Katibu Mkuu msaafu wa Jumuiya ya
Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Suzan Peter Kundambi katikati akitoa
taarifa ya mwaka kwa Wanachama wa Jumuiya hiyo katika mkutano wa Mwaka
wa ZPC ulioambatana na uchaguzi. Mkutano huo uliofanyika ukumbi wa
Ekrotanal Mjini Unguja.
Wajumbe walioshiriki uchaguzi wa
Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) wakipiga kura kuchagua
uongozi mpya katika mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo ambao uliambatana
na uchaguzi huo ambao uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
Wajumbe walioshiriki uchaguzi wa
Jumuiya ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) wakipiga kura kuchagua
uongozi mpya katika mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo ambao uliambatana
na uchaguzi huo ambao uliofanyika ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
Katibu Mpya wa Jumuiya ya
Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) Faki Mjaka akiomba kura kwa Wanachama
(hawapo pichani)kabla ya kufanyika Uchaguzi huo. Katibu huyo anashika
nafasi ya Suzan Peter mara baada ya kushika nafasi hiyo katika mkutano
wa Mwaka wa Jumuiya hiyo uliambatana na uchaguzi huko ukumbi wa
Ekrotanal Mjini Unguja.
Mweyekiti mpya wa Jumuiya ya
Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) kulia akipongezana na aliyekuwa
mpinzani wake katika nafasi ya Uenyekiti Suleiman Abdallah mara baada ya
kutangazwa rasmi kuwa Mwenyekiti mpya katika uchaguzi uliofanyika
ukumbi wa Ekrotanal Mjini Unguja.
………………………………………………………………………………..
Na Mwashungi Tahir-Maelezo Zanzibar
WAANDISHI wa habari nchini
wamesisitizwa kulinda maadili ya kazi zao ikiwemo kutumia kalamu zao
vizuri hasa kipindi hiki wanapoelekea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Imeelezwa kuwa ikiwa waandishi
watatumia vibaya kalamu zao basi wanaweza kuvuruga hali ya amani na
utulivu na kuweka nchi katika hali ya machafuko.
Hayo yalielezwa na Meneja Bima ya
Maisha Tawi la Zanzibar Aisha Rubenic Makorogo, wakati akifungua
mkutano mkuu wa Jumuiya ya Waandishi wa Habari uliombatana na Uchaguzi
wa kuwachagua viongozi wapya uliofanyika katika ukumbi wa Ekrotanal
Mjini Unguja.
Alisema, kazi muhimu ya
wanahabari ni kuona wanaendelea kutoa elimu kwa jamii na kutokubali
kutumiwa vibaya na watu wenye maslahi binafsina badala yake wafanye
majukumu yao kwa kutenda haki kwa pande zote ili nchi iweze kuvuka
salama.
Aidha alisema, tasnia ya habari
ni tasnia muhimu katika jamii ambayo inategemewa na kila mtu kwani
inaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa wanachi wanaoishi mijini na vijijini
kupata habari zinazotokea nchini kupitia vyombo wanavyofanyia kazi.
Meneja huyo, aliwaomba waandishi
kufanya kazi kwa ueledi wa juu ili kuona nchi yao inaendelea kuwa na
hali ya utulivu na usalama.
Hata hivyo, aliwaomba wanachama
wa ZPC kuchagua viongozi ambao wataweza kuiimarisha na kufanya Jumuiya
yao iondokane na utegegemezi wa misaada huku wakiwa wabunifu ambao
watachagua njia mbadala itakayowaletea kipato katika jumuiya yao.
“Ili kuweza kufanikiwa na jumuiya
yenu kuimarika zaidi basi ni vyema kujenga mshikamano na wanachama wenu
na kuwa wabunifu wa kutegemea vyanzo vingi vya kujiingizia mapato ili
kuikuza jumuiya yenu,” Aliwaasa Meneja Aisha.
Sambamba na hayo aliwaomba
wanajumuiya hao kujiunga na Bima ya maisha ambayo inatoa fursa nyingi
kwa malengo ya maisha ya baadae kwa mwanachama.
Nae Mjumbe mstaafu wa Kamati
Tendaji wa Jumuiya hiyo Suleiman Seif Omar, akitoa shukrani kwa niaba ya
wanajumuiya wenzake waliahidi kuendelea kudumisha maadili ya kazi zao
na wajibu wao katika kuitumikia jamii.
Akizungumza kwa niaba ya Viongozi
wapya Mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo Abdalla Abdul-rahman Mfaume
aliwaomba wajumbe kuzidisha mashirikiano na kuwaahidi kufanya kazi kwa
moyo mmoja ili kuiletea ZPC maendeleo na Taifa kwa ujumla.
Mkutano huo mkuu ulimchagua
Abdalla Abdul-rahman Mfaume kuwa Mwenyekiti wa jumuiya hiyo baada ya
kupata kura 40 na kumshinda mpinzani mwenzake Suleiman Abdalla ambae
amepata kura tisa,
Katibu Mtendaji wa ZPC Faki Mjaka
ambaye hakuwa na Mpinzani alipata kura 46 na Naibu Katibu Mwinyimvua
Nzukwi alipata kura 37 baada ya kumshinda Takdir Ali aliyeata kura 13.
Makamo Mwenyekiti wa Jumiya hiyo
ni Abdalla Pandu aliyepata kura 28 na kumshinda Rahma Suleiman aliyepata
kura 23. Mshika fedha Halima Tamim Thuwein aliyekuwa Mgombea pekee
alipata kura 49 .Wajumbe sita wa kamati tendaji ni Aziza Hassan, Ghania
Mohammed, Mwashamba Haji Juma, Ishaka Omar, Maulid Hassan Kipevu na
Saleh Hassan.