Serikali kupitia Idara ya Menejimenti ya maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu imeendelea kuimarisha mifumo ya usimamizi wa masuala ya maafa nchini ili kuendelea kuwa na mikakati thabiti ya kukabiliana na maafa nchini.
PEXPLA TANZANIA, CHEMBA YA BIASHARA YA CHINA KUWAWEZESHA WAFANYABIASHARA WA TANZANIA
Mwenyekiti wa Bodi taasisi ya PEXPLA - TANZANIA) Jenipha Japheth (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chemba ya Biashara ya Jinhua nchini China, anaye shughulika na mahusiano ya Biashara na Afrika, Jin Yongming walipokutana katika kikao cha pamoja kilichofanyika katika Jiji la Hangzhou nchini China Mwenyekiti wa Bodi taasisi ya PEXPLA - TANZANIA) Jenipha Japheth, akizungumza na ujumbe wa Chemba ya Biashara ya Jinhua ya nchini China (hawamo pichani), wakati wa kikao chao kilicholenga kuimarisha ushirikiano wa kibiashara baina ya wafanyabiasha wa Tanzania na China, kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika Jiji la Hangzhou China. Mwenyekiti wa Bodi taasisi ya PEXPLA - TANZANIA) Jenipha Japheth (kulia) akimsikiliza Katibu Mkuu wa Chemba ya Biashara ya Jinhua nchini China, anaye shughulika na mahusiano ya Biashara na Afrika, Jin Yongming (kushoto), wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika Jijini Hangzhou chini China. Mwenyekiti wa Bodi taasisi ya PEXPLA - TANZANIA) Jenipha Japheth (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jumuiya ya Vijana ya Sayansi na Teknolojia ya Jinhua chini China, Jiang Jingwei.
...............................
Na: Hughes Dugilo, Hangzhou, CHINA
Mwenyekiti wa Bodi wa taasisi inayojihusisha na kuwawezesha Wafanyabiasha ya Professional Exchange Platform, (PEXPLA - TANZANIA) Bi Jenipha Japheth, amesema kuwa wafanyabiasha wa Tanzania wanaweza kunufaika na uwepo wa mashirikiano ya Kibiashara baina ya taasisi hiyo na Chemba ya Biashara ya Jinhua ya nchini China, kwa kuwafungulia milango ya kuongeza wigo wa masoko yao na kukopeshwa mitaji.
Akizungumza katika kikao maaluum kati ya taasisi hizo mbili, kilichofanyika mwishoni mwa wiki katika Jiji la Hangzhou nchini China, Jenipha amesema kuwa makubaliano yaliyofikiwa baina yao yanakwenda kuongeza fursa za kibiashara kwa wafanyabiasha wa Tanzania.
"Kikao hiki ni muendelezo wa taasisi yetu ya PEXPLA katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan za kuwainua wafanyabiasha wa dogo, wakati na wakubwa.
"Pia PEXPLA ina jukumu la kukuza mitaji ya Wafanyabiasha, ambapo kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kuanza kuwadhamini wafanyabiasha hao ili waweze kuchukua mzigo kutoka kwa wazalishaji wa China kwa mkopo, na kuziuza na baadae kujisimamia wenyewe katika Biashara zao" amesema Jenipha.
Ameeleza kuwa taasisi hiyo pia imeweza kutoa udhamini kwa wafanyabiasha zaidi ya 300 kwenda nchini China, kujifunza na kujionea fursa mbalimbali za kibiashara, huku ikiwakutanisha na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali katika mazungumzo ya ana kwa ana.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chemba ya Biashara ya Jinhua nchini China, anayeshughulika na mahusiano ya Biashara na Afrika, Jin Yongming ameishukuru taasisi ya PEXPLA kwa kuonesha nia ya kuongeza wigo kwa wafanyabiasha wa Tanzania, na kuahidi kuendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi kwa wafanyabiasha hao ili kufikia malengo yao.:
RAIS SAMIA NA RAIS WA ZAMBIA WAKIWA KATIKA MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI LUSAKA ZAMBIA
Jiji la Mwanza laanzisha mahusiano na Jiji la Tulsa, Marekani
TAASISI ZA FEDHA ZIMEOMBWA KURAHISISHA HUDUMA ZA KIFEDHA KWA WALEMAVU
Na Pamela Mollel,Arusha
Taasisi za Fedha zimeombwa kurahisisha huduma za kifedha Kwa watu wenye ulemavu hususan wa macho.
Hayo yamesemwa kwenye Mkutano wa wiki ya azaki unaoendelea jijinibl Arusha ambapo wameomba kupatiwa mfumo shirikishi utakaowasaidia kwenye utumiaji wa Teknolojia katika eneo la kifedha.
Mmoja wa walemavu wa macho Renatusi Rupoli kutoka Iringa amesema watu wasioona huwa wanatumia mitandao kwa njia ya sauti ambapo alihoji kwanini kusiwepo na Software kama hizo ambazo zinajumlishwa kwenye Mashine za Kutolea pesa (ATM) Benki Ili kupunguza usumbufu wakutafuta wasaidizi wakati wa kutumia huduma hizo.
Akizungumza katika Mkutano huo Amali Baziadi kutoka Benki ya Stanbic amesema changamoto hiyo ameichukua na kwamba wataona namna gani yakulifanyia kazi ili kupata ufumbuzi.
"Ninaimani kuwa siyo tu Stanbic pekee ambao hatuna huduma hii lakini naichukua kama changamoto na tuone namna gani tunaifanyia kazi ili kuwawezesha wateja wetu kupata huduma rafiki kwao"amesema Baziadi.
Aidha wadau hao wameshauri kuwepo kwa huduma rafiki Kwa wazee na wananchi waishio Vijijini namna ambavyo wanaweza kufungua akaunti za Benki kwa kutumia mitandao badala ya kufuata huduma hizo kwa mawakala wa Benki ambao mara nyingi hupatikana mijini.
Mwishooo.
TUME YA MADINI YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA UWEKEZAJI SEKTA YA MADINI
Tume ya Madini kwa kushirikiana na Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Madini leo Oktoba 25, 2023 inashiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji Sekta ya Madini unaoendelea katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa Tume wanaoshiriki ni pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula, Makamishna wa Tume ya Madini, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Eng. Yahya Samamba, Wakurugenzi, Mameneja na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa.
Mkutano huo unafunguliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko