Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi
Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari jioni hii katika ofisi
ndogo ya Makao makuu CCM Lumumba wakati alipotangaza wagombea ubunge
waliopitishwa na Kamati Kuu ya CCM katika majimbo 9 yaliyorudia
uchagmuzi.
…………………………………………………………………………..
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa leo Agosti 17, 2015 katika kikao chake
cha siku moja kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM
Lumumba jijini Dar es Salaa chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dokta Jakaya
Mrisho Kikwete imefanya uteuzi wa Wagombea Ubunge katika majimbo 11
nchini yaliyokuwa yamebakia.
Wagombea Ubunge walioteuliwa na majimbo yao kwenye mabano ni:-
- Ndugu Jerry Slaa – (Ukonga) Dar es Salaam
- Ndugu Edward Mwalongo – (Njombe Kusini) Njombe
- Ndugu Venance Mwamoto – (Kilolo) Iringa
- Ndugu Raphael Chegeni – (Busega) Simiyu
- Ndugu Edwin Ngonyani – (Namtumbo) Ruvuma
- Ndugu Mohamed Mchengerwa- (Rufiji) Pwani
- Ndugu Norman Sigara – (Makete) Njombe
- Ndugu Martin Msuha – (Mbinga Vijijini) Ruvuma
- Ndugu Joel Makanyanga Mwaka- (Chilonwa) Dodoma
Imetolewa na:-
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI
17/08/2015
17/08/2015