RAIS WA FIFA KUSHUHUDIA FAINAL YA NDONDO SUPER CUP

January 26, 2018

Baada ya kufanyika michuano ya Sports Xtra Ndondo Cup kwa mafanikio katika mikoa ya Mwanza na Mbeya sasa yaongeza wigo kwa mabingwa wa mikoa.
leo jijini Mbeya kamati ya mashindano hayo imetangaza rasmi uwepo wa mashindano ya Ndondo Super Cup itakayofanyika jijini Dar es salaam mwezi februari kwa kushirikisha mabingwa wa mikoa ilipofanyika Sports Xtra Ndondo Cup.
Mwenyekiti wa kamata ya Ndondo Cup Shaffih Dauda amewaambia waandishi wa habari kuwa uwepo wa mashindano hayo ni hitimisho la msimu wa Ndondo Cup 2017 kabla ya kuzinduliwa msimu mpya mwezi wa tatu.
"Mashindano hayo yatashirikisha timu nne na kutakua na michezo minne itakayofanyika tarehe 17, 18, 20, na 21 mwezi februari jiji Dar es salaam" amesema Dauda.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya Ndondo Super Cup Gipson George amesema hili ni jambo lingine kubwa kutoka Clouds Media kama support ya wanamichezo wa Tanzania na ulimwenguni kote kwa ujumla hususani ujio wa viongozi wa FIFA nchini.
"Hakuna asiyejua Rais wa FIFA atakuwepo hapa, hii ni heshima kubwa tuliyopewa Duniani lazima na sisi tuwaoneshe kuthamini ujio wao"
"Shaffih Dauda amewasiliana na TFF kuona namna ya kushirikiana kutusaidia kuwezesha kumpata rais wa FIFA kuja kwenye fainali ya Ndondo Super Cup ndio maana tumepanga iwe tarehe 21" amesema Gipson.
Gipson ameongeza kuwa mashindano hayo yanaendana na agenda ya Rais wa sasa wa FIFA ya kurudi chini kabisa (grassroot) mpira unapochezwa na watu wa kawaida wenye vipaji vya hali ya juu.
Msafara wa FIFA ukiongozwa na Rais Infantino unatarajiwa kuwasili nchini tarehe 21 na siku inayofuata watakua katika mkutano utakaofanyika hapa nchini.
Kutangazwa kwa michuano hiyo mikubwa kwa timu za mtaani jijini Mbeya ni heshima kwa chama cha soka cha mkoa huo MREFA ambapo mwenyekiti wake Elias Mwanjala amesema hiyo ni bahati ya kipekee waliyopata kwenda kukutana na Rais wa FIFA.
"Ndondo imefanyika miaka minne lakini sisi tumepata nafasi ya kukutana na rais wa FIFA ni bahati iliyoje, lakini kikubwa ni wana mbeya kuungana kufanikisha jambo hili kwani sio la chama cha soka bali ni jambo la mkoa na nyie Clouds mtusaidie kupata wadhamini" amesema Mwanjala.
Timu zitakazoshiriki Ndondo Super Cup ni mabingwa wa Mwanza timu ya Mnadani Fc, Mabingwa wa Mbeya Itezi United na mabingwa wa Dar es salaam timu ya Misosi Fc huku Goms United iliyocheza fainal msimu uliopita na misosi imeongezwa kama heshima ya mkoa wa Dar es salaam kuwa mwasisi wa mashindano hayo.
Mbali na kutangazwa kwa mashindano hayo Clouds Media imetoa zawadi ya fedha kwa washindi wa mashindano ya Sports Xtra Ndondo Cup Mbeya yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Mabingwa Itezi Fc wamepata milion tatu, washindi wa pili Terminal fc milion mbili, na washindi wa tatu Tukuyu Star milion moja.
Gasper Samwel Mwaipasi wa Tukuyu Star ameibuka mfungaji bora kwa kufunga goli tano, Frank Anthonwa Itezi United amechaguliwa kuwa kipa bora na  beki wa kushoto wa Itezi United Salum Idrisa Chau ametajwa kuwa mchezaji bora

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »