Waziri wa Fedha na Mipango akutana na viongozi waandamizi wa IMF na balozi wa Hungary

May 17, 2017
Na Benny Mwaipaja, WFM
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang ameahidi kufungua madirisha ya mikopo kwa nchi ya Tanzania kutokana na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali za kukuza uchumi.
Bw. Zhang aliyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), katika ofisi za Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.
“Shirika la Fedha la Kimataifa limeziona jitihada za kukuza uchumi wa nchi ambapo mpaka sasa Tanzania inaongoza katika nchi za Afrika Mashariki na ipo juu ya wastani wa ukuaji wa uchumi Barani Afrika” Alisema Bw. Zhang.

Ameishauri Serikali kuendelea kushirikiana na Sekta binafsi  katika ukuaji wa Uchumi ili uchumi huo uwe endelevu. Aidha ameitaka Serikali kuwa na mfumo shirikishi wa kifedha utakao wanufaisha wananchi wengi.
Naye Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), amesema kuwa juhudi za Tanzania  kwa sasa ni  kuchochea ukuaji wa Kilimo na kuongeza uzalishaji wenye tija
“Umasikini haujatatuliwa kwa kiwango ambacho Serikali ingependa kukiona, kwa kuwa mpaka sasa watu walio katika  umasikini na ukosefu wa huduma za lazima ni takribani asilimia 34.4 “, aliongeza Dkt. Mpango
Kama nchi imeamua kwenda kwenye uchumi wa kati na jambo ambalo linatiliwa mkazo ni upatikanaji wa umeme wa kutosha na wenye bei nafuu.
Amesema kuwa Serikali imefanya juhudi za kupeleka umeme mpaka vijijini lakini bado kazi hiyo haijakamilika. Pia suala la miundombinu ya ya usafirishaji ni changamoto, ukiwemo usafiri wa reli kutoka Mashariki hadi Magharibi mwa nchi ambao ni wazamani na umeharibika.
“Serikali imeamua kujenga Reli yenye kiwango cha Kimataifa (Standard gauge)  ambayo ni ya gharama, na kwa makadirio ya awali zinahitajika Dola Bilioni 7.6, lakini umechukuliwa uamuzi huo ili kuharakisha Maendeleo”aliongeza Dkt. Mpango 

“Tayari tumeanza ujenzi wa reli hiyo kwa fedha za ndani kwa takribani Kilometa 200 kutoka Dar es salaam mpaka Morogoro na tutaendelea na ujenzi kadri fedha zinavyo patikana” alifafanua Waziri Mpango.
Amesema kuwa, kumekuwa na tatizo la ahadi za Wahisani kutotekelezwa kwa wakati jambo linalofanya baadhi ya shughuli za maendeleo kutotekelezwa kwa wakati.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba, alisema ni  vema Serikali ikaendelea kuangalia vipaumbele  katika ujenzi wa miundombinu ili iweze kuchochea uchumi.
“Suala la ajira hasa kwa vijana linatakiwa kufanyiwa kazi na pia kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na ufanyaji biashara kwa Sekta Binafsi kwa kuwa Sekta Binafsi imekuwa na mchango mkubwa katika Maendeleo kwa nchi nyingi Duniani” Alishauri Bw. Mkwezalamba.
Ameishauri Tanzania kuendelea kuwekeza kikamilifu katika Sekta ya Elimu kwa kuwa ni moja ya eneo ambalo kama likifanyiwa kazi kikamilifu litaleta Matokeo chanya na ya haraka katika ukuaji wa Uchumi.
Akitoa ufafanuzi wa hoja hizo, Waziri Mpango, amesema Serikali imeendelea kuhakikisha kunakuwa na viwanda vingi ili vijana wengi waweze kupata ajira. Aidha tayari Tanzania imeanza kutekeleza Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne ili kutoa fursa kwa watu wengi zaidi kupata elimu.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa pili kulia) akieleza kuwa Tanzania inakua kwa kasi kiuchumi jambo ambalo linawavutia viongozi wengi kufuatilia kwa karibu maendeleo yake, alipokutana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto), katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam.  
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiongoza Mkutano kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (mbele kulia) ambapo alisema mahitaji makubwa wa nchi ni maendeleo ya kilimo na upatikanaji wa nishati ya umeme ili viweze kuchochea uchumi wa viwanda. Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.  
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba ( kulia)  wakipeana mkono baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao uliohusu suala la Uchumi katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (watatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa tatu kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Maafisa waandamizi wa Wizara hiyo baada ya kumalizika kwa mkutano kuhusu hali ya uchumi katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU TATU YA POLISI WANAWAKE KUTOKA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA JIJINI DAR ES SALAAM

May 17, 2017
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
Dar es Salaam.
Muonekaniko wa picha kutoka juu ukionyesha Wajumbe wakati wakimsikiliza  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuluhu Hassan kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi Mkazi wa UN nchini, Alvaro Rodriguez akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO) ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
 Mwaziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuluhu Hassan akizungumza na Askari wa Kike wa Kikosi cha Kuzuia Fujo (FFU) mara baada ya kufungua Mafunzo ya siku tatu ya Polisi Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
Dar es Salaam.

                        ………………………………………………………………………………….
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka askari polisi wanawake kutoka kwenye Shirikisho la Majeshi la Polisi Kusini mwa Afrika (SARPCCO) washiriki kikamilifu katika oparesheni mbalimbali ambazo zinafanyika kwenye ukanda huo kamahatua ya kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

Makamu waRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya siku Tatu ya Polisi wanawake kutoka nchi wanachama wa SARPCCO katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
 
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahimiza askari polisi wanawake kufanya kazi kwa bidii na kujituma hatua ambayo itasaidia kupanda vyeo kama  askari wanaume katika maeneo yao ya kazi.

Amesisitiza kuwa muda wa kulalamika kuwa hawapandishwi vyeo umeshapitwa na wakati bali kwa sasa wachape kazi na waonyeshe kuwa wanaweza majukumu yao wanayopangiwa ili waweze kupanda vyeo.
 
 “Vyeo haviji tu ni lazima polisi wanawake muonyeshe kuwa mnaweza ili muweze kupandishwa vyeo na kupata nafasi za uongozi katika Majeshi yenu

Kuhusu utendaji kazi wa Polisi wanawake, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka polisi hao kutumia mkutano huo wa siku Tatu kujadili kwa kina namna ya kuondoa changamoto hizo zinazorudisha nyuma utendaji wao wa kazi.
 
Amesema kama polisi wanawake wataacha majungu na kujenga umoja na mshikamano miongoni mwao watafikia malengo yao haraka hasa katika kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya vitendo vya uhalifu ikiwemo biashara ya dawa za kulevya.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amesema anaimani kubwa kuwa mafunzo hayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa polisi hao wanawake kuimarika
ipasavyo katika utendaji wao wa kazi.
  
Masauni pia amewahimiza polisi wanawake wanaopata mafunzo hayo kwenda kuwaelimisha na wenzao mipango na mikakati waliyoweka katika kulinda raia na mali zao katika nchi zao.

MATUKIO KATIKA PICHA: YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA 27, MKUTANO WA SABA BUNGE LA 11 MJINI DODOMA LEO MAY 17, 2017

May 17, 2017


 Naibu Spika  wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk.Tulia Ackson  akiongoza    kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dk.Ashatu Kijaji akifafanua jambo katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri  wa Nishati na Madini Mhe.Prof  Sospeter Muhongo akizungumza jambo na Naibu Waziri wake Mhe.Dk. Medard kalemani  katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mhe.Zaynab Vullu akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akizungumza jambo na Mbunge wa Mtama Mhe.Nape Nnauye  katika kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Naibu Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Mbunge wa Kuteuliwa Mhe.Abdallah Bulembo  akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe.George Simbachawene akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora Mhe.Angellah Kairuki akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora Mhe.Angellah Kairuki leo katika viwanja vya Bunge  Mjini Dodoma.
 Waziri wa Mambo  ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akimskiliza  Mbunge wa Mwibara Mhe.Kangi Lugora katika viwanja vya Bunge leo Mjini Dodoma.Wengine Pichani ni Mbunge wa Mtama Mhe.Nnape Nnauye
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe.Isack Kamwelwe akifafanua jambo katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe.Mwigulu Nchemba  akizungumza jambo na Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe.Dk Hussein Mwinyi,Waziri wa Ardhi,Nyumba  na Maendeleo ya Makazi Mhe.William Lukuvi na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Prof Jumanne Magembe katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Mbunge wa Viti Maalum(CCM) Mhe.Mary Mwanjelwa akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017
 Mbunge wa Sikonge(CCM) Mhe.Joseph Kakunda akiuliza swali katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage akisoma Hotuba ya Mapato na Matumizi ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 leo katika  kikao cha Ishirini na Saba cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Mei 16, 2017.

Picha Zote na Daudi Manongi- Dodoma MAELEZO, DODOMA

Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo

May 17, 2017


Na Nuru Juma-MAELEZO

Serikali inamkakati wa kuhakikisha inajenga Magereza katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa kilimo ambayo pia yana ukubwa wa kutosha ili kazi ya kuwarekebisha wafungwa iwe rahisi kufanyika huku shughuli za uzalishaji zikiwa zinaendelea.

Hayo yamesemwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Mwigulu Nchemba alipokuwa akijibu swali la Mhe Devotha Minja Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro. 

“Magereza hayo yatajengwa katika maeneo yenye Kilimo na yatakuwa ni kwa ajili ya watu waliokwisha hukumiwa huku yale Magereza ya mijini yawe kwa ajili ya mahabusu tu ili wawe karibu na Mahakama,”alisema Mwigulu. 

Aliongeza kuwa mkakati huo wa Serikali ni wa muda mrefu na wanahitaji kufanya hivyo ili kurahisisha shughuli za maendeleo zinazofanywa na wafungwa na pia kupunguza msongamano wa wafungwa katika Magereza.

Hili pia linatokana na tamko la Mh.Rais Dkt John Pombe Magufuli alilowahi kulitoa hivi karibuni kuwa wafungwa wako katika kutumikia adhabu hivyo wanatakiwa kufanya kazi hasa za kilimo ili kwanza kujipatia chakula na sio kukaa tu bure na kusubiri kila kitu wafanyiwe na serikali.

Aliongeza kuwa Serikali ina mkakati wa kutumia bajeti inayotengwa na nguvu kazi wanayoipata kutoka kwa wataaalam walionao kwa upande wa askari Magereza na wafungwa ili kukarabati Magereza chakavu na kujenga nyumba za askari.

Aidha alibainisha kuwa suala la kukatwa kwa umeme katika Magereza, nyumba za askari,pamoja na maeneo na maeneo mengine ya kambi za Jeshi la Polisi na Magereza limeshafanyiwa kazi na serikali kwa kupitia hazina imekwishatoa fedha kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.

Mheshimiwa Waziri aliliambia Bunge kuwa sheria zimeainisha baadhi ya haki za mfungwa zikiwemo huduma za afya kwa wakati,kupewa chakula, uhuru wa kutembelewa na ndugu zake na kupata mawasiliano kwa kusoma magazeti,kusikiliza taarifa za habari na kuandikiwa barua na ndugu zao,haki ya kukata rufaa ikiwa hakuridhika na hukumu yake, malazi safi na yakutosha pamoja na kushiriki michezo mabalimbali.

WADAU WAIPONGEZA SERIKALI KWA UAMUZI WA KUIVUNJA MAMLAKA YA USTAWISHAJI WA MAKAO MAKUU, DODOMA (CDA)

May 17, 2017

Na: Frank Shija – MAELEZO

WADAU mbalimbali wameipongeza Serikali kwa uamuzi wa kuivunja Mamlaka ya Ustawishaji wa Makao Makuu Dodoma (CDA) iliyofikiwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Wakitoa maoni yao juu ya umauzi huo wa Serikali, wameeleza kuwa kuvunjwa kwa Mamlaka hiyo kumekuja wakati muafaka kwani kutapunguza kero na migogoro ya ardhi iliyokuwa ikiendelea katika Manispaa ya Dodoma.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maalum iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana,iliyokuwa inashughulikia changamoto za wananchi dhidi ya CDA, Bw. Aron Kinunda alisema kuwa uamuzi huo huko sahihi kwani umekuja wakati muafaka kwa kuzingatia malengo halisi ya uanzishaji wa mamlaka hiyo kuwa yamekamilika kwa asilimia kubwa ukizingatia na mahitaji halisi ya wakati huu.

“Ni hatua nzuri katika mustakabari wa maendeleo ya Dodoma, kwani sasa migogoro mingi ya ardhi iliyokuwa inatokana na mgongano wa kisheria haitarajiw kujitokeza tena na badala yake Manispaa itajikita katika kuweka mazingira rafiki ya umiliki wa ardhi ikiwemo kuongeza muda wa hati ya umiliki kutoka miaka 33 hadi 99 kama ambavyo maeneo mengine ya nchi yanavyofanya.” Alisema Kinunda.

Aliongeza kuwa wananchi watakuwa wamefarijika sana kwani walikuwa wanaiona CDA kama adui yao mkubwa ambapo imesababisha malalamiko mengi ya kuchukuliwa ardhi zao bila ya kulipwa fidia na urasimu katika upimaji na utoaji wa hati za viwanja.

Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi kuwa CDA hakuna usimamizi mzuri wa ardhi jambo linalosababisha kuwepo kwa migogoro mingi ya ardhi itokanayo na mgongano wa kisheria uliopo kati ya Mamlaka hiyo na Manispaa ya Dodoma.

“Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya mwaka 1999 inatambua umiliki wa ardhi upo chini ya Serikali za Mitaa, kitu ambacho kwa Dodoma ni tofauti kwa kuwa ardhi yote iliyopimwa iko chini ya CDA kitu ambacho hata Manispaa imekuwa mpangaji,” aliongeza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Dodoma, Mzee Chidawali amesema kuwa uamuzi wa uamuzi huo umepokelea kwa nderemo na vifijo na ambapo asilimia kubwa ya wakazi wa Dodoma wanaona ni kama ukombozi kwao.

“ Rais Magufuli anapaswa kupongezwa sana kwa uamuzi aliouchukua wa kuivunja CDA hakika amefanya jambo jema sana, sasa wananchi watapata ahueni katika kushughulikia masuala yao ya umiliki wa ardhi,” alisema Chidawali.

Aidha aliongeza kuwa katika upande wa taaluma ya uandishi wa habari uamuzi huo umewasaidia kurejesha uhusiano mwema baina yao na wananchi kwani wamekuwa wakiacha kuripoti habari za maendeleo badala yake wamekuwa wakijikuta wanaandika habari kuhusu migogoro ya ardhi zaidi iliyokuwa inasababishwa na CDA.

Chidawali alisema kuwa baada ya kupata taarifa juu ya uamuzi huo amepata fursa ya kusikia maoni ya wadau mbalimbali ambapo kwa nyakati tofauti wamempongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchukua hatua jambo linalotoa tafsiri chanya juu ya dhamira njema ya Serikali yake ya kuwajali wanyonge.

“Binafsi nje ya taaluma ya habari mimi ni mzawa wa Dodoma tumekuwa na malalamiko ya muda mrefu hasa kuhusu uhalali wa kumiliki ardhi, tunaitwa wavamizi katika maeneo ambayo tumekuwa tukiyamiliki enzi na enzi,” alifafanua Chidawali.

Naye Mwenyekiti wa Soko la Chadulu Jakton K. Matoto amesema kuwa Jumuiya yao imepokea kwa mikono miwili uamuzi huo na kuongeza kuwa ni imani yao kuwa baada ya Manispaaa kuchukua majukumu ya CDA itakwenda kufanya mapitio na kutatua migogoro yote iliyokuwa ikiendelea kutokana na uwepo wa mamlaka hiyo.

Mwenyekiti huyo ameonyesha matumaini ya mji wa Dodoma kukua kutokana na kile anachodai kuwa CDA ndiyo cahnzo cha Dodoma kubaki nyuma kimaendeleo kwani wawekezaji wengi wamekuwa wakishindwa kuwekeza kutokana na muda mfupi wa hati ya umiliki wa ardhi ambapo mmiliki anapewa miaka 33 wakati maeneo mengine ya nchi muda ni miaka 99.

Wakati huohuo Matoto ametoa rai kwa Manispaa ya Dodoma kujipanga ili kuendana na hali ya mahitaji ya sasa ikiwa ni mapoja na upimaji wa viwanja kwa kuzingatia misingi ya haki na usawa.

Mamlaka ya Ustawishaji wa Makao Makuu Dodoma ilianzishwa mwaka 1973 kwa malengo ya kutengeneza master plan na kufanikisha azma ya Serikali kuhamia Dodoma ambapo zaidi ya ekari 260,000 za ardhi zimepimwa na na kupatiwa hati zinazomilikiwa na CDA, kufuatia kuvunjwa kwake na maelekezo ya Rais kuwa rasirimali zote ziwe chini ya Manispaa ya Dodoma ambayo itaendeleza shughuli zilizokuwa zikifanya na mamlaka hiyo kwa mujibu mtaratibu na sheria za nchi.

SERIKALI: AWAMU YA 3 YA REA KUVIFIKIA VIJIJI, VITONGOJI NA MAENEO YA PEMBEZONI MWA NCHI.

May 17, 2017


Na Nuru Juma ,MAELEZO, DAR ES SALAAM

SERIKALI kupitia mradi wa awamu ya 3 ya usambazaji wa umeme vijijini (REA) imekusudia kusambaza umeme katika vijiji, vitongoji vyote, taasisi za umma na maeneo ya pembezoni mwa nchi ikiwemo visiwa.

Hayo yamesemwa leo bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani alipokua akijibu swali la Mbunge wa Bukoba Mjini (CHADEMA) Wilfred Rwakatale.

Dkt. Kalemani amesema kupitia mradi wa REA, Serikali inatarajia kukamilisha usambazaji umeme vijijini mwaka 2020 hadi 2021, na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) inaendelea kusambaza umeme maeneo yote ya mjini ambayo hayajapata nishati ya umeme.

“Baadhi ya vijiji ambavyo vipo ndani ya mamlaka za miji vinapelekewa umeme na shirika la Tanesco na bei ya Tanesco na REA ni tofauti kwani kwa mteja wa awali wa Tanesco hulipia 177,000 na REA hulipia 27,000””, alisema Mhe.kalemani.

Kwa mujibu wa Kalemani amesema Serikali bado inaendelea kujiridhisha na kuangalia ni vijiji gani vinastahili kupelekewa umeme kwa mradi wa REA ili kuhakikisha kuwa malengo ya mradi yanaweza kufikiwa katika muda uliopngwa.

Dkt. Kalemani ameongeza kuwa wakati wa uzinduzi mradi huo ulianza na mikoa 10 na walibakisha mikoa 15 kwa Tanzania bara na hadi sasa wamemaliza utaratibu wa kuwapata wakandarasi watakaojenga miundombinu ya mradi huo katika mikoa yote nchini.

Aidha Dkt. Kalemani amesema wakati wowote kuanzia sasa Serikali inatarajia kuwapangia vituo vya kazi na wakandarasi hao.

Aliwataka makandarasi hao kufanya kazi kwa bidii katika mikoa yao ili kuhakikisha wanamaliza kazi zao kwa wakati na umeme unapatikana katika vijiji vyote bila kubagua nyumba.

Katika swali lake la msingi, Mbunge huyo alitaka kufahamu mikakati ya Serikali ya kusambaza umeme katika baadhi ya vijiji vilivyopo katika baadhi Wilaya za Mkoa wa Kagera.

Utekelezaji wa mradi wa Rea wa wamu ya 3 umeanza tangu Machi 2017 na unatarajia kukamilika mwaka 2021.

Tigo yazindua kampeni ya ‘Jaza Ujazwe’ kuwashukuru wateja kwa uaminifu wao

May 17, 2017

 Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga akifafanua jambo  kwa waandishi wa habari  kuhusu kifurushi cha Jaza Ujazwe mapema leo  katika uzinduzi rasmi wa kifurushi hicho "JazaUjazwe’ ambapo mteja  atapata bonus kwa njia ya SMS, Muda wa maongezi, MBs kwa ajili ya kuperuzi internet, Whatsapp na You Tube Kulia kwake ni Mtaalamu wa kubuni Ofa kutoka kampuni ya simu za mkononi ya TIGO Jacqueline Nnunduma na kushoto ni   Meneja Mawasiliano ya Umma wa Tigo Woinde Shisael .
Mtaalamu wa kubuni Ofa kutoka kampuni ya simu za mkononi ya TIGO Jacqueline Nnunduma  akijibu maswali kwa waandishi wakati wa uzinduzi wa kifurushi cha Jaza Ujazwe (katikati)  Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga  na mwishoni ni  Meneja Mawasiliano ya Umma wa Tigo Woinde Shisael .

 Dar es Salaam, Jumatano  Mei 17, 2017- Kampuni inayoongoza mfumo wa maisha ya kidijitali, Tigo Tanzania  imezindua kampeni nyingine mpya ya kuvutia inayofahamika kama, ‘JazaUjazwe’ ambapo mteja  atapata bonus kwa njia ya SMS, Muda wa maongezi, MBs kwa ajili ya kuperuzi internet, Whatsapp na You Tube pindi anapoongeza muda wa maongezi iwe ni kupitia vocha ya kukwangua, Tigo Pesa au Tigo Rusha.
Kwa mujibu wa Tigo kampeni ya ‘Jaza Ujazwe’ imekuja kama  shukrani kwa wateja wa kampuni hiyo ya simu kutokana na uaminifu wao mkubwa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo,  Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga alisema, “Tigo inathamini kuungwa mkono kulikotukuka kunakoonyeshwa na wateja wake kwa kipindi cha miaka mingi, na ndio maana tunaamini wanastahili kupewa shukrani kwa kuendelea kutuamini. Kama kampuni, tunayofuraha  kwa mara nyingine tena  kuwapatia wateja wetu bonus ili waweze kuendelea kufurahia huduma zetu za kiwango cha juu duniani.”
Mpinga alibainisha kuwa  kampeni hiyo mpya inadhihirisha nafasi ya kampuni katika kutoa huduma na bidhaa bora zinazokidhi mahitaji ya wateja  wake na wakati huo huo  kuimarisha mchango wake katika soko kama kampuni ya simu za mkononi iliyo na ubunifu wa hali ya juu.
Alisisitiza  kujikita kwa Tigo katika kuendelea  kuwapatia wateja wake bidhaa na huduma bora zaidi na kuongeza, “Bidhaa na huduma zetu zimeundwa baada ya kufanya tafiti  zinazolenga kuhakikisha wateja wetu wanaridhishwa na wanapata thamani kwa kila shilingi wanayotumia kwa mawasiliano. Hivyo ‘Jaza Ujazwe’ ni kuitikia hitaji la mteja na pia kuwapa wateja uzoefu  wa kusisimua kila wakati wanapotumia bidhaa zetu. Tunaamini kwamba wateja wetu watafurahia dakika za ziada, ujumbe mfupi wa maneno (SMS) au data za bonus na hatimaye kuboresha mwenendo wao wa mawasialiano. 
Wateja wote wa Tigo wanastahili kupata bonus hizi kwa kuwa hakuna masharti yoyote.