WAZIRI NAPE NNAUYE AFUNGA MASHINDANO YA AIRTEL RISING STAR MSIMU WA SITA

September 12, 2016


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo mhe. Nape Moses Nnauye (wa pili kulia) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka Airtel Tanzania Bi. Beatrice Singano (wa pili kushoto) wakati akiwasili katika Uwanja wa Karume kuhitimisha mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star Septemba 11, 2016 kushoto ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania Bw. Jamali Malinzi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wa pili kulia) akijadiliana jambo na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania Bw. Jamali Malinzi wakati wa hitimisho la mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star Septemba 11, 2016.
Mkurugenzi wa Airtel Tanzania Bw. Sunil Colaso akizungumza kuhusu maendeleo ya mashindano ya Airtel Rising Star wakati wa hitimisho la mashindano hayo ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akipita katika moja ya geti linalotumia mfumo wa mashine za tiketi za kieletroniki katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na wanamichezo, wadau wa michezo na wanahabari kabla ya kushuhudia fainali ya mashindano hayo yiliyohitimisha mashindano hayo kwa Vijana chini ya umri wa miaka 17 Airtel Rising Star katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikagua wachezaji wa timu ya Morogoro Boys kabla ya kuanza kwa fainali kati yao na timu ya Ilala iliyofanyika katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi kikombe kwa nahodha wa Timu ya wasichana ya Temeke walioibuka washindi wa mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star kwa upande wa wasichana katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi kikombe kwa nahodha wa Timu ya wavulana ya Morogoro walioibuka washindi wa mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star kwa upande wa wavulana katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Timu ya wasichana ya Temeke wakishangilia ushindi wao wakishangilia ushindi wao walioupata katika mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star kwa upande wa wasichana kwa kuwafunga Timu ya temeke kwa mikwaju ya penati katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Timu ya wavulana ya Morogoro wakishangilia ushindi wao wakishangilia ushindi wao walioupata katika mashindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star kwa upande wa wavulana kwa kuwafunga Timu ya Ilala kwa goli moja kwa bila katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Timu ya wavulana ya Morogoro mara baada ya kumalizika kwa mshindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star yaliyofanyika katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiwa katika picha ya pamoja na Timu ya wavulana ya Ilala mara baada ya kumalizika kwa mshindano ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Star yaliyofanyika katika Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam Septemba 11, 2016. Picha zote na Raymond Mushumbusi WHUSM

AZANIA BANK TAWI LA MOSHI YAKABIDHI ZAWADI YA MBUZI KWA WATEJA WAKE NA VITUO VYA KULELEA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU

September 12, 2016
Wafanyakazi wa Benki ya Azania tawi la Moshi ,wakishusha Mbuzi kwa ajili ya kutoa zawadi ya siku kuu ya Idd kwa baadhi ya wateja wake pamoja na makundi yenye mahitaji maalumu.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi ,Hajira Mmambe akimkabidhi zawadi ya Mbuzi mwakilishi wa Mbunge wa jimbo la Moshi mjini Jafary Michael , Bw ,Bashir Seleman wa kampuni ya Zuhad kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank  tawi la Moshi,Hajira Mmambe akikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa msimamizi wa kituo cha kulea watoto waishio kwenye mazingira magumu cha Qadria kilichopo kata ya mji Mpya,Alhaji Taqdir Haji Amir kama sadaka ya siku kuu ya Idd.
Baadhi ya watoto wa kituo cha  kulelea watoto cha Qadria kilichopo kata ya Mji Mpya.
Meneja wa Azania Bank akikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa mteja wa Benki hiyo Aman Idd Mushi kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa mwakilishi wa kampuni ya Ibra line ,Bi Mosi Shayo kwa ajili ya siku kuu ya Idd.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe akizungumza mara baada ya kukabidhi zaadi ya Mbuzi kwa ajili ya siku kuu ya Idd kwa wateja wake pamoja na makundi yenye mahitaji maalumu.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AONGOZA SWALA YA IDD EL HAJI VIWANJA VYA MWEMBE YANGA TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM

September 12, 2016
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitoa hutuba katika swala ya Idd El Haji iliyofanyika Viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo asubuhi.
 Swala ikiendelea.

Waziri Mkuu alivyojumuika na waislam wenzake katika swala hiyo.
 Sheikh Abdu Kadri akiongoza swala ya Idd El Haji 
 Sheikh Nurudin Kishki akihutubia baada ya swala hiyo.
 Waumini wa dini ya kiislam wakishiriki swala hiyo.


Waumini wa dini ya kiislam wakiswali.