Ujenzi wa ofisi za walimu yaanza kutimia-Makonda

January 26, 2018
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa fikira ya kutaka kuwa na ofisi bora za walimu katika mkoa wa Dar es Salaam imeanza kutimia kwa baadhi ofisi kufikia hatua ya upauaji.

Akizungumza leo katika uzinduzi ofisi ya walimu wa shule ya msingi Mapinduzi, Makonda amesema sasa anapata usingizi kuona ndoto yake inanitimia ya kuwapa ofisi nzuri za wanafunzi.

Makonda amesema kuwa wakati alipikuja na wazo hilo alijua hali ni kazi ngumu lakini kutokana na msukumo wa sasa chini ya Serikali ya Dk. John Pombe Magufuli ya elimu bure inatimia.Amesema maendeleo yeyote kwa watoto wa kitanzania yanaanza kwa walimu ambao ndio wataweza kuzalishwa watoto hao kupata elimu na kuinuka kiuchumi.

“Mtu mwenye umasikini hana nyumba ambayo haina bati kamwe hawezi mtu kuwa na nyumba ya bati ili aweze kuwa na nyumba hiyo lazima apate elimu”amesema.Katika uzinduzi huo Mkuu wa Mkoa huyo amesema wanaonunua maeneo ya shule ni kukamatwa pamoja na wanaonunua wakamatwe ambapo mtu mmoja Ajay Shohan amekamatwa kwa kununua eneo la shule ya msingi Mapinduzi.

Katika hafla ya uzinduzi wa upauji wa shule msingi Mapinduzi kampuni ya simu za mkononi ya Halotel imetoa mchango wa fedha taslim Shilingi milioni Hamsini (50,000,000) kwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam ikiwa ni moja ya utekelezaji wa kampuni hiyo katika kuunga mkono jitihada za serikali na ofisi hiyo katika kuboresha sekta ya elimu Tanzania, kupitia ujenzi wa ofisi za walimu kwa shule 402 kati ya hizo shule 295 ni za elimu ya awali/msingi na shule 107 ni za sekondari zilizoko mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi hundi ya mchango huo kwa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam , Paul Makonda, Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Halotel, Le Van Dai amesema mchango huo ni sehemu tu ya jitihada kubwa zinazofanywa na kampuni hiyo katika kusaidia na kuinua sekta ya elimu nchini ikiwa pia ni sehemu ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali katika kuboresha maendeleo ya nchi hasa kupitia sekta ya elimu ambayo ni muhimili wa maendeleo ya kila nchi duniani.

“Tunatambua kuwa, huduma bora ya elimu kwa wanafunzi na waalimu ni moja ya msingi imara katika kukuza sekta ya elimu nchini, kwa kuzingatia hili tumeamua kushirikiana na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kutoa mchango wetu wa kifedha ili kufanikisha mradi wa ujenzi wa ofisi za waalimu ikiwa ni sambamba na kuboresha mazingira utendaji kazi kwa waalimu ya kazi na kurahishisha ufanisi wao katika kuwafunza wanafunzi ambao ni taifa la leo na kesho” alisema Dai.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipokea Hundi ya Milioni 50 kutoka kampuni ya Hallotel kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za walimu 402 Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza katika uzinduzi wa kukamalika kwa ujenzi wa ofisi ya walimu wa shule ya msingi Mapinduzi, leo jijini Dar es Salaam.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi wa Ofisi za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Magereza, Solomon Urio akitoa taarifa ya hatua za mbalimbali za ujenzi wa ofisi za walimu leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa upauaji wa ofisi ya walimu shule ya msingi Mapinduzi leo jijini Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjemini Sitta akizungumza juu hatua ujenzi wa ofisi katika manispaa ya Kinondoni leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipaua jengo la ofisi ya walimu katika shule msingi Mapinduzi leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitoa Cha Polisi Magomeni, Morcase akipata maelezo kwa Ajay Shohan aliyenunua eneo la shule ambapo Mkuu wa Mkoa aliamuru akamatwe,leo jijini Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »