Mkubwa na Wanawe watoa msaada Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke

Mkubwa na Wanawe watoa msaada Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke

June 26, 2016


Kituo cha kuvumbua na kuendeleza vipaji vya muziki cha Mkubwa na Wanawe, kimetoa msaada ya vifaa vya tiba na vifaa mbalimbali vikiwe vile vya usafi, dawa za meno, sabuni, maji na juisi kwa wodi ya Watoto waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, Jijini Dar es Salaam.

Awali akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, kiongoni wa kituo hicho, Said Fella, amesema wameamua kufanya hivyo kutokana na kuguswa na changamoto zinazoikabili hospitali hiyo ya Temeke ambayo pia ni majirani zao ambapo pia amebainisha kuwa kundi hilo limekuwa likifika Hospitalini hapo kuchangia misaada mbalimbali.

Said Fella ameongeza kuwa, alishauriwa na vijana wake waliopo katika kituo chake kuona ni vipi wanaweza kushiriki katika shughuli yoyote ya kijamii kwa kipindi hiki cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na wote kwa pamoja kukubaliana kutoa msaada huo.

“Nasi pia ni kama wagonjwa watarajiwa, hivyo tumeona ni vema kuja kutoa msaada wa vifaa mbalimbali vya tiba kama tulivyoshauriwa na wenyeji wetu, tukiwa pamoja na mabalozi wetu. Msaada tuliotoa una thamani ya Sh milioni tatu,” alisema Fella.

Akipokea msaada huo, mmoja wa madaktari wa hospitali hiyo, Rashid Nyumbiage, alikishukuru kituo hicho kwa kuwakumbuka akiwataka wasanii na viongozi wake pamoja na wengineo wenye nafasi kuendelea kuwakumbuka.

“Vifaa tulivyoletewa ni Paso-Oximeter cha kupimia kiwango cha oksijeni mwilini, HB Culvate cha kupima kiwango cha damu, mashine ya BP ambayo kazi yake ni kufahamu kama presha ya damu (BP) imeshuka au la na Mashine ya Nebulizer yenye kazi ya kuwapimia dawa wagonjwa wa pumu,” alisema Nyumbiage.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake takribani 50 alioambatana nao hospitalini hapo, msanii anayeunda kundi la Yamoto, Dog Aslay, alisema kuwa wamefarijika kuwasaidia wagonjwa akiahidi kufanya hivyo wakati mwingine watakapopata nafasi.

Tukio hilo la aina yake kwa kundi hilo ambalo ufanya mara kwa mara katika kutembelea jamii na kusaidia misaada, limeweza kupongezwa na baadhi ya ndugu wa wagonjwa na wagonjwa wenyewe kwa kueleza kuwa ni tendo la kuigwa na kila mmoja wetu hasa wasanii ambao ni kioo cha jamii.
Baadhi ya vijana wanaounda kundi la Mkubwa na Wanawe Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke wakati wa tukio hilo lililofanyika leo Juni 26.2016.Kiongoni wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella, akielezea namna vijana wake walivyoguswa na kuamua kujitolea kwa ajili ya watu wenye kuhitaji wakiwemo wa Hospitali hiyo ya Temeke.Kiongoni wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella, akimkabidhi baadhi ya vifaa Daktari wa hospitali hiyo, Rashid Nyumbiage Baadhi ya wasanii wa kundi la Yamoto Band ambao pia wanatoka Mkubwa na Wanawe wakitoa vionjo kadhaa wakati wa tukio hilo.

Kiongoni wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella akishukuru kwa hatua hiyo ya kurudisha fedhila kwa JamiiMsanii Kiongozi wa Kundi la Yamoto Band,"Aslay Isihaka"-Dogo Aslay akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake wa Yamoto pamoja na kundi hilo la Mkubwa na Wanawe

Kiongoni wa kituo cha Mkubwa na Wanawe, Said Fella akionyesha moja ya vifaa hivyo vya tiba
Daktari wa hospitali hiyo, Rashid Nyumbiage akionyesha moja ya kifaa huku akielezea namna kinavyofanya kaziMakabidhiano yakiendelea..
Vijana na Mabalozi wa kundi la Mkubwa na Wanawe wakibeba baadhi ya vifaa walivyotoa msaada hospitalini hapo.
Wakielekea wodini...
Amani James a.k.a Chiba wa kundi la Yamoto Band akitoa msaada katika tukio hiloMsanii Kiongozi wa Kundi la Yamoto Band,"Aslay Isihaka"-Dogo Aslay akimfariji mmoja wa Watoto wanaopatiwa matibabu katika hospitali hiyo ya Temeke
Said Fella (kulia) na Mh. Temba (kushoto) wakielezea jambo wakati wa tukio hilo leo Juni 26
Enock Deogratius 'Enock Bella' akimfariji mtoto
Amani James a.k.a Chiba wa kundi la Yamoto Band aliweza kuwafariji watoto na ndugu wanaouguza watoto wao pale walipomuomba awachezee kidogo kwani imekuwa faraja kwa kumuona kwa mara ya kwanza
Mkubwa na Wanawe..
Mkubwa na Wanawe Baadhi ya vijana wanaounda kundi hilo la Mkubwa na Wanawe wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa tukio hilo la kutoa msaada hospitali ya Temeke. leo Juni 26.2016. (Picha zote na Andrew Chale,Modewjiblog).

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya na afanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Mikoa

June 26, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.

Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.

Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.

Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.

Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.

Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.

Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.

Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo 

(Orodha imepangwa kulingana na mikoa)


ARUSHA
1.      Arusha            -           Mrisho Mashaka Gambo
2.      Arumeru        -           Alexander Pastory Mnyeti
3.      Ngorongoro   -           Rashid Mfaume Taka
4.      Longido          -           Daniel Geofrey Chongolo
5.      Monduli         -           Idd Hassan Kimanta
6.      Karatu             -           Therezia Jonathan Mahongo


DAR ES SALAAM
1.      Kinondoni      -           Ally Hapi
2.      Ilala                 -           Sophia Mjema
3.      Temeke         -           Felix Jackson Lyaviva
4.      Kigamboni     -           Hashim Shaibu Mgandilwa
5.      Ubungo          -           Hamphrey Polepole

DODOMA
1.      Chamwino      -           Vumilia Justine Nyamoga
2.      Dodoma         -           Christina Solomon Mndeme
3.      Chemba          -           Simon Ezekiel Odunga
4.      Kondoa          -           Sezeria Veneranda Makutta
5.      Bahi                -           Elizabeth Simon
6.      Mpwapwa       -           Jabir Mussa Shekimweli
7.      Kongwa           -           John Ernest Palingo

GEITA
1.      Bukombe       -           Josephat Maganga
2.      Mbogwe          -           Matha John Mkupasi
3.      Nyang'wale      -           Hamim Buzohera Gwiyama
4.      Geita               -           Herman C. Kipufi
5.      Chato              -           Shaaban Athuman Ntarambe

IRINGA
1.      Mufindi          -           Jamhuri David William
2.      Kilolo              -           Asia Juma Abdallah
3.      Iringa              -           Richard Kasesela

KAGERA
1.      Biharamulo    -           Saada Abraham Mallunde
2.      Karagwe          -           Geofrey Muheluka Ayoub
3.      Muleba           -           Richard Henry Ruyango
4.      Kyerwa            -           Col. Shaban Ilangu Lissu
5.      Bukoba           -           Deodatus Lucas Kinawilo
6.      Ngara              -           Lt. Col. Michael M. Mtenjele
7.      Missenyi         -           Lt. Col Denis F. Mwila

KATAVI
1.      Mlele              -           Rachiel Stephano Kasanda
2.      Mpanda          -           Lilian Charles Matinga
3.      Tanganyika     -           Saleh Mbwana Mhando

KIGOMA
1.      Kigoma           -           Samsoni Renard Anga
2.      Kasulu                        -           Col. Martin Elia Mkisi
3.      Kakonko        -           Col. Hosea Malonda Ndagala
4.      Uvinza                        -           Mwanamvua Hoza Mlindoko
5.      Buhigwe          -           Col. Elisha Marco Gagisti
6.      Kibondo         -           Luis Peter Bura

KILIMANJARO
1.      Siha                 -           Onesmo Buswelu
2.      Moshi             -           Kippi Warioba
3.      Mwanga          -           Aaron Yeseya Mmbago
4.      Rombo           -           Fatma Hassan Toufiq
5.      Hai                  -           Gelasius Byakanwa
6.      Same               -           Rosemary Senyamule Sitaki

LINDI
1.      Nachingwea    -           Rukia Akhibu Muwango
2.      Ruangwa         -           Joseph Joseph Mkirikiti
3.      Liwale             -           Sarah Vicent Chiwamba
4.      Lindi               -           Shaibu Issa Ndemanga
5.      Kilwa               -           Christopher Emil Ngubiagai


MANYARA
1.      Babati              -           Raymond H. Mushi
2.      Mbulu             -           Chelestion Simba M. Mofungu
3.      Hanang'          -           Sara Msafiri Ally
4.      Kiteto              -           Tumaini Benson Magessa
5.      Simanjiro        -           Zephania Adriano Chaula

MARA
1.      Rorya              -           Simon K. Chacha
2.      Serengeti        -           Emile Yotham Ntakamulenga
3.      Bunda             -           Lydia Simeon Bupilipili
4.      Butiama          -           Anarose Nyamubi
5.      Tarime           -           Glodious Benard Luoga
6.      Musoma         -           Dkt. Vicent Anney Naano

MBEYA
1.      Chunya           -           Rehema Manase Madusa
2.      Kyela               -           Claudia Undalusyege Kitta
3.      Mbeya             -           William Ntinika Paul
4.      Rungwe           -           Chalya Julius Nyangidu
5.      Mbarali           -           Reuben Ndiza Mfune

MOROGORO
1.      Gairo              -           Siriel Shaid Mchembe
2.      Kilombero     -           James Mugendi Ihunyo
3.      Mvomero       -           Mohamed Mussa Utali
4.      Morogoro       -           Regina Reginald Chonjo
5.      Ulanga                        -           Kassema Jacob Joseph
6.      Kilosa              -           Adam Idd Mgoyi
7.      Malinyi            -           Majula Mateko Kasika

MTWARA
1.      Newala            -           Aziza Ally Mangosongo
2.      Nanyumbu     -           Joakim Wangabo
3.      Mtwara            -           Dkt. Khatibu Malimi Kazungu
4.      Masasi             -           Seleman Mzee Seleman
5.      Tandahimba  -           Sebastian M. Walyuba

MWANZA
1.      Ilemela           -           Dkt. Leonald Moses Massale
2.      Kwimba          -           Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
3.      Sengerema     -           Emmanuel Enock Kipole
4.      Nyamagana     -           Mary Tesha Onesmo
5.      Magu               -           Hadija Rashid Nyembo
6.      Ukerewe         -           Estomihn Fransis Chang'ah
7.      Misungwi        -           Juma Sweda

NJOMBE
1.      Njombe          -           Ruth Blasio Msafiri
2.      Ludewa                       -           Andrea Axwesso Tsere
3.      Wanging'ombe          -           Ally Mohamed Kassige
4.      Makete                       -           Veronica Kessy

PWANI
1.      Bagamoyo      -           Alhaji Majid Hemed Mwanga
2.      Mkuranga       -           Filberto H. Sanga
3.      Rufiji               -           Juma Abdallah Njwayo
4.      Mafia               -           Shaibu Ahamed Nunduma
5.      Kibaha            -           Asumpter Nsunju Mshama
6.      Kisarawe         -           Happyness Seneda William
7.      Kibiti               -           Gulamu Hussein Shaban Kifu

RUKWA
1.      Sumbawanga  -           Dkt. Khalfan Boniface Haule
2.      Nkasi              -           Said Mohamed Mtanda
3.      Kalambo         -           Julieth Nkembanyi Binyura

RUVUMA
1.      Namtumbo    -           Luckness Adrian Amlima
2.      Mbinga           -           Cosmas Nyano Nshenye
3.      Nyasa              -           Isabera Octava Chilumba
4.      Tunduru        -           Juma Homela
5.      Songea            -           Polet Kamando Mgema

SHINYANGA
1.      Kishapu          -           Nyambonga Daudi Taraba
2.      Kahama          -           Fadhili Nkulu
3.      Shinyanga       -           Josephine Rabby Matiro


SIMIYU
1.      Busega            -           Tano Seif Mwera
2.      Maswa             -           Sefu Abdallah Shekalaghe
3.      Bariadi            -           Festo Sheimu Kiswaga
4.      Meatu             -           Joseph Elieza Chilongani
5.      Itilima             -           Benson Salehe Kilangi


SINGIDA
1.      Mkalama        -           Jackson Jonas Masako
2.      Manyoni         -           Mwembe Idephonce Geofrey
3.      Singida            -           Elias Choro John Tarimo
4.      Ikungi             -           Fikiri Avias Said
5.      Iramba            -           Emmanuel Jumanne Luhahula

SONGWE
1.      Songwe           -           Samwel Jeremiah
2.      Ileje                 -           Joseph Modest Mkude
3.      Mbozi             -           Ally Masoud Maswanya
4.      Momba           -           Juma Said Irando


TABORA
1.      Nzega              -           Geofrey William Ngudula
2.      Kaliua             -           Busalama Abel Yeji
3.      Igunga             -           Mwaipopo John Gabriel
4.      Sikonge          -           Peres Boniphace Magiri
5.      Tabora            -           Queen Mwashinga Mlozi
6.      Urambo          -           Angelina John Kwingwa
7.      Uyui                -           Gabriel Simon Mnyele

TANGA
1.      Tanga              -           Thobias Mwilapwa
2.      Muheza          -           Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
3.      Mkinga           -           Yona Lucas Maki
4.      Pangani           -           Zainab Abdallah Issa
5.      Handeni         -           Godwin Crydon Gondwe
6.      Korogwe         -           Robert Gabriel
7.      Kilindi             -           Sauda Salum Mtondoo
8.      Lushoto          -           Januari Sigareti Lugangika

Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Juni, 2016