TUGHE Muhimbili Wapata Viongozi Wapya, Yaongeza Nafasi ya Vijana na Walemavu

June 08, 2016

Hospitali ya Taifa Muhimbili  (MNH) imepata viongozi wapya  wa Chama cha wafanyakazi wa Serikali  na Afya Tanzania (TUGHE),  Tawi la Muhimbili  katika uchaguzi uliofanyika leo majira ya alasiri katika ukumbi wa CPL hospitalini hapo.
Nafasi zilizogombaniwa  ni pamoja  na Mwenyekiti wa Tawi, Katibu wa Tawi, wajumbe wa Halmashauri ya Tawi, nafasi ya Mwenyekiti Kamati ya wanawake, Katibu kamati ya wanawake, Mjumbe kamati ya wanawake, Muweka Hazina kamati ya wanawake, nafasi ya walemavu  pamoja na nafasi ya vijana.
Katika uchaguzi huo Bwana Mziwanda Salum Chimwege ametetea nafasi yake ya Uenyekiti wa tawi na kuibuka kidedea kwa kupata kura 248, huku nafasi ya Katibu ikichukuliwa na Bwana Faustine Fidelis Kaitaba ambaye amepata kura 215.
Walioshinda nafasi ya halmashauri ya tawi ni Idi Shaweja,  Edina Maneno,  Seif  Athuman, Rama Sultan, Yusuph Mkando, Adam Alfan, Josephine Lwambuka, Shaban  Zubery, Isaya Mbinga, Charles Kayombo, Aly Mkali, Musa Mbuhita,Bure  Nasoro, Joyce Chirwa, Mecktidis Chonga, Aikael Kisanga, Hidal Mtoakani pamoja na Dk. Peter Kibacha.
Nafasi ya Mwenyekiti kamati ya wanawake imechukuliwa na Zainab  Mwagala  kwa kupata kura 71 huku Mwajuma Kisengo ameibuka mshindi kwa kupata nafasi ya Ukatibu kwa kupata kura 75 
Muweka hazina kamati ya wanawake ni Halima Mayumana wakati nafasi ya vijana imechukuliwa na Husein Jalala Mkangazi ambapo  Salama Kasembe ameshinda nafasi ya walemavu.
Awali akifungua mkutano mkuu wa uchaguzi wa Tawi la TUGHE –Muhimbili  , Kaimu Mkurugenzi Mtendaji  wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-MNH- Profesa  Lawrence Museru ameupongeza uongozi uliopita wa TUGHE katika tawi hilo  kwa kushirikiana  vema na Menejimenti pasipo migogoro.
Pamoja na mambo mengine Profesa Museru amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kwamba kuanzia Julai mwaka huu MNH itaanza kutoa mkono wa heri kwa wastaafu wake sanjari na kutoa posho kwa watumishi wote wa hospitali hiyo.
“Posho hizi zinatolewa si kwamba hospitali ina pesa nyingi lakini  tunambua mchango wa ,  kwani  kila mmoja ametimiza  wajibu wake  hatua iliyochangia kuongeza mapato ya  hospitali  , hivyo nawasihi sana muendelee kufanya kazi kwa bidii ili suala hili liwe endelevu.”amesema Profesa Museru.
Pia ametumia fursa hiyo  kuwasisitiza  kwamba MNH itaendelea kuchua hatua kwa wafanyakazi wasiio waaminifu katika utoaji wa huduma .
Viongozi hao wa TUGHE tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili wataongoza kwa muda wa miaka mitano.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Profesa Lawrence Museru wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na wajumbe wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE) wa tawi la hospitali hiyo kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa viongozi wa chama hicho leo kwenye ukumbi wa CPL, Muhimbili.
 Katibu wa Tughe Mkoa wa Ilala Jijijini Dar es Salaam, Gaudence Kadiango akitoa maelekezo kabla ya kuanza kwa uchaguzi  wa viongozi wapya wa TUGHE leo.
 Wajumbe wa TUGHE wakiimba nyimbo za mshikamano leo kabla ya kuanza kwa uchaguzi wa viongozi wapya.
 Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Makwaia Makani akiungana na wajumbe wa TUGHE wakati wakiimba nyimbo za mshikamano.
 Mmoja wa wajumbe wa TUGHE, Helmut Ngalawa akipiga kura leo kuchagua viongozi wapya wa chama hicho.
 Baadhi ya wajumbe wakihesabu kura baada ya wajumbe kupiga kura leo kwenye ukumbi wa CPL-Muhimbili.
 Wajumbe wakishangilia baada ya viongozi waliowapigia kura kushinda uchaguzi huo leo.
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa TUGHE katika Tawi la Muhimbili, Mziwanda Chimwege (kulia) na katibu wake, Faustine Kaitaba wakipongezana leo baada ya kuchaguliwa tena katika nafasi hizo kuongoza chama hicho kwa muda wa miaka mitano.
 Mmoja wa wajumbe akimpongeza Mziwanda Chimwege kwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa TUGHE katika tawi la Muhimbili.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Museru, (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wapya wa tawi la TUGHE Muhimbili akiwamo mwenyekiti, katibu na wajumbe wa halmashauri ya chama hicho. Picha na JOHN STEPHEN, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Mwarobaini wa kukatika kwa umeme Arusha wapatikana, Wateja zaidi ya 89,000 waunganishwa.

June 08, 2016

 Sehemu ya kituo cha  kupoza umeme cha KIA 132/33kV kilichopo mkoani Kilimanjaro kama kinavyoonekana pichani.
 Meneja Miradi ya Usafirishaji na Usambazaji Umeme kutoka  Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Manirabona (wa pili kutoka kulia) akielezea  mafanikio ya  kituo cha kupoza  umeme cha KIA 132/33kV kilichopo mkoani Kilimanjaro.
 Meneja wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mkoa wa Arusha Mhandisi Gaspa Msigwa ( wa pili kutoka kulia) akielezea hali ya upatikanaji wa umeme mkoani Arusha  kutokana na kukamilika kwa kituo cha kupoza umeme cha KIA 132/33kV kilichopo mkoani Kilimanjaro.
 Meneja Miradi ya Usafirishaji na Usambazaji Umeme kutoka  Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Manirabona ( katikati) akielezea namna ya uwekaji  wa nyaya za umeme chini ya sakafu kwa lengo  la kuimarisha usalama  katika kituo cha KIA 132/33kV kilichopo mkoani Kilimanjaro.
 Meneja Miradi ya Usafirishaji na Usambazaji Umeme kutoka  Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Manirabona akielezea jinsi kifaa cha kuongozea mitambo ya umeme  kinavyofanya  kazi  mbele ya waandishi wa habari  (hawapo pichani).
 Sehemu ya  mitambo ya kampuni inayojishughulisha na uzalishaji wa kokoto ya Ravji Aggregate Limited iliyopo wilayani Arumeru mkoani  Arusha ambayo ni moja  ya wanufaika wa umeme kutoka katika kituo cha KIA 132/33kV.
John Augustino mkazi wa wilaya ya  Arumeru mkoani Arusha akielezea mchango wa kituo cha KIA 132/33kV katika ukuaji wa uchumi  wa wakazi wa mkoa huo.

Mwarobaini wa kukatika kwa umeme  Arusha wapatikana.
Ni baada ya kukamilika kwa kituo cha  kupoza umeme cha KIA
Wateja zaidi ya 89,000 waunganishwa; TANESCO kukusanya bilioni 9 kwa mwezi
Juni 06, 2016.

Na  Greyson Mwase, Arusha
 Imeelezwa kuwa kukamilika kwa kituo cha  kupoza umeme  cha KIA kilichopo karibu na  Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kilimanjaro  International Airport) kumepelekea tatizo  la kukatika kwa umeme kuisha katika mkoa wa Arusha na baadhi ya maeneo  ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro na kuongeza kipato   kwa wakazi wa mkoa huo.

Kauli hiyo ilitolewa na Meneja wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Mkoa wa Arusha Mhandisi Gaspa Msigwa,  kwenye ziara ya waandishi wa habari kutoka  vyombo mbalimbali  vya habari nchini katika miradi ya  TEDAP na mradi wa usafirishaji umeme kutoka Iringa  hadi Shinyanga katika msongo wa kilovolti 400 (BITP) inayofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB).
Lengo la ziara hiyo lilikuwa ni kuona hatua za utekelezaji, mafanikio na changamoto za miradi hiyo pamoja na kupata maoni ya wanufaika wa miradi hiyo.

Akielezea mradi huo Mhandisi  Msigwa alisema ujenzi wa kituo hicho uliogharimu Dola za Marekani Milioni 7, ulianza mwaka  2011 na kukamilika mapema   Desemba mwaka  2013.
Alisema   kabla ya ujenzi wa kituo hicho, umeme ulikuwa unasafirishwa kutoka katika kituo cha Kiyungi kilichopo mkoani Kilimanjaro hadi jijini Arusha umeme ambao  ulikuwa hautoshelezi katika matumizi ya  majumbani na katika  viwanda vidogo.

Aliongeza kuwa  pia kulikuwepo na tatizo la kupotea kwa  umeme mwingi kutokana na  kusafirishwa katika umbali mrefu.

Alisema kuwa  tangu  kukamilika kwa kituo hicho  wateja zaidi ya 89,000 waliunganishiwa umeme ambapo mpaka sasa wanapata umeme ambao ni wa uhakika.
Alisema kutokana na ongezeko la wateja pamoja na kupatikana kwa umeme wa uhakika katika mkoa huo, TANESCO imeweza kukusanya  shilingi bilioni tisa kwa mwezi tofauti na kipindi cha awali ambapo makusanyo  yalikuwa  yanafikia wastani wa  shilingi bilioni  nane kwa mwezi.
Aliendelea kusema kuwa kukamilika kwa kituo hicho kumehamasisha kuongezeka kwa  ujenzi wa nyumba pamoja na  kuanzishwa kwa viwanda vidogo katika mkoa wa Arusha.
Wakati huo huo Julius Urassa ambaye ni msimamizi wa kampuni inayojihusisha na uzalishaji wa kokoto ya Ravji Aggregate Limited iliyopo wilayani Arumeru mkoani  Arusha alisema kuwa  kabla ya kukamilika kwa kituo hicho  hali ya umeme  katika mkoa wa Arusha haikuwa nzuri.
“ Kabla ya kuwepo kwa kituo cha KIA, umeme ulikuwa unakatika mara kwa mara na kuathiri  uzalishaji  katika kiwanda chetu; lakini sasa tunapata umeme wa uhakika,” alisema
Aliogeza kuwa kutokana na upatikanaji wa umeme wa uhakika, kampuni yake ina uwezo wa kuzalisha  tani 100 za kokoto kwa siku tofauti na zamani ambapo walikuwa na uwezo wa kuzalisha kati ya  tani  40 hadi  60 za kokoto kwa siku.
Naye  Meneja wa Kampuni inayojihusisha na utengenezaji wa matofali kwa njia ya umeme  ya Melck Hardware iliyopo  Maji ya  Chai nje kidogo ya  jiji la Arusha, Hansi Said alisema kuwa  hali ya umeme katika mkoa wa Arusha imetengemaa hali iliyopelekea uzalishaji  kuongezeka katika kampuni yake.
Alisema kutokana na upatikanaji wa umeme  wa uhakika, kampuni yake ambayo hutengeneza matofali kulingana na oda kutoka kwa wateja, imeongeza uzalishaji kutoka  wastani wa  tofali 700 hadi 2,000 kwa siku.
Naye  John Augustino mkazi wa Arumeru mkoani Arusha aliongeza kuwa  tangu kuanza kupatikana kwa umeme wa uhakika, hali ya maisha katika  familia yake imeboreka kutokana na kuuza bidhaa zaidi ya maziwa tofauti na mwanzo katika duka lake.
“Bidhaa za vinywaji  hususan maziwa  yalikuwa yanaharibika kutokana na  kukatika kwa umeme, lakini  kwa sasa tunapata umeme wa uhakika, hali inayochangia kuuza bidhaa bora zaidi,”alisisitiza.

USAILI WA KIKOSI KAZI CHA 102.5 LAKE FM MWANZA WAENDELEA KUFANYIKA.

June 08, 2016
Hiki ni Kikosi Kazi cha baadhi ya Wafanyakazi wa 102.5 Lake Fm, Raha ya Rock City #Radio ya Wananzengo. Radio hiyo ambayo ni inakiki jijini Mwanza hivi sasa licha ya kwamba bado iko kwenye majaribio, inaendelea na usaili wake ili itakapoanza kurusha vipindi vyake rasmi, ianze kwa mwendo kasi zaidi.
Na BMG

MKUU WA MKOA WA MBEYA AKITAKA CHUO CHA MAGEREZA KIWIRA KUWAANDAA ASKARI WATAKAOSIMAMIA MAGEUZI NDANI YA JESHI LA MAGEREZA

MKUU WA MKOA WA MBEYA AKITAKA CHUO CHA MAGEREZA KIWIRA KUWAANDAA ASKARI WATAKAOSIMAMIA MAGEUZI NDANI YA JESHI LA MAGEREZA

June 08, 2016

 Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amekitaka Chuo cha magereza Kiwira kilichopo wilaya ya Rungwe KUWAANDAA askari watakasimamia MAGEUZI makubwa ndani ya jeshi la magereza na magereza yaliopo nchini

Hayo ameyasema leo katika ziara yake ya kikazi kutembelea Chuo hicho na kuongea na maofisa, askari na wanafunzi wa Chuo wapatao 1,390 . 

Katika nasaha zake amesema mbali ya majukumu waliobaki ya kuwalinda wafungwa magerezani ni vema wakaelewa kuwa jeshi hilo sasa lijielekeze ku jiimarisha kiuchumi kwa kuanzisha na kusimamia miradi mbalimbali itakayosaidia magereza kujitosheleza kwa chakula


Aidha Uwepo wa wafungwa magerezani utengenezaji kuwarekebisha tabia lakini pia kuwapatia ujuzi wafungwa kupitia kazi katika viwanda v na karakana za magereza
 

CHEKI TANZANIA YAZINDUA HUDUMA YA KUTOA MAGARI BANDARINI KWA WANUNUZI WA MAGARI NCHINI

June 08, 2016

 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Cheki Tanzania, Mori Bencus akielezea kuhusu huduma ya uunganishwaji wa uagizaji magari kutoka nje ya nchi na huduma ya utoaji wa magari bandarini (clearing and forwarding), huduma ambayo kampuni yake imeanza kuitoa kwa Watanzania wanaoagiza magari.

 Kaimu Meneja Masoko wa Cheki Tanzania, Juliana Ntemo akionyesha jinsi watumiaji wa mtandao wa Cheki.co.tz jinsi wanavyoweza kutumia huduma ya clearing and forwarding.

Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo wakiendelea na kazi yao ya kuchukua taarifa kwa ajili ya kuupasha umma kuhusu huduma ya clearing and forwading ambayo inatolewa na cheki.co.tz

 Mtandao wa kuuza magari mtandaoni wa Cheki.co.tz umezindua huduma mpya ya uunganishwaji wa uigizaji magari kutoka nje ya nchi na huduma ya utoaji magari bandarini (clearing and forwarding), huduma ambayo itawarahisishia wananchi ambao wanaagiza magari nje ya nchi kuwa na uhakika wa usalama wa magari wanayoagiza mpaka yanakapowafikia.
Akielezea huduma hiyo, Meneja Mkuu wa Kampuni ya Cheki Tanzania, Mori Bencus, alisema kampuni yake imeanzisha huduma hiyo ili kuwarahisishia Watanzania wanaoanzisha magari nje ya nchi kutokana na kubaini kuwa wamekuwa wakisumbuka kukamilisha uagizwaji wa magari na kuyatoa bandarini.
“Tayari tumewapa wateja wetu chaguo kubwa la magari kutoka kwa wauzaji wa kuaminika kutoka nje ya huduma hii ya utoaji wa mizigo itarahisisha utoaji wa magari kutoka bandarini na hivyo wateja kupunguza gharama na muda wa kusubiri,” alisema Bencus.
Nae Kaimu Meneja Masoko wa Cheki Tanzania, Juliana Ntemo, alisema kuwa kampuni hiyo haihusiki na uuzaji wa magari ila inachofanya ni kumuunganisha mnunuzi wa gari na muuzaji ili waweze kufanya biashara kwa haraka na urahisi zaidi.
Ujio wa huduma hiyo imekuwa mwendelezo wa uboreshwaji wa huduma za ununuzi wa magari kwa kupitia mtandaoni ambazo zinafanywa na mtandao wa Cheki.co.tz ambao unafanya kazi na wauzaji wa magari wa kimataifa wa  nje ya nchi na wauzaji wa magari wa hapa nchini.

WAHITIMU WA USCF - TAASISI YA UHASIBU TANZANIA WATAKIWA KUWA WAADILIFU MAKAZINI

June 08, 2016
Wanafunzi wametakiwa kuwa waadilifu pindi wanapomaliza chuo na kwenda kuingia makazini. Kauli hiyo ameitoa Mwenyekiti wa bodi ya Ushauri TAREA, Godwin Msigwa (pichani) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya umoja wa wanafunzi wa kikiristo wa vyuo vikuu Tanzania katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika weekend iliyopita. Msingwa alisema ni vyema vijana wakatambua kuwa maisha mazuri ni yake ya kufanya kazi kwa uadilifu na kuacha ujanja ujanja katika kazi. "Leo mnaenda mtaani mtapata kazi ninawaomba mkafanye kazi kwa uadilifu, mfano wewe ukipata kazi ya kusimamia manunuzi ya dawa muendele ukanunue dawa zenye ubora maana usipofaya hivyo utasababisha vifo vya watu na hiyo dhambi si ndogo, Muogopeni Mungu,' Alisema Msigwa. Aliongeza kuwa wakati umefika kwa watanzania wakaonyesha uzalendo kwa mambo yao wenyewe, wasingoje mpaka wasukumwe katika kufanya kazi kwa bidii. PICHA ZOTE NA CATHBERT KAJUNA WA KAJUNASON BLOG.
Mchungaji wa KKKT akitoa neno wakati wa mahafali ya umoja wa wanafunzi wa kikiristo wa vyuo vikuu Tanzania katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika weekend iliyopita.
Wahitimu wakifuatilia neno kutoka kwa mchungaji wakati wa mahafali ya umoja wa wanafunzi wa kikiristo wa vyuo vikuu Tanzania katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika weekend iliyopita.
Katika neno alililolitoa mchungaji huyu aliwaasa wahitimu kuwa na hofu ya Mungu pindi wanapopewa majukumu ya kazi.
Mgeni rasmi mwenyekiti wa bodi ya Ushauri TAREA, Godwin Msigwa (wa tatu toka kushoto) akiserebuka na mchungaji wa KKKT pamoja na wageni waalikwa.
Wahitimu wakijimwaga.
 Mchungani akiwaombea wanafunzi wakafanye vyema katika mitihani yao wakati wa mahafali ya umoja wa wanafunzi wa kikristo wa vyuo vikuu Tanzania katika Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) yaliyofanyika weekend iliyopita. -- ---- Cathbert Angelo Kajuna, Founder and Mananging Director Kajunason Blog, P.O Box 6482, Dar es Salaam. Tel: +255 787 999 774 Alt: +255 765 253 445 www.kajunason.blogspot.com "Everything is Possible Through Peace & Stability''

VITUO VYA TAARIFA NA MAARIFA VYAPIGWA MSASA NA TGNP

June 08, 2016
 Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi Lilian Liundi akifungua semina  kwa Wanaharakati pamoja na viongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa waliofika katika semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa TGNP Mtandao leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Geofrey Adroph)
Mkuu wa Program ya Taarifa na Utafiti kutoka TGNP, Gloria Shechambo akitoa elimu kwa wanaharakati kuhusu utendakazi wao wa kila siku wakati wa semini iliyofanyika katika ukumbi wa TGNP Mtandao.
 Katibu wa Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Kibuko, Bw. Valentino Lukoo akitoa ufafanuiz kuhusu maendelea yaliyofikia katika kata yao baada ya kuonekana kwa changamoto nyingi katika kata hiyo
 Mwenyekiti wa Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Igale, Bi Lidya Sankemwa Mwakalinga akizungumzia mipango ya kata yao kuhusu utoaji wa taarifa husika katika kata yao.
 Mwanaharakati kutoka Kituo cha Taarifa na Maarifa cha Kata ya Nsalal  Bi. Felister Kais akizungumzia changamoto wanazozipata katika utoaji wa taarifa.
Mwanaharakati kutoka  Mabibo, Bw. Furaha Mbakile akichangia mada
 Afisa program Utafiti na Uchambuzi kutoka TGNP, Bw. Alphonce Stima akiongea jambo wakati wa utoaji wa Semina kwa Wanaharakati pamoja na viongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa waliofika katika semina hiyo

Wanaharakati pamoja na iongozi wa vituo vya taarifa na Maarifa wakitazama hotuba ya  Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango anasoma na kuwasilisha Hali ya Uchumi kwa mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo Bungeni 
 Afisa program Utafiti na Uchambuzi kutoka TGNP, Bw. Alphonce Stima akiongea jambo mara baada ya kumalizika kwa Hotuba  ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango anasoma ama kuwasilisha Hali ya Uchumi kwa mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo Bungeni Dodoma
Afisa Programu mwandamizi wa Ushawishi na utetezi kutoka TGNP Mtandao, Bi. Anna Sangai akitoa elimu wanaharakati pamoja na viongozi wa Taarifa na Maarifa katika ukumbi wa TGNP jijini Dar es Salaam leo
Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake katika Jitihada za Maendeleo (WAJIKI), Janeth Mawinza akichangia mada
 Afisa Program uchambuzi na Machapisho kutoka TGNP Mtandao, Bw. Deogratius Temba akiwaeleza wanaharakati pamoja na viongozi wa Taarifa na Maarifa jinsi ya ufanyakazi wa TGNP Mtandao

Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Bi Lilian Liundi(kulia) akifuatilia Bunge kupitia njia ya Television katika ofisi ya TGNP  Mtandao



 Baadhi ya Wafanyakazi wa TGNP Mtandao, Wanaharakati, viongozi wa Taarifa na Maarifa pamoja na wananchi wakifuatilia Bunge kwa njia ya Televisioni ndani ya Ukumbi wa TGNP Mtandao jijini Dar es Salaam