MAKALA KUHUSU MAJINA YA A.K.A

August 06, 2017
Na Mohammed Hammie Rajab
A.K.A ni kirefu cha maneno ya kiengereza ambayo ni "Also known as", ikiwa na maana ya 'Pia nafahamika kama', ambapo mtu akitaka kujulikana ama kufahamika kwa jina jengine ambalo sio rasmi, huwa anatumia a.k.a kwa kiashirio cha jina mbadala.
Jina linapokuwa rasmi mara nyingi hutumika zaidi kwenye vitambulisho, vyeti, shuleni na hata maofisini kutokana na taratibu za kisheria zilizowekwa na serikali, huwezi kukuta mtu anatumia a.k.a kwenye masuala yanayotaka utaratibu.
Muziki wa Bongo Fleva umekuwa maarufu sana hapa nchi na hata nje, umaarufu wa muziki huu pia unachagizwa na majina ya wasanii wake ambapo tumeshuhudia wasanii wengi  wakitumia zaidi a.k.a pasipo majina yao halisi, japokuwa kuna wasanii wachache wanaotumia majina yao.
Alli Kiba na ndugu yake Abdul, ukiacha uhalisia wa majina yao ya kati ambapo wote wanatumia Salehe lakini utagundua fika kuwa hawakutengeneza a.k.a ili kupata majina yao ya kisanii, badala yake wametumia majina yao rasmi.
Wengine ni Banana Zorro na ndugu yake Maunda Zoro ambao hawakutumia muda kutengeneza a.k.a na bado wanafahamika, wapo pia wasanii ambao A.K.A zao zinashahabiana na majina yao halisi ambao ni Bernad Paul (Ben Paul), Jaffar Msham Ally (Jaffarai), Snura Mushi (Snura) na Ambwene Yesayah (AY) ambaye ameunganisha jina lake na ubini wake kupata A.K.A.
Kwa majina haya kidogo unaweza kusema afadhali kwa kuwa ni rahisi hata kuyatabiri, tofauti unaposikia jina kama Omari Faraji Nyembo halafu ukaambiwa kuwa ndio Ommy Dimpoz, au  Ibrahim Mussa ambaye ni ROMA, unaweza usielewe kidogo.
Wapo wasanii wengine pia ambao lazima ikuchukue muda kufahamu majina yao halisi, mfano ni Emmanuel Simwanga (Izzo B), Abdul-Aziz Abubakar Chende (Dogo Janja), Emmanuel Elibariki (Ney Wa Mitego), na hata Khery Sameer Rajab (Mr Blue), zaidi utaangua kicheko tu.
Hao ni wachache tu, lakini ukienda ndani zaidi utagundua kuna wimbi kubwa la wasanii wa Bongo Fleva wanaotumia zaidi a.k.a kiasi cha kupoteza majina yao halisi nchini tofauti na fani nyengine kama vile soka na filamu.
Tofauti kubwa iliyopo baina ya wasanii wa Bongo Flava na waliopo kwenye fani ya soka au filamu ni uwazi wa majina yao, mfano marehemu Steven Kanumba pamoja na kutumia a.k.a  ya the Great, lakini jina lake halisi lilikuwa likifahamika zaidi kuliko jina lake mbadala. Wengine ni Shamsa Ford, Jackline Wolper, na Yusufu Mlela ambao hata kama wana A.K.A lakini hazisikiki kama yalivyo majina yao halisi.
Japokuwa utakubaliana na mimi kuwa wapo baadhi ya wasanii wa filamu nchini ambao nao wamepoteza majina yao halisi na kutumia zaidi majina mbadala, mmoja wapo ni Elizabeth Michael (Lulu), Blandina Chagula (Johari), Mahsein Awadhi (Dokta Cheni), Single Mtambalike (Richie), na Vincent Kigosi ambaye anafahamika zaidi kama Ray.

RAIS DKT. MAGUFULI PAMOJA NA RAIS MUSEVENI WA UGANDA WAWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA KUTOKA HOIMA UGANDA MPAKA BANDARI YA TANGA

August 06, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake, Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga huku viongozi mbalimbali wa Tanzania na Uganda wakishuhudia. Shughuli hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake, Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga huku viongozi mbalimbali wa Tanzania na Uganda wakishuhudia. Shughuli hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono wa pongezi na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga huku Viongozi mbalimbali wa Tanzania na Uganda wakishuhudia. Shughuli hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari mbalimbali waliohudhuria shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga katika kijiji cha Chongoleani nje kidogo ya jiji la Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Chongoleani kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la Msingi mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka nchini Uganda hadi Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono pamoja na mke wake Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati wakiagana na Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika uwanja wa ndege wa Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akicheza ngoma ya msanja na Mama Janeth Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kumsindikiza Rais wa Uganda Yoweri Museveni katika uwanja wa ndege wa Tanga.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia katika viwanja vya Chongoleani kabla ya tukio la uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta.
Makamu wa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akimpa mkono Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni baada ya kumaliza kuhutubia katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Tanga Nchini Tanzania.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martin Shigela akiongea wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Tanga Nchini Tanzania ambapo aliwaahidi Rais Magufuli na Rais Museveni kuwa wataulinda mradi huo kwa faida ya nchi hivi mbili na Afika Mashariki kwa Ujumla.
Baadhi ya wananchi wakifurahia jambo wakati wa hotuba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la Msingi la Mradi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Tanga Nchini Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimueleza jambo Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la Msingi la Mradi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Tanga Nchini Tanzania.

MHANDISI LWENGE ATOA HEKO KWA WIZARA YA NISHATI NA MADINI KWA KUANZISHA MFUMO RAHISI KWA WANANCHI KUPATA TAARIFA ZIHUSUZO NISHATI JADIDIFU

August 06, 2017
Na Mathias Canal, Lindi

Wizara ya Nishati na Madini imetambua kadhia iliyokuwa inawakumba wananchi kupata taarifa sahihi na za uhakika kuhusu masuala ya nishati jadidifu hapa nchini na hatimaye kuanzisha mfumo rahisishi wa taarifa unaojulikana kama Tanzania Renewable Energy Information Management System (TREIMS).

Mfumno huu utasaidia kuhakikisha kwamba taarifa sahihi za masuala ya nishati jadidifu zinapatikana ambapo pindi taarifa zinapopatikana zitakuwa zinahakikiwa kabla ya kuwafikia watumiaji.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge (Mb) amesifu mfumo huo kuwa utapunguza muda wa wadau unaotumika kutafuta taarifa zinazohusu nishati jadidifu sambamba na kufuatilia kwa urahisi maenedeleo ya miradi ya nishati jadidifu inayotekelezwa hapa nchini.

Mhe Lwenge alisema kuwa kulikuwepo na upatikanaji hafifu wa taarifa za masuala ya nishati jadidifu hapa nchini tatizo ambalo lilichangia kuwa na maendeleo kidogo katika sekta ndogo ya nishati jadidifu.

Alisema serikali isingeweza kufikia malengo kwa uduni wa taarifa lakini hatua ambao imefikiwa sasa na Wizara ya nishati na madini itakuwa mbadala wa mafanikio kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Mfumo huu unajumuisha taarifa zihusuzo sera, sheria na mifumo mingine ya kisheria inayohusika na usimamizi na uendeleaji wa sekta ndogo ya nishati jadidifu.

Mhandisi Lwenge pia amesifu Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvvuvi kwa kurejesha tena Maonesho hayo na Nanenane katika Mkoa wa Lindi ikiwa ni mara ya nne mfululizo huku akieleza kufurahishwa jinsi wananchi wanavyoendelea kujitokeza kupata elimu ya Kilimo Mifugo na Uvuvi.

Alisema kuwa kauli mbiu ya maonesho ya Nanenane kwa mwaka 2017 inayosema “Zalisha kwa Tija Mazao na Bidhaa za Kilimo Mifugo na Uvuvi ili kufikia Uchumi wa Kati” inaakisi mafanikio na fursa kwa kila mwananchi kupata mbinu bora za kilimo mifugo na uvuvi.

Sikukuu ya wakulima inayofahamika kuwa Nanenane ina sherekewa nchini kote tarehe 8 Agosti kila mwaka. Sherehe hiyo inatayarishwa na kuratibiwa na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na kuhusisha Taasisi, Wizara na mtu mmoja mmoja wanaoshughulika na kilimo. 

Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge (Mb) alipotembelea banda la Wizara ya Nishati na Madini wakati wa Maonesho ya Nanenane ambayo kitaifa yanafanyika Katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge (Mb) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Wizara ya Nishati na Madini wakati wa Maonesho ya Nanenane ambayo kitaifa yanafanyika Katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI TIGO YATOA OFA KABAMBEYA SIMU ZA KISASA MAONESHO YA NANE NANE -LINDI

August 06, 2017
Meneja Mauzo Kampuni ya Tigo Mkoa wa Mtwara, Lilian Mwalongo akionesha simu mpya ya Tecno R6 kwa baadhi ya wananchii waliofika katika banda la Tigo katika maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea Mkoa wa Lindi.
.Moja ya kikundi cha Timu ya  Mauzo Tigo wakiwa katika picha ya pamoja katika maonesho ya Kilimo yanayoendelea Mkoani Lindi.



Meneja Mauzo Kampuni ya Tigo Mkoa wa Mtwara, Lilian Mwalongo akionesha simu mpya ya Tecno R6 kwa baadhi ya wananchii waliofika katika banda la Tigo katika maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea Mkoa wa Lindi.

MHANDISI LWENGE AIPONGEZA WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI KWA ELIMU WANAYOITOA KUHUSU UTUNZAJI WA MALISHO

August 06, 2017
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge Akisisitiza jambo mara baada ya kutembelea Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi wakati wa Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akisalimiana na Afisa habari wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi Ndg Issa Sabuni mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akipata ufafanuzi kuhusuidara ya uzalishaji wa mifugo na masoko inavyofanya kazi mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akipata ufafanuzi kuhusuidara ya uzalishaji wa mifugo na masoko inavyofanya kazi mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akipata ufafanuzi kuhusuidara ya uzalishaji wa mifugo na masoko inavyofanya kazi mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge akipata ufafanuzi kuhusuchangamoto za masoko ya bidhaa zinazotengenezwa kwa ngozi kutoka kwa meneja wa Robi Leather Product Bi Rose Otieno mara baada ya kutembelea Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
Mgeni rasmi Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge alipowasili kwenye Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.
 
Na Mathias Canal, Lindi

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Greyson Lwenge ameipongeza Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kwa elimu wanayoitoa kwa wananchi kuhusu utunzaji wa malisho ambayo ni nyasi na mikunde kwa ajili ya mifugo kwani jambo hilo litawawezesha wananchi kuwa na mifugo yenye afya bora.

Mhandisi Lwenge ameyasema hayo alipotembelea banda la Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi idara ya uzalishaji wa mifugo na masoko wakati wa Maonesho ya wakulima (Nanenane) ambayo kitaifa yanafanyika katika Viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

Alisema kuwa malisho ni chakula cha msingi cha mifugo ambacho kinajumuisha aina mbalimbali za nyasi na mikunde.

Pamoja na kutolewa elimu juu ya umuhimu wa utunzaji wa malisho lakini pia amesisiza zaidi wizara ya kilimo kutoa elimu kuhusu utunzaji wa malisho hayo jambo ambalo litawawezesha wafugaji kuipatia mifugo yao chakula bora na cha kutosha wakati wote.

Zipo faida nyingi za kupanda malisho ikiwa ni pamoja na kurahisisha upatikanaji wa chakula cha mifugo chenye viini lishe kama wanga, protini madini na vitamin.

Faida Zingine ni kurutubisha ardhi hasa malisho aina ya mikunde sambamba na kuzuia mmomonyoko wa ardhi.

Mhandisi Lwenge amesema kuwa malisho ndio chakula kikuu cha mifugo inayochengua (Ng’ombe, mbuzi, kondoo, punda na ngamia.

Mradi wa Bomba la Mafuta Waurejesha Mkoa wa Tanga Katika Historia

August 06, 2017
Na: Judith Mhina – MAELEZO

Hakika historia imejirudia, mkoa wa Tanga ni kati ya mikoa mashuhuri nchini Tanzania kabla ya uhuru wa Tanganyika katika kupigania uhuru, kwa kuwa ni mkoa uliokuwa na wasomi wengi kuliko mikoa mingine wakati huo.

Hii ilitokana na uwepo wa shule za wamisionari wa kanisa la Anglikana (UMCA) ambalo ni la kwanza kuingia katika Pwani ya Afrika Mashariki mwaka 1878 na waliojenga shule za Magila na Kiwanda Muheza, Korogwe misheni, Kideleko Handeni (Shule za Kati) na Saint Andrew Minaki Pwani (shule ya Sekondari).

Hata baada ya uhuru chini ya Serikali ya Awamu ya Kwanza na ya Pili ya uongozi wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere na Rais Msataafu Ali Hassan Mwinyi, mkoa wa Tanga ulikuwa maarufu kutokana na uwepo wa viwanda vingi, njia za reli na Bandari yenye kina kirefu yenye uwezo wa kuingiza meli kubwa za mizigo za Kitaifa na Kimataifa.

Viwanda ambavyo vilijengwa katika mkoa wa Tanga ni pamoja na vya chuma, mbolea, saruji, maziwa, kamba za katani na mazulia, amboni plastic, mbao, sabuni maarufu ya mbuni, gardenia, foma na mafuta ya nazi.

Historia hii sasa inajirudia katika mkoa wa Tanga baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli, kupigania kwa nguvu zote Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda kuja nchini Tanzania ambalo litaishia katika kijiji cha Chongoleani.

Wananchi wote wa Tanzania wana kila sababu ya kujivunia ujenzi wa bomba hilo la mafuta ambalo litawapatia ajira Watanzania hususan wananchi wa mkoa wa Tanga. Pongezi kubwa ziende kwa Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za kuhakikisha kwamba Mradi huu unakuja Tanzania. Wananchi wa mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla wana kila sababu ya kulinda heshima ya nchi yetu kwa kuhakikisha kuwa kunakuwepo na ulinzi mkali wa Bomba hilo kila mahali lilikopita.

Kurejea kwa mkoa wa tanga katika ramani ya Tanzania ya viwanda umedhihirishwa na Wananchi wa Chongoleani ambao siku ya uwekaji jiwe la msingi walikuwa wawakilishi wa Watanzania ambao hawakupata fursa ya kwenda Tanga kumshuhudia Mheshimiwa Rais na na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Kaguta Museveni wakifungua pazia la jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa Mradi huo.

Kutokana na tukio hilo la uwekaji wa jiwe la msingi wana Chongoleani walitoa ya moyoni kwa kuonyesha furaha yao isiyo na kifani kupitia kwa Mwenyekiti wao wa kijiji Ndugu Mbwana Nondo wakisema; “Kwa moyo wa dhati kabisa tunamshukuru sana Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutujali Wananchi wake kwa kutuletea neema ya mradi huu wa bomba la mafuta”.

Aidha, Mwenyekiti huyo aliongeza kwa kusema kwamba, katika maisha yetu Wananchi wa Chongoleani hatutaweza kumsahau Mheshimiwa Rais kwa mambo mengi anayowafanyia Watanzania na Taifa kwa ujumla na itakuwa ni kumbukumbu kwa kizazi kijacho.

“Napenda kusisitiza kwamba tunamuahidi Rais, kuwa wote watakaopata fursa kwenye Mradi huu wa Bomba la Mafuta, watafanyakazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla”. Alihitimisha Bw Nondo.

Naye Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Bibi Ummy Mwalimu, amewaomba wanawake wa Mkoa wa Tanga kuchangamkia fursa zinazojitokeza, kutokana na uwepo wa mradi wa bomba la mafuta.

Akisisitiza kuhusu ajira hizo amesema; “Kwa wale wenye ujuzi wanaweza kupata ajira za kudumu katika mradi, ila kwa wale ambao hawana ujuzi wachangamkie fursa nyingine kama mama lishe ambapo mkoa unjulikana kwa kujua kupika mapishi yanayovutia walaji wengi”

Aidha, amewaasa wakulima kuona fursa ya kulima mazao ambayo yataliwa kwa wingi kwa watumishi watakaoajiriwa Tanga katika mradi wa bomba la mafuta. Mfano matunda na mbogamboga ambavyo ni sehemu ya kuimarisha lishe za watumishi hao watakao kaa Tanga.

Mradi wa Bomba la Mafuta ni ishara njema kwa Watanzania, Serikali na Taifa kwa ujumla maana inaonyesha dhahiri kukosekana kwa fursa kama hii kwa miaka mingi katika mkoa wa Tanga ni fundisho kwa Watanzania hususan Wananchi wa mkoa wa Tanga kama waswahili wasemavyo “usichezee shilingi chooni” ikiwa na maana shilingi ikitumbukia kuipata sio rahisi.

Kila jambo jema lina fursa zake, nalo bomba la mafuta limekuja na neema zake, mfano wana Chongoleani kupata barabara ya kilometa 8 inayowaunganisha na barabara kuu ya kutoka Tanga kwenda Horohoro. Hii ina maana kubwa kwa wana chongoleani kiuchumi, maana watakuwa na wepesi wa usafiri wa mabasi na malori. Hivyo, bidhaa zitokazo chongoleani sasa zitaenda Tanga na nje ya mkoa wa Tanga kwa urahisi. Mfano samaki, mazao ya chakula na mengineyo.

Wafanyabiashara wetu wachangamkie fursa iliyojitokeza watembelee eneo husika na kudadisi kipi wanachoweza kufanya biashara kwa ajili ya kuinua kipato chao binafsi na Taifa kwa ujumla.

Kama tujuavyo Taifa letu liko kwenye harakati za kuelekea katika uchumi wa viwanda, na kama ujuavyo Tanga ni Mkoa wenye kuzalisha matunda ya aina mbalimbali na mbogamboga kwa wingi, nazi, katani, mahindi, viazi, maharagwe, samaki, viungo kama tangawizi, iliki, pilipili manga, mdalasini, chai na mifugo kama ngombe mbuzi na kondoo wapo kwa makundi katika ranchi zinazotambulika na wale wanaofugwa kiasili.

MHANDISI MTIGUMWE AIPONGEZA TWCC KWA KUENDELEZA BIASHARA ZA WANAWAKE WAJASIRIAMALI NA WAFANYABIASHARA TANZANIA

August 06, 2017

Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mifugo na Uvuvi Mhandisi Methew Mtigumwe akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Mhe Rukia Muwango alipotembelea banda la Chama Kikuu cha kuendeleza biashara za wanawake wajasiriamali na wafanyabiashara Tanzania (TWCC)

Na Mathias Canal, Lindi

Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mifugo na Uvuvi Mhandisi Methew Mtigumwe amekipongeza Chama Kikuu cha kuendeleza biashara za wanawake wajasiriamali na wafanyabiashara Tanzania (TWCC) kwa kazi kubwa ya kuwaunganisha wanawake wafanyabiashara kutoka sekta zote.

Mhandisi Mtigumwe ameyasema hayo alipotembelea banda la TWCC wakati wa Maonesho ya Wakulima Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.

Msisitizo mkubwa alisema chama hicho kinapaswa kuwafikia wanawake wengi zaidi nchini wenye dhamira na ndoto ya kufanikiwa katika ujasiriamali na biashara ndogondogo na kubwa ikiwa ni sehemu ya kubaini fursa zilizopo kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi.

Alisema kuwa wawake wanatakiwa kuandaliwa kuwa na umoja wa kutetea haki na kukuza biashara zao kwa kutumia za mikakati nje na ndani ya nchi.

Mhandisi Mtigumwe aliongeza kuwa wanawake wanatakiwa kuwa na umoja, nguvu, sauti na mikakati ya pamoja yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kujikwamua kiuchumi na kijamii.

Mwanachama wa Chama Kikuu cha kuendeleza biashara za wanawake wajasiriamali na wafanyabiashara Tanzania (TWCC) ni mwanamke yeyote mjasiriamali anayemiliki kampuni au biashara iliyosajiliwa au kikundi, Taasisi binafsi, chama na vikundi, vya wanawake wafanyabiashara wa sekta yoyote.

Maonesho ya sikukuu ya wakulima Nanenane yanahusisha shughuli za wakulima, wafugaji wa mifugo, wafugaji wa nyuki, wavuvi, wanamazingira, wasindikaji wa bidhaa za mazao ya kilimo na mifugo, wizara taasisi/makampuni ya umma, makampuni binaf si, mabenki, Taasisi za umma na binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali.
 
Pia uzalishaji bora wa mazao ya nafaka, ubunifu wa teknolojia rahisi za kutotoa mayai, Kuongeza thamani ya mazao ya mifugo, Makampuni ya mawasiliano, ambapo Taasisi za elimu zitaonyesha ubunifu wa kumsaidia mfugaji, Tiba za asili, Wasindikaji wakubwa na wadogo wa mazao ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Asali, na Nta. 

WILAYA YA NEWALA MKOANI MTWARA INAKABILIWA NA UHABA MKUBWA WA MAOFISA UGANI NA MIFUGO

August 06, 2017

Mwezeshaji kutoka Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Emmarold Mneney (kulia), akitoa mafunzo ya siku moja ya kilimo chenye tija  kwa wakulima wa Mkoa wa Mtwara  kwenye Maonyesho ya Kitaifa ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Ngongo mkoani Lindi jana.
MPINA ALIPONGEZA JIJI LA MWANZA KWA UJENZI WA DAMPO NA MACHINJIO YA KISASA

MPINA ALIPONGEZA JIJI LA MWANZA KWA UJENZI WA DAMPO NA MACHINJIO YA KISASA

August 06, 2017
DSC_0006
Karakana za kisasa zilizojengwa katika Dampo la jiji la Mwanza.
DSC_0012
Mwenye Kofia Nyeupe Msimamizi wa Dampo la jiji la Mwanza (Site Manager) Bw. Desderius Pole akimuonyesha Naibu Waziri Mpina tokea mbali karakana za kisasa hazipo katika picha zilizojengwa katika Dampo la jiji hilo, kulia ni wana habari kazini.
DSC_0040
Afisa Mazingira wa jiji la Mwanza wa pili kulia Bi Lidya Nyeme, akimuelezea Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira na Ujumbe wake katika picha kuhusu machinjio ya kisasa ya Jiji la Mwanza iliyojengwa kwa ufadhili wa Bank ya Dunia kupitia  Mradi wa hifadhi ya mazingira ya Ziwa Victoria (LVEMP) uliyopo chini ya Wizara ya Maji, Naibu Waziri Mpina yupo katika Ziara ya kikazi jijini Mwanza.
…………………………………………………..
NA EVELYN MKOKOI – MWANZA
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu w rais Muungano na mazingira amelipongeza jiji la mwanza kwa hatua iliyochukua ya kutunza mazingira kwa ujenzi wa Dampo na machinjio ya kisasa kwa lengo la kupunguza uharibifu na uchafuzi wa mazingira kutokana na utupaji taka ovyo.
Aidha, amelipongeza jiji hilo kwa maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya dampo la kisasa kama mizani ya kupimia taka, ofisi na maabara ya kemikali katika dampo hilo uliopelekea jiji hilo kufuzu kupata ufadhili kupitia Bank ya dunia licha ya kutumia mapato ya ndani.”Nikiangalia naona mmewekeza kama zaidi ya milioni 700 ambayo mumewekeza kama manispaa ya Jiji la mwanza.” Alisema Mpina.
Mpina aliongeza kwa kusema kuwa kwa jiji la mwanza kufanya hivyo ni hatua kubwa na kulitaka jiji hilo kuendelea na ari hiyo katika suala zima la hifadhi na utunzaji wa mazingira. Mpina pia aliitaka Manispaa hiyo kukamilisha kwa wakati hatua nyingine za ujenzi wa dampo hilo kama vile za Tathmini ya Athari kwa Mazingira na kulipa fidia kwa wananchi na kaya zilizobakia  ili kukamilisha upanuzia wa dampo hilo, na kuepuka vipingamizi visivyo vya lazima.
Katika hatua nyingine Mpina pia aliwapongeza wahisani kwa kuiamini serikali ya awamu ya tano katika mambo mengi ikiwa ni pamoja na   kuwekeza katika suala zima la hifadhi ya mazingira. “Naamini katika mradi huu unaokuja wa zaidi ya shilingi Bilioni 19.8 miundombinu ya hapa itakuwa ni mizuri na rafiki zaidi kwa mazingira, kikubwa zaidi ni kuwekeza nguvu zetu katika mradi huu na kuhakikisha kuwa unatekelezwa kama ulivyopangwa”. Alisema Mpina.
Wakati huo huo Naibu Waziri Mpina alitembelea Machinjio ya kisasa ya jiji la Mwanza na kujionea ukarabati wa machinjio unahusisha utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mtambo wa kisasa wa kutibu majitaka yanayotoka katika machinjio hayo ambapo mtambo huo utazalisha pia biagas kwa ajili ya kuzalisha nishati ya umeme na kuzalisha mbolea. Ukarabati huo unahusisha pia ujenzi wa chumba cha kisasa cha kuhifadhia nyama kitakachowezesha wafanyabiashara ya nyama kusafirisha nje ya nchi.
Katika hali isiyo ya kawaida Naibu Waziri Mpina alitembelea kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Senrun Investment kilichopo eneo la Igoma na kusisitiza kiwanda hicho kiendelee kufungwa kutokana na kubainika kuendesha shughuli zake kinyume na Sheria kwa kutokuwa na vibali vya uchenjuaji dhahabu, cheti cha Tathmini ya athari kwa Mazingira na kibali cha matumizi ya kemikali kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali. “Nasisitiza kwamba kiwanda hiki kiendelee kufungwa kama ambavyo NEMC wamekifunga na nawataka wamiliki kuwasilisha vibali husika ndani ya siku 7 na wasiendelee na uzalishaji mpaka watakapomaliza zoezi la kufanya tathmini ya athari kwa mazingira”. Awali kiwanda hicho kilifungwa na NEMC kufuatia malalamiko ya wananchi wa maeneo hayo kwa kutiririsha maji yenye kemikali, kutoa moshi mkali kutokana na uchomaji wa taka zenye sumu na kutokuwa na vibali muhimu vya kuruhusu uendeshaji wa shughuli za uchenjuaji dhahabu.

Makonda, Ruge na Tanzania All Stars wanogesha sherehe za uwekaji jiwe la msingi la mradi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga kijijini Chongolieni

August 06, 2017
 Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzania All Stars wakijiandaa kupanda jukwaani kutumbuiza kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
 Wasanii nyota wa filamu wa Bongo Movie wakiwa  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwaomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wamalize tofauti zao na kuweka maslahi ya nchi mbele wakati alipohutubia kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
 Baada ya kupatanishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba walishuka jukwaani bega kwa bega huku wakitabasamu.
 Kisha wakaelekea kwenye jukwaa la wasanii wa Tanzania All Stars
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wakiwa jukwaani bega kwa bega huku wakiimba na Tanzania All Stars
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wakiwa jukwaani bega kwa bega huku wakiimba na Tanzania All Stars
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wakiwa jukwaani bega kwa bega huku wakiimba na Tanzania All Stars
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wakiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wakiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
  Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigella  akiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
 Naibu Waziri Mkuu wa Uganda Dkt Ali Kirunda Kivenjija akiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016

   Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wakiwa jukwaani bega kwa bega huku wakiimba na Tanzania All Stars. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.  Ashatu Kijaji wakiwatuza Tanzania All Stars kwa kutumbuiza vyema  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016