Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akisalimiana na Rais wa Namibia Mheshimiwa Hage Geingob mara baada ya
mgeni huyo kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu
Julius Nyerere kwa ziara ya kiserikali nchini Tanzania tarehe
11.10.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akifuatana na mgeni wake Mke wa Rais wa Namibia Madam Monica Geingos
wakiwapungia mikono wananchi waliofika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere. Madam Monica ameambatana na mumewe Rais Hage
Geingob kwa ziara ya kiserikali nchini.
Rais Jakaya Kikwete na Mkewe Mama
Salma wakiwakaribisha wageni wao Rais Hage Geingob na Mkewe Madam
Monica Geingos Ikulu. Kiongozi huyo wa Namibia aliwasili nchini tarehe
11.10.2015 kwa ziara ya kiserikali.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akiwa katika mazungumzo ya faragha-tete a tete-na mgeni wake Mke wa Rais
wa Namibia Madam monica Geingos huko Ikulu tarehe 11.10.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete
akigonganisha glasi na Rais Hage Geingob wa Namibia wakati wa dhifa ya
kitaifa iliyoandaliwa na Rais Kikwete huko Ikulu tarehe 11.10.2015.
PICHA NA JOHN LUKUWI.