Rais wa Shirikisho la Riadha
Tanzania (RT), Anthony Mtaka akimpongeza rais mpya wa Shirikisho la
Riadha Duniani (IAAF), Lord Sebastain Coe mara baada ya kushinda katika
uchaguzi mkuu nchini China. Mtaka yupo nchini China akiwakisha RT katika
mkutano mkuu wa IAAF na kupiga kura kumchagua kiongozi mpya.
Rais wa Shirikisho la Riadha
Tanzania (RT), Anthony Mtaka akipokea msaada wa wa vifaa vya michezo
kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Nike, Rebet Jones mjini Beijing
China. Mtaka yupo nchini China akiwakisha RT katika mkutano mkuu wa IAAF
na kupiga kura kumchagua kiongozi mpya.
……………………………………………………………………………………
Wanariadha
wanne wa Tanzania, Jumamosi (Agosti 22) wataingia uwanjani kuwania
medali za mashindano ya 15 ya Shirikisho la Riadha Duniani (15th IAAF World Championship) upande wa mbio ndefu (marathon) yanayoanza leo mjini Beijing nchini China.
Wanariadha
hao Fabian Joseph, Alphonce Felix na Ezekiel Jaffery ambao watashindani
katika marathon wakati Ismail Juma atashindana katika mbio za mita
10,000. Mashindano hayo yatafanyika kwenye uwanja wa Taifa wa Beijing
maarufu kwa jina la Kiota cha Ndege.
Rais wa
Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka alisema kuwa
wanatarajia kupata medali kupitia wanariadha hao kutokana na maandalizi
waliyoyafanya.
Mtaka
ambaye yupo China alisema kuwa wanariadha hao wapo katika hali nzuri na
morali yao ipo juu tayari kuiwakilisha vyema nchi yao.
“Wanariadha
wetu wapo katika hali nzuri na lengo lao kubwa ni kushinda katika mbio
hizo, wanaoshiriki marathon wataingia uwanjani alfajiri wakati Ismail
ataingia uwanjani jioni kuwania medali pia,” alisema Mtaka.
Mtaka ambaye
pia ni Mkuu wa wilaya ya Hai, alisema kuwa Rais mpya wa Shirikisho la
Riadha Duniani, Lord Sebastian Coe ameahidi kuisaidia Tanzania katika
kuboresha mchezo wa riadha.
“Nimezungumza
naye na ameahidi kutupa sapoti kubwa na kurejesha heshima ya mchezo huo
kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma, nimefarijika sana,” alisema.
Katika hatua
nyingine Mtaka alisema kuwa RT limepokea msaada wa vifaa vya michezo
vya timu ya shirikisho hilo kutoka kwa kampuni ya Nike vifaa hivyo
watatumia wanariadha wetu waliopo Beijing.
Alisema
kampuni hiyo imetoa msaada huo kufuatia maombi yaliowasilishwa RT mapema
mwaka huu ambapo pia kampuni hiyo imeahidi kuuanga mkono mchezo huo kwa
kuendelea kutoa msiaada ya vifaa vya michezo katika mashindano yajayo
ya kimataifa.