TIRA YAIKABIDHI BENKI YA CRDB LESENI YA KUANZISHA KAMPUNI TANZU YA BIMA CRDB INSURANCE COMPANY LTD

May 17, 2023
 Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA), Dkt. Baghayo Saqware (wapili kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela leseni ya kuanzisha kampuni tanzu ya huduma za bima CRDB Insurance Company Ltd katika hafla iliyofanyika leo katika hoteli ya Gran Melia jijini Arusha. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Insurance Company, Gerald Kasato (wakwanza kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Insurance Company, Wilson Mnzava.
 
=============   ===========    ============
 
Arusha 17 Mei 2023 - Katika kutanua huduma za bima nchini, Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imeipa Benki ya CRDB leseni kuanzisha kampuni tanzu ya kampuni ya bima ijulikanayo kama CRDB Insurance Company (CIC) Ltd hivyo kuwa benki ya kwanza nchini kumiliki kampuni kamili ya bima.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi leseni hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Gran Melia jijini Arusha, Dkt Baghayo Saqware, ameipongeza Benki ya CRDB kwa kukua katika utoaji wa huduma za bima kutoka kuwa wakala mpaka kampuni kamili ya bima.

“CRDB Insurance ni mtoto mpya kwenye soko la bima na mtoto mwingine kwa Benki ya CRDB kwenye soko la fedha nchini. Inafurahisha kuona mnakua kutoka hatua moja kwenda nyingine. Naamini ndani ya miaka mitano ijayo mtaenda kwenye hatua nyingine kubwa zaidi ya hii. Kuna fursa kubwa kwenu kukua katika soko letu,” amesema Dkt. Saqware.

Dkt. Saqware alisema kwa uzoefu ambao Benki ya CRDB inao katika sekta ya bima, TIRA ina imani CRDB Insurance Company (CIC) Ltd itakwenda kusaidia utekelezaji wa lengo la Serikali la kuchochea ujumuishi wa wananchi kwenye huduma za bima ili Watanzania wanaotumia bidhaa zake wawe walau asilimia 50 ifikapo mwaka 2030 kutoka asilimia 18 ya sasa.

“Katika kuchochea ujumuishi wa kibima Serikali imepitisha sheria ya kufanya baadhi ya bima kuwa za lazima ikiwamo bima ya majengo, makandarasi, afya, na za vyombo vya usafiri. Mkiweza kuja na mkakati madhubuti wa kuchangamkia vizuri maeneo haya na kuhudumia kwa walau asilimia 30 niwahakakikishie ndani ya kipindi kifupi mtatoka kuwa kampuni changa na kuwa moja ya kampuni kubwa za bima nchini,” amesema Dkt Saqware.
Akipokea leseni hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema ni furaha kubwa kwao kupata leseni ya huduma za bima za jumla yaani ‘general insurance’ ukiwa ni muda mfupi tangu walipopata leseni ya kutoa huduma za benki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

“Benki ya CRDB inayo historia kubwa ya kufanya biashara ya bima kwani takriban miaka 15 iliyopita imekuwa ikiifanya kwa namna tofauti ikianza kama wakala na sasa ni kampuni kamili ya bima. Mafanikio haya yanadhihirisha mazingira rafiki ya kufanya biashara nchini,” amesema Nsekela.

Nsekela amesema kampuni ya CRDB Insurance Company itajikita katika ubunifu wa bidhaa na huduma za bima za jumla “general insurance” kwa kuzingatia viwango vilivyo bora na kuhakikisha huduma hizo zinawafikia wananchi walio wengi ili kuchcohea maendeleo ya uchumi wa nchi. 

“Malengo yetu ni kuwa kiongozi katika sekta ya bima nchini kama ilivyo kwa Benki yetu na kampuni zetu tanzu nyengine. Lakini ili kuwa kiongozi ni lazima tuweze kutoa huduma zilizo bora na za mfano katika soko, lazima tuweze kuwekeza katika miundombinu ya usambazaji na uuzaji wa bima ikiwamo kuwatumia mawakala, madalali, banc assurance, na majukwaa ya kidijiti kuuza bima. Naomba nikuhakikishie Kamishna tumejipanga kutekeleza hayo yote,” amesema Nsekela.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Insurance Company Ltd, Wilson Mnzava amesema wamejipanga kikamilifu kuanza kutoa huduma za bima kwa wananchi kuanzia bima zote za jumla huku akielezea kuwa tayari kampuni hiyo imeshaanza mchakato wa kuleta huduma bunifu za bima katika sekta za kimakati nchini ikiwamo sekta ya kilimo.

“Napenda kuwakaribisha Watanzania wote binafsi, taasisi, na kampuni kupata huduma katika kampuni yao ya CRDB Insurance Company Ltd. Niwahakikishie wananchi kwamba CRDB Insurance Company Ltd ndio chaguo sahihi kwao. Tumejiandaa kikamilifu kuwahudumia. Nikuahidi Kamishna kuwa kampuni yetu itashirikiana kwa karibu na TIRA kuboresha huduma na kuyafikia matarajio ya sekta ya bima kwa ujumla,” amesema Mnzava.

Taarifa za TIRA zinaonyesha mpaka Desemba 2022, kulikuwa na kampuni 32 za bima nchini hivyo CRDB Insurance Compaany Ltd inakuwa kampuni ya 33. Katika kipindi hicho, pia kulikuwa na mawakala wa bima 1,500, benki 32 zinazotoa huduma za bima na kampuni tano zinazotoa huduma za bima kidijitali.

Kwa sasa sekta ndogo ya bima inachangia asilimia 1.68 kwenye pato la taifa, malengo yaliyopo ni kufikisha asilimia tatu hadi mwaka 2030 na dalili za kufanikisha hilo zinaonekana kwani mwaka 2022 tozo za bima zilizolipwa (premiums) zilikuwa na thamani ya TZS 1.154 trilioni kutoka TZS 913 bilioni mwaka 2021.

 



BENKI YA NMB KANDA YA KASKAZINI YAFANYA KIKAO NA WAFANYABIASHARA MKOANI TANGA

May 17, 2023


Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini Praygod Godwin akizungumza na wafanyabiashara mkoani Tanga jana kuhusu namna walivyojipanga kuendelea kutoa huduma nzuri kwa wafanyabiashara pamoja na ,kuwaelezea fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye benki hiyo kushoto n i Meneja wa NMB Tawi la Madaraka Elizaberth Chawinga



Meneja wa NMB Tawi la Madaraka Elizaberth  Chawinga akizungumza wakati wa Halfa hiyo

Meneja wa NMB Tawi la Madaraka Elizaberth Chawinga akizungumza wakati wa Halfa hiyo


Meneja Mwandamizi wa Mikopo wa Benki ya NMB Makao Makuu Mashaga Changarawe akizungumza wakati wa kikao hicho


Meneja Mwandamizi wa Mikopo wa Benki ya NMB Makao Makuu Mashaga Changarawe akizungumza wakati wa kikao hicho
Meneja Mwandamizi wa Mikopo wa Benki ya NMB Makao Makuu Mashaga Changarawe akizungumza wakati wa kikao hicho

Sehemu ya Washiriki wa Kikao wakifuatilia kikao hicho



Na Mwandishi Wetu,Tanga

BENKI ya NMB Kanda ya Kaskazini leo wamefanya kikao na wafanyabiashara mkoani Tanga (NMB Business Club) huku wakieleza kwamba wamekuwa wakitoa zaidi ya Bilioni 60 kila mwezi kwa ajili ya wajasiriamali wadogo wadogo hapa nchini

Hatua hiyo inatajwa kama juhudi za benki hiyo kuunga mkono Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu kuwawezesha wajasiriamali wadogo wasogo ili waweze kujikwamua kiuchumi na hivyo kuchochea kasi ya ukuaji maendeleo.

Akizungumza wakati wa kikao hicho na wafanyabiashara ambao wanawahuduma na Meneja Mwandamizi wa Mikopo wa Benki ya NMB Makao Makuu Mashaga Changarawe ambapo alisema kwamba walianza kutoa mikopo hiyo kwa wajasiriamali tokea mwaka 2000.

Mashaga alisema kwamba hatua hiyo imewajengea uzoefu mkubwa namna ya kuwahudumia wajasiriamali hao na kwamba kutokana na utoaji wa mikopo hiyo umewawezesha kuongeza nguvu kwenye mitaji yao na hivyo kuweza kujikwamua kiuchumi.

“Leo hapa Tanga tulikutana na wateja kuwaambia kitu gani wamekianzisha na wakifanye ili kuweza kuboresha huduma zao kwa sasa wana huduma waliyoanzisha kwa ajili ya wateja wanaofanya huduma kwenye masoko yanayosimamiwa vizuri na serikali yana vizimba na wateja wameandikishwa”Alisema

Alisema kwamba ili kuhakikisha nao wananufaika na mikopo hiyo wameanza kutoa mikopo kuanzia 100,000 mpaka 1000000 bila dhamana na baadae milioni 1 hadi 2 mteja anaweka dhamana na wana mikopo mengine zaidi ya hapo inakwenda mpaka Milioni 5 kwa wateja wao.

“Lakini pia tumeanzisha mikopo kwa ajili ya vijana wanaojihusisha na bodaboda ambapo kitu ambacho kinahitajika ni kujiandikisha kwenye vyama vyao ambavyo vinatambulika na serikali na yeye ni kutafuta asilimia 20 ya chombo anachokitaka akishapata benki inaongzekja kiasi kilichobaki ili kumpatia”Alisema Meneja huyo Mwandamizi wa mikopo NMB Makao Makuu.

Hata hivyo alisema kwamba baadae wanafanya biashara na kufanya marejesho kila wiki kumaliza deni kwa kipindi cha miezi sita hadi 12 mpaka watakapoikamilisha ili kuwezesha na wengine kunufaina nayo.

Awali akizungumza Kaimu Meneja wa Kanda ya Kaskazini wa Benki ya NMB-Playgod Godwin alisema kwamba leo wamekutana na wafanyabiashara kuweza kutengeneza mtandao na kubadilishana uzoefu ikiwemo kuwapa mafunzo ya vitu mbalimbali na mwaka huu wamewafundisha vitu vitatu.

Alisema kikao hicho kilikuwa ni mahususi kuwakutanisha wafanyabiashara (Bussness Club) kuwakutanisha ili kuwaeleza kwamba mteja anatakiwa kuaangalia mfano anafanyabiashara ya usafirishaji anatumia petrol lakini dunia inabadilika magari mengi yanabadilika kwenye matumizi ya gesi na mama lishe anatumia mkaa lakini dunia ya leo wanatoka kwenye mkaa kwenda kwente gesi hivyo watawafundisha mbinu mbalimbali na mambo ya kurekodi taarifa za mapato na matumizi na umuhimu wake na wapo wataalamu wazuri.

Hata hivyo alisema pia wataalamu hao watawafundisha jinsi mfanyabiashara kuangaa ikitokea amepata changamoto za kiafya,uzee nani atasimamia biashara zake pia wataangalia namna ya kuwafudnisha katika mambo hayo muhimu.

Katika kikao hicho kiliwakutanisha wafanyabiashara 150 wa mkoa wa Tanga wenye matawi 12 kwa mkoa ambapo inaelezwa kwamba kitakuwa na tija kwa siku zijazo katika kuendeleza biashara zao na hatimaye kukuza mtaji wao.

Naye kwa upande wake Mfanyaabiashara Celina Ndumbaro alisema kwamba alichojifunza katika mafunzo hayo yamewajengea uwezo wa kuweza kuona namna ya kufanya biashara zao kwa tija na kuweza kupata mafanikio.

Mwisho.

PROGRAMU YA KUENDELEZA KILIMO NA UVUVI AFDP KUNUNUA MELI NANE ZA UVUVI WA BAHARI KUU.

May 17, 2023
Katikati, Mratibu wa Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Salimu Mwinjaka akiongea na wakurugenzi wa program hiyo, (kushoto) Bw. Robson Mutandi aliyemaliza muda wake na Bw.Boleslaw Stawicki anayechukua nafasi hiyo.

Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe (kulia) akizungumza na Ujumbe na wataalam hawapo katika picha, kuhusu utekelezaji wa Programu ya kuendeleza kilimo na Uvuvi, (AFDP) kisiwani humo, kushoto ni Mkurugenzi mpya wa Program hiyo Bw. Boleslaw Stawicki.



K Katikati mhandisi Pius Ntwale, kutoka kampuni ya Uvuvi Zanzibar (ZAFICO) akionesha Ujumbe kutoka Program ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) pamoja na wataalamu,rasimu ya kwanza ya ramani ya kiwanda cha kuchakata samaki kitakachojengwa katika eneo la Fungurefu katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.





Kushoto Mkurugenzi wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP)Bw. Robison Mutandi anayemaliza muda wake akiongea na Mkurugenzi mpya wa Programu hiyo Bw.Boleslaw Stawicki, wakati Ujumbe na wataalam wa Programu hiyo ulipotembea maeneo yanayotekeleza Programu hiyo Kisiwani 

Picha ya pamoja ikionesha baadhi ya washiriki wa mkutano wa ujumbe kutoka AFDP pamoja na
wataalam, wakati ujumbe huo ukiwa katika ziara ya kikazi kisiwani Zanzibar ya kutembelea maeneo
yanayotekeleza mradi huo.
Bi. Jacquline Motcho Afisa kutoka Programu ya kuendeleza kilimo na uvuvi nchini (AFDP) akizungumza wakati wa mkutano wa wataalamu na ujumbe kutoka AFDP, ulipokuwa katika ziara ya kikazi kisiwani Zanzibar ya kutembelea maeneo yanayotekeleza mradi huo.


Na, Mwandishi wetu – Zanzibar



Programu ya kuendeleza kilimo na Uvuvi (AFDP) inayoratibiwa na Ofisi ya Waziri  Mkuu Sera Bunge na Uratibu kwa kushirikiana na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar chini, ya ufadhili wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), ipo katika hatua za utekelezaji wa ununuzi ya meli nane zitakazotumika katika uvuvi wa bahari kuu kwa Tanzania Bara na Zanzibar.


Hayo yamesemwa Leo 17 Mei 2023, na mratibu wa Progamu ya AFDP Bw. Salimu Mwinjaka, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu alipozungumza na waandishi wa habari  wakati ujumbe wa programu hiyo ulipokuwa kisiwani Zanzibar, katika ziara ya kutembelea maeneo yanayotekeleza programu hiyo.


Bw. Mwinjaka amesema kuwa Programu hiyo ina mpango mkakati unaotekelezwa kwa pamoja na   Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya kilimo na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar, ambapo katika utekelezaji wa mpango huo kwa upande wa kilimo, Programu inalenga kuboresha upatikanaji wa mbegu bora kwa wakulima kwa mazao ya alizeti, mahindi na maharage.


Alibainisha kuwa, kwa Upande wa Uvuvi, malengo makuu yapo katika maeneo mawili makubwa ikiwa ni pamoja na uvuvi katika maeneo ya Bahari kuu. “Takribani tunategemea kupata Meli nane (8) ambapo, meli nne zitatumika kwa upande wa Tanzania Bara na Meli nne zitatumika kwa Upande wa Zanzibar.


 Aidha, alibainisha kuwa ili meli hizi zifike kuna mchakato ambao unafanyika ikiwa ni pamoja na upembuzi yakinifu, ili kuona kuwa, meli hizo zitaleta matokeo tarajiwa. Vilevile pia ni lazima kuangalia tathmini ya athari ya mazingira na kijamii na pindi maswala haya yakishakamilika ndipo mchakato wa ujenzi wa Meli hizo utaanza.”  Alifafanua ndugu Mwinjaka.


Sambamba na hilo, Bw, Mwinjaka aliendelea kufafanua kuwa katika kipengele cha upembuzi yakinifu, ndipo itajulikana meli hizo zinatakiwa kuwa na ukubwa na uwezo kiasi gani wa kuchukua na kuhifadhi samaki, na aliongeza kwa kusema kuwa upembuzi huu ukikamilika mapema inatarajiwa kuwa kufikia mwezi June mwaka 2024 meli hizi zitakuwa tayari kwani tathmini ya athari ya mazingira na maandalizi mengine ya awali ikiwa ni pamoja na michoro ya meli hizo imeshakamilika.


Awali, akizungumza katika mkutano uliohusisha ujumbe kutoka katika programu hiyo pamoja na wataalamu, Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Dkt Aboud Suleiman Jumbe alisema, kwa upande wa Zanzibar pia Programu hii imejikita katika maeneo mengine matatu ya kuboresha sekta ya uvuvi, ikiwa ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa samaki, kuboresha miundombinu ya sekta ya uvuvi pamoja na kuimarisha mnyororo wa thamani wa uvuvi na mazao ya baharini.

Ujumbe huo kutoka AFDP na IFAD pia umetembelea mkoa wa Kaskazini Unguja, katika shehia ya mto wa pwani Kijiji Cha Fungurefu, mahala ambapo programu hiyo itaenda kujenga kiwanda cha kuchakata samaki, maghala ya baridi kwa ajili ya kuhifadhi samaki  na mitambo ya kutengeneza barafu, na eneo la Mangapwani pahala ambapo itajengwa Bandari ya Uvuvi.


= MWISHO =