Na
Mbaruku Yusuph,Tanga
WILAYA ya Tanga katika mwaka huu wa 2013 mefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika sekta ya
elimu kwa ufaulu wa wanafunzi wa darasa
la saba ambao walifanya mtihani wao wa Taifa mwezi wa kumi ukilinganisha na matokeo ya mwaka jana.
Akizungumza
ofisini kwake kaimu Afisa elimu Jiji, Damas Kifanga alisema kuwa ufaulu huo
uliojumuisha shule 93 za Tanga mjini na Vijijini umeongezeka mwaka huu ingawa sekta hiyo ya
elimu inakabiliwa na changamoto nyingi.
Aidha
alisema katika sekta hiyo ya elimu Wilaya ya Tanga mwaka huu imefanikiwa kutoa
wanafunzi 4266 kati ya wanafunzi 6261 sawa na 40% ya ufaulu wa matokeo ya
darasa la saba ambapo ni tofauti na mwaka jana kitu ambacho kinaleta hamasa
katika sekta hiyo muhimu katika maisha ya kila siku.
Hata
hivyo Kifanga alisema kuwa ili kukabiliana na idadi ndogo ya wanafunzi
waliokosa nafasi za kujiunga na shule za serikali,ni lazima kuunganisha nguvu
kutoka serikalini,wazazi na taasisi zisizo za kiserikali ili kuweza kuinua
sekta hiyo ya elimu katika Wilaya ya Tanga Mjini.
Alisema
kuwa upo umuhimu wa utolewaji wa chakula mashuleni ili kuboresha mahudhurio na
kuwepo na usikivu mzuri wa wanafunzi pindi wawapo madarasani kitu ambacho bado
kinasuasua kwa baadhi ya shule na kupelekea kufikia malengo mazuri
waliojiwekea.
Kifanga
alizidi kusema kuwa uboreshwaji wa mindombinu ni muhimu katika sekta hiyo ili
kupunguza msongamano wa wanafunzi katika baadhi ya shule kitu ambacho kwa namna
moja au nyingine kinaweza kupunguza umakini kwa wanafunzi wawapo katika masomo
yao.
Bwana
Kifanga alitumia fursa hiyo kuiomba serikali kuongeza jitihada katika utowaji
wa fedha za uwendeshaji wa shughuli zote za elimu na kuwa saidia kukamilisha kwa wakati miundombinu amabyo wananchi
wanayanzisha kwa nguvu zao katika kuboresha elimu Wilayani humu.
Ameiomba
serikali kuwa Halmashauri zinapaswa kuboreshewa uewzo wa kifedha ili kuweza kusaidia mafunzo ya walimu waliopo
makazini ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi wa kielimu.