March 15, 2014

MATUKIO MBALIMBALI KUELEKEA MIAKA 50 YA MUUNGANO KUFANYIKA.

Msemaji wa Serikali Bw.Assah Mwambene akizungumza na waandishi wa Habari jana jijini Dar es salaam.
****************************************
Na. Aron Msigwa - MAELEZO.
SERIKALI imetoa wito kwa wananchi na vyombo vya habari kushiriki katika shughuli na matukio  mbalimbali ya  maadhimisho ya Sherehe za miaka 50 ya Muungano  yanayofanyika katika maeneo mbalimbali nchini  ambayo kilele chake kitakuwa tarehe 26,April 2014,  siku ya maadhimisho ya sherehe hizo.

Akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es salaam, Msemaji wa Serikali  na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu ambayo ni ya kipekee yanaongozwa na kauli mbiu isemayo Utanzania wetu ni Muungano Wetu, Tuulinde, Tuuimarishe na Kuudumisha  yanaambatana na matukio mbalimbali yanayozihusisha wizara na taasisi mbalimbali za Muungano.
March 15, 2014

RIDHIWANI AANZA MBIO ZA KUSAKA KURA JIMBO LA CHALINZE

 
Meneja wa Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Steven Kazidi (kushoto) akimuinua mkono juu kwa ishara ya kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo jana Machi 14,2014.
 
Mgombea Ubunge katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze (CCM),Ndg. Ridhiwani Jakaya Kikwete akiwahutubi wananchi wa Kijiji cha Matipwili,Saadani Wilayani Bagamoyo,wakati wa mkutano wa kwanza wa kampeni zake ulioanza rasmi jana Machi 14,2014.
March 15, 2014

KINANA KUHITIMISHA KAMPENI KALENGA LEO

Leo historia itaandikwa kwa mara ingine katika jimbo la Kalenga,mahala ambapo inaaminika kuwa ndipo alipotokea Chifu Mkwawa, Historia inaonyesha watu wa Iringa ni wastaarabu sana na wana penda kushirikiana katika kupanga maendeleo yao.

Katika kuhitimisha kampeni za Ubunge jimbo la Kalenga CCM leo itafanya mkutano mkubwa wa aina yake kutokea katika jimbo la Kalenga kukiwa na viongozi mbali mbali kutoka ngazi ya Taifa na Jumuiya zake wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

Kinana ambaye anaaminika kukirudisha Chama kwenye mstari kutokana na sera zake za uwazi na ukweli na kushirikiana vizuri na kila mwananchi wa Tanzania leo ataungana na mgombea Ubunge jimbo la Kalenga kupitia CCM Ndugu Godfrey Mgimwa kuhitimisha safari ndefu ya kampeni huko Kidamali.
Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia) ,Naibu Katibu Mkuu CCM (Bara) Mwigulu Nchemba (Kushoto) kwa pamoja wakiinua mikono juu pamoja na mgombea wa ubunge jimbo la Kalenga Ndugu Godfery Mgimwa .
Godfrey Mgimwa akiwa amebebwa juu na wanachama na wapenzi wa CCM wakati akiingia kwenye viwanja vya mkutano Kalenga A. Moja ya sifa kubwa inayomuhakikishia ushindi Godfrey Mgimwa ni kutambua kuwa wana Kalenga ni ndugu zake ,wazazi wake, na marafiki zake na yupo tayari usiku na mchana kushiriki kuleta maendeleo ya jimbo hio.