Na Oscar Assenga,Tanga.
BENDI ya mziki wa Dansi
nchini ya Mashujaa Music Band chini ya Rais wao Charles Baba wanatarajiwa
kufanya maonyesho mawili mkoani Tanga ambapo moja litafanyika kwenye ukumbi
wa Hotel ya Nyumbani Tanga mjini Januari 11mwaka huu.
Akizungumza na TANGA RAHA BLOG,Mratibu wa
Onyesho hilo,Steven Ngonyani “Maji Marefu”alisema onyesho hilo linatarajiwa
kuwa la aina yake hasa ukizingatia umahiri wa bendi hiyo mpaka ikafanikiwa chukua
tuzo tano za Kilimanjaro music award hapa nchini.
Maji Marefu ambaye pia ni
Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) alisema kabla ya kufanyika onyesho hilo bendi hiyo itafanya
onyesho lake la kwanza wilayani Korogwe Januari 10 mwaka huu ambapo
watatumbuiza kwenye ukumbi wake wa Mamba Club.
“Ninachoweza kusema maandalizi ya maonyesho
yote mawili yanaendelea vizuri na ninaamini wakazi wa wilaya ya Korogwe na jiji
la Tanga watapata burudani ya aina yake “Alisema Maji Marefu.
Kwa upande wake,Mkurugenzi wa
Masoko na Mawasiliano wa Mashujaa Group Limited,Maximilian Luhanga alisema
baada ya bendi hiyo kupata tuzo tano za Kilimanjaro Music Award wakaona wakati
huu wafanya maonyesho kwa wapenzi wao ili kuweza kuwapa shukrani.
Alisema bendi hiyo baada ya
kumaliza maonyesho yao
mkoani Tanga itazunguka nchi nzima ili kuweza kuwapa wapenzi wao ila kitu roho
inapenda kwa kuwapa burudani isiyo na kifani.
Aidha alisema wasanii wa
bendi hiyo watatua mkoani Tanga wakiongoza na Rais wao Charles Baba,Rapa mahiri wao Furgeson ambaye ni pia alipata tuzo
kutokana na umahiri wake.