Na Nteghenjwa Hosseah, TAMISEMI.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Selemani
Jafo ameitaka Tume ya Utumishi wa Walimu(TCC) kusimamia na kuhakikisha
Walimu wote wanapanda madaraja kwa wakati na kwa mujibu wa Elimu zao ili
kupunguza Malalamiko ya Walimu wetu Nchini.
Waziri
Jafo ameyasema hayo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Wajumbe wa Kamati
ya Tume za Utumishi wa Walimu za Wilaya kwa Mikoa ya Dodoma, Morogoro na
Singida uliofanyika katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini
kilichopo Mkoani Dodoma mapema leo Tarehe 26/01/2017.
Waziri
Jafo alisema kuwa kumekuwa na malalamiko, manunguniko na masononeko ya
muda mrefu toka kwa Walimu kuhusu suala hili ya Upandaji wa madaraja
halifuati taratibu aliyeajiriwa mwaka 2000 na anaweza kuwa sawa na yule
aliyeajiriwa mwaka 2008 na wengine wamejiendeleza Kielimi lakin hakuna
mabadiliko yoyote madaraja yao.
‘Tume
hii ifanye kazi ya kurudisha hadhi ya Walimu, iwajengee heshima na
thamani yao katika Jamii, shughulikieni malalamiko yao ya Msingi
madaraja yao yapande kwa kuzingatia muda waliokaa kazini, elimu yao na
Utendaji wao wa kazi; Hilo lisitegemee “favour” ya Katibu wa Watumishi
wa Tume waliopo katika eneo husika’
Wakato
huo huo Waziro Jafo alisisitiza wajumbe wa Kamati za Tume ya Utumishi
wa Walimu kuwa Mkutano huu utumike kupeana maarifa ya kazi, jinsi gani
mnaweza kufanya kazi kwa Usahihi zaidi kwa kuzingatia Sheria iliyounda
TUME YA UTUMISHI WA WALIMU ya mwaka 2015 na Kanuni zake za mwaka 2016.
‘Tume
hii Ndio iwe Kimbilio la Walimu, iwe tegemeo la Utatuzi wa matatizo
yote ya Walimu kwa sababu Tume ya Walimu ndio muajiri wa Walimu,
Inasimamia Nidhamu za Walimu na mchakato mzima unaohusi Ajira za Mwalimu
awapo kazini hivyo mfanye kazi kwa Haki, mkaepuke rushwa, Mkawe na
busara na Hekima katika kutatua changamoto za Walimu’
Aidha
Waziri Jafo hakusita kuwakumbusha wajumbe wa Tume ya Utumishi wa walimu
kuhusu mgawanyo wa Walimu katika halmashauri kwa kuzingatia vipindi
wanavyotakiwa kufundisha na uwekaji wa takwimu sahihi za Walimu waliopo
sasa, wanaotarajiwa kustaafu kwa mwaka huu na kuweka maoteo ya ajira
mpya zitakazohitajika kutokana na nafasi zitakazoachwa na wale
wanaostaafu hivi karibuni.
“Takwimu
zisiwe za kubahatisha tena kupitia Tume hii mhakikishe mnakuwa na
Takwimu sahihi kwanza za mgawanyo wa Walimu katika kila Halmashauri je
mgawanyo wa walimu waliopo Malinyi ni sawa na mgawanyo wa Walimu waliopo
Manispaa sio Mwalimu wa Manispaa anafundisha vipindi viwili kwa wiki
wakati anatakiwa kufundisha 20 na pia mahitaji ya walimu kulingana na
masomo wanayofundisha maoteo kwa kuzingatia idadi ya wale wanaostaafu”
Alisema Jafo.
Waziri
Jafo alimalizia hotuba yake kwa Tume hiyo kufanya tadhimini ya kina
kuhusu maadili ya waalimu na wanafunzi na kwa waalimu wanaovunja
Sheria, Kanuni na maadili ya kazi ya waalimu ikiwemo uzembe , utoro
kazini, rushwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi wachukuliwe hatua
za kinidhamu.
Naye
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu Ndg.Oliva Mhaiki alisema
wajumbe wa kamati za TSC Wilaya waliteuliwa rasmi na Tume katika mkutano
wa Tar 20-25/02/2017 na tangu walipoteuliwa na kuanza kutekeleza
majukumu yao hawakuwahi kupewa mafunzo yeyeote hivyo Sekretariet imeona
upo umuhimu wa kufanya mkutano wa kazi kwa lengo la kuelekezana wajibu
na majukumu yao kama kamati.
Waziri
WA Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,
Mhe.Selemani Jafo akifungua Mkutano wa Kazi wa Wajumbe wa Kamati za Tume
ya Utumishi wa Walimu unaofanyika katika chuo cha Mipango,Mjini Dodoma.
Katibu
wa Tume ya Walimu (kushoto aliyesimama) Mwl. Winifrida G. Rutaindurwa
akiwasilisha taarifa ya Tume katika Mkutano wa Kazi wa Wajumbe wa Kamati
za Tume ya Utumishi wa Walimu unaofanyika katika chuo cha Mipango,Mjini
Dodoma.
Mwenyekiti
wa Tume ya Utumishi wa Walimu, Bw.Oliva Paul Mhaiki akitoa neon la
utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua mkutano wa wa Kazi
wa Wajumbe wa Kamati za Tume ya Utumishi wa Walimu unaofanyika katika
chuo cha Mipango,Mjini Dodoma.
Baadhi
ya wajumbe wakifuatilia Mkutano wa wa Kazi wa Wajumbe wa Kamati za Tume
ya Utumishi wa Walimu unaofanyika katika chuo cha Mipango,Mjini Dodoma.
Waziri
WA Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Mhe.Selemani Jafo(Aliyekaa katikati) katika Picha ya Pamoja na
Sekretariet ya Mkutano wa Kazi wa Wajumbe wa Kamati za Tume ya Utumishi
wa Walimu unaofanyika katika chuo cha Mipango,Mjini Dodoma.