November 16, 2016
Dkt.Leonald Subi

Na George Binagi-GB Pazzo
Mganga Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonald Subi, amewahimiza wananchi kuwa na desturi ya kupima afya zao mara kwa mara hususani kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza ili kuepukana na madhara yake ikiwemo vifo vinavyofikia asilimia 27 nchini.

Dkt Subi aliyasema hao wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya bure ya uchunguzi wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi mkoani Mwanza, inayofanyika kwa siku mbili kuanzia jana katika Uwanja wa Furahisha, Vituo vya afya Igoma, Karumbe na Makongoro.

Aidha Dkt.Subi aliwahimiza wanajamii kubadili mfumo wa maisha kwa kuzingatia kanuni za afya ili kuepukana na madhara yatokanayo na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambayo ni pamona na kansa, presha pamoja na kisukari.

“Magonjwa haya yanatokana na namna ya maisha tunavyoishi ikiwemo kutokufanya mazoezi, ulaji wa chakula usiozingazi kanuni, ulevi, uvutaji wa sigara, kuwa na wapenzi wengi na kutokuzingatia kanuni za afya kwa ujumla”. Alisema Dkt.Subi.

Kampeni ya uchunguzi wa saratani ya matiti na mlango wa kizazi inaratibiwa na Chama cha Madaktari Wanawake nchini MEWATA katika mikoa ya Mwanza, Iringa na Mbeya kwa lengo la kuhamasisha wananchi kupata huduma mapema kwani magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo saratani hutibika ikiwa mgonjwa ataanza matibabu mapema.
Tazama HAPA Picha za Uzinduzi
November 16, 2016

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi jana Novemba 15, 2016 alimtembelea Mstahiki Meya wa Jiji la Seongnam, Jae-myung Lee kumshukuru kwa namna ambavyo ameipokea timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kwa jina la Serengeti Boys.
Serengeti Boys walioko Korea kwa michezo ya kirafiki ya kimataifa ambako Jiji la Seongnam ni mshirika wa klabu ya Seongnam FC ambao ndio wenyeji wa timu yetu ya vijana ambayo ilifanya michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa.

Katika mazungumzo kocha huyo, Meya Jae-myung Lee aliiakikishia TFF kuwa jiji lake litaendelea kushirikiana na shirikisho katika kuendeleza mpira wa vijana wakike na wakiume.

Katika kumtembelea Meya huyo, Rais Malinzi aliambatana na Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi na benchi nzima la ufundi, linaloongozwa na Kocha Bakari Nyundo Shime na msaidizi wake, Muharami Mohammed Sultan pamoja na Mshauri Mkuu wa Maendeleo ya soka la vijana, Kim Poulsen.

Baadaye jioni ya Novemba 15, 2016 Rais Malinzi alikutana na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Korea Kusini (KFA), Chung Mong-Gyu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Hyundai.

Rais wa KFA Mong-Gyu naye alihakikishia TFF kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Korea litasaidia kuendeleza soka la vijana Tanzania sambamba na kusaidia mafunzo ya makocha..
 Sport Azam U-20 kuanza na Mbao Ligi ya Vijana kesho

Sport Azam U-20 kuanza na Mbao Ligi ya Vijana kesho

November 16, 2016

Team: 
Azam B
TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam U-20’, kesho saa 8.30 mchana inatarajia kuanza kutupa karata ya kwanza kwenye Ligi ya Taifa ya Vijana kwa kukipiga dhidi ya Mbao katika Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, mkoani Kagera.
Azam U-20 iliyojiandaa vema kuelekea michuano hiyo, imepangwa kwenye kituo cha Bukoba chenye timu nane kinachounda Kundi A, kikiwa na timu nyingine za Kagera Sugar, Toto African, African Lyon, Mwadui, Stand United na Yanga.
Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Kocha Mkuu wa kikosi hicho, Idd Cheche, alisema kuwa wamejipanga vilivyo kuanza vema michuano hiyo kwa kupata ushindi kesho.
“Kikosi changu kipo kamili kwa ajili ya michuano hiyo, kimefanya maandalizi mazuri na malengo yetu makubwa ni kumaliza nafasi ya kwanza kwenye kituo hiki na hatimaye kuibuka mabingwa,” alisema.
Cheche aliwatoa hofu mashabiki wa Azam FC kwa kuwaaambia kuwa wakae mkao wa kula kutokana na ubora wa timu yao na ipo vizuri kwa ajili ya kushindana na hatimaye kutwaa ubingwa.
Mabingwa hao wa kihistoria wa michuano ya awali ya vijana ya Uhai Cup, wanatarajia kung’arishwa vilivyo na baadhi ya mastaa wake wakiwemo mshambuliaji Shaaban Idd na kiungo Masoud Abdallah, ambao pia wamepandishwa kucheza kwenye timu ya wakubwa ya kikosi hicho.
Tayari mchezo wa ufunguzi wa kituo hicho umefanyika jana, ambapo ilishuhudiwa Kagera Sugar ikitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Yanga huku leo Jumatano ukitarajiwa kupigwa mtanange mwingine utakaohusisha watani wa jiji la Shinyanga, Stand na Mwadui.

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUCHANGAMKIA NYUMBA ZA BEI NAFUU ZINAZOJENGWA NA SERIKALI

November 16, 2016
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ujenzi  wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC) Fredy Msemwa (katikati), akitoa taarifa kwa Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki (kushoto), kuhusu mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa Umma zinazojengwa Gezaulole Kigamboni jijini Dar es Salaam. Waziri Kairuki alikuwa katika ziara ya siku moja kutembelea miradi ya ujenzi ya Taasisi hiyo iliyopo Dar es Salaam. Kulia ni Mjumbe wa Bodi ya WHC, Daud Msangi.
 Mjumbe wa Bodi ya WHC, Daud Msangi akitoa taarifa kwa 
Waziri Kairuki.
 Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki (kushoto), akizungumza na watendaji wa mradi huo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ujenzi  wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC) Fredy Msemwa (kushoto), akimuelekeza Waziri Kairuki jinsi ujenzi wa magorofa unavyoendelea katika mradi huo wa Gezaulole. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, Mjumbe wa Bodi ya WHC, Daud Msangi na Kaimu Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi Robert Wambura.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki (katikati), akikagua nyumba zinazojengwa na Taasisi ya Ujenzi  wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC) katika mradi ya Gezaulole Kigamboni Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa WHC, Fredy Msemwa na kulia kwake ni Mjumbe wa Bodi ya WHC, Agnes Meena.
 Waziri Kairuki (kushoto), akimuelekeza jambo Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi Robert Wambura wakati wa ziara hiyo.
 Wafanyakazi wa WHC, wakijadiliana jambo kwenye ziara hiyo.
 Ukaguzi wa mradi huo ukiendelea.

Msanifu Majengo kutoka Onspace Consult. Co.Ltd, Edmund Kahabuka (kulia), akitoa taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa Magomeni kwa Waziri Kairuki.
 Mwonekano wa ujenzi wa magorofa yanayo jengwa katika mradi huo wa Gezaulole Kigamboni.
 Mwonekano wa nyumba za chini zinazojengwa katika mradi huo.
 Mwonekano wa jengo la ghorofa la mradi huo baada ya kukamilika ujenzi wake.

Na Dotto Mwaibale

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Angella Kairuki amewataka watumishi wa Umma kuchangamkia nyumba za bei nafuu zinazojengwa na Serikali ili kuondokana na changamoto ya makazi.

Katika hatua nyingine Kairuki ameiagiza Taasisi ya Ujenzi  wa Nyumba za Watumishi wa Umma (WHC), kuzingatia ujenzi utakaokidhi mahitaji ya watumishi wenye mishahara ya kima cha chini wakiwemo walinzi, wahudumu, madereva na makatibu muhtasi.

Kairuki aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipofanya ziara kwenye mradi wa nyumba za WHC, zilizopo Kigamboni, Magomeni na Bunju jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuangalia ujenzi unavyoendelea.

Alisema asilimia 80 ya watumishi wa serikali wana mishahara midogo hivyo endapo nyumba hizo zitauzwa kwa gharama kubwa hawataweza kuzinunua, na azma ya serikali ni kuwa na nyumba bora zenye gharama nafuu kwa watumishi wake.

"Kwa asilimia 80 ya watumishi wa umma kiwango watakachoweza kumudu kununua nyumba hizo hakiwezi kuzidi sh. milioni 20 kwa miaka 18, Tujitahidi kupunguza gharama kwa kadiri inavyowezekana ili kutoa fursa kwa watumishi wa umma wa kipato cha chini kuweza kupata nyumba za bei nafuu za kuishi" alisema.

Waziri huyo alisema azma ya serikali ni kuhakikisha wanaboresha na kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi wa umma ambazo zinatakiwa ziwe sio chini ya nyumba 10,000.

Aliwataka WHC, kuwa na mpango mkakati wa kuweza kujenga nyumba zaidi ya 10,000 kwa mwaka ili kuwafikia watumishi wengi zaidi hasa waliopo vijijini.

Alisema katika manunuzi ya nyumba hizo serikali inaangalia jinsi ya kupunguza kodi ya ongezeko la thamani (VAT), ili kumpunguzia mtumishi gharama.

Nyumba hizo zinazojengwa kwa mkopo kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na Pensheni zitauzwa kulingana na ukubwa wa nyumba husika kwani ile ya chumba kimoja itauzwa kwa sh.milioni 35, vyumba viwili milioni 75 na vyumba vitatu itauzwa sh.milioni 91.

Mkurugenzi Mtendaji wa WHC, Fredy Msemwa alisema katika eneo la Kigamboni lenye ekari 24 wanatarajia kujenga nyumba 790, mradi unaotekelezwa kwa awamu mbili.

Alisema katika nyumba za awamu ya kwanza wapo katika hatua ya umaliziaji ambapo nyumba hizo zinatarajia kukamilia Februari mwakani.

Nyumba hizo pia zinajengwa katika maeneo mbalimbali nchini, ambazo gharama zake ni kati ya sh. milioni 33 mpaka sh. milioni 190 pamoja na VAT.

Mwenyekiti wa Bodi ya WHC, Daud Msangi alielezea changamoto za mradi huo kuwa waliomba nyumba hizo zisiwe na vat, kupata viwanja bure na vya bei rahisi pamoja na serikali kuangalia huduma za maji, umeme na barabara.

Nyumba nyingine zimeanza kujengwa katika mikoa ya Morogoro, Mwanza, Dodoma, Mtwara, Lindi, Mbeya, Shinyanga, Singida na Arusha huku katika baadhi ya mikoa hiyo kukiwa na viwanja vya ujenzi huo.


TIGO YAZINDUA 4G LTE SAME MKOANI KILIMANJARO

November 16, 2016
  Katibu Tawala wa Wilaya ya Same Sospeter Mabenga, akihutubia wakati wa kuzindua mtandao wenye kasi wa 4G LTE, hafla ambayo ilifanyika jana mjini Same.

 Wafanyakazi wa Kampuni ya simu za mononi ya Tigo wakishuhudia uzinduzi wa mtandao wa 4G LTE, uliofanyika jana mjini Same.

Baadhi ya wakazi wa mji wa Same wakisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi, Katibu Tawala wa Wilaya ya Same Sospeter Mabenga 

   Katibu Tawala wa wilaya ya Same Sospeter Mabenga (kulia) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi wa mtandao wa 4G LTE uliofanyika jana mjini Same, wengine kutoka kushoto ni wafanyakazi wa kampuni ya simu za mononi ya Tigo Tanzania, Mwajuma Mshana, Patrick Utouh na Vitalis Stephen.

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini George Lugata akimkabidhi mgeni rasmi zawadi ya line mpya ya 4G LTE kwa ajili ya matumizi yake