MAJANGA.....BASI LAGONGANA NA TRENI MANYONI!!!!
UONGOZI WA SIMBA WAWEKA WAZI SUALA LA KUMUONGEZEA MKATABA KOCHA WAO
Uongozi
wa Klabu ya Simba umeweka wazi kuwa suala la kumuongezea mkataba kocha
wake mkuu wa sasa, Zdravko Logarusic limewekwa pembeni kwa kuwa
wanasubiri kuona mwelekeo wa timu yao ambayo imekuwa haina matokeo
mazuri hivi karibuni.
Loga raia wa Croatia alisaini mkataba wa miezi
sita wakati alipotua klabuni hapo mwishoni mwa mwaka jana, ambapo
mkataba huo unatarajiwa kufikia tamati Juni mosi, mwaka huu.
Katibu
Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga, aliweka wazi kuwa matokeo ya timu
katika mechi zilizosalia ndiyo yatapa picha uongozi juu ya kuongeza au
kutoongeza mkataba huo.
DR.MAGUFULI AKAGUA MRADI WA MABASI YAENDAYO KASI (BRT) JIJINI DAR ES SALAAM
Waziri
wa Ujenzi Dr.John Pombe Magufuli Kituo cha
BRT kivukoni jijini Dar es salaam leo akiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam
Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
(aliyekaa kulia) akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Eng. Mussa Iyombe
(katikati) pamoja na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Patrick Mfugale
(aliyesimama) wakisafiri kwa basi kukagua utekelezaji wa ujenzi wa barabara za
mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam.
Wanafunzi wa Tanzania Thailand Waizungumzia sekta ya Madini.
Kamishna
Msaidizi wa Madini Mhandisi Hamis Komba katikati akiwa pamoja na
Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha
‘Asian Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand. Wa
kwanza kulia ni Agatha Mwinuka, anayefuata ni Emmanuel Minja na wa
kwanza kushoto ni Doricas Moshi. Wanafunzi
wa Kitanzania nchini Thailand, wakiwa katika picha ya pamoja na
wanafunzi wenzao kutoka mataifa mbalimbali , ambao wamelitembelea banda
la Tanzania. Wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini katika picha ya pamoja na wanafunzi hao katika banda la Tanzania.
……………………………………………………………………………………
Na Asteria Muhozya, Bangkok
Wanafunzi
wa Kitanzania wanaosoma masomo ya Geomolojia katika Chuo cha ‘Asian
Institute of Geological Science’ (AIGS) nchini Thailand, wamewataka
wadau wa tasnia ya madini ya vito na usonara nchini Tanzania kuichukua
sekta hiyo kwa umakini mkubwa kutokana na mchango wake kiuchumi.
Aidha,
wameeleza kuwa, nchi ya Thailand imepiga hatua kubwa katika sekta ya
madini ukilinganisha na Tanzania lakini bado Tanzania inaweza kufaidika
zaidi katika sekta hiyo ikiwa kila mdau atatimiza wajibu wake kikamilifu
ili madini ya vito yaongeze mchango katika pato la taifa.
MWIGULU NCHEMBA AZINDUA KAMPENI ZA CCM JIMBO LA KALENGA
Naib
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Mwigulu Nchemba akiwahutubia
wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Ifunda mkoani
Iringa, ambapo CCM ilizindua rasmi kampeni katika
jimbo la Kalenga wakimnadi mgombea wao kwa tiketi ya chama hicho Bw.
Godfrey Mgimwa na kuwaasa wanakalenga kumchagua Godfrey Mgimwa kwani ni
mwakilishi wao kamili kutokana na kwamba ilani inayotekelezwa mpaka
mwaka 2015 ni ya Cmaha cha Mapinduzi hivyo Mgimwa ataisimamia vyema na
kukimalizia kipindi cha miezi ishirini iliyobaki kwa maendeleo ya
wanakalenga. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-IFUNDA)Naibu
Katibu Mkuu wa CCM, Bara Mwigulu Nchemaba akimnadi mgombea ubunge kwa
tiketi ya CCM katika uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga Gedfrey Mgimwa,
katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika leo, kwenye
Uwanja wa Chuo Cha Ifunda, Iringa Vijijini. (Picha na Bashir Nkoromo)
*RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN AKUTANA NA UJUMBE WA MEYA WA JIMBO LA CALIFONIA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana
na Meya wa Jimbo la Califonia nchini Marekani Mstahiki Osby
Davis,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar akiwa na ujumbe aliofuatana nao leo asubuhi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akibadilishana
mawazo na Meya wa Jimbo la Califonia nchini Marekani Mstahiki Osby
Davis,leo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo akiwa na ujumbe aliofuatana
nao .Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
*MALINZI AUNDA KAMATI YA MIAKA 50 FIFA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
ameunda kamati ya watu tisa kuratibu maadhimisho ya miaka 50 tangu TFF
ilipojiunga na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).
TFF ilipata uanachama wa
shirikisho hilo la kimataifa Oktoba 8, 1964 ambapo itaadhimisha miaka hiyo 50
kwa kufanya shughuli mbalimbali za mpira wa miguu.
Subscribe to:
Posts (Atom)