FURAHA YA KUPITISHWA KWA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI BUNGENI MJINI DODOMA

June 03, 2014

 Waziri wa Nishati na  Madini Profesa Sosipiter Muhongo akijibu hoja za wabunge kabla ya kupitishwa bajeti ya wizara yake mjini Dodoma juzi.Bunge lilipitisha  Sh. tirioni moja kwa wizara hiyo.
 Waziri Muhongo (kulia) na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakimu Maswi wakipongeza baada ya Bunge kupitisha bajeti ya wizara yao.
 Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete (kulia), akimpongeza Waziri Muhongo baada ya Bunge kupitisha bajeti ya wizara hiyo.
 Mdau wa sekta ya Nishati na Madini (kushoto), akimpongeza Waziri Muhongo kwa bajeti ya wizara yake kupitishwa na Bunge.
Mdau mwingine wa sekta ya Nishati na Madini akimpongeza Waziri Muhongo (kulia) baada ya Bunge kupitisha bajeti ya wizara hiyo.


Wabunge wamfagilia Muhongo

Dotto Mwaibale, Dodoma


WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamempongeza Waziri wa Nishati na madini Profesa Sosipiter Muhongo, kwa jitihada zake za kuisimamia kikamilifu wizara hiyo ambapo wamemtaka aendelee kuchapa kazi na aache kusikia majungu na maneno ya watu.

Hayo yalisemwa na Wabunge walipokuwa  wakichangia hotuba ya Bajeti ya mwaka 2014/2015 ya Wizara ya Nishati na Madini mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. 

Akichangia hotuba hiyo Mbunge wa Same Mashariki (CCM)Anne Kilango Malesela, alisema kazi inayofanywa na Wizara ya Nishati na Madini chini ya uongozi wa waziri Muhongo na timu yake haipaswi kubezwa kwani wanafanya vizuri kuhakikisha wananchi kila kona wanapata umeme.

"Waziri Muhongo na timu yake wanafanya kazi nzuri ni lazima tuwapongeze na kama kutakuwa na watu wanaopinga jitihada wanazo zifanya watakuwa na sababu zake kwani hivi sasa umeme upo hadi maeneo ya milimani" alisema Kilango.


kwa upande wake Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde alisema kazi inayofanywa na wizara hiyo ni kubwa hivyo Muhongo na watendaji wake wasiogope vitisho na majungu wachape kazi kwani wanachokifanya kinaonekana kwa wananchi.


Mbunge wa Karagwe,Gosbert Blandes alisema wananchi wa jimbo lake wanapongeza kazi inayofanywa na wizara hiyo na kuwa iwapo ikitokea siku moja waziri Muhogo akifika jimboni humo atajionea mwenyewe jinsi anavyowa kubalika.

Hata hivyo walimpongeza kwa kitendo chake cha kufanya jiji la Dar es salaam kutokuwa na umeme wa mgao toka aingie wizarani.

RAIS KIKWETE AONANA NA RAIS MSTAAFU WA NAMIBIA MHE SAM NUJOMA LEO

June 03, 2014

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimtembezea sehemu mbali mbali za Ikulu na Rais Mstaafu wa Namibia Mhe. Sam Nujoma aliyemtembelea  leo. Mhe Nujoma alikuwa ni mmoja wa watu mashuhuri waliohudhuria sherehe za miaka 50 ya Muungano jana.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimtembezea sehemu mbali mbali za Ikulu na Rais Mstaafu wa Namibia Mhe. Sam Nujoma aliyemtembelea  leo April 27, 201

AZAM TV WAIKABIDHI BODI YA LIGI KUU FEDHA ZA MSIMU WA PILI

June 03, 2014


Mtendaji Mkuu wa Azam TV, Rhys Torrington kulia na Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu, Mwakibinga leo
KAMPUNI ya Azam Media imetangaza kuwa tayari imeshatuma fedha kwa Bodi ya Ligi kwa ajili ya msimu wa ligi wa Vodacom kwa mwaka 2014/ 2015.
Fedha hizo zimetolewa mapema zaidi kwa ajili ya kusaidia maandalizi mapema kwa timu kama ilivyokubaliwa kwenye mkataba wa miaka mitatu ya udhamini wao katika ligi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Azam zilizopo Tazara, Dar es salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington, alisema kuwa kampuni hiyo inavutiwa na aina nzuri ya ushirikiano kati yake na bodi ya Ligi.

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM,KINANA NDANI YA MERERANI,AKUTANA NA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO WA MADINI NA KUSIKILZA CHANGAMOTO ZAO

June 03, 2014


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akioneshwa vipande vya madini aina ya Tanzanite ,katika mgodi wa mchimbaji mzawa wa madini ya Tanzanite Bi.Suzie Didas Kennedy.Katibu Mkuu wa CCM alitembelea migodi ya wachimbaji wadogo wa Mererani na kuzungumza nao juu ya changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua. Pichani kati aneshuhudia ni Mbunge wa Jimbo la Simanjiro,Mh.Christopher Ole Sendeka.
 Moja ya jiwe lenye madini kabla ya kufanyiwa mchakato. 
   Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia namna wachimbaji wadogo wanavyotumia mashine kubebea mchanga kutoka kwenye mgodi wa mchimbaji mzawa wa madini ya Tanzanite Bi.Suzie Didas Kennedy.Katibu Mkuu wa CCM alitembelea migodi ya wachimbaji wadogo wa Mererani na kuzungumza nao juu ya changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua. 
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Mererani ambao aliwaambia vyama vya Upinzania ni sawa na Jogoo kwani hata awike vipi hawezi fungua mlango na kwa sababu vyama hivyo havipo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi basi vinelekea kufa kwani havina sera mpya za kujinadi kwa wananchi. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mererani wilaya ya Simanjiro ambao wengi ni wachimbaj wa wadogo wadogo wa madini kwenye mkutano wake wa mwisho baada ya kumaliza ziara ya siku 26 ambapo alitembelea mikoa mitatu ya Tabora, Singida na Manyara.


 Jengo la Kituo cha Afya cha Endiamtu,Mererani Simanjiro,ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alikwenda kukagua na kujionea ujenzi wake ulipofikia
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akitoka kukagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Mama na Matoto cha Endiamtu,Mererani wilayani Simanjiro.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu abdulrahman Kinana akikagua mradi wa ujenzi wa tanki la maji litakaloweza kuhudumia watu 25,000 na kutoa  lita 36,000 kwa saa linalojengwa Naisinyai Mererani.
  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kijiji cha Landanai,Wilayani Simanjiro
   Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Landanai,Wilayani Simanjiro
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akishiri ujenzi wa Ofisi  ya tawi jipya la CCM la Kandasikira.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipandisha bendera ya Chama Cha Mapinduzi baada ya kuzindua tawi jipya la CCM tawi la Kandasikira.
 Baadhi ya Wazee wa Kimasai wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipofanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.
    Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.
    Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana  akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Kandasikira,Wilayani Simanjiro.

PICHA NA MICHUZIJR-MERERANI SIMANJIRO

MBONA UMENUNA YA MB DOG KUANZA KUONEKANA KWENYE LUNINGA WIKI HII.

June 03, 2014

MWIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya, Mbwana Mohamed, Mb Dog, amesema mashabiki wake wataanza kuona video ya wimbo wake wa Mbona Umenuna katika vituo vya luninga ndani ya wiki hii.

Mb Dog, pichani.
Video hiyo iliyoandaliwa kwa kiwango cha juu iliingizwa katika mitandao ya kijamii, huku kwenye luninga ikianza kusambazwa wiki hii ili kuwapa burudani mashabiki wake.

Akizungumza leo mchana, Mb Dog alisema kwamba alianza kwanza kuingiza kwenye mitandao ya internet ili kuwapa nafasi watu wote, wakiwamo wan je ya nchi kuitazama video hiyo.

“Hii ni video nzuri ambayo iliingia kwanza kwenye mtandao na kuwapa fursa watu kuitazama, ambapo natarajia mashabiki wengine wataanza kuangalia luningani wiki hii.

"Naamini mashabiki wangu wote watapata burudani ya kutosha, ukizingatia kuwa nimefanya video nzuri inayoonyesha umahiri wangu kisanaa,” alisema.

Mb Dog ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Fleva wenye uwezo wa juu wa kutunga na kuimba, ambapo wimbo wake wa kwanza uliomuibua ni Latifa na nyinginezo

*TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MSIBA WA KIONGOZI WA FAM

June 03, 2014

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mwakilishi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM) katika Mkutano Mkuu wa TFF, William Chibura kilichotokea leo asubuhi (Juni 3 mwaka huu) katika Hospitali ya Mkoa wa Mara mjini Musoma.

Chibura aliyezaliwa mwaka 1969 alikuwa mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF akiwakilisha klabu za Mkoa wa Mara kupitia FAM. Aliwahi kuichezea Musoma Shooting, na baadaye kuwa kiongozi katika klabu hiyo na ile ya Polisi Mara iliyoko Ligi Daraja la Kwanza (FDL).

Hadi mauti yanamkuta alikuwa kiongozi wa Butiama FC, na mwakilishi wa klabu Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Butiama (MUFA) kwenye Mkutano Mkuu wa FAM.

Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu nchini kwani, Chibura enzi za uhai wake alitoa mchango mkubwa katika mchezo huu tangu akiwa mchezaji na baadaye kiongozi.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Chibura, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM), Jeshi la Polisi Tanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Taratibu za mazishi zinaendelea kufanywa na familia yake kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Tanzania- Mkoa wa Mara, kwani marehemu Chibura alikuwa mtumishi wa jeshi hilo. TFF tunasubiri taratibu hizo ili tujipange jinsi ya kushiriki katika msiba huo.


Bwana alitoa, na Bwana ametwaa. Jina lake lihimidiwe. Amina
WAZIRI WA ULINZI HUSSEN MWINYI AZINDUA KIWANDA CHA KUTENGEZA VIFAA VYA UJENZI CHA UTURUKI.JUN 2-2014

WAZIRI WA ULINZI HUSSEN MWINYI AZINDUA KIWANDA CHA KUTENGEZA VIFAA VYA UJENZI CHA UTURUKI.JUN 2-2014

June 03, 2014
1 (8)  
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussen Mwinyi (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi kiwanda cha kutengezea vifaa vya ujenzi cha Uturuki STONE BLOCK BUILDING. Jun 2,2014.kilichopo Kawe Mbezi Beach jijini Dar es Salaam (wakwanza kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki,  Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Ali Davutoglu na maofisa wa Uturuki.
2 (9) 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki wakijadiliana jambo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Ali Davutoglu, wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho.
3 (7)  
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe.Hussen Mwinyi (kushoto), akijadiliana jambo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania Ali Davutoglu,wengine ni maofisa kutoka Uturuki.
4 (7)  
Wageni waalikwa wakiangalia burudani.
5 (3)  
Vijana wa kabila la Kimasai wakitoa burudani.
6 (2)  
Deus Kamwela, kutoka kikundi cha sanaa KCC akionyesha umahiri wake wa viongo.
7Wafanyakazi wa kiwanda hicho.
PICHA NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE
SHULE YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VYOO

SHULE YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VYOO

June 03, 2014

SAM_4810  
Diwani wa kata ya Mgama Denis Lupala akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mgama wakati alipowatembelea na kula pamoja chakula cha mchana.
SAM_4824  
Diwani wa kata ya Mgama, Denis Lupala akimpakulia chakula mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mgama wakati alipowatembelea na kula pamoja chakula cha mchana
SAM_4815 
Diwani wa kata ya Mgama Denis Lupala akizungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Simeone Lihuluku.
Na Denis Mlowe,Iringa
 
SHULE ya sekondari Mgama iliyoko katika kata ya Mgama jimbo la Kalenga wilaya ya Iringa Vijijini inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa matundu ya vyoo  30 yaliyopo 12 na miundo mbinu mibovu.
 
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi wakati wa hafla iliyoandaliwa na diwani wa kata hiyo Denis Lupala,Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Simeone Lihuluku alisema kuwa licha ya upungufu wa matundu ya choo shule hiyo inakabiliwa na ukosefu wa maktaba na maabara kwa wanafunzi wanaosoma shuleni hapo tangu kuanzishwa kwake miaka saba iliyopita.
 
Luhuluku alisema  shule hiyo inakabiliwa na ukosefu wa mabweni ya wanafunzi na nyumba za kuishi walimu kitu kinachochangia wanafunzi kupanga mbali na maeneo ya shule changamoto inayosababisha ufaulu hafifu kutokana na utoro pamoja na upatikanaji wa mimba kwa watoto wa kike.
 
Alisema mwaka huu tayari wanafunzi watatu wamekatisha masomo kutokana na kupata ujauzito huku nyumba za walimu zinazohitajika zikiwa 18 na zilizopo kwa sasa ni nyumba mbili za walimu.
 
“Licha ya upungufu wa matundu ya vyoo vilevile tunakabiliwa na changamoto nyingi sana katika shule hii lakini kubwa zaidi ni ukosefu wa maabara na maktaba kwa ajili ya wanafunzi na tumekuwa tunatumia chumba kimoja cha darasa kama maabara kitu kinachosabisha wanafunzi kutosoma vizuri na kupunguza ufaulu naomba sana wadau waweze kuwasaidia kuondokana na changamoto hizi” alisema Lihuluku
 
Aliongeza kuwa shule hiyo imekosa huduma ya umeme,vyanzo vya kuaminika vya maji safi na vifaa vya kufundishia pamoja na uchangiaji hafifu wa michango ya shule kwa wazazi.
 
Kwa upande wao wanafunzi  wa shule hiyo wamemshukuru diwani huyo kwa kuwaandalia chakula huku wakimuomba kuwasaidia kutatua changamoto zinazowakabili katika shule yao  kwa lengo la kuongeza ufaulu shuleni hapo.
Shule ilianzishwa mwaka 2007 ikiwa inatoa elimu ya kidato cha kwanza hadi cha nne ikiwa na jumla ya wanafunzi 516 kati ya hao wavulana wakiwa 221 na wasichana 295 na walimu 20.