MHE UMMY AFANYA MKUTANO WA HADHARA WA JIMBO LA TANGA

May 28, 2023





MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya akizungumza na wananchi wa Kata ya Makorora katika Jimbo hilo mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano wake wa hadhara akielezea utekelezaji wa Ilani kwa miaka miwili

Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow akizungumza wakati wa mkutano huo









*Aanza na matembezi kuhimiza utunzaji wa mazingira na kufungua shina la vijana wa bodaboda Mikanjuni.
*Aelezea utekelezaji wa Ilani kwa miaka miwili.
*Amshukuru Mhe.Rais Dkt. Samia kwa kuendelea kumwaga mabilioni Tanga Mjini.


Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini Mhe Ummy Mwalimu ambae pia ni Waziri wa Afya tarehe 27/5/2023 amefanya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kuelezea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka miwili. Mkutano huo umefanyika katika viwanja vya Makorora Sokoni, Kata ya Makorora Jijini Tanga.


Katika mkutano huo uliofunguliwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba, Mhe Ummy ameelezea utekelezaji wa yale yote yalioahidiwa na Mgombea uRais, ubunge na madiwani katika mikutano ya kuomba kura Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.


Mhe Ummy ameeleza mafanikio yaliyopatikana katika sekta za Elimu, Afya, Miundombinu ya Barabara, upatikanaji wa Maji na umeme hususani katika kata za pembezoni mwa jiji, maboresho ya Bandari ya Tanga, Masoko, Ongezeko la viwanda vya kati vitatu (3) na viwanda vidogo 21 na utoaji wa Mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 3,032,030,000 kwa vikundi 176 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Katika mkutano huo uliohudhuriwa na Mjumbe wa Kamati ya siasa Mkoa wa Tanga Ndugu Omari Ayoub, Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Hashim Mgandilwa, Katibu wa CCM Wilaya ya Tanga, ndugu Selemani Sankwa, Katibu Itikadi na Uenezi ndugu Joel Mulenga, wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Wilaya na sekretariet wilaya ya Tanga, Viongozi wa CCM Kata ya Makorora, wanaCCM na wananchi wa Jiji la Tanga, Mhe Ummy alirudia tena kuwashukuru wanatanga kwa kuendelea kumuamini na kuwaahidi hatawaangusha katika utekelezaji wa majukumu yake ya kibunge. Aidha alieleza kufurahishwa kwa jinsi wananchi walivyojitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo.


Imetolewa na;
Ofisi ya Mbunge, Jimbo la Tanga Mjini
28/5/2023