TANZANIA NA MAREKANI ZAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MICHEZO NA SANAA

June 08, 2022

 






Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa wakiambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi wamekutana na Balozi wa Marekani hapa nchini leo Juni 8, 2022 wamekutana jijini Dar es salaam na kujadili masuala mbali mbali ya sekta za ikiwa ni pa moja na ujio wa msanii mashuhuri wa uchoraji ,Ashley Collins hapa nchini.


Wakizungumza katika  kikao hicho ambacho Mhe. Balozi  wa Marekani nchini Tanzania Dkt. Donald Wright ameambatana na Afisa Uhusiano wa Ubalozi huo, James Rodriguez wamejadili pia ujio wa Timu ya wachezaji nguli wanawake ya mchezo wa kikapu wa ligi  ya NBA nchini Marekani  hapa nchini ambao watakuja Tanzania kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wachezaji wanawake wa mchezo huo hapa nchini. 


Mhe. Mchengerwa amesema viongozi hao wamekubaliana  kuendeleza  malengo ya Royal Tour kwa kushirikiana zaidi  kwenye kuendeleza sekta  za sanaa na michezo ikiwemo kuendeleza  filamu za hapa nchini za “Swahiliwood” ili ziwe  katika  kiwango cha kimataifa kama zile za nchini Marekani kwa kupata walaam ambao watasaidia katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa miswada (script)


Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na maeneo ya kipekee ya kuchezea  filamu ambazo zingeweza  kuwa bora na kusisitiza kuwa ni azma ya serikali kujenga mazingira  wezeshi ikiwa ni pamoja na kuangalia kodi mbalimbali ili kuwavutia wageni kuja  kurekodia  hapa nchini.


Aidha amesema eneo jingine ambalo limejadiliwa ni pamoja na kutoa mafunzo maalum katika eneo la haki miliki na hakishiriki kwa kazi mbalimbali za wasanii ikiwa ni pamoja na tuzo za muziki na Kwa upande mwingine amesema wamejadili namna ya kushirikisha wataalam kwenye program maalum ya kuibua vipaji vya wasanii na wanamichezo ya mtaa kwa mtaa.

UONGOZI WA WIZARA WAITAKA TEMBO WARRIORS KUTUMIA MECHI ZA ULAYA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA, WAIAGA RASMI LEO

June 08, 2022

 





Na John Mapepele


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na michezo.Mhe, Mohamed Mchengerwa ameitaka Timu ya soka ya walemavu ya (Tembo Warriors) kutumia mechi za maandalizi na nchi mbalimbali za Ulaya kujinoa ili kushinda kombe  hilo na kulirejesha nchini.


Mhe Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Juni 8, 2022 uwanja wa Benjamini Mkapa wakati akiikabidhi bendera ya Taifa timu hiyo akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Hassan Abbasi inayokwenda kuanza kucheza mashindano kwenye maandalizi na timu  mbalimbali za Ulaya kwa kuanzia na timu ya Poland ili kuweza kupata uzoefu wa kucheza na nchi za mabara mbalimbali  kabla ya kuanza mashindano haya.


“Tumeamua kama Serikali kuendelea kuhaakikisha kuwa tunazisaidia timu zinazofanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa ili kuwasaidia kukuza ajira na kuwafanya  waajiriwe  kwenye vilabu  vikubwa  duniani” amefafanua Mhe. Mchengerwa 


Amesema watanzania wamechoka kuona kuwa nchi inasuasua kwenye michezo na amesisitiza kuwa  wakati huu watanzania wanataka  kombe  la dunia kuja  Tanzania ambapo amesema  hilo litafanikiwa kwa kuweka mbele utaifa na uzalendo wanapokuwa kwenye mashindano haya.


Ameongeza kuwa jambo kubwa kwa sasa ni kuwa na nidhamu na kuzingatia misingi ambayo wanapewa na  makocha wa timu zao ili waweze  kufika mbali na kuboresha  maisha yao na uchumi wan chi yetu kwa ujumla.


“Naomba kuwaambia mkifanya vizuri katika mashindano  haya ya maandalizi tu nina uhakika  mtanunuliwa na timu kubwa na mtabaki ulaya, mtabadilisha maisha ya familia zenu na watanzania kwa ujumla” ameongeza Mhe. Mchengerwa


Wakizungumza kwa nyakati tofauti  viongozi wa timu hiyo  wamemwahidi Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuwa wanakwenda  kuanza kutema cheche  katika maandalizi ya timu hizo za awali ili kujihakikishia  kutwa kombe hilo.


Katibu Mkuu. Dkt, Abbasi amesema  Tembo Warriors ndiyo timu ya kwanza nchini kufuzu kuingia kwenye mashindano hayo na kuitaka kuendelea kushikilia heshima  hiyo kwa kuwa timu ya kwanza kurejesha kombe  nyumbani.