KAMISHNA CHAGONJA AWAPOKEA WANAMICHEZO WALIOTOKA SWAZILAND NA KUWAHUTUBIA

August 07, 2015

HP1
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo  wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akiwa katika picha ya pamoja na wanariadha wa Jeshi la Polisi walioshiriki Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO).Wengine ni Viongozi wa Michezo wa Jeshi la Polisi (Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
HP2
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo  wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akizungumza na Wanariadha wa  Jeshi la Polisi, Wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza iliyofanyika Makao Makuu ya Polisi Jana baada ya kufanya vizuri katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO).Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Jonas Mahanga (Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
HP3
Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja akimpongeza Mwanariadha wa  Jeshi la Polisi, PC Basil John aliyeshinda medali tatu za dhahabu katika Michezo ya Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO), Wakati wa hafla fupi ya kuwapongeza iliyofanyika Makao Makuu ya Polisi Jana.(Picha na Alexander Mpeka-Jeshi la Polisi)
……………………………………………………………………………………….
Michezo ya SARPCCO ilianzishwa kwa lengo la kuwakutanisha Maafisa na Askari Polisi ili kuweza kubadilishana mbinu za kukabiliana na uhalifu pamoja na kuwasaidia kujenga afya na kuwa wakakamavu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Michezo ni sehemu ya kuitambulisha nchi yoyote kama Taifa huru lenye utamaduni wake. Michezo ni mojawapo ya viungo muhimu katika utamaduni wa kila jamii ya binadamu duniani. Michezo ni chombo muhimu sana katika kuiendeleza jamii. Aidha, michezo huweza kuwa kielelezo na utambulisho wa Taifa kwa kutoa burudani, kujenga na kukomaza afya ya mwili na akili, kujenga nidhamu, kujitangaza kiuwezo na vipaji. Ushiriki katika michezo ya kimataifa husaidia kulitangaza Taifa nje ya mipaka yetu. Vile vile michezo huwaweka pamoja Askari na kuwawezesha kufahamiana na kuondoa misongo ya mawazo “STRESS”. Hivyo Ni wazi kuwa mmetumia vyema fursa mliyoipata katika michezo hiyo ikiwemo ya kubadilishana mawazo na uzoefu katika kutenda kazi za polisi, Hongereni sana.
Nimepewa taarifa kuwa kulikuwa na ushindani mkubwa katika michezo hiyo na ninyi pamoja na uchache wenu  mmfenakiwa kupata medali 12, 6 za dhahabu, 4 za fedha na 2 za shaba, Pia timu yetu ya riadha (wanaume) ya mbio ndefu imefanikiwa kuwa timu bora katika mashindano hayo na Askari PC Basil John aliibuka mchezaji bora wa mashindano baada ya kushinda medali 3 za dhahabu katika mbio za mita 800, 1500 na mbio za nyika (Km 12 cross country).Nawapongeza sana walioshinda
Mmefanya kazi kubwa  na mmehakikisha kuwa heshima ya Jeshi letu la Polisi iliyojijengea katika michezo hiyo tangu kuanzishwa kwake inaendelea kudumu pamoja na uchache wenu kutokana na wanamichezo wengine kutofanikiwa kwenda kutokana na sababu mbalimbali.
Aidha nawapongeza sana kwa nidhamu mliyoionyesha katika kipindi chote cha michezo hiyo, Nidhamu na kujituma kwa juhudi ndio msingi wa kufanikiwa katika mchezo wowote hivyo ninyi mmekuwa mabingwa katika kipengele hicho.
Aidha, napenda pia kutumia fursa hii kuwashukuru wadhamini waliotuwezesha kwa kutupatia vifaa vya michezo ambao ni Benki ya CRDB, NMB, African Life Assuarance, na PPF, kwani kwa ufadhili wao walioutoa umefanyiwa kazi na hivyo kupata mafanikio ya ushindi, Hivyo wakati mwingine wasisite kuiunga mkono timu yetu ya Polisi.
 napenda kuwaahidi kuwa tutaendelea kuipa kipaumbele michezo ili kuweza kuwaimarisha kiafya na kuwakutanisha na wenzenu katika mataifa mengine na nawatakieni maandalizi mazuri katika michezo mingine iliyopo mbele yenu na safari njema ya kurudi katika mikoa yenu.
AHSANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »