TAASISI YA AGRI-BUSNESS MEDIA INNITIATIVE YA JIJINI MWANZA YAWAHIMIZA VIJANA KUJIKITA KWENYE KILIMO

January 22, 2017
Mkurugenzi wa Taasisi ya Agri-Busness Media Innitiative In Tanzania (AMI-TZ) ya Jijini Mwanza, Deborah Mallaba, akikagua shamba la hekari mbili la taasisi hiyo ambalo lina mkusanyiko wa matunda na mbogamboga za aina mbalimbali, lililopo Igombe Ziwani, Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza.

Na Binagi Media Group
Taasisi ya AMI-TZ inajihusika na kilimo cha matunda na mbogamboga kama vile matikiti maji, nyanya, bamia, nyanya, pilipili mbuzi na aina nyinginezo nyingi.

Baada ya mavuno, taasisi hiyo hufanya usindikaji wa mazao kwa ajili ya kuwafikishia wateja wake majumbani, maofisini na mengine huuzwa moja kwa moja shambani.

"Baadhi ya vijana ukiwaeleza suala la kilimo wanakuona kama vile umepitwa na wakati lakini wale wanaojitambua wameingia kwenye kilimo na kinawalipa. Hivyo niwahamasishe watumie muda wao vizuri kwa kujishughulisha kwenye kilimo hivyo wasisubiri tu kazi za maofisini". Anasisitiza Deborah Mallaba, Mwanahabari na Mkurugenzi wa Taasisi ya AMI-TZ.

Mallaba anawasisitiza viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya Kata hadi Wilaya, kuongeza jitihasa za kuwakusanya vijana pamoja na kuwapatia mitaji ikiwemo pembejeo ili wajikite kwenye kilimo maana kilimo ni biashara na kinalipa ambapo pia hatua hio itasaidia kupunguza vijana mitaani.

"Napenda kuwaambia akina dada waamuke maana si vyema kuzurura tu wakisema hakuna ajira. Mfano mimi nimeanza kujiwekea kipato changu kupitia kilimo na nataka kuwa mafano bora kwa vijana wengine". Anasisitiza Aneth Shosha ambaye ni Afisa Masoko wa taasisi ya AMI-TZ huku akiwakaribisha vijana wengine kwenye taasisi hiyo ili wajifunze zaidi kuhusu kilimo.
Aneth Shosha ambaye ni Mratibu/ Afisa Masoko wa Taasisi ya Agri-Busness Media Innitiative In Tanzania (AMI-TZ), akimwagilia maji kwenye shamba la bamia
Wachapa kazi wakichakarika
Kilimo cha nyanya
Mfumo wa umwagiliaji kwa kutumia mashine kutoka Ziwa Victoria ndio hutumika kwenye shamba hili. 
Kwa msaada na ushauri, piga simu nambari 0754 99 66 13

RAIS WA UTURUKI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

RAIS WA UTURUKI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

January 22, 2017
WQA
 Rais wa  Uturuki,  Mheshimiwa  , Recep Tayyip Erdogan akiongozana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam kwa ziara rasmi Januari 21, 2017.Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WQQQ
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   na Rais wa Uturuki, Mheshimiwa Recep Tayyip Erdogan  aliyefuatana na  mkewe, Mheshimiwa Emine Erdogan (kulia) wakifuhia ngoma kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage jijini Dar es salaam baada ya Rais huyo  kuwasili kwa ziara rasmi nchini Januari 21, 2017. Mheshimiwa Majaliwa alimpokea Rais huyo kwa niaba ya Rais John Magufuli. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini leo jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupokelewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na niaba ya Mheshimiwa Rais. Dkt. John Magufuli.

Rais huyo ameambatana na mkewe Mama Emine Erdogan pamoja na Mawaziri watatu ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mevlüt ÇavuÅŸoÄŸlu, Waziri wa Uchumi Mheshimiwa Nihat  Zeybekekci na Waziri wa Nishati na Maliasili Mheshimiwa Berat Albayrak
.
Pia Rais huyo ameambatana na wafanyabiashara wapatao 85 wa nchi hiyo.


IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU
SIMBA YATINGA 16 BORA YA FA CUP,YAILAZA POLISI DAR

SIMBA YATINGA 16 BORA YA FA CUP,YAILAZA POLISI DAR

January 22, 2017
PAST
Klabu ya Simba imewafuata wapinzani wao Yanga katika hatua ya 16 bora ya Michuano ya Kombe la Azam Sport Federation baada ya kupata ushindi wa magoli 2-0 kwenye mechi yake dhidi ya Police Dar mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Uhuru, Dar.
Athanas Pastory aliifungia Simba bao la kwanza kipindi cha kwanza lakini Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’ akaifungia Simba bao la pili kipindi cha pili.
IMG-20170122-WA0053
Simba inasonga mbele katika hatua inayofata baada ya kuifunga Polisi Dar es Salaam na kuiondosha kwenye mashindano hayo ambayo mshindi wake atapata fursa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye kombe la shirikisho Afrika.
Matokeo ya mechi nyingine za kombe la FA
Mbeya Kwanza 1-2 Tanzania Prisons
Toto Africans 2-0Mwadui FC
Ruvu Shooting 1-2 Kiluvya United

MKUU WA WILAYA YA MKURANGA FILBERTO SANGA AFUNGUA RASMI LIGI YA MBUNGE (ULEGA CUP)

January 22, 2017
Na Emanuel Masaka, Globu ya Jamii

LIGI ya Mbunge wa Jimbo la Mkuranga  (Ulega Cup) imefunguliwa  rasmi leo kwa kuzikutanisha timu za Kipalang'anda  kombaini Fc na Mkuranga kombaini uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga.

Mashindano  hayo yamefunguliwa  na mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Firbato Sanga  ukishuhudiwa na Mbunge wa Jimbo hilo Abdallah Ulega, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga,Juma Abed pamoja na baadhi ya madiwani wanaounda halmashauri hiyo.

Michuano hiyo ambayo ilianzia ngazi ya Vijiji ilishirikisha timu  125 na  baadae kuchujwa na kubakia timu 25 ambazo zimeingia ngazi ya wilaya na mshindi wa ligi hiyo ndio atakuwa bingwa wa wilaya. 

Akizungumza  na wachezaji wa timu hizo katika ufunguzi wa michuano hiyo Mkuu wa Wilaya hiyo Firbato Sanga  alisema michezo ni udugu na ujirani mwema hivyo aliwatakia michezo mwema.

Akizungumzia michuano hiyo Mbunge wa jimbo hilo Abdallah Ulega amesema kuwa ni matarajio yake michuano hiyo itakwenda vyema  na lengo lake kubwa nikuona wanapata vijana wenye vipaji na watakaoweza kuipaisha Mkuranga.

"Nimatarajio yangu mambo yatakwenda kama nilivyopanga na kama mnavyoona wenyewe waandishi wa habari  vijana wa kutoka Mkuranga ndio wanaocheza "alisema Ulega

Amesema  tangu awali alisha kataa timu hizo kukodi watu Kutoka nje ya Mkuranga na anashukuru Mungu hayo yamezingatiwa na katika michuano hiyo mshindi ndio atakuwa bingwa wa Wilaya.

Amesema kuwa ana matumaini makubwa kwamba kupitia ligi hiyo watapatikanika vijana wenye uwezo ambao wataweza kuchukuliwa  na timu kubwa.

Aidha amesema kuwa michezo ni Afya ,ajira,na upendo kwani kupitia mashindano hayo watakuwa wametengeneza ujirani mwema hivyo watumie fursa hiyo kudumisha Umoja na mshikamono miongoni mwao.

Mchezo huo ulimalizika kwa goli moja lililofungwa na mchezaji wa timu ya Mkuranga Kombaini,Abdallah Mohamed  katika dakika ya kumi kipindi cha kwanza.

 Mbunge wa Jimbo la Mkuranga,Abdallah Ulega  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika ufunguzi wa Ligi ya Mbunge wa Jimbo la Mkuranga  (Ulega Cup)  uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga mkoani Pwani

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,Firbato Sanga akizungumza  na wachezaji wa timu  za Kipalang'anda  kombaini Fc na Mkuranga kombaini katika ufunguzi wa Ligi ya Mbunge wa Jimbo la Mkuranga  (Ulega Cup)  uliofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mkuranga mkoani Pwani.

ALHAJ ALI HASSAN MWINYI AWATAKA WATANZANIA KUWA NA TABIA YA KUENDELEZA YALIYO MEMA.

January 22, 2017


Rais mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi amewataka watanzania kuwa na tabia ya kuyafanyia muendelezo yale mema wanayoyafanya, kama walivyofanya kampuni ya NIDA TEXTILES kusherekea kumbukumbu ya mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W).
Akizungumza  katika hafla hiyo ya Maulid iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam Alhaji Mwinyi amesema  kuwa Mtume Muhammad (S.A.W) alikuwa akifunga kila siku ya Jumatatu ikiwa ni ishara ya kusherekea siku aliyozaliwa.
 Hivyo ni vyema kuiga mfano huo wa kufanya matendo mema kwa kuyarudia mara kwa mara na kuyadumisha, huku akipongeza uongozi wa NIDA kwa kuwaalika na kusherekea pamoja kwani amejifunza mengi kupitia mawaidha yaliyotolewa na viongozi wa dini waliohutubia akiwemo Sheikh Ally Basaleh.
Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali akiwemo Makamu wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Gharib Bilal, Naibu Waziri Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Suleiman Jafo, Naibu Waziri Wizara ya Afya Hamis Kigwangala, Waziri wa zamani wa Ulinzi Profesa Juma Kapuya, Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahimu Lipumba, Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega. Viongozi wa dini waliokuwepo ni pamoja na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum na Kadhi Mkuu wa Tanzania Abdallah Mnyaa.
 Rais mstaafu wa awamu ya pili  Alhaj Ali Hassan Mwinyi akizungumza na  viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali juu ya watanzania  kuyafanyia muendelezo wa yale mema kama walivyofanya kampuni ya NIDA TEXTILES kusherekea kumbukumbu ya mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W). leo jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib  Bilal, akizungumza na  viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali katika kusherekea kumbukumbu ya mazazi ya Mtume Muhammad (S.A.W). leo jijini Dar es Salaam.
 Shehe Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam,Sheikh Alhadi Mussa Salim akizungumza machache katika hafla hiyo ya Maulid iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib akisalimiana na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Dk. Hamisi Kigwangalla leo jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib akisalimiana na  Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, Seleman Jaffo  leo jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya waumini wakiwa katika hafla hiyo ya Maulid iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
 Sehemu ya viongozi mbalimbali  wa dini wakiwa katika hafla hiyo ya Maulid iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akutana na mamlaka za udhibiti na utoaji leseni.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akutana na mamlaka za udhibiti na utoaji leseni.

January 22, 2017
EVO
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya marekebisho ya wepesi wa kufanya shughuli nchini, kushoto kwa waziri ni Katibu Mkuu biashara na uwekezaji Mhe. Prof. Adolf Mkenda, Mwenyekiti wa kamati ya kuboresha mazingira ya biashara Dkt. John Mduma, kulia kwa waziri ni Katibu tawala Kibaha Ndg. Anatory Mhango.
EVO 1
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
EVO 2
Katibu Mkuu Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
EVO 3
Wadau kutoka taasisi mbalimbali za serikali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
EVO 4
Wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
EVO 5
Wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
………………
Waziri wa viwanda, Biashara na uwekezaji akutana na kamati ya kuboresha ya mazingira ya biashara ambayo inahusisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali katika wizara zote, TBS, EWURA, SUMATRA, TRA, OSHA, WMA, NCC,  n.k na kujadili changamoto mbalimbali ambazo ni vikwazo katika wepesi wa kufanya shughuli.
Waziri amehimiza wataalamu hawa kujadili changamoto na kutoa mapendekezo ya namna ya kuondoa kero hizo ili kuboresha urahisi wa kufanya shughuli nchini Tanzania na kuvutia wawekezaji.
Waziri amehimiza ulipaji wa kodi ili kuleta maendeleo ya watu, kwani kwa takwimu Tanzania ni ya 154 kati ya nchi 190 hivyo kuhimiza wafanyabiashara wote kuwa na Tin namba na pia kulipa kodi.
Mkutano huu umefanyika jumamosi tarehe 21/1/2017 ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
NAIBU WAZIRI MASAUNI ATEMBELEA GEREZA LA RUANDA JIJINI MBEYA

NAIBU WAZIRI MASAUNI ATEMBELEA GEREZA LA RUANDA JIJINI MBEYA

January 22, 2017


Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiongozana na Mkuu wa Jeshi la Magereza jijini Mbeya Kamishna Msaidizi Paul Kajida (kulia) wakati alipowasili kukagua shughuli za uzalishaji thamani za ndani na sabuni katika gereza la Ruanda .Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Kiwanda cha Gereza la Ruanda ASP Michael Kuga, akisoma taarifa ya hali ya uzalishaji wa sabuni na thamani za ndani mbele ya Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa shughuli za maendeleo zinazofanyika katika magereza yaliyopo jijini Mbeya.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto) akipata maelezo juu ya utengenezwaji wa kiti kinachotengenezwa na wafungwa wa gereza la Ruanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (wakwanza kulia waliokaa), akiangalia picha za thamani za ndani zinazotengenezwa na wafungwa wa Gereza la Ruanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Wengine waliokaa baada ya Naibu Waziri ni Mkuu wa Kiwanda hicho,ASP Michael Kuga ,Kamanda wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Jesuald Ikonko na Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya Emmanuel Lukula.Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza alipotembelea Kiwanda cha sabuni zinazotengenezwa na wafungwa wa gereza la Ruanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Wanaomsikiliza ni Mkuu wa Kiwanda() na Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Paul Kajida. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akiangalia moja ya sabuni zinazozalishwa na wafungwa wa Gereza la Luanda wakishirikiana na wataalamu wa Jeshi la Magereza.Kulia ni Mkuu wa Kiwanda hicho.Naibu Waziri yupo jijini Mbeya kwa ziara ya kikazi.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).


IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

SIMIYU KUONGOZA MAPINDUZI YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI NCHINI

January 22, 2017


**sasa uzalishaji mwaka mzima

**Mtaka asema ni aibu Simiyu kuomba chakula wakiwa na maji tele Busega
**Aahidi kushiriki kuchimba mitaro na wananchi

MWANJALE MCHEZAJI BORA WA DESEMBA 2016

January 22, 2017
Sentahafu wa Simba, Method Mwanjale amechaguliwa kuwa mchezaji bora Desemba wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2016/2017. 
Beki huyo wa kati, aliwashinda kiungo mshambuliaji wa Yanga, Haruna Niyonzima na beki Yakubu Mohamed wa Azam FC. Mwezi Desemba ulichezwa raundi tatu za Ligi hiyo, huku Simba ikicheza mechi mbili ugenini na moja nyumbani. Raundi hizo ni ya 16, 17 na 18.
Mwanjali aliiongoza Simba kushinda mechi zote tatu, hivyo timu yake kupata ushindi wa asilimia 100 kwa kunyakua pointi zote tisa, na kubaki katika nafasi yao ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi, nafasi ambayo walikuwa nayo wakati wanaingia raundi ya 16.
Pia katika raundi hizo tatu ambapo Simba haikufungwa bao hata moja, Mwanjali alicheza dakika zote 270, na bila kuonyeshwa kadi yoyote. Alichangia kwa kiasi kikubwa katika mafanikio ya timu yake huku akiongoza safu ya ulinzi.
Kwa kushinda tuzo hiyo ya mchezaji bora, Mwanjali atazawadiwa kitita cha sh. 1,000,000 (milioni moja) na wadhamini wakuu wa Ligi hiyo Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania.
Wachezaji wengine walioshinda tuzo za mchezaji bora kwa msimu wa 2016/2017 hadi sasa ni John Raphael Bocco wa Azam (Agosti), Shiza Ramadhan Kichuya wa Simba (Septemba), Simon Happygod Msuva wa Yanga (Oktoba), na Rifati Hamisi wa Ndanda (Novemba).
..…………………………………………………………………………........................
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)   

KANISA LA EAGT LUMALA MPYA LAFURAHISHWA NA HUDUMA YA KWAYA YA EAGT KAANGAYE

January 22, 2017
Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la EAGT Kaangaye kutoka Nyakato Jijini Mwanza, leo wamefanyika Baraka kubwa baada ya kuhudumu vyema katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu la Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza.

Waumini wengi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya wamefurahishwa na huduma ya kwaya hiyo. Pongezi kubwa ziwaendee Mwenyekiti wa kwanya hiyo, Abednego Magesa na Mchungaji Samson Mniko kwa malezi mema yaliyofanikisha wanakwaya hao kumtumikia Mungu kwa bidii kubwa.
Na Binagi Media Group
Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la EAGT Kaangaye lililopo Nyakato Jijini Mwanza, wakihudumu kwa bashasha kubwa kwenye ibada za hii leo jumapili katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola, akisisitiza jambo kwenye ibada za hii leo jumapili. Ibada ya kwanza kila jumapili huanza saa 12:00 asubuhi, ibada ya pili saa 01:00 asubuhi na ibada ya tatu saa 04:30 asubuhi.
Waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, wakimsikiliza Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Moses Kulola
Waumini wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo nyuma ya Soko Kuu Sabasaba Ilemela Jijini Mwanza, wakifuatilia ibada za leo jumapli
Mahubiri na Mafundisho ya neno la Mungu kutoka Kanisa la EAGT Lumala Mpya pia yanarushwa kupitia runinga ya Star Religion inayopatikana kwenye kisimbuzi cha Continental ambapo visimbuzi hivyo vinapatikana kanisani hapo kwa punguzo kubwa.
Picha na Craty Cleophace @EAGT Lumala Mya