MAOFISA WAFAWIDHI NCHINI WAPIGWA MSASA

September 11, 2015




Tangakumekuchablog
KATIBU Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira, Erick Shitindi, amewagiza Maofisa Kazi Wafawidhi nchini kupiga vita utumikishaji kazi kwa watoto wadogo maeneo ya kazi ikiwa na pamoja na kuwafikisha wahusika katika vyombo vya sheria.
Akifungua kongamano la siku tatu lililoitishwa na Wekeza Mkoani hapa na kuwashirikisha Maofisa Kazi  Wafawidhi kutoka Mikoa mbalimbali nchini jana, Shitindi alisema tabia ya utumikishaji watoto bado ni tatizo nchini.
Alisema tabia hiyo imekuwa ikitumiwa na matajiri na kuwalipa ujira mdogo na hivyo kuwataka kuhakikisha kila Ofisa anasimama katika nafasi yake na kuweza kutokomeza hali hiyo ambayo inakuwa kila kona ya nchi.
“Utumikishaji kazi watoto wadogo kunawaathiri mambo mengi ikiwemo kuwaharibia maisha yao ya mbeleni-----elimu na malezi wanakoseshwa na baadae kuwa watoto wa mitaani” alisema Shitindi na kuongeza
“Unapomtumikisha kazi mtoto mdogo utambue kuwa umemuharibia mfumo mzima wa maisha yake---na hii mara nyingi mtoto anakuwa katika makuzi mabaya na kuweza kujitumbukiza katika vitendo vya uporaji na ujambazi” alisema
Alisema ili kuweza kumaliza tatizo la utumikishaji kazi kwa watoto ni wajibu wa kila mtu kuhakikisha eneo lake hakuna kero hiyo ambayo kadri ya siku linaelekea kukua kwa kasi kila Mkoa.
Akizungumza katika kongamano hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Masha Mshomba, amewataka waajiri kuwawekea mazingira mazuri wafanyakazi wao ikiwemo ajali kazini.
Alisema waajiri wengi wamekuwa hawawekei mazingira mazuri wafanyakazi wao hasa pale itokeapo ajali pamoja na kifo jambo ambalo limekuwa likisababisha kesi na kupotezeana muda.
“Waajiri wengi hawana utaratibu mzuri kwa wafanyakazi wao na kusababisha malumbano hasa wakazi wa ajali au kifo------hili limekuwa tatizo kubwa sana kila kona” alisema Mshomba
Alisema ili kuwawezesha wafanyakazi kufanya kazi kwa weledi ni vyema waajiri kuhakikisha wanawawekea mazingira mazuri na salama na kuweza kutokomeza kero na usumbufu kwa mwajiri na mwajiriwa.
         



Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira, Erick Shitindi, akifungua mafunzo ya siku tatu ya Maofisa Kazi Wafawidhi kutoka Mikoa mbalimbali nchini yaliyoandaliwa na WEKEZA ikiwa na lengo la kupunguza kutumikishwaji kazi  kwa watoto pamoja na fidia kwa wafanyakazi, katikati ni Kamishna wa kazi Wizara ya Kazi na AJIRA Saul Kinemela, kushoto ni  Mkurugenzi Mkuu Mradi wa Wekeza Yuonne Prempeh Furgerson .





 Maofisa Wafawidhi kutoka Mikoa mbalimbali wakishiriki katika Semina ya siku tatu juu ya kupiga vita utumikishwaji kazi kwa watoto iliyoanza jana hoteli ya Tanga Beach

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »