvunja kambi ya timu hiyo ambayo iliweka kwenye Hoteli ya Blue Pear iliyoko Ubungo, Dar es Salaam.
Mchezo huo uliratibiwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ambalo huwa na kalenda ya wiki ya mechi za kimataifa kwa wanachama wake – Tanzania ni miongoni mwao. EFF, ndio walioomba nafasi hiyo.
Ingekuwa ni faida kwa Tanzania kama ingeshinda mchezo huo kwa maana kina alama za nyongeza kama inatokea unaifunga timu mwenyeji.
Matokeo yake yangekuwa ni sehemu malumu kupima viwango vya ubora na uwezo wa timu za taifa. Kwa sasa Tanzania inashika nafasi ya 132 kati ya nchi 205 wanachama wa FIFA zilizopimwa ubora. Ethiopia yenyewe inashika nafasi ya 126.
Argentina inaongoza ikifuatiwa na Ubelgiji anakocheza Mbwana Samatta – nyota wa kimataifa wa Tanzania. Samatta anacheza klabu ya K.R.C Genk inayoshiriki Ligi Kuu ya Ubelgiji. Timu nyingine bora kimataifa ni Ujerumani, Colombia na Brazil.
Katika Bara la Afrika, Ivory Coast ambayo ni ya 34 kwa ubora duniani ndiyo inayoongoza ikifuatiwa na Algeria, Senegal, Tunisia na Ghana.

MAKAMU WA RAIS WA CUBA AMALIZA ZIARA YA SIKU TATU YA KIKAZI NCHINI

October 04, 2016



 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akiagana na mgeni wake Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa ambaye amemaliza ziara ya siku 3 ya kikazi nchini.
                                          ............................................................
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Salvador Antonio Valdes Mesa ameondoka nchini mchana huu baada ya kumaliza ziara ya kiazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. 


Lengo la ziara hiyo ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Salvador Antonio Valdes Mesa ni kuendeleza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Cuba hasa katika sekta mbalimbali ikiwemo elimu,afya,utamaduni,michezo na utalii.

Katika sekta ya utalii, Serikali ya Cuba imeahidi  kuisaidia Tanzania katika kuendeleza utalii katika fukwe pamoja na kubadilishana uzoefu na wataalamu wa hapa nchini katika sekta hiyo ili kusaidia kuongeza pato la taifa kupitia shughuli  za utalii nchini.


Aidha kwenye sekta ya viwanda Tanzania na Cuba zimekubaliana kushirikiana katika ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha kutengenezea madawa ya binadamu nchini.
Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Salvador Antonio Valdes Mesa ameagwa na mwenyeji wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan baada ya kuhitimisha ziara yake nchini.                                     
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kulia) akimsindikiza  mgeni wake Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Antonio Valdes Mesa ambaye amemaliza ziara ya siku 3 ya kikazi nchini.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

RC SHIGELLA AFUNGUA KIKAO CHA PILI CHA BODI YA BARABARA

October 04, 2016

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akifungua kikao cha pili cha bodi ya barabara kilichofanyika leo kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kulia akifuatilia makabrasha ya kikao cha bodi ya barabara leo kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi,kulia ni Mbunge wa Jimbo la Mlalo(CCM)Rashid Shangazi,Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM)Adadi Rajabu
Meneja wa Wakala wa Barabara nchini Tanroad Mkoani Tanga,Mhandisi Alfred Ndumbaro akiwasilisha taarifa ya mpango wa barabara kwenye kikao hicho

Mkuu wa wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe kushoto akibadilishana mawazo na Mbunge wa Jimbo la Handeni,Omari Kigoda kabla ya kuanza kikao cha pili cha bodi ya barabara

Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM) kulia akiteta jambo na Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Korogwe,Daudi Gao kabla ya kuanza kikao cha bodi ya barabara picha ya kwanza ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM)Marry Chatanda akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso

 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM)Stephen Ngonyani alimaarufu Maji Marefu kulia akiteta jambo wakati wa kikao hicho kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini (CCM),Marry Chatanda
Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM)Jumaa Aweso akiteta jambo na Mkuu wa wilaya hiyo,Zainabu Issa wakati wa kikao hicho

 Meneja wa Wakala wa Barabara nchini Tanroad Mkoani Tanga,Mhandisi Alfred Ndumbaro akifuatilia kwa umakini  jambo katika kikao cha bodi ya barabara leo
Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini,(CCM)Omari Kigoda kushoto akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe wakati wa kikao cha pili cha bodi ya barabara

wa kwanza kulia ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini,(CCM)Stephen Ngonyani alimaarufu Maji Marefu akipitia maelezo ya makabrasha ya kikao cha bodi ya barabara aliyesimama kulia ni Mbunge wa Jimbo la Lushoto (CCM),Shabani Shekilindi kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe mji(CCM)Marry Chatanda na anayefuata ni Mbunge wa Jimbo la Mkinga (CCM)Dastan Kitandula


Wajumbe wa Kikao cha Pili cha Bodi ya Barabara kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa,Mkuu wa wilaya ya Pangani,Zainabu Abdalla Issa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Mussa Mbaruku katikati akisikiliza kwa umakini hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wakati akifungua kikao cha pili cha bodi ya barabara
Mbunge wa Jimbo la Kilindi (CCM) Omari Kigua akipitia maelezo kwenye kabrasha kabla ya kuanza kikao cha bodi ya barabara
Mkuu wa wilaya ya Muheza,Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kilindi wakifuatilia kwa umakini kikao cha bodi ya pili cha barabara leo