President Kikwete Conferred Leadership Award in Arusha

President Kikwete Conferred Leadership Award in Arusha

March 29, 2015

1
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete in conversation with Zimbabwe’s President Robert Mugabe in Arusha shortly before president Mugabe officiated the opening of the 3rd Africa-China Young Leaders Forum yesterday.
3
The President of Pan African Youth Union Ms.Francine Muyumba presents a Leadership Excellence Award to President Dr,Jakaya Mrisho Kikwete in recognition for his outstanding leadership in the continent especially in promoting youth  development
(photos by Freddy Maro)
KITENGO SHIRIKISHI CHA AFYA ZANZIBAR CHA ANDAA MJADALA JUU YA UZAZI WA MPANGO KATIKA UISLAM.

KITENGO SHIRIKISHI CHA AFYA ZANZIBAR CHA ANDAA MJADALA JUU YA UZAZI WA MPANGO KATIKA UISLAM.

March 29, 2015

1
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar Dkt Issa Haji Zidi akizungumza na vijana katika mjadala kuhusu uzazi wa mpango katika uislamu ulioandaliwa na Kitengo cha Shirikishi cha Afya ya mama na mtoto kwenye ukubi wa Chuo cha Mafunzo Kilimani Mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
3
Mkufunzi kutoka Chuo cha  Sayansi ya Afya ya Mbweni Asha Ali Khamis akionyesha moja ya dawa za kisasa za uzazi wa mpango katika mjadala huo.
4
Mmoja wa washiriki wa mjadala kuhusu uzazi wa mpango katika uislamu  Dosa Omar Machano akitoa mchango wake kuhusu umuhimu wa uzazi wa mpango.
6
Mshiriki wa mjada huo kutoka Mkoa Kaskazini  Unguja Asha  Makame Mohd akichangia mada zilizowasilishwa. Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
5
Baadhi ya washiriki wakifuatilia mada zilizowasilishwa katika mjadala kuhusu uzazi wa mpango katika uislamu uliofanyika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo Kilimani.
………………………………………………………..
Na RAMADHANI ALI –MAELEZO ZANZIBAR       
Mhadhiri  na Mtafiti wa masuala ya Kiislamu kutoka Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) Dkt. Issa Haji Zidi amesema Dini ya Kiislamu haipingani na uzazi wa mpango na ulikuwepo  tokea wakati wa Mutume Muahmmad hivyo amewashauri waislamu kuzitumia kwa ajili ya kulinda afya zao.
Akizungumza katika mjadala kuhusu uzazi wa mpango katika Uislamu ulioandaliwa na Kitengo Shirikishi cha Afya ya uzazi na mtoto katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo Kilimani, Dkt. Zidi alisema  lengo la uzazi wa mpango ni kulinda afya ya mama na mtoto aliezaliwa kabla ya  mtoto mwengine.
Alisema zipo njia za asili za uzazi wa mpango  zilizokuwa zikitumiwa na masahaba wakati wa Mtume Muhammad lakini hivi sasa njia hizo zinaonekana kuwa ngumu  kwa watumiaji na  zipo njia za kisasa ambazo ni salama na za uhakika zaidi.
Alisema  tafiti   zinaonyesha kuwa familia  nyingi, hasa za vijijini zenye kipato kidogo,  ambazo zinapinga  mpango huo zimekuwa zikikabiliwa na  matatizo ya kiuchumi na afya  na kupelekea wanaume kuwatelekeza wake zao.
“ Uzazi wa mpango ni makubaliano ya mke na mume kutumia visaidizi katika uzazi ili kuchelewesha uzazi kutokana na matatizo ya kiuchumi na kiafya na wala sio njia ya  kuua ama kupunguza watoto,” alisisitiza Dkt.  Zidi.
Ameongeza kuwa lengo jengine la  uzazi wa mpango ni kulinda hadhi ya mwanamke na  kuhofia kukosa utulivu ndani ya nyumba kutokana na watoto wengi wasioweza kuhudumiwa.
Mwalimu wa  chuo cha  Sayansi ya Afya  Asha Ali Khamis  alisisitiza umuhimu wa wazazi  wawili kukubaliana kunyonyesha  mtoto miaka miwili na kupata mapumziko ya mwaka mmoja kabla ya kuzaliwa mtoto mwengine.
Aliwaeleza washiriki wa mjadala huo ambao wengi ni wanafunzi wa  Vyuo vikuu vya Zanzibar, taasisi za Serikali na NGO kwamba zipo njia za muda mfupi, muda mrefu na njia ya kudumu na zote ni salama pamoja na  baadhi ya  watumiaji kupata mabadiliko madogo madogo ya kimwili.
“Mabadiliko ya kiafya yanayotokea kwa baadhi ya watu wanaotumia dawa hizi isiwe tatizo kwani mara nyingi hutokea katika siku za mwanzo wakati mwili bado haujazoea, ” alisema mwalimu Asha.
Akitoa takwimu za mama wanaopoteza maisha  wakati wa kujifungua Zanzibar , muwezeshaji kutoka UMATI  Mwanajuma Othman  alisema kila wanawake laki moja  288 hufariki.
Alsema idadi hiyo ya  vifo ni kubwa ikilinganishwa na nchi nyengine hasa ikizingatiwa kuwa  vifo hivyo vinaweza kuepukika ikiwa hatua muafaka zitachukuliwa mapema.
Baadhi ya washiriki wa mjadala huo  walionyesha  wazi  wazi kuwa  baadhi ya familia zimekuwa na mashaka ya kutumia dawa za uzazi wa mpango kutokana na imani zao za  dini na kuhofia matatizo ya afya zao .
ASKARI MAGEREZA ALIYEKAMATWA NA FEDHA ZA BANDIA AFUKUZWA KAZI

ASKARI MAGEREZA ALIYEKAMATWA NA FEDHA ZA BANDIA AFUKUZWA KAZI

March 29, 2015

???????????????????????????????
Jeshi la Magereza nchini limemfukuza  kazi askari wake wa Gereza Bariadi, Mkoani Shinyanga (pichani) kwa kosa la kupatikana na fadha za bandia kinyume na Sheria za Nchi.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa jana Machi 28, 2015 na kusainiwa na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja, askari Na. B. 6499 Wdr. Edmund Masaga amefukuzwa kazi kwa fedheha kuanzia Machi 28, 2015 kwa kosa la kulidhalilisha Jeshi mbele ya Umma kinyume na Kanuni 22(xlix) ya Kanuni za Utumishi wa Jeshi la Magereza za Mwaka 1997.
Aidha, Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja amekemea vikali vitendo hivyo kwani ni kinyume cha Maadili na Utendaji ndani ya Jeshi la Magereza huku akiwataka askari wote wa Jeshi la Magereza nchini kutenda kazi zao kwa uadilifu na uaminifu mkubwa.
Imetolewa na;
Lucas Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
       Afisa Habari wa Jeshi la Magereza,
           Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
   DAR ES SALAAM
  Machi 29, 2015.
MATEMBEZI YA KUPIGA VITA MAUAJI YA ALBINO – IMETOSHA

MATEMBEZI YA KUPIGA VITA MAUAJI YA ALBINO – IMETOSHA

March 29, 2015


1
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaymar Kweigyr, Balozi wa Harakati ya Imetosha, Henry Mdimu, Mwakilishi wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Abdillah Omar sambamaba na wadau wengine wakishiriki kuimba wimbo ‘Tanzania Tanzania’ kabla ya kuanza kwa shughuli nzima ya hamasa ya kupiga vita mauaji ya albino nchini, iliyofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es salaam.
Picha zote Othman Michuzi
10
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe akisoma hotuba yake.
8
Mbunge wa Viti Maalum, Al Shaymar Kweigyr akicheza muziki wa sambamba na Mwanamuziki wa Reggae,Jhiko Manyika “Jhikoman” wakati wa shughuli nzima ya hamasa ya kupiga vita mauaji ya albino nchini, iliyofanyika leo kwenye viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es salaam.Kulia ni Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network ambao ni wadau wakubwa wa harakati ya Imetosha, Joachim Mushi.
9
- Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Matembezi ya Hamasa ya kupiga vita mauaji ya albino nchini (Imetosha), Ally Masoud “Kipanya” akimkaribisha Balozi wa Harakati ya Imetosha, Henry Mdimu ili kuzungumza na Watanzania waliofika kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam leo.
2 3 4 5 6 7

ZITTO ACHAGULIWA KWA KISHINDO KUIONGOZA ACT-WAZALENDO

March 29, 2015
Mwanasiasa kijana, Zitto Kabwe, amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama kipya cha siasa cha upinzani ACT Wazalendo, katika uchaguzi uliokamilika usiku wa kuamkia leo Jumapili Machi 29, 2015.Kwa mara ya kwanza chama hicho ambacho katika katiba yake, kinaonyesha patakuwa na viongozi wakuu, wakiongozwa na kiongozi wa chama, mwenyekiti wa chama, makamu wenyeviti wawili kutoka bara na visiwani, katibu mkuu, na manaibu katibu wakuu wawili kutoka pande zote za muungano kitakuwa chini ya uenyekiti wa mwana mama Mwanasheria msomi.
Matokeo hayo yanaonyesha, mwanamama huyo, Anna Mghwirim, ndiye aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, makamu mwenyekiti bara, Shaban Mambo, na makamu mwenyekiti Zanzibar, Ramadhan Suleiman Ramadhan.
Katibu Mkuu na manaibu wake, wanasubiri mapendekezo ya kamati Kuu ya chama ambayo ilitarajiwa kukamilisha kazi yake mapema alfajiri ya Jumapili. Pichani kiongozi huyo wa chama, Zitto Kabwe, akilakiwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho, wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika kwenye ukumbi wa Kadinali Rugambwa, Oysterbay jijini Dar es Salaam, Jumamosi Machi 28, 2015. Zitto alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama hicho nafasi ambayo kwa katiba ya chama hicho ndiyo ya juu zaidi. Chama hicho kitazinduliwa rasmi Jumapili Machi 29, 2015 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
Zitto akionyesha alama ya chama ambayo ni "Uwazi"
Zitto akihutubia wajumbe
Zitto akihutubia wajumbe wakati wa uchaguzi huo
Zitto akipongezwa
Wajumbe wakiserebuka, wakati wa uchaguzi huo
Wajumbe wakifurahi kwa kushikana mikono kuonyesha umoja
Wajumbe wakipiga kura
Askofu Gerald Mpango akiongoza sala
Mzee Kastiko, akiwakilisha waislamu kuomba dua
Aliyekuwa katibu mkuu wa muda wa ACT-Wazalendo, Samson Mwigamba, akihutubia
Msimamizi wa uchaguzi huo, Profesa Kitila Mkumbo

BAADA YA KUZIMIA, AKIZINDUKA ASKOFU GWAJIMA ATAKIWA KURIPOTI KWA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI KESHO KUTWA KUTOA MAELEZO

March 29, 2015
Wakati Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akijisalimisha kwa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amemtaka aliroti ofisini kwake kesho kutwa kutoa maelezo kuhusiana na tuhuma za kumkashifu kiongozi mwenzake wa dini
Makonda amemwandikia barua Askofu Gwajima akimtaka kufikia ofisini kwake kutoa ufafanuzi juu ya maneno makali dhidi ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki.
Katika barua yake, Makonda alisema ofisi yake inataka kufahamu kama uhuru wa kuabudu kikatiba ni kutokuheshimu watu wengine. 
“Hatuamini kama imefika wakati kwenye nyumba za ibada kumegeuka sehemu ya kutukana na kuwasema watu badala ya kuhubiri habari njema. Tunataka kujidhihirisha malengo hasa ya kutumia maneno hayo ni nini.”
Gwajima alipoteza fahamu jana alipokuwa akihojiwa na Polisi kwa tuhuma za kumkashfu Kardinali Pengo.

UONA JINSI WA MALAWI WALIVYOFANYA MAZOEZI CCM KIRUMBA JANA, TAYARI KUKUTANA NA TAIFA STARS LEO JUMAPILI

March 29, 2015


Na Faustine Ruta, Mwanza.
Timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) pichani leo jioni imefanya mazoezi ya mwisho tayari kwa kuwakabili Wenyeji wao Tanzania Timu ya (Taifa Stars) mchezo utakaochezwa kesho jumapili saa 10.30 jioni katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Wakibadilishana Mawazo wakati Wachezaji wa Malawi wanajifua mara ya mwisho kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jioni ya leo.

Tiketi za mchezo tayari zimeshaanza kuuzwa katika vituo vya Uwanja wa Nyamagana na uwanja wa CCM Kirumba kwa bei za sh. 5,000 kwa mzunguko, sh. 12,000 kwa jukwaa kuu na sh.20,000 kwa viti vya jukwaa kuu maalum. 
Taifa Stars inashika nafasi ya 100 katika msimamo wa viwango vya FIFA vilivyotolewa mwezi Machi, huku Malawi (The Flames) wakishika wakiwa nafasi ya 91 kwenye vinago hivyo. 
Akiongea na waandishi wa habari leo kaika hoteli ya La Kairo iliyopo Kirumba jijini Mwanza, kocha msaidizi wa Taifa Stars Salum Mayanga amesema kikosi chao kipo katika hali nzuri , na sasa kilichobakia ni mchezo wenyewe wa kesho jumapili.


Mayanga amesema vijana wake wote 22 waliopo kambini wapo fiti, wamefanya mazoezi kwa siku tano katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, wachezaji wapo kwenye ari na morali ya juu, kikubwa wanachosubiri ni kesho tu kushuka dimbani kusaka ushindi. 
Aidha Mayanga amewaomba wapenzi wa mpira wa miguu waliopo jijini Mwanza na mikoa ya jirani ya kanda ya ziwa, kujitokeza kwa wingi kesho uwanjani kuja kuwapa sapoti vijana kwa kuwashangilia muda wote wa mchezo. 
Tayari waamuzi na kamishina wa mchezo wameshawasili jijini Mwanza, mwamuzi wa kati atakua ni Munyazinza Gervais kutoka nchini Rwanda, akisaidiwa na mshika kibendera wa kwanza Hakizimana Ambroise (Rwanda), mshika kibendera wa pili Niyitegeka Bosco (Rwanda), mwamuzi wa akiba Martin Saanya kutoka Morogoro huku na Kamishina wa mchezo ni Afred Rwiza kutoka Mwanza.

Mashabiki nao walikuwepo kutazama mazoezi hayo ya The Flames kutoka Mjini Malawi
Baadhi ya Viongozi wa Soka wakiteta jambo Uwanjani hapo CCM Kirumba
Katikati ni Baraka Kizuguto Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) akiteta jambo.

RAIS ROBERT MUGABE AFUNGUA MKUTANO WA VIJANA VIONGOZI WA CHINA NA AFRIKA NGURUDOTO

March 29, 2015

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe akihutubia katika ufunguzi wa Kongamano la Tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China lililofanyika leo kwenye hotel ya Ngurdoto ,Arusha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akipokea tuzo ya Heshima ya kuhamasisha amani na utulivu barani Afrika kutoka kwa Rais wa Umoja wa Vijana wa Afrika uliochini ya Umoja wa Afrika (AU) Francine Furaha Muyumba.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wajumbe wa waliohudhuria Kongamano la Tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China lililofanyika Ngurdoto,Arusha.
Rais wa Umoja wa Vijana wa Afrika ulio chini ya Umoja wa Afrika Francine Furaha Muyumba akihutubia katika kongamano hilo.
Rais Jakaya Kikwete (kulia),Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  (katikati) na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)Stepehen Masele wakisikiliza hotuba ya Rais wa Umoja wa Vijana wa Afrika ulio chini ya Umoja wa Afrika Francine Furaha Muyumba
Bendi ya Polisi ya Moshi (brass band) ikitumbuiza wakati wa Kongamano
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akifuatilia kwa makini hotuba za viongozi mbali mbali wakati wa Kongamano.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Ushauri wa
Kisiasa la Watu wa China pia Waziri wa Idara ya Kimataifa wa Kamati Kuu
ya Chama cha Kikomunisti cha China Dk.Wang Jiarui akiingia ukumbini akiongozana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira)Stepehen Masele
Baadhi ya wajumbe kutoka China
Baadhi ya wajumbe wa kongamano
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahaman Kinana akihutubia katika Kongamano la Tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China lililofanyika Ngurdoto,Arusha.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Ushauri wa Kisiasa la Watu wa China pia Waziri wa Idara ya Kimataifa wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Dk.Wang Jiaruiakihutubia wakati wa Kongamano la Tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China lililofanyika Ngurdoto,Arusha.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu abdulrahman Kinana (kulia) Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu(katikati) na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya ukumbi wa mkutano wa Kongamano la Tatu la Viongozi Vijana wa Afrika na China lililofanyika Ngurdoto Arusha.