NAPE AANZA ZIARA KWENYE VYOMBO VYA HABARI
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali, Bwana
Gabriel Lyimo Nderumaki ( wa pili kutoka kushoto) akielezea masuala
mbali mbali yanayohusu tasinia ya habari wakati wa mkutano na Katibu wa
NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye uliofanyika kwenye ofisi za
Kampuni ya Magazeti ya Serikali,Tazara jijini Dar es Salaam.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza wakati wa kikao chake
na Viongozi na waandishi wa Magazeti ya Serikali alipowatebelea leo
ikiwa sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea vyombo vya habari.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wahariri wa Magazeti ya Serikali.
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali, Bwana Gabriel Lyimo Nderumaki akizungumza na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimina na Mhariri Mkuu wa
Magazeti ya Raia Mwema na Raia Tanzania kwenye ofisi za magazeti hayo
mtaa wa Mwinyijuma,Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akionyeshwa sehemu ya waandishi
wanapoandaa habari na Mhariri Mkuu wa Magazeti ya Raia Mwema na Raia
Tanzania
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na baadhi ya viongozi
na wahariri wa gazeti la Raia Tanzania na Raia Mwema.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa kwenye picha ya pamoja na wahariri wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania.
WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA JAMHURI YA KIISLAMU YA IRAN.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammed Javad Zarif alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na ujumbe aliofuatana nao,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammed Javad Zarif (wa pili kulia) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na ujumbe aliofuatana nao,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Mohammed Javad Zarif (kulia kwa Rais ) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na ujumbe aliofuatana nao,[Picha na Ikulu.]
MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI DODOMA LEO
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akijibu maswali Bungeni mjini Dodoma Februari, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Musoma Mjini, Vincent
Nyerere kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Februari 5, 2015
Waziri
Mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na wananchi kutoka wilaya ya
Wanging’ombe mkoani Njombe walitembelea Bunge mjini Dodoma kwa mwaliko
wa Mbunge wao wa jimbo la Njombe Magharibi, Gerson Lwenge ambaye pia ni
Naibu Waziri wa Ujenzi Februari 5, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wananchi kutoka
wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe waliotembelea Bunge mjini Dodoma
kwa mwaliko wa Mbunge wao wa jimbo la Njombe Magharibi, Gerson Lwenge
ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi Februari 5, 2015. (Picha na Ofisi
ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Viti Maalum, Al
Shaimaa John Kwegyir, kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Februari 5,
2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
MKUU WA MKOA WA RUKWA ENG. STELLA MANYANYA AONGOZA SIKU YA SHERIA NCHINI MKOANI RUKWA
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya kulia akihutubia katika
maadhimisho ya siku ya sheria nchini Mkoni Rukwa leo tarehe 04/02/2015
katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga. Kaulimbiu ya
maaadhimisho hayo ikiwa “Fursa ya kupata haki: Wajibu wa Serikali,
Mahakama na Wadau”. Katika hotuba yake hiyo alisema ipo haja kubwa kwa
Serikali kubadili sheria zake ili lugha ya mahakamani na hukumu
ziandikwe kwa kiswahili. Kwa upande wa wananchi aliwaasa kujiepusha na
tabia ya kujichukulia sheria mkononi ili kudumisha amani nchini.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Jaji Sambo akipokea
gwaride la heshima kutoka kwa kikosi cha Jeshi la Polisi wakati wa
maadhimisho ya siku ya Sheria Mkoani Rukwa leo tarehe 04/02/2015.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Mhe. Jaji Sambo katikati
akisoma hotuba yake ya maadhimisho ya siku ya sheria Mkoani Rukwa ambapo
aliwataka mahakimu wote Mkoani Rukwa kutimiza majukumu yao ipasavyo kwa
mujibu miongozo ya mahakama ili kusaidia uharakishwaji wa utoaji haki
kwa wananchi kwa wakati. Aliwaeleza pia wadau wote wa sheria wakiwepo
mawakili wa kujitegemea kuwa mashauri yote ya kesi yatakua yakisimamiwa
na kutolewa maamuzi na mahakama na sio mawakili kutaka kuingilia
utendaji wa mahakama.
Baadhi ya wadau na viongozi wa Sheria na Serikali katika meza kuu.
Sehemu ya mahakimu, mawakili, wanasheria na wageni waalikwa katika maadhimisho hayo.
(Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa@rukwareview.blogspot.com)
KIZUGUTO AULA TFF,SASA AWA OFISA HABARI MPYA
TFF YAPATA OFISA HABARI MPYA
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Baraka Kizuguto kuwa Ofisa Habari
kuanzia Februari 1 mwaka huu.
Kabla ya
uteuzi huo, Kizuguto alikuwa Ofisa Habari wa klabu ya Young Africans, nafasi
aliyoitumikia kwa miaka miwili.
Kizuguto
ana Stashahada ya Juu ya Habari na Mawasiliano kutoka Chuo cha LEARN IT cha Dar
es Salaam. Pia ana ujuzi wa kusanifu tovuti, ufundi wa kompyuta na uchambuzi wa
mifumo ya kompyuta.
Mei mwaka
jana, Kizuguto aliteuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)
kuhudhuria mafunzo ya usajili na uhamisho wa kimataifa wa wachezaji kwa njia ya
mtandao (TMS) yaliyofanyika Johannesburg, Afrika Kusini.
TFF
inamtakia kila la kheri katika majukumu yake mapya.
KAMATI YA NIDHAMU YAADHIBU TISA
Kamati ya
Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa adhabu kwa watu
tisa wakiwemo viongozi, wachezaji na kocha mmoja kwa kupatikana na hatia ya
makosa ya kinidhamu.
Katika
kikao chake kilichofanyika juzi (Februari 3 mwaka huu) jijini Dar es Salaam,
Kamati hiyo imewafungia mwaka mmoja viongozi wawili wa Chama cha Mpira wa Miguu
wa Wanawake Tanzania (TWFA) Mkoa wa Mwanza kwa kuwashawishi wachezaji wa Mwanza
Queens kugomea uamuzi halali.
Sophia
Tigalyoma (Mwenyekiti) na Katibu wake Hawa Bajanguo walitiwa hatiani kwa
kuwashawishi wachezaji kugomea uamuzi wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake
ya TFF kutupa rufani yao dhidi ya Kigoma.
Kocha wa
Polisi Tabora, Eliakim Christopher amefungiwa mechi kumi na kupigwa faini ya
sh. 300,000 kwa mujibu wa Kanuni ya 39(2) ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baada
ya kutiwa hatiani kwa kumtukana refa wakati wa mechi kati ya timu yake na
Panone FC iliyochezwa mjini Moshi.
Wachezaji
wa JKT Oljoro FC, Dihe Makonga, Swaleh Idd Hussein, Ramadhan Mnyambegu na
nahodha Shaibu Nayopa wamefungiwa mechi tatu na faini ya sh. 300,000 kila mmoja
kwa kuzingatia kanuni ya 36(10) ya FDL kutokana na kufanya vurugu kwenye mechi
kati yao na Burkina Faso iliyochezwa mjini Morogoro.
Mtunza Vifaa
(Kit Man) wa JKT Oljoro FC, Eliud Mjarifu amefungiwa miezi sita na kupigwa
faini ya sh. 200,000 kwa kumpiga Kocha wa Burkina Faso, CR Mwakambaya kwenye mechi
kati ya timu hizo iliyofanyika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Pia Mjarifu
amepewa onyo kali na kutakiwa kutorudia tena kutenda kosa, kwani hata mwenendo
wake wakati wa shauri hilo ulionyesha utovu wa nidhamu mbele ya Kamati.
Naye
Mtunza Vifaa wa Rhino Rangers FC, Albert Mbuji amefungiwa miezi sita na faini
ya sh. 200,000 kwa kupatikana na hatia ya kuwatukana na kugomea uamuzi wa marefa
kwenye mechi dhidi ya Polisi Dodoma. Adhabu hizo zimetolewa kwa mujibu wa
kanuni ya 40(2) ya FDL.
Kamati
hiyo imeondoa malalamiko dhidi ya Ofisa Habari wa klabu ya Ruvu Shooting, Masau
Bwire kwa vile refa Israel Mujuni Nkongo ambaye ni mlalamikaji hakufika kwenye
shauri hilo.
Nkongo
alimlalamikia Bwire akidai alitoa maneno yenye kuweza kuchochea chuki dhidi
yake kwa waamuzi, kwani kupitia redio 100.5 Times FM, Bwire alidai refa huyo
ndiye aliyeshinikiza kuondolewa kwa refa Mohamed Theofil kwenye ratiba ya Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL).
Pia Kamati
hiyo imemkuta bila hatia Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Singida (SIREFA), Gabriel Gunda ambaye TFF ilimlalamikia kuwa akiwa mtendaji
mkuu wa chama hicho alishindwa kuhakikisha timu ya Singida inaingia uwanjani
kucheza na Dodoma kwenye mechi ya Kombe la Taifa kwa Wanawake.
Kamati
ilikubaliana na utetezi wa Gunda kuwa, jukumu la timu hiyo lilikuwa mikononi
mwa viongozi wa TWFA Singida, na tayari SIREFA kupitia Kamati yake ya Nidhamu
ilishatoa adhabu kwa viongozi wa timu hiyo kutokana na kitendo hicho.
Nayo
malalamiko ya Polisi Tabora FC kutaka mechi yao dhidi ya Toto Africans FC
irudiwe kwenye uwanja huru (neutral ground) kwa madai ya kuchezeshwa zaidi ya
muda unaotakiwa, na kutokuwepo ulinzi wa kutosha kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini
Mwanza yamekataliwa.
Pia Kamati
ya Nidhamu imeelekeza malalamiko ya timu za Mwadui FC na Polisi Mara FC dhidi
ya Toto Africans kwa kumchezesha mchezaji Ladislaus Mbogo bila kuonyesha leseni
yake yasikilizwe haraka na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) kwa vile si ya
kinidhamu.
Wakati
huo huo, Kamati ya Nidhamu inaendelea na kikao chake leo (Februari 5 mwaka huu)
kusikiliza malalamiko mengine ya kinidhamu yaliyofikishwa mbele yake.
TFF YAONYA KUHUSU UENDESHAJI
MPIRA WA MIGUU
Kutokana
na matatizo mbalimbali ya kiutendaji yaliyojitokeza kwenye uendeshaji,
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa hadhari kuwa shughuli zote
za mpira wa miguu zinazohusu mkoa wowote wa Tanzania Bara zitasimamiwa na Chama
cha Mpira wa Miguu cha Mkoa husika, yakiwemo mashindano ya Kombe la Taifa la
Wanawake.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Tanzania mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Wahasibu
Mhasibu
Mkuu wa Serikali,Mwanaidi Mtanda akiongea na waandishi wa habari jana
jijini Dar es salaam kuhusiana na mkutano wa 22 wa kimataifa wa Chama
cha Wahasibu Wakuu wa Serikali wa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika
(ESAAG) utakaofanyika nchini kuanzia Machi 09, hadi 12 mwaka 2015.
Mwenyekiti
wa Kamati ya maandalizi ya mkutano wa 22 wa kimataifa wa Chama cha
Wahasibu Wakuu wa Serikali wa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika
(ESAAG) ambaye pia ni Makamu Mhasibu Mkuu wa Serikali Azizi Kifile
akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam
(hawapo pichani) kuhusu mkutano utakaofanyika nchini kuanzia Machi 09,
hadi 12 mwaka 2015.
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Tanzania
itakuwa mwenyeji wa mkutano wa 22 wa kimataifa wa Chama cha Wahasibu
Wakuu wa Serikali wa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAAG)
utakaofanyika nchini kuanzia Machi 09, hadi 12 mwaka 2015.
Kauli
hiyo imetolewa na Mhasibu Mkuu wa Serikali,Mwanaidi Mtanda kwa niaba ya
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile jana jijini Dar
es salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano
huo utakaofanyika nchini.
Mhasibu
Mkuu wa Serikali Mwanaidi alisema kuwa mgeni rasmi katika mkutano huo
anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya
Kikwete.
Katika
mkutano huo, mada mbalimbali zinatarajiwa kujadiliwa zikilenga kwa
lengo la kukuza ushirikiano miongoni mwa nchi wanachama katika masuala
ya hesabu za serikali na kutoa fursa ya kuwa na jukwaa kwa ajili ya
washiriki ili kufanya tathmini kwa kujadiliana na kushirikishana uzoefu
mbali mbali.
Aidha,
mkutano huo unalenga kuhamasisha maendeleo ya watendaji wahasibu wa
Serikali na kutoa mafunzo stahiki kupitia utekelezaji wa program
shirikishi kwa kujifunza uzoefu wa masuala mbali mbali ndani ya nchi
wanachama.
Mkutano
wa wahasibu hao unatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 1000 wakiwemo
Wahasibu wakuu 14 kutoka nchi wanachama na wadau wengine.
Ujio
wa wageni hao pamoja na ushiriki wao katika mkutano wa siku tano utakuwa
wa tija na fursa muhimu katika utoaji wa huduma za jamii wakati wote
watakapokuwa nchini.
Aidha,
katika mahitaji yao ya malazi, chakula, usafiri na mahitaji mengine ya
msingi, makadirio ni kwamba kila mgeni anaweza kutumia zaidi ya shilingi
milioni moja, hivyo basi kwa hesabu za haraka haraka kutakuwa na
matumizi ya shilingi za kitanzania zaidi ya bilioni tano katika muda wa
siku tano tu.
“Wito
wangu kwa watanzania, nawaomba wajitokeze kushiriki katika mkutano huu
wa ESAAG wa 2015, hivyo natoa rai kwa wataalam, wahasibu na wadau wetu
wote kwa ujumla wao ili tuweze kushirikiana kuufanikisha mkutano huu wa
kimataifa unaofanyika nyumbani, Tanzania” alisema Mwanaidi.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mkutano huo ambaye pia
ni Makamu Mhasibu Mkuu wa Serikali Azizi Kifile amesema kuwa nchi
washiriki zinazounda umoja huo ni Botswana, Kenya, Lesotho, Malawi,
Mauritius, Msumbiji, Namibia, Rwanda, Afrika Kusini, Swaziland, Uganda,
Zambia, Zimbabwe na mwenyeji Tanzania.
Azizi
aliwahakikishia washiriki wote kuwa maandalizi ya mkutano huo katika
masuala ya usafiri, usalama na malazi yapo katika hatua nzuri na kamati
yake imejipanga vema ili mkutano huo uwe wa mfano wa kuigwa kwa nchi
zote wanachama watakapopata fursa ya kuandaa mkutano wa mwaka katika
nchi zao.
ni wa serikali wa nchi za mashariki na kusini mwa Afrika,Kwa bahati nzuri chama hiki kikiwa na malengo yafuatayo
ESAAG
ni chama cha wahasibu wakuu ambacho kilizaliwa miaka 20 iliypoita Arusha
hapa nchini mwaka 1995 na mkutano wa mwaka huu wa 22 wa ESAAG
unaongozwa na kauli mbiu “Uimarishaji na usimamizi wa fedha kwa ajili ya
Maendeleo ya kijamii na Kiuchumi katika kanda’’.
RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA IRAN
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete akimlaki na kisha kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
IKULU Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake baada ya kufanya mazungumzo
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
Kikwete akimlaki na kisha kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
IKULU Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake baada ya kufanya mazungumzo
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake baada ya kufanya mazungumzo
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
IKULU
Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje
wa Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif na ujumbe wake baada ya kufanya mazungumzo
Ikulu jijini Dar es salaam jana, Jumatano, Februari 4, 2015. PICHA NA
IKULU
………………………………………………………………………………………………..
Tanzania imesema kuwa dhamira yake
ya kufungua balozi katika baadhi ya nchi duniani iko pale pale na
itatekeleza mpango wake huo kwa kadri hali ya fedha na uchumi
inavyoruhusu.
Aidha, Tanzania imesema kuwa itaendelea kushirikiana na Iran
katika kupambana na kukabiliana na ugaidi duniani kwa sababu nchi mbili
hizo, kama ilivyo dunia nzima, zinahitaji dunia tulivu na inayosaka
maendeleo ya watu bila usumbufu na matishio ya ugaidi.
Mambo hayo mawili yamejadiliwa leo, Jumatano, Februari 4, 2015
katika mazungumzo kati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya
Kiislam ya Iran, Mheshimiwa Javad Zarif.
Mheshimiwa Zarif amewasili nchini leo akitokea Burundi katika
ziara ambayo pia imemfikisha Kenya, Uganda na Rwanda akifuatana na
maofisa wa Serikali na kundi kubwa la wafanyabiashara wa Iran.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais
Kikwete amemwambia Mheshimiwa Zarif kuwa Tanzania bado inakusudia
kufungua ubalozi mjini Teheran, mji mkuu wa Iran, kama ilivyoahidi na
kuwa itafanya hivyo hali ya kifedha na kiuchumi itakaporuhusu. Rais
ametoa maelezo hayo kufuatia ombi la Waziri Zarif kukumbushia umuhimu wa
kuwepo kwa ubalozi wa Tanzania katika Iran.
“Tunakusudia kufungua balozi katika nchi marafiki ambako kwa
sasa hakuna balozi ikiwamo Jamhuri ya Kiislam ya Iran. Katika Afrika,
kwa mfano, tunapanga kufungua balozi katika Namibia, Angola, Algeria na
Ghana. Hizi ni nchi rafiki ambazo baadhi yake zimekuwa na balozi katika
Tanzania tokea uhuru wetu. Mbali na Iran katika Asia, tunaangalia nchi
kama Uturuki, Qatar na Kuwait na nyingine marafiki,” Rais Kikwete
amemwambia Mheshimiwa Zarif.
Kuhusu mapambano dhidi ya magaidi, Rais Kikwete amesema kuwa ni
muhimu kwa Tanzania na Iran kuwa na msimamo ulio sawa wa jinsi ya
kukabiliana na ugaidi.
“Wakati wote, sote tunakabiliwa na matishio ya ugaidi na hivyo
tunalazimika wakati wote kuwa macho na uwezekano wa mashambulizi ya
kigaidi. Sisi Tanzania bado tunakumbuka shambulio dhidi ya Ubalozi wa
Marekani hapa nchini. Ulishambuliwa Ubalozi wa Marekani lakini watu wote
waliopoteza maisha yao ni Watanzania.”
Rais Kikwete na Mheshimiwa Zarif pia wamejadili jinsi gani
Tanzania na Iran zinavyoweza kuongeza ushirikiano wa kibiashara na
uwekezaji katika maeneo mbali mbali ya uchumi na Rais Kikwete amemweleza
Waziri fursa zilizoko katika sekta za nishati na reli.
Waziri Zarif pia amemkumbusha Rais Kikwete mwaliko wa kumwomba Rais Kikwete kutembelea Iran kwa ziara ya Kiserikali.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
4 Februari, 2015
Subscribe to:
Posts (Atom)