DK. Shein Aendelea na Mikutano yake ya Kampeni Zanzibar Akiwahutubia Wananchi wa Bumbwini Makoba Wilaya ya Kaskazini B.

October 06, 2015

Mama Fatma Karume akishuka jukwaani baada ya kuwahutubia Wananchi na Wana CCM katika viwanja vya mpira bumbwini makoba wakati wa mkutano wa Mgombea Urais wa Zanzibar Dk Shein, mkutano uliofanyika katika Jimbo la Bumbwini Unguja.
Mgombea wa Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, akimpongeza Mama Fatma Karume baada ya kuwahutubia Wananchi na kumuombea Kura kwa Wananchi wakati wa Mkutano huo wa Kampeni katika Wilaya ya Kaskazini B uliofanyika viwanja vya mpira bumbwini makoba.
Umati wa Wanachama wa CCM wakiwa katika viwanja vya mpira bumbwini makoba wakihudhuria mkutano wa mgombea wa CCM Dk Ali Mohamed Shein. 
Mbunge wa Jimbo la Mpendae Mhe Salim Turky (Mr White) akiwa katika mkutano wa mgombea Urais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein, uliofanyika katika viwanja vya bumbwini makoba wakimsikiliza Mgombea.
Mwakilishi wa Jimbo la Tumbatu Mhe Haji Omar Kheri akiwahutubia Wananchi katika mkutano wa kampeni ya Mgombea wa CCM Dk Shein, katika viwanja vya bumbwini makomba na kumuombea Kura Dk Shein, ili kuendeleza amani na utilivu na Masendeleo ya Wazanzibar.
Kada wa CCM Balozi Amina Salim Ali akiwahutubia Wananchi na Wanachama wa CCM katika mkutano wa kampeni ya Mgombea wa CCM Dk Shein 
Baadhi ya Wagombea wa CCM wakifuatilia mkutano wa Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia CCM Dk. Ali Mohamed Shein, uliofanyika Wilaya ya Kaskazini B Unguja katika viwanja vya mpira bumbwini makoba.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »