VIWANDA MOROGORO VYAPONGEZWA KWA KUNUSURU UHARIBIFU WA MAZINGIRA

September 29, 2017
Katikati Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Mhe. Luhaga Mpina, Mbele yake ni Bw. George Mratibu wa Kiwanda cha Ngozi Morogoro , cha ACE LATHER TANZANIA LTD, wakiwa katika ukaguzi wa mtambo wa kisasa wa kutibu majitaka kiwandani hapo ambapo Mpina yupo Mkoani Morogoro katika ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Sheria ya Mazingira na kanuni zake, kufuatia maagizo aliyoatoa awali katika ziara ya viwanda hivyo.
 
Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji  Safi na Taka Mjini Morogoro,Injinia Halima Mbiru akimuonyesha Naibu Waziri Mpina mpaka wa mabwawa ya maji taka mali ya mamlaka hiyo hayapo pichani Mh Mpina ambaye alifanya ukaguzi wa mabwawa hayo

Naibu Waziri Mpina akikagua mabwawa hayo kama inayoonekana
Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Luhaga Mpina kulia ni Mwenyeji wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Dkt Kebwe Stephen Kebwe katika kikao kabla ya kuanza ukaguzi viwandani mkoani humo leo (Picha na Evelyn Mkokoi)
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina Amekipongeza kiwanda cha nguo cha 21st century na kiwanda cha ngozi cha ACE LEATHER TANZANIA LTD kwa kutekeleza sheria ya mazingira kwa kujenga mtambo wa kisasa wa kutibu majitaka yanayotoka katika viwanda hivyo.

Akiwa katika Ziara ya ukaguzi na utekelezaji wa Sheria ya mazingira Mkoani Morogoro leo, Mpina aliwataka wamiliki wa viwanda hivyo kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC pamoja na Bonde la Wami Ruvu, kuchukua Sampuli za maji hayo  yanayotibiwa katika viwanda hivyo kwa ajili ya vipimo ili kujiridhisha kuwa hayana madhara kwa mazingira na viumbe hai wengine.

Katika ziara hiyo Mpina, Aliagiza NEMC kumuandikia Barua msajili wa hazina ili kujua ukweli wa mmiliki halali wa mabwawa ya majitaka yaliyotelekezwa katika maeneo ya kilimahewa, ili mmiliki halali wa mabwawa hayo kama ni mamlaka ya majitaka iweze kuyahudumia kwa kuyajengea miundombinu ya kisasa  na kuyatibu ili kunususu mazingira, awali ilielezwa na baadhi ya wakazi wa eneo hilo kuwa wakati wa msimu wa mvua maji hayo yamekuwa ni kero kwa wakazi hao kwa kutoa harufu kali.

Naibu Waziri Mpina anaendela na ziara yake ya ukaguzi wa mazingira na utekelezaaji wa shieria ya mazingira mkoani Morogoro.

TANGA CEMENT YATOA MIFUKO YA SARUJI 660 KWA AJILI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAJENGO KOROGWE NA MAABARA KATA YA MLALO LUSHOTO MKOANI TANGA

September 29, 2017
 Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga kushoto akimkabidhi mifuko 500 ya Saruji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Mji,Jumanne Shauri kulia kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Majengo wilayani Korogwe ikiwa ni kuunga mkono kusaidia sekta ya afya nchini kulia ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe,Dokta Elizaberth Nyema katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (DAS) Rehema Bwasi

Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga kushoto akimkabidhi mifuko 500 ya Saruji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Mji,Jumanne Shauri kulia kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Majengo wilayani Korogwe ikiwa ni kuunga mkono kusaidia sekta ya afya nchini kushoto ni
Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo


 Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi Mifuko 500 ya Saruji Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (Das) Rehema Bwasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Majengo wilayani humo wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Korogwe Mji,Jumanne Shauri ,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Korogwe,Dkt Elizaberth Nyema wa pili kutoka kushoto ni Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 


  Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi Mifuko 500 ya Saruji Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (Das) Rehema Bwasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Majengo wilayani humo wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Korogwe Mji,Jumanne Shauri ,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Korogwe,Dkt Elizaberth Nyema wa pili kutoka kushoto ni Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga




 Meneja Ubora wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 160 Afisa Mtendaji wa Kata ya Mlalo Catherine Mwakatundu kwa ajili ya Ujenzi wa Maabara katika Kata hiyo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kuinua elimu hapa nchini wanaoshudhia ni  Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 


 Meneja Ubora wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 160 Afisa Mtendaji wa Kata ya Mlalo,Catherine Mwakatundu  kwa ajili ya Ujenzi wa Maabara katika Kata hiyo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kuinua elimu hapa nchini wanaoshudhia ni  Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 


 Muonekano wa Saruji ambayo imekabidhiwa leo na Kiwanda cha Simba Cement kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Korogwe Mji na Ujenzi wa Maabara katika shule mbalimbali za sekondari Jimbo la Mlalo wilayani Lushoto mkoani Tanga katika halfa iliyofanyika kiwandani hapa 






BODI YA WADHAMINI YA SHIRIKA LA HIFADHI ZA TAIFA (TANAPA) YATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KATAVI.

September 29, 2017
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi ,George Waitara akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi ,Izumbe Msindai baada ya kuwasili na wajumbe wa Bodi hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Mtango Mtahiko akizungumza mara baada ya kuwapokea wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA .
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi,Izumbe Msindai akieleza jambo kwa Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA wakati wakitembelea hifadhi hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Wananchi ,George Waitara akitizama Viboko katika Hifadhi hiyo.
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) wakichukua taswira ya viboko katika Hifadhi ya taifa ya Katavi walipotembelea .
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Jenerali Mstaafu ,George Waitara akizungumza na askari waliopo katika mafunzo ya awali ya Uhifadhi katika kambi ya mafunzo ya Mlele iliyopo mkoani Katavi .
Askari waliopo katika mafunzo ya awali ya Uhifadhi katika kambi ya mafunzo ya Mlele iliyopo mkoani Katavi wakimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Jenerali Mstaafu ,George Waitara alipowatembelea.

Na Mwandishi wetu ,Katavi.

Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ikiongozwa na Mwenyekiti wa bodi Jenerali Mstaafu George Waitara imetembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi kwa ajili ya kukagua utendaji kazi ambapo ilipata fursa ya kupokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Hifadhi Izumbe Msindai.

Bodi imepongeza utendaji kazi katika Hifadhi ya Katavi hususani suala zima la kupambana na ujangili na juhudi zinazofanywa katika kuongeza idadi ya watalii hifadhini.

Aidha, Jenerali Waitara aliutaka uongozi wa hifadhi kuongeza jitihada katika kukabiliana na changamoto za mifugo ambayo ni kubwa kwa Katavi na pia alipongeza uongozi wa mkoa chini ya Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali mstaafu Raphael Muhuga kwa ushirikiano mkubwa anaotoa kwa hifadhi katika kupambana na mifugo hifadhini.

Mapema kabla, bodi iliweza kutembelea kituo cha mafunzo cha Mlele na kupokea taarifa kutoka kwa Mkuu wa Kituo Mhifadhi Genes Shayo na kupata nafasi ya kuongea na askari wapya wanaoendelea na mafunzo katika kituo hicho.

Jenerali Waitara aliwataka askari hao kuwa na nidhamu, uwajibikaji, bidii na uzalendo katika mafunzo yao na kuwa ni lazima waonyeshe kuiva ili waweze kupambana vilivyo na changamoto ya ujangili katika Hifadhi za Taifa nchini
.

MAKAMU WA RAIS, MHE. SAMIA SULUHU HASSAN KUZINDUA MAKUMBUSHO MAPYA YA OLDUVAI NA ONESHO LA CHIMBUKO LA MWANADAMU TAREHE 03 OKTOBA, 2017 MKOANI ARUSHA

September 29, 2017
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani Morogoro kuhusu uzinduzi wa Makumbusho Mapya ya Olduvai na Onesho la Chimbuko la Mwanadamu ambayo yatazinduliwa tarehe 03 Oktoba, 2017 na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olduvai wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. 
 Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani Morogoro kuhusu uzinduzi wa Makumbusho Mapya ya Olduvai na Onesho la Chimbuko la Mwanadamu ambayo yatazinduliwa tarehe 03 Oktoba, 2017 na Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika eneo la Olduvai wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. (Picha na Hamza Temba - WMU)

Morogoro, Septemba 28, 2017
.........................................................................
Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kushirikiana na Umoja wa Ulaya imekamilisha ujenzi wa Makumbusho mapya ya Olduvai ambayo yanaonesha Chimbuko la Binadamu (The Cradle of Humankind) katika Bara la Afrika.
Makumbusho hayo mapya pamoja na Onesho la Chimbuko la Binadamu, yatafunguliwa rasmi na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tarehe 03 Oktoba, 2017 katika eneo la Olduvai, ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro.
Onesho hilo ni matokeo ya utafiti wa muda mrefu uliofanyika katika Bonde la Olduvai na Laetoli katika Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. Wananchi, viongozi mbalimbali wa kitaifa na Mabalozi wanatarajiwa kuhudhuria kwenye hafla hiyo.
Idadi kubwa ya vioneshwa katika Makumbusho hiyo, vilipatikana katika bonde la Olduvai na Laetoli nchini Tanzania kupitia utafiti wa kisayansi wa muda mrefu na vilikuwa vimehifadhiwa katika Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es Salaam. Vioneshwa hivi ni pamoja na masalia ya zamadamu, zana za mawe na masalia ya wanyama walioishi takribani miaka milioni 4 iliyopita.
Makumbusho hayo yamepangwa kuonesha sehemu kuu nne zinazowiana.  Sehemu ya kwanza inahusu ushahidi wa nyayo za zamadamu zilizongunduliwa huko Laetoli mwaka 1978 na mtafiti Dr. Mary D. Leakey.  Nyayo hizi ziliachwa na zamadamu anayeiitwa Australopithecus afarensis na ndio ushaidi usiopingika wa zamadamu kutembea wima kwa miguu miwili takribani miaka milioni 3.6 iliyopita.
Sehemu ya pili inahusu hadithi ya kusisimua ya kuwa binadamu (Genus Homo); ambapo kutakuwa na masalia ya zamadamu wanaoitwa Zinjanthropus au Paranthropus boisei na Homo habilis, zana za mawe za mwanzo zilizotumika (Oldowan) katika kujipatia chakula na ushahidi wa kale wa ulaji wa nyama katika historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka million 2 iliyopita.
Sehemu ya tatu inahusu maisha ya jamii ya Homo erectus.  Jamii hii ilikuwa inafanana zaidi na binadamu wa sasa kuliko jamii zilizotangulia. Kutakuwa na masalia zamadamu Homo erectus, zana za mawe (Acheulian) na ushahidi wa ulaji wa wanyama wakubwa kama vile Nyati na tembo katika historia ya mabadiliko ya binadamu, takribani miaka million 1.7 iliyopita.

MADIWANI WA MANISPAA YA SHINYANGA WAPITISHA TAARIFA ZA LAAC NA HESABU ZA MWISHO WA MWAKA 2016/2017

September 29, 2017
Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga,Mheshimiwa Agnes Machiya akifungua kikao maalum cha baraza la madiwani leo Ijumaa Septemba 29,2017.-Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog
******

VIDEO: MWINJILISTI KUTOKA MAREKANI AWASHA MOTO JIJINI MWANZA

September 29, 2017
Mamia ya wananchi wanazidi kujitokeza kwa wingi kwenye mkutano mkubwa wa injili ulioandaliwa na kanisa la kimataifa la EAGT Lumala Mpya kwenye uwanja wa Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza. Mhubiri ni  mwinjilist Rojas Matias kutoka Marekani huku mchungaji mwenyeji akiwa ni Dkt.Daniel Moses Kulola.

PROF. MAGHEMBE AFUNGUA MKUTANO WA KIMATAIFA WA NCHI 21 DUNIANI KWA AJILI YA KUJADILI UKUKUZAJI WA SEKTA YA UPANDAJI WA MITI KIBIASHARA

September 29, 2017
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. Aliwataka wajumbe hao kujadili namna ya kuwawezesha wakulima wa miti wakati wanasubiri kuvuna mazao yao waweze kujishuulisha na kilimo cha mazao ya muda mfupi kwa kutumia mbinu bora za kisayansi ili waweze kujikimu kimapato.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. 
Baadhi ya wajumbe kutoka nchi 21 duniani wakifuatilia mkutano huo. Nchi hizo ni Burkina Faso, Chad, Ethiopia, Gambia,Ghana, Italy, Mali, Niger, Nigeria, Senegal, Sudan, Liberia, Cameroon, Swaziland, Finland, Zambia, Canada,Mozambique, Zimbabwe, Kenya na Tanzania.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Steven Kebwe akizungumza katika mkutano huo. Aliwataka wajumbe wa mkutano huo kujadili na kuishauri dunia namna bora ya kutunza na kuendeleza misitu kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho ikiwemo utekelezaji wa sheria za usimamizi wa misitu.
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akizungumza katika mkutano huo ambapo aliwataka wajumbe kujadili kwa uwazi kuhusu mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto za sekta ya misitu na kwamba Serikali kupitia Wizara itapokea maoni na mapendekezo yao kwa ajili ya kuyafanyia kazi ili kuimarisha ustawi wa sekta hiyo. 
Waziri Maghembe akieleza jambo kwenye ka mkutano huo ambapo aliwataka wajumbe wajumbe wajadili namna bora ya kuwafundisha wakulima wa miti kufanya kilimo bora ikiwa ni pamoja na mafunzo uvunaji wa hewa ukaa ili kuwainua kimapato. Aliwataka pia kusaidia wakulima wa miti katika upatikanaji wa masoko ya uhakika.
  Prof. Maghembe akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza mkoani Morogoro jana na baadhi ya viongozi waliondaa mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika muda mfupi kabla ya kufungua mkutano huo wa siku mbili uliowashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. 
  Baadhi ya wajumbe walishiriki mkutano huo kutoka nchi 21 duniani.
 Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akizungumza na Mbunge kutoka Kenya, Chariti Katambi mkoani Morogoro jana baada ya kufungua mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akizungumza na waandishi wa habari mkoani Morogoro jana baada ya kufungua mkutano wa pili wa Mashirika yanayohamasisha upandaji wa miti kibiashara na uzalishaji wa mazao ya misitu barani Afrika, mkutano huo wa siku mbili umewashirikisha wajumbe kutoka nchi 21 duniani kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya kuboresha uzalishaji na upatikanaji wa masoko. 
Picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo. (PICHA NA HAMZA TEMBA - WMU)

TANGA CEMENT YATOA MIFUKO YA SARUJI 660 KWA AJILI YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MAJENGO KOROGWE NA MAABARA KATA YA MLALO LUSHOTO MKOANI TANGA

September 29, 2017
 Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga kushoto akimkabidhi mifuko 500 ya Saruji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Mji,Jumanne Shauri kulia kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Majengo Jijini Tanga ikiwa ni kuunga mkono kusaidia sekta ya afya nchini kulia ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe,Dokta Elizaberth Nyema katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (DAS) Rehema Bwasi
Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga kushoto akimkabidhi mifuko 500 ya Saruji Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Mji,Jumanne Shauri kulia kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Majengo Jijini Tanga ikiwa ni kuunga mkono kusaidia sekta ya afya nchini kushoto ni
Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo
 Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi Mifuko 500 ya Saruji Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (Das) Rehema Bwasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Majengo wilayani humo wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Korogwe Mji,Jumanne Shauri ,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Korogwe,Dkt Elizaberth Nyema wa pili kutoka kushoto ni Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 
  Meneja Usambazaji wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi Mifuko 500 ya Saruji Katibu Tawala wa wilaya ya Korogwe (Das) Rehema Bwasi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya cha Majengo wilayani humo wanaoshuhudia wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Korogwe Mji,Jumanne Shauri ,Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Korogwe,Dkt Elizaberth Nyema wa pili kutoka kushoto ni Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga

 Meneja Ubora wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 160 Afisa Mtendaji wa Kata ya Mlalo kwa ajili ya Ujenzi wa Maabara katika Kata hiyo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kuinua elimu hapa nchini wanaoshudhia ni  Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 
 Meneja Ubora wa Kampuni ya Saruji ya Simba Cement,Samuel Shoo kushoto akimkabidhi mifuko ya saruji 160 Afisa Mtendaji wa Kata ya Mlalo kwa ajili ya Ujenzi wa Maabara katika Kata hiyo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kuinua elimu hapa nchini wanaoshudhia ni  Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga 
 Muonekano wa Saruji ambayo imekabidhiwa leo na Kiwanda cha Simba Cement kwa ajili ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Korogwe Mji na Ujenzi wa Maabara katika shule mbalimbali za sekondari Jimbo la Mlalo wilayani Lushoto mkoani Tanga katika halfa iliyofanyika kiwandani hapa