PICHA ZA MAPOKEZI MAKUBWA : JANUARY MAKAMBA ATUA BUKOBA LEO KUZOA WADHAMINI LUKUKI
Mh.
January Makamba na mkewe, Ramona Makamba(kulia) baada ya kuwasili
mkoani hapa Kagera kwa ajili ya kutafuta wadhamini watakaotia saini fomu
zake za kuwania Urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama
hicho cha CCM. Picha na Faustine Ruta, Bukoba.
Mh.
January Makamba na mkewe, Ramona(kulia) mara baada ya kushuka kwenye
Ndege leo hii Jumatano asubuhi juni 24, 2015. Picha na Faustine Ruta,
Bukoba.
Mh. January Makamba akisalimiana na Katibu wa Vijana Mkoa wa Kagera
Mh.
January Makamba akisalimiana na Wanafunzi wa Sekondari waliokuwa
Uwanjani hapo ambao bila Shaka walikuwa wanasoma masomo ya Ndege
inavyoruka na kutua na mengineyo kiujumla leo jumatano juni 24, 2015.
Picha na Faustine Ruta, Bukoba
Mh. January Makamba akisaini kwenye kitabu cha Wageni kwenye Uwanja Ndege Bukoba.
Mh. January Makamba na mkewe, Ramona wakiteta jambo kwa furaha.
Msafara wa Bodaboda kuelekea Mjini kwenye mzunguko na kugeuka kwenye Makao makuu ya CCM Mkoa wa Kagera
Mjini Bukoba, Bodaboda wakimsindikiza Mh. Januari Makamba
Makamba akisalimia Wakazi wa Mji wa Bukoba walijitokeza kwa wingi
January
Makamba ameendelea na Ziara yake ya Kusaka Wadhamini katika Mikoa
mbalimbali ya Tanzania na leo hii jumatano juni 24, 2015 yupo hapa
Mkoani Kagera akiomba Uzamini. Mh. January Makamba amepokelewa na wakazi
wengi wa Mkoa wa Kagera wakiwemo Vijana walijitokeza kwa wingi
kumpokea. Picha na Faustine Ruta, Bukoba
Mh.
Januari Makamba baada ya kusalimiana na Wakazi waliojitokeza kwenye
Makao makuu ya CCM ameelekea katika Hospitali ya Mkoa kuwaona wagonjwa
mbalimbali na Baada ya hapo ameelekea Wilayani Misenyi kwenda kusalimia
Wakazi wa huko na Kuwaomba wamdhamini kwa kuweka saini fomu zake za
kuwania Urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho cha
CCM.
Mh. Januari Makamba Akitia saini Katika kitabu cha wageni Ofisi za CCM
January Akizungumza na wakazi wa Bukoba waliojitokeza kumsikiliza katika katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kagera leo
Wakazi wa Mji wa Bukoba wakimsikiliza Mh. January Makamba kwa makini leo hii jumatano.
RAIS KIKWETE NA DKT. REGINALD MENGI IKULU, DAR ES SALAAM
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na
Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha
Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT) Dkt Reginald Mengi wakiongea na
kubadilishanma mawazo Ikulu, Jijini Dar es salaam katika hafla ya
kutunuku nishani kwa watumishi wa umma na wananchi waliofanya vyema na
kwa uadilifu kwenye sehemu zao za kazi. Dkt Mengi alikuwa mmoja wa watu
mashuhuri walioalikwa hapo Ikulu.
PICHA NA IKULU
Mawakala wa forodha nchini waaswa kujisajili kwenye mfumo wa himaya moja ya forodha ya afrika mashariki (SINGLE CUSTOM TERRITORY)
Kamishna wa Forodha Kutoka
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Kabisi akiongea na viongozi
wa Chama cha Mawakala wa Forodha na kuwataka mawakala wa Tanzania
kujisajili katika mfumo wa uondoshaji wa Himaya moja ya Forodha(SINGLE
CUSTUM TERRITORY) ili kuwezesha uondoshwa wa mizigo kwa haraka zaidi
pindi mfumo huo utakapoanza kutumika kwani mifumo huo na watanzania
tayari zinawasiliana mpaka sasa, Wakati wa Mkutano uliofanyika leo
Jijini Dar es Salaam Kushoto ni Naibu Kamishna wa Forodha Dkt. Patrick
Mugoya.
Rais wa Chama cha Mawakala wa
Forodha (TAFA) Bw. Stephen Ngatunga akiongea na viongozi wa Chama cha
Mawakala wa Forodha na wawakilishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
ambapo aliipongeza serikali kupitia Mamlaka hiyo katika kuhakikisha
wanaweka mazingira mazuri kwa mawakala wa forodha na kuiasa kuendelea
kushughulikia changamoto mbalimbali katika sekta hiyo ili kuiwezesha
serikali kupata mapato kwa maendeleo ya Taifa, Wakati wa Mkutano
uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam Kulia ni Kamishna wa Forodha Kutoka
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Kabisi.
Baadhi ya Viongozi na wanachama wa
Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA) wakimsikiliza Kamishna wa Forodha
Kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Kabisi, Wakati wa
Mkutano uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanachama wa Chama cha
Mawakala wa Forodha (TAFA) wakichangia wakati wa mkutano uliokutanisha
Viongozi na wanachama wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA) pamoja na
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
………………………………………………….
Habari Picha Na Hassan Silayo-MAELEZO
Mawakala wa Forodha nchini wameaswa kujisajili katika mfumo wa
uondoshaji mizigo wa Himaya moja ya Forodha ya Afrika Mashariki (Single
Custom Territory) utakao anza kutumika hivi Karibuni.
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Forodha Kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Kabisi wakati mkutano na Viongozi na wanachama wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA)
Bw. Kabisi alisema kuwa mawakala wa forodha nchini hawana budi kufanya hivyo ili kuwezesha uondoshwaji wa mizigo kwa haraka zaidi pindi mfumo huo utakapoanza kutumika.
“Sasa tunaelekea katika matumizi ya Himaya moja ya Forodha ya Afrika Mashariki yaani Single Custom Territory ili kuwa na uwezo wa kupata huduma kwa kutumia mfumo huo pindi matumizi yatakapoanza mapema ili kuondoa usumbufu utakaoweza kutokea”. Alisema Bw. Kabisi
Bw. Kabisi aliongeza kuwa mpaka sasa ni makampuni mawili (2) ya mawakala waliojisajili mpaka sasa.
Aidha Bw. Kabisi alisema kuwa mawakala wa forodha hawana budi kuendelea kuwa waamifu ili waendelee kuongoza katika makusanyo ya fedha kwa mwaka ujao ambapo kwa mwaka huu wamechangia kwa asilimia 40 ya mapato ya serikali.
Naye Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA) Bw. Stephen Ngatunga alisema kuwa wataendelea kushirikiana na Mamlaka la Mapato Tanzania (TRA) katika kuhakikisha wanaifanya idara ya forodha inafanya vizuri katika makusanyo ya fedha.
Pia Bw. Ngatunga aliitaka serikali kuendelea kushughulikia changamoto mabalimbali zinazoikabili idara hiyo ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu na kuendelea kuongoza katika makusanyo ya mapato ya serikali.
Hayo yamesemwa na Kamishna wa Forodha Kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Tiagi Kabisi wakati mkutano na Viongozi na wanachama wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA)
Bw. Kabisi alisema kuwa mawakala wa forodha nchini hawana budi kufanya hivyo ili kuwezesha uondoshwaji wa mizigo kwa haraka zaidi pindi mfumo huo utakapoanza kutumika.
“Sasa tunaelekea katika matumizi ya Himaya moja ya Forodha ya Afrika Mashariki yaani Single Custom Territory ili kuwa na uwezo wa kupata huduma kwa kutumia mfumo huo pindi matumizi yatakapoanza mapema ili kuondoa usumbufu utakaoweza kutokea”. Alisema Bw. Kabisi
Bw. Kabisi aliongeza kuwa mpaka sasa ni makampuni mawili (2) ya mawakala waliojisajili mpaka sasa.
Aidha Bw. Kabisi alisema kuwa mawakala wa forodha hawana budi kuendelea kuwa waamifu ili waendelee kuongoza katika makusanyo ya fedha kwa mwaka ujao ambapo kwa mwaka huu wamechangia kwa asilimia 40 ya mapato ya serikali.
Naye Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha (TAFA) Bw. Stephen Ngatunga alisema kuwa wataendelea kushirikiana na Mamlaka la Mapato Tanzania (TRA) katika kuhakikisha wanaifanya idara ya forodha inafanya vizuri katika makusanyo ya fedha.
Pia Bw. Ngatunga aliitaka serikali kuendelea kushughulikia changamoto mabalimbali zinazoikabili idara hiyo ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu na kuendelea kuongoza katika makusanyo ya mapato ya serikali.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete afungua Kongamano la Nne la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu-juni 24, 2015
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akifungua Kongamano la Nne la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwenye
ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
leo Juni 24, 2015
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata
maelezo kutoma kwa Profesa Nerey Mvungi wa Chuo Kikuu Cha Dar es salaam
juu ya Ubunifu wake wa kutengeneza mfumo wa kidigitali wa kusaidia
kupambana na ajali barabarani kabla hajafungua Kongamano la Nne la
Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa
Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Juni 24, 2015
Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akipata maelezo kutoma kwa kijana Godfrey Magila wa Magilatech Company
Ltd. juu ya Ubunifu wake wa kutengeneza mfumo wa teknolojia ya
mawasiliano rahisi kabla hajafungua Kongamano la Nne la Sayansi,
Teknolojia na Ubunifu kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es salaam leo Juni 24, 2015
PICHA NA IKULU
WAZIRI BERNARD MEMBE AKUTANA NA WASANII WA FILAMU MKOA WA MOROGORO
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
akizungumza na wasanii wa tasnia ya filamu mkoa wa Morogoro jana, wakati
alipokuwa mkoani humo kwa ajili ya kutafuta wadhamini ili aweze kuwania
urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
(CCM), ambapo wanaCCM zaidi ya 950 walimdhamini.
Picha zote na John Badi
Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe
akiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa tasnia ya filamu mkoa wa
Morogoro jana, wakati alipokuwa mkoani humo kwa ajili ya kutafuta
wadhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi
ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo wanaCCM zaidi ya 950 walimdhamini.
Subscribe to:
Posts (Atom)