Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Vijana, James Kajugusi akiongea na Vijana kutoka sehemu mbalimbali
(hawapo pichani) waliohudhuria Kongamano la Vijana lililofanyika katika
ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa
Kimataifa, Wizaraya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi
Celistine Mushy akitoa mada kwa vijana waliohudhuria Kongamano hilo
lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Vijana, James Kajugusi akisisitiza jambo kwa wanahabari mara baada ya
kufungua Kongamano la Vijana lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee
jijini Dar es Salaam leo (jana).
Baadhi ya Vijana wakipima afya
wakati wa Kongamano la vijana lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee
jijini Dar es Salaam leo (jana).
Mwakilishi Mkazi UNFPA Tanzania,
Dr. Natalia Kanem akiongea na vijana waliohudhuria Kongamano la Vijana
lililofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo (jana).
………………………………………………………………………….
………………………………………………………………………….
Benjamin Sawe Melezo.Dar es Salaam
Imeelezwa kuwa ushiriki wa Vijana katika shughuli mbalimbali
bado ni mdogo kutokana na ukweli kwamba vijana wengi bado hawana
utamaduni wakujitolea katika masuala ya maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bw.
James Kajugusi kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga wakati wa ufunguzi wa Siku ya
Kimataifa ya Vijana Duniani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Bw. Kajugusi alisema vijana wengi pia hawana elimu ya stadi za
maisha, uzalendo, uraia pamoja na stadi za uongozi ikiwa ni pamoja na
moyo wa kujituma na kutafuta taarifa na fursa muhimu hasa zile
zinazohusu maendeleo yao.
“Ni vigumu mtu kujua jambo linaloendelea mahala kama hafanyi utafiti wa kutosha juu ya mambo yanayoendelea”.AlisemaBw. Kajugusi.
Amewaasa kutumia mitandao ya vijana katika ngazi za Kata na
Wilaya pamoja na taasisi za kiraia ili waweze kuonekana na kupaza sauti
zao.
Amesema ni jukumu la Vijana kuhakikisha wanajiunga na Baraza la
Vijana la Taifa ili waweze kuwa na sehemu muafaka ya kujadili mambo
yanayohusu maendeleo yao ikiwa ni pamoja na kuwa na uwanja mpana wa
kuishauri serikali kuhusu masuala yanayowahusu.
“Hivi sasa Serikali ina shughulikia mchakato wa uundwaji wa
Baraza la Vijana la Taifa ambapo tayari Mswada huo umesharidhiwa na
Bunge na Mh. Rais kutia saini uundwaji wake na mara Baraza hili
litakapoundwa kwa mujibu wa sheria mtakuwa na chombo madhubuti cha
uwakilishi wenu katika ngazi mbalimbali za maamuzi Kitaifa na
Kimataifa”.AlisemaBw. Kajugusi.
Wakati huo huo Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa,
Wizaraya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Celistine Mushy
amewashauri vijana nchini kufanya kazi na taasisi za Umoja wa Mataifa
ili kujijengea uzoefu wa kujieleza ikiwa ni pamoja na kujiamini.
“Vijana wengi hamjiamini na washauri mfanye kazi na haya
mashirika ya Umoja wa Mataifa, huko ndipo sehemu muhimu sana ya
kujipatia uzoefu kwani mtafanya kazi na watu kutoka mataifa mbalimbali
na ambao wana uzoefu wa hali ya juu”.Alisema Balozi Mushy.
Siku ya Kimataifa ya Vijana ilianza tangu mwaka 1991 nchini
Australia ikiwa na lengo la kuziwezesha Jumuiya za Kimataifa na Jamii
kwa ujumla kupata fursa ya kusheherekea na kutambuana fasi ya vijana
katika kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika nchi zao
Maadhimisho ya Siku ya vijana hufanyika kila Agosti 12 ambapo
mwaka huu kilele chake kitafanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja na
kaulimbiu yake ni Ushiriki wa Vijana kwenye Maamuzi ya Maendeleo