SIMBA YASHINDWA KUITAMBIA COASTAL UNION

October 23, 2013
KOCHA MSAIDIZI WA SIMBA,JAMHURI KIWELU "JULIO"AKIFUATILIA MCHEZO WAO NA COASTAL UNION LEO AMBAPO TIMU HIZO ZILITOKA SULUHU PACHA YA KUTOKUFUNGANA.

KOCHA MKUU WA SIMBA,ABDALLAH KING KIBADENI AKIFUATILIA MCHEZO HUO




MCHEZAJI WA COASTAL UNION  CRISPIAN ODULLA AKIPEWA MAELEKEZO NA JOSEPH LAZARO AMBAYE LEO ALIKAA KWENYE BENCHI LA COASTAL KAMA KOCHA.


SIMBA YAVUTWA SHARUBU NA COASTAL UNION.

October 23, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
TIMU za soka Simba SC na Coastal Union “Wagosi wa Kaya” leo zimeshindwa kutambiana baada ya kulazimishana suluhu pacha ya kutokufungana kwenye mecho wa Ligi kuu Tanzania bara uliokuwa na upinzani mkubwa.

Mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la CCM Mkwakwani ulikuwa na upinzani mkubwa kutokana na timu zote kuonyesha kandanda nzuri na kushambuliana kwa zamu ambapo katika dakika ya 5 iliwachukua Coastal Union kufika langoni mwa Simba lakini shuti la Yayo Lutimba likatoka nje.

Baada ya shambulio hilo,Simba nao walijibu pigo hilo kwenye dakika ya 9 mpira adhabu uliopigwa na Nassoro Cholo uliwababatiza mabeki wa Coastal Union ukamfikia tena Cholo lakini shuti lake likapaa nje ya lango.

Dakika 20 Coastal Union tena walipata nafasi nzuri baada ya Chrispian Odula kuwatoa walinzi kaze na shamte na kutoa krosi kwa Daniel lyanga aliyogongewa vyema na Yayo Lutimba lakini shuto lake likapaa juu.

Kwenye dakika ya 32 Boban alipata nafasi akiwa na mlinda mlango wa Simba Abel Dhaira akazembea na kupiga shuti kali na kujikuta mpira ukitoka nje na kubakia kugongana na mlinda mlango huyo.

Katika dakika ya 37 Simba wanapata pigo baada ya mlinda mlango wao Abel Dhaira kutolewa nje kutokana na tukio la kugongana na boban na nafasi yake kuchukuliwa na Abuu Hashim aliyepandishwa kutoka Simba B.

Mlinda mlango huyo aliweza kuwa imara langoni mwa Simba ikiwemo kuokoa mpira uliotaka kwenda langoni mwao uliopigwa na Haruna Moshi Boban na hatimaye kuweza kuuokoa.

Mpaka timu zote zinakwenda mapumziko hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzie ambapo kipindi cha pili kilianza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana kwa zamu.

Katika dakika ya 78 Zahoro Pazi alipata pasi ya Messi na kuambaa winga ya ya kulia na kupiga krosi ambayo kado alitokea na kuiokoa huku akiishia kufanyiwa madhambi na kusababisha kutibiwa kwa dakika mbili.

Dakika ya 82Uhuru Seleman alishindwa kuungisha kori ya Haruna Moshi na kujikuta wakizidiwa maarifa na Gilbert Kaze aliweza kucheza vema na kuuokoa mpira.

Katika mchezo wa leo,Simba iliwakilishwa na Abel Dhaira,/Abuu Hashim,,Said Masoud,/Christopher Edward,Haruna Shamte,Joseph Owino,Gilbert Kaze,Jonas Mkude,Ramadhani Singano,Said Ndemla,Hamis Tambwe,Amri Kiemba/Zahoro Pazi na William Lucian.

Coastal Union waliwakilishwa na Shabani Kado,Mbwana Hamis,Othuman Tamim,Marcus Raphael,Juma Nyoso,Jerry Santos,Daniel Lyanga,Christopher Ochela,Yayo Lutimba,Haruna Moshi Bobani,Keneth Masumbuko.