Rais wa Zanzibar Mh. Dk. Shein apokelewa na Rais wa Djbout Mhe.Ismail Omar Guelleh

May 08, 2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais wa Djbout Mhe.Ismail Omar Guelleh alipofika katika Ikulu ya Djbout leo akiwa katika ziara ya kiserikali na ujumbe wake,Picha na 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Rais wa Djbout Mhe.Ismail Omar Guelleh alipofika katika Ikulu ya Djbout leo akiwa katika ziara ya kiserikali na ujumbe wake,Picha na Ikulu.07/05/2017 

………………………………………………………………………. 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amefanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Djibouti Ismail Omar Guelleh ambapo katika mazungumzo hayo viongozi hao wamekubaliana kuanzisha uhusiano na ushirikiano kati ya pande mbili hizo hasa katika sekta za maendeleo na uchumi. 

Viongozi walifanya mazungumzo katika ukumbi wa Ikulu ya Djibouti ambapo Rais Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi na shukurani kwa Rais Guelleh kwa mwaliko wake huo nchini mwake. 

Katika mazungumzo hayo viongozi hao kwa kauli moja walieleza haja ya kuanzisha uhusiano na ushirikiano katika sekta mbali mbali za maendeleo na uchumi kwa manufaa ya pande mbili hizo. 

Rais wa Djibouti Ismail Omar Guelleh kwa upande wake alimuhakikishia Dk. Shein kuwa nchi yake iko tayari kushirikiana na Zanzibar katika kuimarisha sekta za mawasiliano, utalii, uwekezaji pamoja na usafiri na usafirishaji sambamba na utayari wa kujifunza mambo mbali mbali kutoka Zanzibar ikiwemo sekta ya utalii. 

Rais Guelleh, alieleza kuwa nchi yake inathamini sana uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Tanzania ambao una historia nzuri na kueleza kuwa Djibout iko tayari kujifunza mbinu zilizotumika na Zanzibar katika kuimarisha sekta ya utalii. 

Ambapo pia, kiongozi huyo alieleza utayari wa kushirikiana na Zanzibar kutokana na mafanikio waliyoyapata na njia sambamba na mikakati waliyoitumia katika kufikia mafanikio waliyoyapata na mikakati waliyoitumia kufikia mafanikio waliyonayo hasa katika suala zima la uimarishaji wa bandari, mawasiliano na vitega uchumi. 

Kiongozi huyo wa Djibouti alimkaribisha Dk. Shein pamoja na ujumbe wake nchini humo huku akisisitiza kuwa Tanzania na Djibouti zina ukaribu mkubwa na zimekuwa zikishirikiana katika kupambana na uharamia wa baharini kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Mamlaka ya Serikali ya Kimaendeleo (IGAD). 

Aidha, Rais Guelleh alitumia fursa hiyo kumueleza Dk. Shein mafanikio yaliyopatikana nchini mwake hasa kutokana na uimarishaji wa bandari, mawasiliano na kueleza azma ya nchi yake hivi sasa kujikita katika sekta ya utalii kutokana na baadhi ya vivutio vilivyopo ikiwemo Ziwa Assal ambalo chimbuko lake ni Bonde la Ufa pamoja na mambo mengineyo. 

Hivyo kiongozi huyo alimueleza Dk Shein kuwa pande hizo mbili zina mengi ya kujifunza kwa pamoja kwani kila upande umeweza kupata mafanikio yake. 

Kwa upande wake Rais Dk. Shein, alitumia fursa hiyo kutoa pongezi na shukurani kwa Rais Guelleh kwa mualiko wake huo aliompa pamoja na mapokezi makubwa aliyoyapata yeye na ujumbe aliofuatana nao na kueleza kuwa ziara hiyo itakuwa ndio kichocheo kikubwa cha mashirikiano kati ya Zanzibar na Djibouti. 

Dk. Shein alimueleza Rais Guelleh kuwa Zanzibar ina mengi ya kujifunza kutoka Djibouti hasa ikizingatiwa kuwa nchi hiyo wa kiuchumi inategemea sekta ambazo Zanzibar nayo imeamua kwa makusudi kuziimarisha ili ziweze kuimarisha uchumi na kuleta tija. 

Alizitaja miongoni mwa sekta hizo ambazo Djibouti imepata mafanikio ni uendeshaji wa Bandari,mawasiliano na Maeneo Huru ya Kiuchumi ambayo yamekuwa ndio kichocheo kikubwa cha uchumi wa nchi hiyo. 

Aidha, Dk. Shein alieleza kuwa ziara hiyo ni kielelezo cha urafiki, heshima na udugu baina ya Serikali zote mbili pamoja na wananchi wake ambapo itasaidia sana kuimarisha uhusiano na kuibua maeneo mapya ya ushirikiano. 

Katika maelezo yake, Dk. Shein alimueleza Rais Guelleh kuwa Zanzibar katika ziara hiyo ina hamu kubwa ya kufahamu maendeleo makubwa yaliyofikiwa na Djibouti tokea mwaka 1977 ilipopata uhuru wake kutoka kwa Koloni la Kifaransa. 

Dk. Shein alieleza kuwa ana hamu kubwa kuona maendeleo yaliofikiwa na nchi hiyo katika sekta muhimu za kiuchumi na kijamii ikiwemo sekta ya bandari, kuendeleza maeneo Huru, mawasiliano, uvuvi, viwanda, usafiri na usafirishaji, afya, elimu na sekta zote muhimu za utoaji wa huduma kwa wananchi wa nchi hiyo. 

Alipongeza juhudi kubwa zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya nchi hiyo chini ya uongozi wa Rais Guelleh ambazo zimepelekea Djibouti kuwa ni mfano mzuri kwa nchi za Afrika ambazo zinatafuta maendeleo ya haraka, demokrasia pamoja na kuimarisha hali ya utulivu na usalama wa nchi. 

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kumueleza Rais wa Djibouti mafanikio yaliopatikana kwa upande wa kisiasa na kimaendeleo na kupelekea kuimarika kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ni Muungano wa mfano kwa bara la Afrika na kutoa salamu za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa kiongozi huyo. 

Aidha, Dk. Shein alimuhakikishia Rais huyo utayari wa Zanzibar kushirikiana na Djibouti na kutoa uweledi wake katika sekta ya utalii kwa nchi hiyo kutokana na Zanzibar kupata mafanikio makubwa katika sekta ya Utalii. 

Pamoja na hayo, Dk. Sheuin alimuelkeza Rais huyi wa Djibout hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha uchumi wake ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Bandari mpya ya Mpiga Duri, mradi ambao utasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza uingizaji wa mizigo na makontena na kuipunguzia mzigo Bandari ya Malindi. 

Aidha, alieleza azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuifanya Zanzibar kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2020, huku akitumia fursa hiyo kumualika kiongozi uyo wa Djibouti kutembelea Zanzibar kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa pande mbili hizo. 

Dk. Shein yupo nchini Djibouti kwa ziara ya siku tatu kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Ismail Omar Guelleh. 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

MFUMUKO WA BEI WA TAIFA KWA MWEZI APRILI HAUJAONGEZEKA UMEBAKI ASILIMIA 6.4

May 08, 2017
 Mkurugenzi wa Sensa za watu na Takwimu  Ofisi ya Taifa ya Takwimu,(NBS), Ephraim Kwesigabo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu mfumuko wa bei ya taifa kwa mwezi Aprili. Kulia ni Mtakwimu, Hashim Njowele.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Wanahabari wakichua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MFUMUKO wa bei wa Taifa kwa kipimo cha mwaka umebaki kuwa asilimia 6.4 kama ilivyokuwa mwezi uliopita.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi wa Sensa za watu na takwimu wa Ofis ya Taifa ya Takwimu,(NBS), Ephraim Kwesigabo, alisema hii inamaanisha kuwa kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioisha March 2017 imekuwa sawa na kasi ya upandaji  ilivyokuwa mwaka ulioisha.

Kwesigabo, alisema fahirisi za bei zimeongezeka hadi 109.4 mwezi April 2017 kutoka 1o2 mwezi April 2016.

"Mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwaka umebaki kuwa asilimia 6.4 kama ilivyokuwa mwezi marchi 2017  kasi ya upandaji wa bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioisha mwezi Aprili imekuwa sawa na mwezi Marchi 2017,"alisema

Pia alisema mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Aprili 2017 umeongezeka hadi 11.8 kutoka asilimia 11.0 ilivyokuwa mwezi Marchi.

Aidha mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwaka kwa bidhaa za vyakula nyumbani na migahawani kwa mwezi Aprili 2017 umeongezeka hadi asilimia 12.0 kutoka asilimia 11.7 mwezi Marchi 2017.

Alisema badiliko la fahirisi za bei kwa bidhaa sisizo za vyakula umepungua kidogo hadi asilimia 3.4 mwezi Aprili kutoka asilimia 3.6 mwezi Ma
chi.

Akizungumzia kuhusu ukuaji wa dhamani ya shilingi, Kwesigabo alisema  uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 91 na senti 71, mwezi Aprili 2017 ikilinganisha na shilingi 92 na senti 21 ilivyokuwa mwezi Marchi 2017.


WANAHABARI WA ISRAEL WATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA GOMBE, WAAHIDI KUTANGAZA VIVUTIO VYA TANZANIA NCHINI HUMO

May 08, 2017


Kundi la waandishi kumi wa habari kutoka nchini Israel wakiwa katika hifadhi ya Taifa ya Gombe hivi karibuni kwa ajili ya kurekodi vivutio mbalimbali vya utalii vinavyopatikana katika hifadhi hiyo kwa ajili ya kuvitangaza nchini kwao ikiwa ni mkakati wa Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii Tanzania kwa kushirikiana na Hifadhi za Taifa (TANAPA). Kwa sasa soko la utalii la mashariki ya kati limeanza kufunguka kwa kasi ambapo hivi karibuni Waziri Mkuu Mstaafu wa Israel Ehud Barak ametembelea hifadhi za Ngorongoro na Serengeti.

HAMZA TEMBA - WMU

Kundi la wanahabari kumi akiwemo muigizaji mmoja na maofisa wa kampuni ya utalii ya Safari kutoka nchini Israel limetembelea hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyopo mkoani Kigoma na kufurahia vivutio lukuki vya utalii vinavyopatikana katika hifadhi hiyo na kuahidi kuvitangaza watakaporudi nchini kwao ikiwa ni mkakati wa Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia TANAPA na Bodi ya Utalii kutangaza vivutio hivyo nchini humo.

Akizungumza hivi karibuni mara baada ya kukamilika kwa ziara hiyo ya siku mbili, Kiongozi wa kundi hilo, Ronit Hershkovitz alisema ziara hiyo imekuwa na mafanikio makubwa ambapo wamefurahia kuona vivutio vya kipekee katika hifadhi hiyo na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa vivutio hivyo nchini Israel. 

Timu maalum ya wanahabari kutoka nchini Israel ikiwa na wajumbe kumi ilipowasili katika uwanja wa ndege wa Kigoma tayari kwa ajili ya ziara ya kitalii ya siku mbili katika hifadhi ya Taifa ya Gombe. Ziaza hiyo iliandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa kushirikiana na Shirika ya Hifadhi za Taifa Tanzani (TANAPA) kwa ajili ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania nchini Israel ikiwa ni mkakati maamlum wa kukamata soko la Mashariki ya Kati. Kutoka kulia wanaongoza msafara huo ni Meneja Mawasiliano TANAPA, Paschal Shelutete na Meneja Mahusiano wa TTB, Geofrey Tengeneza.

“Ni furaha kubwa kuwa hapa Gombe, tumeona makundi ya Sokwe na fukwe nzuri za Ziwa Tanganyika, tuko hapa kwa ajili ya kwenda kueleza kivutio hiki na vivutio vingine vya Tanzania nchini Israel, Waisrael wanaipenda Tanzania na wanapenda kutembelea Tanzania, tumeona ongezeko kubwa la watalii katika miaka ya hivi karibuni kutoka Israel baada ya kazi ngumu ya muda mrefu, sasa tuna furaha kuona watalii wengi wanaongezeka na tungependa kuona pia Watanzania wengi wakitembelea Israel,” Alisema Ronit.

Aliongeza kuwa, “Tunaenda kueleza taarifa hizi kwenye mitandao ya kijamii, magazeti, televisheni na popote tutakapoweza, lakini kubwa zaidi ni kuwaeleza marafiki zetu ana kwa ana uzuri wa Tanzania kwasababu tunaipenda Tanzania, nakupenda sana”.

Wanahabari kutoka Israel wakipanda kwenye boti kwa ajili kunza safari kuelekea hifadhi ya Taifa ya Gombe. Msafara huo ulikuwa na wanahabari kutoka vyombo maarufu nchini humo ikiwemo kituo cha Televisheni cha Channel 2, Jarida la Atmosphere, Jarida la National Geographic, Jaria la wiki la Yediot Acharanot -7 Yamim na waandishi wawili wa mitandao ya kijamii. Wengine ni maofisa wawili wa kampuni ya Utalii ya Safari  ya nchini humo.

Walfson Noa, ambaye ni Mwandishi wa Mitandao ya Kijamii na Meneja Masoko wa Kampuni ya Utalii ya Safari ya Israel alisema, “Tulifanya matembezi kuwaona Sokwe wanaovutia sana huku wakiishi katika mazingira yao ya asili, hili ziwa ni la maajabu sana (Ziwa Tanganyika), hata nyani nao walikuwa wakijaribu kuingia kwenye mahema yetu ni jambo la kuvutia, katika mtizamo wa kimasoko hili ni eneo ambalo nitawashauri wateja wangu watembelee, ni kitu ambacho watu wanatakiwa kukifahamu, kugundua siri ya uzuri wa hifadhi ya Taifa ya Gombe” 

Kwa upande wake Meneja wa Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, Paschal Shelutete ambaye alikuwa kiongozi wa msafara huo akishirikiana na Meneja Mawasiliano TTB, Geofrey Tengeneza, Meneja Mawasiliano wa TFS, Glory Mziray na Afisa Mawasiliano wa Wizara ya Maliasili, Hamza Temba alisema ujio wa wanahabari hao utaleta chachu ya kuongezeka kwa watalii wengi kutoka Israel pamoja na kupanua soko la utalii kwa hifadhi za mikoa ya magharibi mwa Tanzania ikiwemo hifadhi ya Gombe.

Mhifadhi wa hifadhi ya Taifa ya Gombe, Elihuruma Wilson (kushoto) akitoa maelezo mafupi kwa wanahabari kutoka nchini Israel kuhusu hifadhi hiyo kabla ya kuanza ziara ya kutembelea vivutio vilivyopo. Alieleza kuwa hifadhi hiyo ina vivutio vingi wakiwemo  Sokwe zaidi 100, Nyani, Kima, maporomoko ya maji, ndege aina mbalimbali na fukwe nzuri za kuogelea za ziwa Tanganyika. 

“Tumekuja na kundi hili la wanahabari ambao wameamua kama mlivowasikia kwa dhati kabisa kwamba watakaporudi nyumbani watatumia mitandao ya kijamii, radio mbalimbali, Televisheni lakini kubwa zaidi magazeti, wataandaa makala na vipindi mbalimbali hivyo tunaamini kwa dhati kabisa watakaporudi nyumbani na kuzifanyia kazi taarifa zote walizozipata katika hifadhi ya Taifa ya Gombe ama kwa hakika tutashuhudia ongezeko kubwa la watalii kutoka nchini Israel katika siku chache zijazo,” Alisema Shelutete.

Aliongeza kuwa, “Ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha rasilimali hizi za hifadhi zinazopatikana katika hifadhi za taifa zinaendelea kutunzwa kwa ajili ya kizazi hiki na vizazi vijavyo, watalii hawaji kuangalia ng’ombe kwenye hifadhi zetu, nasisitiza kuwa mifugo haikubaliki kwenye hifadhi zetu”.

Msafara huo ulikuwa na wanahabari kutoka vyombo maarufu nchini humo ikiwemo kituo cha Televisheni cha Channel 2, Jarida la Atmosphere, Jarida la National Geographic, Jaria la wiki la Yediot Acharanot -7 Yamim na waandishi wawili wa mitandao ya kijamii. Wengine ni maofisa wawili wa kampuni ya Utalii ya Safari ya nchini humo.

Hifadhi ya Taifa ya Gombe ilianzishwa mwaka 1968 kwa ajili ya tafiti za kisayansi, hususani katika kuwalinda na kuwahifadhi wanyamapori adimu wa jamii ya Sokwe Mtu (chimpanzees) ambao wapo hatarini kutoweka. Hifadhi hii inaelezwa kuwa na Sokwe wasiopungua mia moja ambao huishi kwa makundi na kuwa kivutio kikubwa na adimu katika hifadhi hiyo ambayo ina ukubwa wa kilomita za mraba 52.
Msafara wa Wanahabari wa Israel wakiwa kwenye boti tayari kwa safari ya kuelekea hifadhi ya Taifa ya Gombe ambapo kutoka Kigoma mjini hadi kwenye hifadhi hiyo ni mwendo wa saa moja na nusu hadi masaa mawili.
Meneja Mawasiliano wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Paschal Shelutete (kulia), Meneja Mahusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania (Geofrey Tengeneza) na Meneja Mawasiliano wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Glory Mziray) wakiongoza msafara wa wanahabari wa Israel kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Gombe.
Timu ya wanahabari wa Israel wakianza safari ya kuingia ndani ya msitu wa hifadhi ya Taifa ya Gombe kwa ajili ya kuona makundi mbalimbali ya Sokwe. Lengo kuu la ziara hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii na TANAPA ni kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania nchini Israel.
Wanahabari kutoka Israel wakipata maelezo kutoka kwa mhifadhi wa hifadhi ya Taifa ya Gombe kuhusu utarartibu wa kuzingatia wawapo ndani ya hifadhi hiyo ikiwemo kutokupiga kelele na kuepuka matumizi ya mwanga wa kamera (Flash Lights).
Mmoja ya wanahabari wa Israel, Gerald Eddie wa Jarida la National Geographic akiwa katika harakati za kupata taswira mwanana ya picha za Sokwe ndani hifadhi ya Taifa ya Gombe.
Wanahabari wa Israel wakiwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Gombe.
Sokwe akirukia matawi ya miti akiwa na mtoto wake ndani ya hifadhi ya Taifa ya Gombe wakati wa ziara ya wanahabari wa Israel kwenye hifadhi hiyo.

WANANCHI WAIOMBA SERIKALI KUKAMILISHA DARAJA LA SIBITI

May 08, 2017
Wananchi wa kata ya Mpambala, wilaya ya Mkalama mkoani Singida wameiomba Serikali kuhakikisha inamaliza ujenzi wa Daraja la Mto Sibiti haraka iwezekanavyo ili kurahisisha huduma za mawasiliano kati ya wilaya ya hiyo na mikoa jirani ya Simiyu, Manyara na Mara.

Wananchi hao wamemweleza Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, alipofika kukagua daraja hilo mkoani humo jana, ambapo pamoja na mambo mengine wamesema kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutatatua changamoto za usafiri hususan katika kipindi cha masika.
Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), mkoa wa Singida, Eng. Yohanes Mbegalo, akitoa taarifa kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa kwanza kulia), kuhusu maendeleo yaliyofikiwa ya ujenzi wa Daraja la Sibiti lenye urefu wa M 82 linalounganisha Mikoa ya Singida, Simiyu, Manyara na Mara.

"Tunaomba Mheshimiwa Naibu Waziri utusaidie  kukamilisha daraja hili mapema ili  tupate huduma muhimu kama usafiri hasa kipindi cha masika", amesema mmoja wa wananchi.

Aidha, wananchi hao wameipongeza Serikali kwa kuendelea na jitahada za ujenzi wa barabara za maingilio zenye urefu wa KM 25 katika daraja hilo ambapo kwa sasa mradi wote umefika asilimia 43.9.

Kwa upande wake Naibu Waziri Eng. Ngonyani ameuagiza Uongozi wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoani humo kuhakikisha kuwa wanamsimamia mkandarasi na kuhakikisha anamaliza ujenzi wa daraja hilo pamoja na barabara hizo kufikia mwezi Machi mwakani.
Mhandisi Mshauri Mr. Sunil Singh, akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (kulia), nguzo za Daraja la Sibiti zilizosimamishwa wakati alipokuwa akikagua ujenzi wa Daraja hilo na barabara za maingilio kwa kiwango cha changarawe KM 25, mkoani Singida jana.

Kuhusu deni la mkandarasi huyo analoidai Serikali, Eng. Ngonyani amesema kuwa watahakikisha wanamlipa mapema ili kufanikisha mradi kumalizika kwa muda uliopangwa.

"Tutahakikisha tunalipa deni lote linalodaiwa ili kurahisisha mradi huu kuisha haraka kwa ajili ya wananchi kuweza kutumia daraja hili pamoja na barabara yake kwa kuwa ni kiungo muhimu kwao", amesisitiza Naibu Waziri.

Ametoa rai kwa wananchi wa maeneo hayo  mara tu mradi unapomalizika kuhakikisha wanalinda miundombinu yake kwani Serikali inatumia gharama kubwa katika utekelezaji wake.
Muonekano wa nguzo za Daraja la Sibiti lenye urefu wa Mita 82 ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 48. Daraja hilo ni kiungo muhimu kwani litaunganisha Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida na Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu.

Naye, Kaimu Meneja wa TANROADS mkoani humo, Eng. Yohanes Mbegalo,  amemuahidi Naibu Waziri huyo kuwa atahakikisha mradi huo unaisha kwa wakati ili kuwaondolea wananchi kero ya usafiri.

Daraja la Sibiti lenye urefu wa mita 82 linajengwa na mkandarasi China Hanan ambalo linatarajiwa kukamilika mwezi Machi mwakani na kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 16.
Mwananchi Petro Daudi, kutoka Wilaya ya Meatu akimweleza Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Wa pili kulia), changamoto wanazozipata kipindi cha masika na kukosa mawasiliano na wenzao wa Wilaya nyingine jirani.

KIJANA GIRL GUIDES APAMBANA MEXICO KUWA MLIMA KILIMANJARO UPO TANZANIA BADALA YA KENYA

May 08, 2017
 Mmoja wa viongozi wa vijana wa Chama cha  Tanzania Girl Guides  (TGGA), Dk. Helga Mutasingwa (kulia), akilakiwa na Katibu wa Taifa wa TGGA, Grace Shaba baada ya kuwasili jana kwenye Uwanja wa wa Kimataifa wa  Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam jana. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)


Na Richard Mwaikenda 
KIONGOZI wa Vijana wa Chama cha  Tanzania Girl Guides  (TGGA), Dk. Helga Mutasingwa amefanya kazi kubwa ya kuwashawishi Wananchi wa Mexico kuwa Mlima Kilimanjaro upo Tanzania badala Kenya.

Dk. Mutasingwa ambaye alikuwa nchini Mexico kwa mafunzo ya miezi minne ya kubadilishana uzoefu katika nyanja za utamaduni na  uongozi alitumia fursa hiyo kutangaza vivutio vya Tanzania.

Akizungumza  mara baada ya kuwasili jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, alisema kuwa moja ya mambo yaliyompa wakati mgumu ni kuwabadilisha wamexico kuwa Mlima Kilimanjaro upo Tanzania na si Kenya kama wanavyofahamu wao.

Alisema Wamexico wengi kwanza wanajua Afrika ni nchi, jambo ambalo pia ilibidi awaeleze kuwa  siyo nchi bali ni bara kama yalivyo mabara mengine duniani na katika bara hilo kuna nchi nyingi na mojawapo ni Tanzania anayotokea yeye.

Alisema akiwa huko licha ya kuwafundisha kiswahili pia alitangaza vivutio vingi  vya utalii vilivyopo nchini, ambapo aliwatajia wadudu, ndege za kila aina na  wanyama mbalimbali waliomo kwenye hifadhi za Serengeti, Ngorongoro Crater na nyinginezo.

Pia aliwafundisha kuhusu utamaduni wa Tanzania zikiwemo ngoma za asili, upikaji wa vyakula vya kitanzania kama vile ndizi na pilau, mambo ambayo walifurahishwa nayo.

Dk. Mutasingwa alisema kuwa ambaye katika ziara hiyo ya mafunzo alikuwa na vijana wenzie wa Girl Guids kutoka Venezuela,  Canada, Uingereza  na Argentina alipata wasaa wa kujifunza utamaduni wa mexico na kutoka nchi hizo zingine.

Alisema kuwa alijifunza mambo mengi ikiwemo ujasiri wa kufanya kazi bila woga, siasa za mataifa mbalimbali,  mambo ambayo ameahidi kuwafundisha vijana wenzie wa TGGA hapa nchini.

Dk. Mutasingwa aliwasili nchini jana, ambapo kwenye Uwanja wa Ndege wa JNIA, alilakiwa na Katibu wa Kitaifa wa TGGA, Grace Shaba pamoja na wanachama wenzie Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi.



 Dk. Mutasingwa akiwa na Katibu wa TTA Taifa, Grace Shaba (kushoto), Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi baada ya kulakiwa akitokea Mexico
Dk. Mutasingwa akifurahia jambo na  Elieshupendo Michael na Maryrehema Kijazi.
 Dk Mutasingwa akikumbatiana kwa furaha na Maryrehema Kijazi
 Ni furaha iliyoje kukutana
  Dk. Mutasingwa akifurahi wakati akilakiwa na Elieshupendo Michael
Grce Shaba na Dk. Mutasingwa wakiwa na furaha

MITANDAO YA KIJAMII INAVYOWEZA KUNUFAISHA BIASHARA YAKO

May 08, 2017
Na Jumia Travel Tanzania 

Mitandao ya kijamii si tu inatumika kwa kuwaunganisha watu au kupata taarifa mbalimbali bali hata kibiashara pia. Yapo makampuni, mashirika na watu binafsi wanaitumia vema kibiashara na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa tu. Sasa na wewe unashindwa nini kufanya hivyo ikiwa unawashuhudia wengine wakinufaika na biashara zao?
Lakini kabla ya kuamua kutumia mitandao ipi ya kijamii kwa ajili ya biashara yako,  Jumia Travel ingependa kukushauri kwanza kuzingatia masuala matatu yafuatayo:  

Chagua mitandao wa kijamii itakayofaa. Sio mitandao yote inaweza kukusaidia kibiashara kama unavyoona wengine wanavyoitumia. Kwa mfano, mtandao wa facebook unafaa zaidi kwa kuwashirikisha wateja wako taarifa, picha na video kuhusu bidhaa zako, instagram nayo ni picha kwa kiasi kikubwa ingawa wametambulisha na huduma ya video pia, huku Twitter yenyewe kitaalamu inafaa zaidi kama uko na mtu ambaye atakuwa makini katika kujibu masuala mbalimbali yatokanayo na taarifa unazowashirikisha wateja wako paop kwa papo.