Na Oscar Assenga,Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umemwagia sifa
Kocha mkuu wa timu hiyo Yusuph Chipo kutokana na uwezo wake kiutendaji alioufanya
kwa kipindi kifupi ambacho amekabidhiwa timu hiyo ambacho kinaonyesha
mafanikio makubwa kwao siku za mbeleni.
Akizungumza jana,Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union ya
Tanga,Hemed Aurora “Mpiganaji”alisema uwezo wa mwalimu huo umeweza kuchangia
kwa kiasi kikubwa timu yao ya pili kuweza kuchukua ubingwa wa kombe la uhai Cup
na kuweza kuipa heshima timu hiyo na mkoa wa Tanga kwa ujumla.
Aurora alisema kilichofanywa na kamati ya utendaji kwa kuamua
kumuondoa aliyekuwa kocha wao Hemed Moroco kilikuwa ni sahihi na cha kizalendo ambacho leo
hii kimeweza kuleta mapinduzi makubwa na maendeleo ya timu yao hasa kikosi cha pili.
Alisema kutokana na uwezo wake wana imani kubwa mzunguko wa
pili wa ligi kuu Tanzania bara wataweza kufanya vizuri kutokana na kocha huyo kupewa kila
anachokitaka na mshikamano uliopo baina wa wapenzi viongozi na wanachama wao.
Mwenyekiti huyo alisema kabla ya kuanza mzunguko wa pili wa
ligi kuu wanatarajiwa kuweka kambi ya wiki mbili Maskati nchini Omani ambayo
itakuwa na lengo la kukipa makali kikosi chao ambacho kinakabiliwa na michezo
yao ligi hiyo.
Alisema wakiwa nchini Omani wanatarajiwa kucheza mechi nne
za kirafiki ambapo hilo linategemea na ratiba ya wanyeji wao timu ya Finya FC
ya Omani ambayo inashiriki ligi kuu nchini humo.
Wakati huo huo,Aurora alioupongeza uongozi mpya wa
shirikisho la soka nchini (TFF)chini ya Rais wake Jamali Malinzi na Makamu wake Walece Karia kwa kuchaguliwa
kuongoza shirikisho hilo na kueleza kuwa anaamini watakuwa chachu ya maendeleo
ya mpira wa miguu hapa nchini.