RAIS NKURUNZIZA HAJULIKANI ALIKO, UWANJA WA NDEGE WAFUNGWA

May 13, 2015
Raisi Pierre Nkurunziza
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, inasemekana ameondoka nchini Tanzania saa moja baada ya kupatikana taarifa za kupinduliwa kwake na kiongozi mkuu wa majeshi yake Meja jenerali Godefroid Niyombare kutangaza kwamba amempindua.
Jenerali huyo mara baada ya tangazo lake, akaweka amri ya kufungwa kwa kiwanja cha kimataifa cha ndege nchini humo ikiwemo mipaka ya Burundi.
Hata hivyo haiko wazi ikiwa jeshi linamuunga mkono Meja jenerali Godefroid Niyombare. Naye msemaji wa rais wa Burundi, amesema kwamba wanajeshi watiifu kwa Rais ambaye alikuwa akihudhuria mkutano wa viongozi nchini Tanzania, amesema nchi iko shwari.
Maelfu ya watu wamekuwa katika shamra shamra katika mji mkuu wan chi hiyo Bujumbura baada ya wiki kadhaa za maandamano kumpinga katika maamuzi yake ya kugombea muhula wa tatu wa uongozi,na tayari mpaka sasa viongozi wakuu wa kanda wamelaani mapinduzi hayo.
Mgogoro wa Burundi umezusha wasi wasi wa kurejea katika ghasia baada ya miaka kumi na miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Zaidi ya watu elfu tatu walikufa katika vita vya kikabila kati ya wahutu na watutsi ,vita vilivyomalizwa muongo uliopita.na mgogoro wa sasa nchini humo umehusisha kwa kiasi kikubwa na masuala ya kisiasa. lakini,yaliyojiri Burundi hayana tofauti na kilichojiri katika nchi jirani ya Rwanda ambayo ilikumbwa na mauaji ya kimbari nayo ilikabiliwa na masuala ya ukabila.
Umoja wa mataifa umeonya hivi karibuni kwamba ikiwa ghasia zitasitishwa Burundi itakuwa na Amani na kama itakuwa vinginevyo basi nchi hiyo itarejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe .
CREDIT: BBC

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »