Katika picha, wa pili kushoto
Mhe. Luhaga Mpina Waziri wa Mifugo na Uvuvi akizungumzia suala ya
uwekezaji wa viwanda katika sekta ya mifugo wa pili kulia ni Waziri wa
Uwekezaji wa Oman Mhe. Salim Al Ismail, akimsikiliza kwa makini. Kulia
ni Balozi wa Oman nchini Mhe. Ali Mahroqi, na kushoto ni Katibu Mkuu
Uvuvi Dkt. Yohana Budeba.
Kushoto Waziri wa Uwekezaji wa
Oman Mhe. Salim Al Ismail, akimtembeza Mhe. Luhaga Mpina Waziri wa
Mifugo na Uvuvi katika meli ya Oman baada ya mazungumzo yalohusu sekta
ya Mifugo na Uvuvi Dar es Salaam leo.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.
Luhaga Mpina kulia akijadili jambo na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe.
Mhe. Salim Al Ismail, baada ya kuuonyeshwa mandhali ya meli ya Oman
iliyotia nanga katika bandari ya Dar es Salaam.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.
Luhaga Mpina kulia akijadili jambo na Waziri wa Uwekezaji wa Oman Mhe.
Mhe. Salim Al Ismail, baada ya kuuonyeshwa mandhali ya meli ya Oman
iliyotia nanga katika bandari ya Dar es Salaam.
Wakiwa katika picha ya Pamoja
,Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina, Waziri wa Uwekezaji wa
Oman Mhe. Salim Al Ismail, Balozi wa Oman Nchini Mhe. Ali Mahroqi,
Katibu Mkuu wa Wizara Uvuvi Dkt Yohana Budeba na watumishi wa Wizara
hiyo baada ya Mawaziri hao kufanya mazungumzo kuhusiana na sekta ya
Uvuvi na Mifugo leo ndani ya meli ya Oman iliyotia nanga katika bandari
ya Dar es salaam.
…………………………………………………………..
NA; MWANDISHI MAALUM
Waziri anayeshughlia masuala ya
Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina amekutana na Waziri wa Uwekezaji wa
Oman Mhe. Salim Al Ismail na kujadili suala zima la uwekezaji wa viwanda
katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi.
Katika Mazungumzo hayo Waziri
Mpina amemueleza Waziri huyo wa uwekezaji wa Oman kuwa Tanzania imekuwa
ikizalisha nyama kwa kiasi cha tani 36 kwa siku na imekuwa ikifanya
biashara kwa kuuza tani za nyama ambazo hazijakatwa katika nchi za falme
za kiarabu ikiwemo Oman, na wakati umefika sasa kwa nchi hizi mbili
kushirikiana kwa pamoja katika Sekta hii kwa Oman kuwekeza katika
Viwanda vya ndani vya nyama kwa kuendeleza viwanda vilivyopo na hata
kujenga Viwanda vipya, akitolea mfano ujenzi wa kiwanda cha nyama cha
Ruvu ambao umefikia 51% kukamilika.
“Tunataka viwanda vyote vya nyama vya ndani vikidhi mahitaji na kuweza kuuza nyama nje ya nchi”. Alisema Mpina.
Kwa upande wake Waziri Salim Al
Ismail alipoelezwa kuhusu viwango na madaraja mbali mbali ya nyama
nchini na mmoja wa mtaalam kutoka wizara hiyo, alisema kuwa Oman ipo
tayari kuwekeza katika sekta ya viwanda vya nyama na kuisaidia Tanzania
kutafuta soko la Marekani kupitia Oman kwani nchi hiyo ya Falme za
kiarabu ina cheti na kibali kilichothibitishwa na mamlaka ya chakula na
dawa cha Marekani, “Tunaweza kuchukua nyama kutoka Tanzania na kuingiza
Marekani bila kulipa Ushuru, tunapaswa kuwa na vyeti halali ili kuweza
kupata soko katika nchi nyingine, Alisema Waziri Ismail.”
Waziri Ismail aliendelea kusema
kuwa, Makampuni Binafsi kutoka Oman yapo tayari kufanya biashara katika
eneo hili hivyo ni wakati wa Tanzania sasa kuonyesha utayari.
“Hizi bidhaa za nyama ni lazima
zitoke kwenu sababu sisi hatuna maji wala majani ya kulisha mifugo kama
ngombe, mbuzi na kondoo ambao huchinjwa kwa wingi baada ya Hijja.
Alisisitiza.”
Kwa Upande wa Sekta ya Uvuvi
Waziri Huyo wa Oman alisema Oman imenunua teknolojia ya kisasa ya
uwekezaji katika fukwe ya Bahari kutoka Texas Marekani, Teknolojia
inayojulikana kitaalam kama Shrim farming inayoruhusu uzalishaji wa
chakula cha samaki wavuliwao katika maji marefu bila kuharibu mazingira.
Alisema Tenkolijia hiyo inaweza
kutumika katika uwekezaji wa Fukwe ya bahari ya Hindi akitolea mfano
eneo la bagamoyo kwa kuzingatia tathmini ya athari ya mazingira na
ujenzi wa miundombinu ya barabara ili kuwasaidia wavuvi wadogo.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt
Yohana Budeba Alisema ni furaha yake kuona wafanya biashara wa Oman
wanakuja kuwekeza Tanzania au kushirikiana na wavuvi wa ndani kwani kuna
samaki wengi wa kutosha kumudu viwanda vya kuchakata na kuwezesha
biashara kubwa ya samaki.