TAARIFA
RASMI YA MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI WA SIMBA SC, WAKILI DKT.
DAMAS DANIEL NDUMBARO KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUPINGA MAAMUZI YA
RAIS WA TFF, JAMAL MALINZI KUSIMAMISHA UCHAGUZI WA SIMBA SC
Kamati ya Uchaguzi ya
Simba Sports Club, ilifanya mkutano wake kawaida tarehe 15 Juni 2014 kujadili
mambo mbalimbali ambayo yanayohusu uchaguzi mkuu wa Simba Sports Club ambao
umepangwa kufanyika tarehe tarehe 29 Juni 2014. Kamati ya Uchaguzi ya Simba
sports Club inapenda kuujulisha umma, hususan wapenzi wa Simba
Sports Club mambo yafuatayo:
1. Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club, kwa
mujibu wa Ibara ya 10(6) ya Kanuni za uchaguzi za TFF toleo la mwaka 2013,
ndiyo chombo pekee chenye mamlaka ya kutangaza, kubadilisha, kusimamisha au
kufuta tarehe ya Uchaguzi ya Simba Sports Club. Kwakuwa Kamati haijafanya
hivyo, wala hakuna mdau yoyote aliyeleta hoja ya kusimamisha uchaguzi,
tunawajulisha kuwa uchaguzi wa Simba Sports Club upo pale pale kama ambayo
Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club ilivyopanga. Maandalizi ya uchaguzi huo
yanaendelea vema na Uchaguzi utafanyika tarehe 29 Juni 2014 kama ilivyopangwa
hapo awali.
2. Kamati
imesikia kupitia vyombo vya habari kuwa TFF imesimamisha uchaguzi wa Simba
Sports Club mpaka hapo Kamati ya Utendaji ya Simba Sports Club itakapoteua
Kamati ya Maadili. Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club inapenda kusema
yafuatayo:
i. Mamlaka ya
kusimamisha uchaguzi ni kazi ya Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club kwa
mujibu wa ibara 10 (6) ya Kanuni za Uchaguzi, 2013
ii. Kamati ya
Uchaguzi ya Simba Sports Club ilipoanza mchakato wa uchaguzi ilitoa tamko kuwa:
“kwasababu Simba Sports Club haina kanuni za Uchaguzi, Kamati ya Rufaa ya
uchaguzi, wala Kamati za Maadili kwa mujibu wa ibara za 16 (e) na (f) ya Katiba
ya Simba Mwaka 2014, vyombo husika vya TFF vitatumika”. Kulikuwa hakuna
pingamizi toka kwa mtu yoyote juu ya kauli hiyo, ikiwemo TFF.
iii. Tarehe 26
Mei 2013, Rais wa TFF aliialika Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club katika
chakula cha mchana. Katika mkutano huo, kauli ya aya (ii) hapo juu ilirejewa na
Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club ilikabidhi rasmi mchakato mzima wa
uchaguzi na kutoa ufafanuzi kuwa kamati husika za TFF zitahusika, jambo ambalo
halikupingwa na TFF.
iv. TFF iliruhusu
Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF kusikiliza Rufaa za uchaguzi za Simba, hivyo
basi haiwezi kuzuia Kamati zake nyingine kusikiliza Masuala ya kimaadili.
“Estopel” inawazuia TFF kufanya hivyo sasa.
v. Wajumbe wote
wa Kamati ya Utendaji ya Simba Sports Club, isipokuwa watatu tu, ni wagombea
katika uchaguzi huu. Na hao watoto tayari wapo kwenye Kambi za Kampeni za
uchaguzi hii ambazo zipo bayana kabisa. Kuiagiza Kamati ya Utendaji ya Simba
iunde Kamati ya Maadili kusikiliza kesi za maadili dhidi yao wenyewe ni kukiuka
msingi wa haki ya asili (natural justice). Ni dhahiri kuwa haki haiwezi
kutendeka kwa wajumbe wa kamati ya utendaji ya Simba Sports Sports Club, ambao
ni watuhumiwa katika masuala ya maadili, wachague majaji wa kuwahukumu. Hapo
haki haitatendeka.
Ifahamike kuwa, baada ya Kamati ya Utendaji ya
Simba Sports Club kuteua Kamati ya uchaguzi ya Simba Sports Club, Kamati hiyo
haina mamlaka tena ya kujadili, kuingilia au kuteua chombo kingine kufanya
shughuli zinazohusu uchaguzi ukizingatia kuwa wajumbe wake ni wagombea.
vi. Katika
Uchaguzi Mkuu wa TFF wa Mwaka 2013, ambao ulimuingiza Jamal Malinzi Madarakani,
FIFA walikuja, wakongea na pande zote na hatimaye, walisema kuwa;
“tunapendekeza kuwa uchaguzi mkuu usimame ili kuunda kamati mbalimbali”.
Mapendekezo hayo yalipokelewa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Bw. Deo Lyato, na
hatimaye ni Kamati ya Uchaguzi ya TFF ndio iliyotangaza kusimamisha Uchaguzi na
sio Sepp Blatter.
vii. Kamati ya
Uchaguzi ya Simba Sports Club ni Kamati huru ambayo haipaswi kuingiliwa na
Chombo chochote kile. Ili kulinda uhuru huo, tunalazimika kukanusha matamshi ya
TFF kuhusu kusitisha Uchaguzi Mkuu wa Simba Sports Club.
3. Malalamiko ya
Kimaadili Kupelekwa FIFA.
Kwa mujibu wa Ibara ya 11 (9) ya Kanuni za Uchaguzi
za TFF, 2013, inatoa mamlaka kwa Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club
kupeleka masuala ya maadili katika kamati ya maadili ya TFF. Tarehe 9 Juni
2014, Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club ilipeleka Masuala ya Maadili
katika Kamati ya Maadili ya TFF. Kwakuwa TFF imekataa kusikiliza masuala ya
maadili ambayo yanakiuka Kanuni za maadili, Katiba za Simba, TFF na FIFA,
Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club, itapeleka Masuala ya Maadili FIFA ili
haki itendeke.
4. Kamati ya
Uchaguzi ya Simba Sports Club ilijadili kuhusu vitendo vya wagombea kupiga
kampeni kabla ya muda wa kampeni ulioruhusiwa. Kwa mujibu wa Mchakato wa
Uchaguzi ya Simba Sports Club, muda wa kampeni unaanza tarehe 24 -28 Juni 2014.
Hapo awali kamati ilibaini kuwa wagombea wawili wa nafasi ya urais; Michael
Richard Wambura na Evans Aveva walifanya vitendo vya kampeni siku ya kuchukua
na kurejesha fomu za kugombea. Tarehe 25 Mei 2014, Kamati iliwapa ONYO KALI la
maandishi wagombea hao na kuwataarifu kuwa hatua kali zaidi zitachukuliwa dhidi
yao, ikiwemo kuondolewa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi.
Baada ya Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club
kumuondoa Bw. Michael Richard Wambura katika kinyang’anyiro cha uchaguzi Mkuu
wa SImba Sports Club, Bw. Wambura aliitisha Mkutano na waandishi wa habari,
aliitukana Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club, na kutoa matamshi ambayo ni
Kampeni.
Baadaya ya Kamati ya Rufaa ya uchaguzi ya TFF
kumrejesha Bw. Wambura katika Kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu wa Simba, Bw.
Wambura aliitisha tena mkutano wa waandishi wa habari, aliisifu kamati ya Rufaa
ya Uchaguzi ya TFF, kwa mara kwanza aliisifu Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports
Club na kutoa matamshi ambayo ni wazi kuwa ni kampeni. Baadhi ya Matamshi
aliyoyatoa kupitia vyombo vya habari ni kama ifuatavyo:
i. “Simba Sports
Club inahitaji zaidi wadhamini na sio wafadhili”
ii. “Wafadhili
kazi yao in kutoa fedha mfuko wa kushoto na kuepeleka mfuko wa kulia”
iii. “Simba
ilikuwa na viwanja vitatu lakini kimoja kimeuzwa na wajanja na vimebaki viwili
tu”
Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club ilitafakari
matamshi hayo, na kubaini kuwa hiyo ni kampeni ya waziwazi wakati muda wa
kampeni bado haujaanza.
Kamati ya Uchaguzi ya Simba Sports Club ililipa
jambo ili uzito wa kipekee kwasababu Mkosaji amekuwa na tabia ya kurudia kosa
hilo hata baada ya kupewe onyo la maandishi.
HIVYO BASI: Kwa mujibu wa mamlaka ya kikanuni,
hususan Ibara za: 6 (1) (a) – (g); 6 (1) (L) na 14(3) za Kanuni za uchaguzi za
TFF – 2013, Bw. Michael Richard Wambura anaondolewa Katika Kinyang’anyiro cha
Uchaguzi wa Simba Sports Club, 2013, kwa kosa la kurudia kufanya kampeni kabla
ya muda wa kampeni ambao umepangwa,".