RAIS KIKWETE ALIPOKUTANA NA RAIS GOODLUCK JONATHAN WA NIGERIA JIJINI ABUJA JANA

May 08, 2014


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akikaribishwa na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Goodluck Jonatahn wa Nigeria jijini Abuja jana pembeni ya Mkutano wa Dunia wa Uchumi. PICHA NA IKULU

LULU AOMBA BASATA WARUHUSU KUFANYA MOVIE NUSU UTUPU WAENDANE NA SOKO LA KIMATAIFA

May 08, 2014
DIVA wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ ameziomba mamlaka zinazosimamia maadili ya filamu nchini ziwaruhusu wasanii waigize nusu utupu ili kuendana na soko la kimataifa.
Akitetea hoja yake mbele ya paparazi wetu, staa huyo aliyeitendea haki filamu ya Foolish Age alitolea mfano Tamthiliya ya Shuga iliyomtoa Lupita Nyong’o ambayo alicheza akiwa nusu utupu.

“Wanasema hatufuati maadili wakati kuna muvi ambazo zipo theatre na watu wanaangalia hazina maadili, wao wanataka tufanye vitu kwa kudanganya wakati sasa hivi tuko dunia ambayo tuna takiwa tuweke vitu wazi, wasibane sana,” alisema Lulu.
Na Andrew Carlos, GPL

BASI DOGO AINA YA COASTER LAPATA AJALI MOMBO NA KUJERUHI KADHAA

May 08, 2014

Ajali imetokea mombo leo hii. Coastal iliyoanguka ilikuwa na watu 25, Mungu kasaidia hakuna aliyekufa. Hongereni sana madaktari wa Magunga kwa kazi nzuri! - Mkuu wa wilaya ya Korogwe, Mrisho Gambo. 




 Tunawapa pole majeruhi wote na tunawatakia nafuu ya haraka

EU KUISAIDIA TANZANIA MSAADA WA SHILINGI BILIONI 134

May 08, 2014


 Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacious Likwelile (kulia) akisaini mkataba wa msaada wa sh. Bilioni 134 kwa niaba ya Serikali ya Tanzania leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Balozi EU nchini Filberto Sebregond.



Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacious Likwelile (kulia) akibadilishana hati ya mkataba wa msaada wa sh. Bilioni 134 waliosaini kwa niaba ya Serikali ya Tanzania leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Balozi EU nchini Filberto Sebregond.

Na Eleuteri Mangi-MAELEZO


SERIKALI ya Tanzania imetiliana saini mkataba wa msaada wa zaidi ya Shilingi Bilioni 134 sawa na Euro milioni 59.5 kutoka Umoja wa Ulaya (EU) kusaidia sekta ya kilimo na usafirishaji nchini.

Mkataba huo ulisainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa EU nchini Filberto Sebregond leo jijini Dar es salaam.

Akizungumza baada ya kutia saini mkataba huo, Dkt. Likwelile alisema kuwa sehemu ya msaada huo ambao ni Shilingi Bilioni 82.4 ambazo ni sawa na Euro milioni 36.5 utatumika kuendeleza sekta ya kilimo na kukuza uchumi nchini kwa kupitia kituo  maalum cha uendelezaji kilimo ukanda wa Kusini Tanzania (SAGCOT) na kuboresha miundombinu ya barabara za ukanda huo.

Vilevile Dkt. Likwelile alisema kuwa sehemu iliyobaki ya msaada huo ambao ni Shilingi Bilioni 51.9 ambazo ni sawa na Euro milioni 23 itatumika kuimarisha biashara na ushirikiano katika jumuiya kwa kuanzisha  kituo cha pamoja cha ukaguzi mipakani (OSIS).
“Vituo hivyo vya ukaguzi mipakani vitakuwa na manufaa si kwa Tanzania tu, bali hata katika nchi mbalimbali zinazopakana na Tanzania” alisema Dkt. Lkwelile.

Alifafanua kuwa msaada uliosainiwa unamanufaa kwa wananchi kwa kuboresha miundombinu vijijini na kusambaza umeme vitu ambavyo vitasaidia kukuza uchumi na kupunguza umaskini nchini.

MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA WAANZA LEO MKOANI TANGA.

May 08, 2014

KAIMU  KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA AKITOA HOTUBA YAKE LEO WAKATI AKIFUNGUA   MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA LEO KWENYE UKUMBI WA HOTEL YA TANGA BEACH RESORT.

KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI,CHARLES CHACHA AKIZUNGUMZA KATIKA MKUTANO HUO KUSHOTO NI  MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU WA WIZARA YA UCHUKUZI,ISSA NCHASI KULIA NI KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA

MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU WA WIZARA YA UCHUKUZI,ISSA NCHASI AKIZUNGUMZA LEO WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA NCHINI,KATIKATI NI KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE,CHARLES CHACHA NA KAIMU  KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA AMBAYE ALIMUWAKILISHA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA
WA KWANZA KULIA NI KAIMU  KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA AMBAYE ALIMUWAKILISHA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KATIKATI NI KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI,CHARLES CHACHA NA WA KWANZA KUSHOTO NI MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU WA WIZARA YA UCHUKUZI,ISSA NCHASI.

KUSHOTO WA KWANZA NI KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI,CHARLES CHACHA AKISISITIZA JAMBO KWENYE MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA ULIOFANYIKA LEO KWENYE HOTEL YA TANGA BEACH RESOT.
KAIMU KATIBU TAWALA WA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA WA KWANZA KUSHOTO AMBAYE ALIMUWAKILISHA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KWENYE UFUNGUZI WA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA LEO ULIOFANYIKA KWENYE HOTEL YA TANGA,BEACH RESORT AKIFUATILIA KWA UMAKINI HOTUBA YA  KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI,CHARLES CHACHE
SEHEMU YA WAJUMBE KWENYE MKUTANO HUO LEO
WAJUMBE WAKIFUATILIA HOTUBA YA MGENI RASMI KWENYE MKUTANO HUO
WAJUMBE WAKIFUATILIA HOTUBA YA MGENI RASMI KWENYE MKUTANO HUO
KATIKATI NI KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI,CHARLES CHACHA KUSHOTO NI KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA,MONICA KINALA AMBAYE ALIMUWAKILISHA MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA WA KWANZA NI
MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU WA WIZARA YA UCHUKUZI,ISSA NCHASI WAKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA WAJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA NCHINI.