Na Anitha Jonas-Maelezo Dar es salaam
………………………………………………….
Tume ya Taifa ya Uchaguzi
yawaasa wapiga kura kote nchini kuhakiki taarifa zao katika vituo vya
vya kupiga kura siku nane kabla ya uchaguzi.
Hayo yamesema jana Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva alipokuwa akizungumza
katika mkutano na viongozi wa vyama vya siasa uliyofanyika Oktoba 12,
2015 jijini Dar es Salaam,
Jaji Lubuva amesema kuwa lengo
la mkutano huo ni kushauriana na vyama vya siasa katika kuelekea siku
ya uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 25 mwaka huu.
“Tume imepanga kuhakikisha kila
mpiga kura mwenye sifa ya kupiga kura anapata haki ya kupiga kura na
imeagiza wasimamizi wa kura kutoa nafasi za upendeleo kwa watu wenye
ulemavu wa aina mbalimbalina na imeandaa karatasi maalum za kupigia
kura kwa watu wenye walemavu wa kuona”,alisema Jaji Lubuva.
Aidha Jaji Lubuva aliwasihii
viongozi hao kunadi sera zao majukwaani badala ya kuilalamikia Tume
katika majukwaa wakati wa kampeni pia amewasaa wanasiasa hao kupeleka
malalamiko yao katika ofisi husika na kuacha kukimbilia waandishi wa
habari.
Mbali na hayo Mwenyekiti wa Tume
hiyo aliendelea kusisitiza juu ya viongozi wa vyama vya siasa wanao
walazimisha wapigia kura kubaki katika vituo vya kupigia kura kuacha
kauli hizo kwani kwa uzoefu unaonyesha kwamba wafuasi wa vyama
wanapokutana pamoja huweza kuchangia uvunjifu wa amani.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa
Uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw.Kailima Ramadhani alisema
Tume ilibani kuwa jumla ya watu 3,870 walioandikishwa hawakuwa raia wa
Tanzania na hivyo vitambulisho vyao vimerejeshwa Tume na taarifa zao
kufutwa kwenye kanzidata ya daftari la kudumu la kupiga kura.
“Katika kuelekea uchaguzi Tume
imeandaa vituo vya kupigia kura 65,105 ambapo Tanzania Bara ni vituo
63,525 na Zanzibar ni vituo 1,580 kila kituo kitakuwa na uwezo wa
kuhudumia wapiga kura 450 na kituo kitakacho kuwa na wapiga kura zaidi
ya 500 kitagawanywa katika vituo viwili,”alisema Bw.Ramadhan.
Mpaka sasa tume imeshasambaza
vifaa mbalimbali vya uchaguzi nchini, vifaa ambavyo havijasambazwa ni
pamoja na karatasi za kura, wino maalumu, karatasi za matokeo na muhuri
wa kituo kutokana na umuhimu wake ila vinatarajiwa kuisambazwa hivi
karibuni.