WAZIRI WA HABARI,VIJANA UTAMADUNI NA MICHEZO AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA SHULE ZA SEKONDARI JIJINI DAR ES SALAAM.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella
Mukangara (wa kwanza kushoto) na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom (wa
pili kushoto), Salum Mwalim,Wakikabidhi baadhi ya vifaa vya michezo kwa
mwanafunzi wa shule ya sekondari Mnazi Mmoja, Shaha Bakari(kulia)Vifaa
hivyo vilivyotolewa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya mashindano
yatakayoanza hivi karibuni yatahusisha shule za sekondari kumi na
mbili(12)za jijini Dar es Salaam.Akishuhudia makabidhiano hayo wapili
kutoka kushoto ni Mwalimu michezo wa shule hiyo, Alex Dumien.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella
Mukangara (kushoto)Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania (wa pili
kushoto), Salum Mwalim wakikabidhi vifaa vya michezo kwa mwanafunzi wa
shule ya sekondari Mugabe, Juma Shabani (kulia)Vifaa hivyo vimetolewa na
Vodacom Tanzania kwa ajili ya mashindano yatakayo anza hivi karibuni na
kuhusisha shule za sekondari kumi na mbili(12) za jijini Dar es
Salaam.Akishuhudia wapili kutoka kushoto ni Mwalimu wa shule hiyo,
Farouk Kaburwa.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella
Mukangara(wapili toka kushoto)akishuhudia Meneja Uhusiano wa Nje wa
Vodacom Tanzania(kulia) Salum Mwalim akikabidhi mfano wa hundi ya
Milioni moja(1,000,000) kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania
(BMT), Henry Lihaya (wa pili kushoto) fedha hizo zitatumika katika
maandalizi wakati wa mashindano ya michezo shule za sekondari za Mkoa wa
Dar es Salaam.Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,Prof. Elisante
Ole Gabriel.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mh. Dk. Fenella
Mukangara (wa pili kushoto)akikabidhi moja ya vifaa vya michezo kwa
mwanafunzi wa shule ya sekondari Kibasila, Simon Nungu (kulia)Vifaa
hivyo vya michezo vilivyotolewa na Vodacom Tanzania kwa ajili ya
mashindano ya michezo mbalimbali itakayoanza hivi karibuni na
kuzihusisha shule za sekondari kumi na mbili(12)za jijini Dar es
Salaam.Wanaoshuhudia makabidhiano hayo kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa
wizara hiyo, Prof. Elisante Ole Gabriel, Meneja Uhusiano wa Nje wa
Vodacom Tanzania(wa tatu kushoto),Salum Mwalim.