Release No. 002
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 7, 2014
SEMINA YA WAAMUZI, MAKAMISHNA JAN 13
Semina
ya waamuzi na makamishna wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la
Kwanza (FDL) inafanyika Januari 13 na 14 mwaka huu jijini Dar es
Salaam.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ndiye anayetarajiwa kufungua semina hiyo.
Wakati
huo huo, Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kimemwalika Rais
Malinzi kuwa mgeni rasmi kwenye mechi ya robo fainali ya Kombe la
Mapinduzi kati ya Simba na Chuoni itakayochezwa kesho (Januari 8 mwaka
huu) saa 2 usiku Uwanja wa Amaan.
MAKOCHA WA LESENI B WAKABIDHIWA VYETI
Katibu
Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine
amekabidhi leseni B kwa makocha walioshiriki kozi iliyofanyika mjini
Zanzibar mwaka jana.
Jamhuri
Kihwelo alipokea leseni hiyo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira wa
Miguu Afrika (CAF) kwa niaba ya washiriki wengine tisa waliofuzu mafunzo
hayo.
Makocha
wengine waliofuzu kozi hiyo iliyoendeshwa na mkufunzi Bhekisisa Boy
Mkhonta kutoka Swaziland ni Abdulghan Msoma, Hafidh Badru, Nasra Juma
Mohamed, Gulam Abdallah Rashid, Mohamed Ayoub Suleiman, Shaaban
Ramadhan, John Simkoko na Hemed Suleiman Ali.
Hivi
sasa Tanzania ina makocha 40 wenye leseni B za CAF baada ya wengine 31
kufuzu katika mafunzo yaliyofanyika mapema mwaka juzi jijini Dar es
Salaam chini ya mkufunzi Honor Janza kutoka Zambia.
Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)