CHADEMA KANDA YA KASKAZI:TUTAPITISHA WAGOMBEA WANAOKUBALIKA.

January 07, 2014
Na Oscar Assenga,Tanga.
KATIBU wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa amesema chama hicho kitahakikisha kinawapitisha wagombea wanaokubali kwenye chaguzi za udiwani na wenyeviti wa serikali za vijiji ambao unatarajiwa kufanyika hivi karibuni katika mikoa ya Tanga ,Kilimanjaro na Arusha kuziba nafasi zilizoachwa wazi lengo likiwa ni kushika hatamu ya uongozi kwenye chaguzi hizo.
 
Golugwa alisema hayo leo wakati akizungumza na TANGA RAHA ambapo alisema mikakati hiyo itakwenda sambamba na ufanyaji wa kampeni za kiustarabu kwa kueleza sera makini ambazo zitawapa hamasa wananchi kuweza kukichagua chama hicho lengo likiwa kuwapa maendeleo pamoja na kuzipatia ufumbuzi kero zinazowakabili.
 
Alisema umuhimu wa kuwaweka wagombea wanaokubali kwenye chaguzi hizo ni mkubwa sana kutokana na kutaka kutengeza historia ya kipekee kwa kuwa na madiwani wawili kwenye jimbo la Tanga ambao wataweza kuleta mabadiliko ya kiutendaji kwa viongozi wengine waliopo.
 
     “Chama chetu kitaingia kwenye mchakato wa kuangalia nani anaweza kuipeperusha bendera kwenye chaguzi hizo na ambaye atakuwa akikubalika kwa asilimia kubwa na wananchi wa mahala husika na sio vyenginevyo “Alisema Bolugwa.
 
Alisema kuelekea uchaguzi huo lazima wanachama na wapenzi wa chama hicho kuachana na makundi ambayo hayana tija kwao badala yake kuwa na mshikamano ambao utawawezesha kupata mafanikio ambayo yanapeleka kushika nyazifa za uongozi kwenye kata na vijiji hivyo.
 
Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika kutokana kata mbili mkoani Tanga ambazo ni Kiomoni na Mtae Jimbo la Mlalo wilayani Lushoto viongozi wao kutokuwepo kwa kufariki na kujiuzulu na hivyo kupelekea nafasi zao kubaki wazi.
 
Aliyataja maeneo mengine yaliyowazi ambapo uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika ni kata ya Sombeni Jimbo la Arusha,Kata ya Kiboroloni Jimbo la Moshi na Karachimbi Jimbo la Kiteto Manyara
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »