CHUO CHA KODI KUWAJENGEA UWEZO MAWAKALA WA FORODHA ZANZIBAR

January 28, 2018
Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB) Omar Hussein Mussa wakibadilishana hati za makubaliano ya ushirikiano katika kuwajengea uwezo wanachama wa ZFB.

Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar Omar Hussein Mussa wakizungumza na wajumbe wa Kamati ya Makubaliano kutoka Chuo cha Kodi (Kulia) na Zanzibar (kushoto) kabla ya kusaini hati za makubaliano katika chumba cha mikutano ITA.


Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB) Omar Hussein Mussa (wa pili Kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala Tanzania (TAFFA) Stephen Ngatunga (wa kwanza kulia) katika picha ya pamoja na wajumbe wa kamati ya ushirikiano mara baada ya kusaini makubaliano ya kuwajengea uwezo mawakala wa Forodha Zanzibar. (PICHA ZOTE NA OLIVER NJUNWA).

…………………………………………………………………………………..

Na Oliver Njunwa- Dar es Salaam

Chuo cha Kodi (ITA) pamoja na Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar (ZFB), vimeingia katika makubaliano ya kushirikiana katika kuwajengea uwezo Mawakala wa Forodha Zanzibar.

Akizungumza mara baada ya hafla fupi ya kutiliana saini makubaliano hayo, iliyofanyika hivi karibuni katika Chuo cha Kodi jijini Dar es salaam, Mkuu wa Chuo hicho Prof. Isaya Jairo amesema kwamba, makubaliano hayo ni muhimu kwani kila upande una watalaam wa kutosha kuwasaidia Mawakala wa Forodha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“ITA inajivunia utaalam wake wa kufundisha na ZFB ina utaalamu katika masuala ya kiforodha. Kwa hiyo wote kwa pamoja tutashirikiana ili malengo ya makubaliano haya yaweze kufikiwa”, alisema Prof. Jairo.

Prof. Jairo aliongeza kuwa, katika makubaliano hayo, Chuo cha Kodi kitatoa mafunzo ya muda mfupi na utaalamu wa masuala ya forodha kwa ZFB ili kuhakikisha kuwa kunakuwa na Mawakala wa Forodha wanaofanya kazi kwa weledi.

Mkuu wa Chuo cha Kodi pia amesema kwamba lengo la vyuo sio kupata fedha bali kutoa wataalamu wa kutosha ambapo uwezo wa Chuo hupimwa kwa idadi ya wanafunzi wanaohitimu na aina ya sifa walizonazo.

Aidha, Prof. Jairo ameiomba ZFB kulinda hadhi ya jina la Chuo cha Kodi kwani kina jina zuri kutokana na uzoefu wake wa kutekeleza makubaliano ya ushirikiano na taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi.

“ITA ina makubaliano na Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) pamoja na Bodi ya Mapato ya Zanzibar (ZRB) na kwa nchi za nje ina makubaliano na Malawi, Zambia, Botswana na iliisadia Sudan Kusini kuanzisha Mamlaka ya Mapato nchini humo”, alisema Prof. Jairo.

Makubaliano hayo yamefanyika katika Chuo cha Kodi Dar es salaam Ijumaa tarehe 26 Januari 2017 na kutiwa saini kati ya Mkuu wa Chuo cha Kodi Prof. Isaya Jairo na Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar Omar Hussein Mussa na kushuhudiwa na Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) Stephen Ngatunga.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar ZFB, Omar Hussein Mussa amesema kwamba makubaliano hayo ni msingi mzuri wa kupata Mawakala wa Forodha wenye weledi na hivyo kupunguza changamoto zinazojitokeza katika tasnia ya uwakala wa forodha.

“Makubaliano haya ni jambo jema na yatakuwa endelevu kwa kuwa sisi tuko tayari kuhakikisha yanaleta mabadiliko katika utendaji wa mawakala wetu wa Forodha”, alisema Bw. Mussa.

Kwa upande wake Rais wa Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania Stephen Ngatunga ambaye alihudhuria hafla hiyo, amekipongeza Chuo cha Kodi pamoja na ZFB kwa makubaliano hayo muhimu na kusema kwamba anafarijika kuona jitihada zake zimefanikiwa kwani yeye alichangia kufanikisha suala hilo.

Katika makubaliano hayo, Chuo cha Kodi kitasimamia kiwango cha taaluma itakayotolewa kwa kuzingatia vigezo vya Baraza la Taifa la Mafunzo ya Ufundi (NACTE) na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU). Aidha, Chuo hicho pia kitasimamia udahili, mitihani, kutoa walimu na vyeti baada ya kuhitimu wakati Chama cha Mawakala wa Forodha Zanzibar kitapokea ada, kutoa wanafunzi, madarasa pamoja na vitendea kazi.

Chuo cha Kodi ni sehemu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania ambacho kilipata ithbati kutoka Baraza la Taifa la Mafunzo ya Ufundi kutoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa watumishi wa TRA pamoja na wadau mbalimbali katika fani za Kodi na Forodha.
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATETA NA MAHABUSU GEREZA KEKO MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA, DKT. JUMA MALEWA ATETA NA MAHABUSU GEREZA KEKO MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI

January 28, 2018
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiwasili katika Gereza la Mahabusu Keko jijini Dar es salaam katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo leo Januari 28, 2018 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Jeshi la Magereza ni moja ya wadau muhimu katika sekta ya Sheria hapa nchini.  
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah alipowasili katika ziara yake ya kikazi kukagua gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini. Wengine ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo.
????????????????????????????????????
 Mkuu wa Gereza la Mahabusu Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah akitoa taarifa fupi mbele ya Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa kabla ya kumkaribisha kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko(hawapo pichani).
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akiongea na Mahabusu wa Gereza Keko(awapo pichani) leo Januari 28, 2018 alipotembelea gereza hilo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria hapa nchini.
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimsikiliza Mahabusu ambaye ni raia wa kigeni mara baada ya kuongea na Mahabusu wa Gereza Keko.
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akikagua jiko la gesi katika Gereza la Mahabusu Keko. Jeshi la Magereza tayari limeanza kutekeleza maelekezo ya Serikali ya kuachana na matumizi ya kuni kwa kutumia nishati ya gesi katika baadhi ya magereza nchini hivyo kutunza mazingira.
????????????????????????????????????
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakiwa katika chumba Maalum, Gereza Keko ambapo chumba hicho kitatumika katika Uendeshaji wa Mashauli mbalimbali kwa kutumia njia ya TEHAMA. Uwepo wa mfumo huu utalipunguzia gharama Jeshi la Magereza katika kuwasafirisha Mahabusu mahakamani na kuwarejesha magerezani.
????????????????????????????????????
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati) akiwa katika Chumba Maalum ambacho kitatumika katika uendeshaji wa mashauli kwa kutumia njia ya  TEHAMA(wa kwanza kushoto) ni  Kaimu Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Noel James(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Gereza Keko, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kiangi Abdallah (Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILI NCHINI ETHIOPIA,KUMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KATIKA KONGAMANO LA VIONGOZI WAKUU WA UMOJA WA NCHI ZA AFRIKA,LINALOFANYIKA MJINI ADDIS ABABA

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILI NCHINI ETHIOPIA,KUMWAKILISHA RAIS MAGUFULI KATIKA KONGAMANO LA VIONGOZI WAKUU WA UMOJA WA NCHI ZA AFRIKA,LINALOFANYIKA MJINI ADDIS ABABA

January 28, 2018

PMO_5218
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Comoros, Azali Assoumani, kwenye ndege ya shirika la Ethiopian Airline, wakiwa safarini kueleke Ethiopia, katika Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU, Waziri Mkuu, anamwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018.
PMO_5236
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga, wakati alipo wasili kwenye uwanja wa Kimataifa wa ndege wa Addis Ababa, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Viongozi Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika AU Nchini Ethiopia. Januari 28, 2018.
PMO_5254
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, kwenye hafla ya miaka 100 ya kumkumbuka Rais wa kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018.
PMO_5289
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisainiwa kitabu cha kumbukumbu, cha Rais wa kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, kwenye hafla ya miaka 100 ya kumkumbuka Kiongozi huyo, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Sheraton, Mjini Addis Ababa, Waziri Mkuu yupo Nchini Ethiopia kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli kwenye Mkutano huo. Januari 28, 2018.
Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA YAPONGEZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA KILOLO

KAMATI YA BUNGE YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA YAPONGEZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA KILOLO

January 28, 2018
image1
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa ikiwasili katika Hospital ya Kilolo kukagua ujenzi wa Hospital ya Wilaya.
image2
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa ikipokea Taarifa ya Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Kilolo ilipofanya ziara ya Ukaguzi wa Katika Mradi huo!
image3
Huu ndio muonekano wa  Sehemu ya Jengo la Hospital ya Wilaya ya Kilolo inayoendelea kujengwa.
image4
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Josephat Kakunda(Pili Kushoto) akijadili jambo na Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikalinza Mitaa wakati wa Ziara katika Mradi wa Ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Kilolo.
………………
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imepongeza  ujenzi wa majengo mbalimbali ya kutolea huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa.
Kamati hiyo imetoa Pongezi hizo wakati walipotembelea Kilolo na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali hiyo.
Wabunge wamepongeza kazi inayofanywa na wakandarasi kwani ipo katika ubora mzuri na kiwango cha kuridhisha.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Mwanne Mchemba aliyeongoza Waheshimiwa hao amesema “naipongeza sana Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, uongozi na watumishi kwa ujumla kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, ujenzi ni wa kiwango cha juu na thamani ya fedha inaonekana”.
Kamati imeagiza Halmashauri kuhakikisha inakamilisha majengo yote kwa wakati ili huduma ianze kutolewa mara moja.
Ameongeza kuwa ni vizuri kipindi hiki ambacho ujenzi unaendelea Halmashauri ijipange kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba, vitendanishi na dawa pamoja na kuajiri watumishi.
Naye Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege ameziagiza Halmashauri zote nchini ambazo hazina Hospitali za Wilaya zianze taratibu za ujenzi mara moja ili kuimarisha utoaji wa huduma za afya nchini.
Hadi sasa ujenzi uliofanyika ni wa majengo matano ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje; jengo la maabara; jengo la huduma ya mionzi; jengo la huduma ya afya ya uzazi na mtoto; na jengo la wagonjwa wa ndani. Ujenzi wa majengo haya hadi kukamilika unatarajia kutumia kiasi cha fedha shilingi bilioni  4.4.
Aidha, mradi mzima wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo utagharimu Tsh. Bil 12.

RAIS MAGUFULI NA MAMA JANETH MAGUFULI WATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU JAJI MSTAAFU ROBERT KISANGA

January 28, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Januari, 2018 ametia saini kitabu cha maombolezo na kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwake Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Mhe. Rais Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli pia wametoa mkono wa pole kwa mke wa Marehemu Mama Maria Kisanga na kufanya maombi ya pamoja na familia ya marehemu.
Jaji Mstaafu Robert Kisanga alifariki dunia tarehe 23 Januari, 2018 katika hospitali ya Regency Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na mtoto wa marehemu Amani Kisanga alipowasili na Mama Janeth Magufuli kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na mtoto wa marehemu Amani Kisanga alipowasili na Mama Janeth Magufuli kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa  Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 208.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa  Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 208.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwafariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga na mtoto wa marehemu Amani Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakifanya maombi pamoja na mjane wa marehemu Mama Maria Kisangana mtoto wa marehemu Amani Kisanga na waombolezaji wengine baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa waombolezaji baada ya kutoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa waombolezaji baada ya kutoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akitoa pole kwa waombolezaji baada ya kutoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Mama Janeth Magufuli akimfariji mjane wa marehemu Mama Maria Kisanga baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo na kisha kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na mtoto wa marehemu, Amani Kisanga, baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. Pamoja nao kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma na kulia ni Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi.  
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na mtoto wa marehemu, Amani Kisanga, baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. Pamoja nao kushoto ni Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Hamis Juma na kulia ni Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi.  
 Waheshimiwa Majaji na waombolezaji wengine wakiwa kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  
 Waheshimiwa Majaji na waombolezaji wengine wakiwa kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  
 Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph sinde Warioba akiwa na waombolezaji wengine kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  
 Majaji Wastaafu na waombolezaji wengine kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Sehemu ya waombolezaji kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Jaji Kiongozi  Jaji Ferdinand Wambali baada ya kutoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Jaji Mstaafu Thomas Mihayo  baada ya kutoa  heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Mstaafu Joseph sinde Warioba  baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018. 
 Kikosi cha Skauti kikiwa chini  Kamishna Mkuu wa Skauti Tanzania MheshimiwaAbdulkarim Shah kikiwa tayari kuhudumia kwenye msiba wa Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Tanzania Mhe. Robert Kisanga nyumbani kwa marehemu  Oysterbay Jijini Dar es Salaam leo Jumapili Januari 28, 2018.  Picha na IKULU