Wanariadha wanne Tanzania kuwania medali leo China

August 21, 2015

ant1
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka akimpongeza rais mpya wa Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF), Lord Sebastain Coe mara baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu nchini China. Mtaka yupo nchini China akiwakisha RT katika mkutano mkuu wa IAAF na kupiga kura kumchagua kiongozi mpya.
ant2 
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka akipokea msaada wa wa vifaa vya michezo kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya Nike, Rebet Jones mjini Beijing China. Mtaka yupo nchini China akiwakisha RT katika mkutano mkuu wa IAAF na kupiga kura kumchagua kiongozi mpya.
……………………………………………………………………………………
Wanariadha wanne wa Tanzania, Jumamosi (Agosti 22) wataingia uwanjani kuwania medali za mashindano ya 15 ya Shirikisho la Riadha Duniani (15th IAAF World Championship) upande wa mbio ndefu (marathon) yanayoanza leo mjini Beijing nchini China.
Wanariadha hao Fabian Joseph, Alphonce Felix na Ezekiel Jaffery ambao watashindani katika marathon wakati Ismail Juma atashindana katika mbio za mita 10,000. Mashindano hayo yatafanyika kwenye uwanja wa Taifa wa Beijing maarufu kwa jina la Kiota cha Ndege.
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka alisema kuwa wanatarajia kupata medali kupitia wanariadha hao  kutokana na maandalizi waliyoyafanya.
Mtaka  ambaye yupo China alisema kuwa wanariadha hao wapo katika hali nzuri na morali yao ipo juu tayari kuiwakilisha vyema nchi yao.
 “Wanariadha wetu wapo katika hali nzuri na lengo lao kubwa ni kushinda katika mbio hizo, wanaoshiriki marathon wataingia uwanjani alfajiri wakati Ismail ataingia uwanjani jioni kuwania medali pia,” alisema Mtaka.
Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Hai, alisema kuwa Rais mpya wa Shirikisho la Riadha Duniani, Lord Sebastian Coe ameahidi kuisaidia Tanzania katika kuboresha mchezo wa riadha.
“Nimezungumza naye na ameahidi kutupa sapoti kubwa na kurejesha heshima ya mchezo huo kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma, nimefarijika sana,” alisema.
Katika hatua nyingine Mtaka alisema kuwa RT limepokea msaada wa vifaa vya michezo vya timu ya shirikisho hilo kutoka kwa kampuni ya  Nike vifaa hivyo watatumia wanariadha wetu waliopo Beijing.
Alisema kampuni hiyo imetoa msaada huo kufuatia maombi yaliowasilishwa RT mapema mwaka huu ambapo pia kampuni hiyo imeahidi kuuanga mkono mchezo huo kwa kuendelea kutoa msiaada ya vifaa vya michezo katika mashindano yajayo ya kimataifa.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »